Monday, September 10, 2012

NHC ARUSHA YAFANIKIWA KUJENGA NYUMBA 100 ZENYE THAMANI YA BILIONI SITA HUKU KATI YA NYUMBA HIZO 30 ZIKITUMIKA


NHC ARUSHA YAFANIKIWA KUJENGA NYUMBA 100 ZENYE THAMANI YA BILIONI SITA HUKU KATI YA NYUMBA HIZO 30 ZIKITUMIKA KAMA NYUMBA ZA DHARURA

 

Na Queen Lema,ARUSHA

 

 

SHIRIKA la Taifa la Nyumba hapa nchini (NHC)limefanikiwa kumaliza kujenga mradi wa nyumba 100 zenye garama ya zaidi ya Bilioni sita ambapo nyumba hizo zitachangia kwa kiwango kikubwa sana kutumika kama makazi bora hasa kwa watumiaji mbalimbali wa nyumba wa shirika hilo ambao watahamishwa ili kupisha ujenzi wa miradi mbalimbali ya shirika hilo

 

Akiongea jana mara baada ya kuzindua Mradi huo uliopo kwenye eneo la Levolosi Mjini hapa Mkurugenzi wa maendeleo ya biashara katika shirika hilo Bw David Shambe alisema kuwa ujenzi wa mradi huo umedumu kwa muda wa mwaka mmoja

 

Aliongeza kuwa kupitia mradi huo wa nyumbautakuwa ni wa tofauti sana na miradi mingine kwani mradi huo pia utaweza kuwanufaisha hata wale ambao wanahamishwa kwa haraka katika nyumba mbalimbali za shirika hilo ili kupisha ujenzi wa miradi mbalimbali

 

Alifafanua kuwa mradi huo wa nyumba 100 kwa sasa utaweza kuuzwa nyumba 70 huku nyumba 30 zilizobakia zitatumika kama nyumba za dharura na hali hiyo itaweza kuwasaidia watanzania ambao wanahamishwa huku wakiwa hawana makazi ya kusihi kwa haraka sana

 

“huu mradi utakuwa ni wa tofauti sana kwani mradi huu umejiwekezaa hata kwa ajili ya masuala mbalimbali ya dharura tofauti na miradi mingine na kwa hali hiyo utaweza kuokoa maisha ya watanzania walio wengi sana ambao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za kuwataka kuhama na kupisha ujenzi kwa haraka kwani wengi wao wanaposikia hali kama hizo wanajikuta wakiwa katika wakati mgumu sana”aliongeza Bw David

 

Mbali na hayo alisema kuwa shirika hilo limedhamiria kujenga nyumba bora na za kisasa zaidi ambazo zitaweza kuwanufaisha wananchi wote hasa wale ambao wapo pembezoni mwa miji na majiji mbalimbali ndani ya nchi ya Tanzania ingawaje kwa sasa kuna changamoto kubwa sana ya uhaba wa Ardhi za kujengea nyumba za kisasa ili kuwa na makazi bora na yenye viwango vya hali ya juu sana

 

Alibainisha kuwa changamoto hiyo ya Ardhi kama itaweza kutatulika kupitia Halmashauri basi itaweza kuongeza idadi hata ya nyumba bora  na  za kisasa tofauti na sasa ambapo kuna uhaba mkubwa sana wa Ardhi kwa ajili ya kujengea makazi bora  nay a kisasa zaidi.

 

Katika hatua nyingine alisema kuwa ili kujenga nyumba za viwango tofauti tofauti Shirika hilo kwa sasa lina mipango na mikakati mbalimbali ya kujenga nyumba bora na za kisasa hasa kwa wenye vipato vya chini ambapo watajenga nyumba 223 katika mkoa wa Dar es saalam na nyumba hizo zitawajumuisha wale wote wenye kipato cha chini sana.

 

“Moja ya mikakati yetu ni kuhakikisha kuwa tunajenga nyumba elfu kumi na tano lakini kwa sasa hizi nyumba za bei ya chini kwa watu wenye kipato kidogo wataweza kunufaika nazo na baada ya kumaliza kwa Dar es saalam baadaye tutaenda mahala pengine kwani hii nayo itachangia sana kuweza kuepusha jamii na makazi holela ndani ya jamii zetu”aliongeza Bw David.

 

MWISHO

No comments:

Post a Comment