Saturday, August 11, 2012

KITUO CHA UTAFITI WA MAZAO CHASHINDWA KUFIKISHA TEKNLOJIA 30 KWA WAKULIMA KWA UKOSEFU WA FEDHA


KITUO CHA UTAFITI WA MAZAO CHASHINDWA KUFIKISHA TEKNLOJIA 30 KWA WAKULIMA KWA UKOSEFU WA FEDHA

KITUO cha Utafiti wa mazao ya kilimo kanda ya kaskazini(SARI) kimeshindwa kufilkisha teknolojia mpya  thelathini kwa wakulima kwa zaidi ya miaka minne mfululizo kutokana na kukabiliwa na uhaba wa Fedha hali ambayo inafanya malengo mbalimbali ya Kilimo kwanza kufikiwa

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi mkuu wa Kituo hicho Dkt Mboya Mgendi wakati akiongea na mkuu wa mkoa wa Arusha bw Magesa Mulongo ndani ya viwanja vya Taso Nane Nane Mjini wakati alipotembelea banda la Kituo hicho

Dkt Mgendi alisema kuwa kwa Muda mrefu Serikali imekisahau kituo hicho huku kituo hicho kikiwa ni moja ya vituo ambavyo vinahudumia Mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro, na Tanga ambapo pia mikoa hiyo ni Mikoa ambayo inaitaji msaada mkubwa sana katika kuimarisha shuguli za kilimo hasa vijijini

Alisema kuwa hapo awali Kituo hicho kilikuwa ni moja ya vituo ambavyo vilikuwa vinamsaidia sana mkulima hasa wa chini na wa kijijini na matunda yake yaliweza kuonekana katika uzalishaji na ukulima tofauti na sasa ambapo baadhi ya Vijiji vinashindwa kufikiwa kutokana na uhaba wa fedha ambao umedumu katika kituo hicho kwa miaka minne sasa.

“tunasikitika sana kwa kuwa tuna buni teknolijia kila siku tena teknolojia ambazo ni mpya kabisa kisha zinashindwa kuwafikia walengwa kwa kuwa tunafikaje ni lazima fedha itumike kusafirisha hata hawa wataalamu, na kutokana na hilo tunabaki na hizi teknolojia wakati walengwa wa hizi teknolojia ni wananchi tena wa  chini sasa Serikali inatakiwa kuliangalia suala hili kwa undani sana ili kuweza kuboresha zaidi Kilimo kwanza”alionngeza Dkt Mgendi.


Aidha Dkt Mgendi alisema kuwa kutokana na hali hiyo imesababisha malengo mbalimbali ambayo yanakusudiwa na kituo hicho kushindwa kufikiwa huku  Serikali nayo ikilia na kuweka Mikakati mbalimbali juu ya Kilimo kwanza hali ambayo kama ingetumika kwa kuwawezesha wataalamu mbalimbali  wa kituo hicho basi Kilimo hasa kwa mikoa ya Kaskazini ingeboreka zaidi.


Pia aliiomba Serikali kuhakikisha kuwa inaangalia kwa undani sana umuhimu wa kituo hicho hassa kwa Mikoa ya Kanda ya Kaskazini ambapo kuna changamoto kubwa sana ya Matumizi sahihi ya  utafiti  wa kilimo, Mbegu bora za kilimo,pamoja na dhana ambazo bado wakulima wanaitaji elimu zaidi kutoka kwa wataalamu hao  wa kilimo bora.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha bw Magesa Mulongo alisema kuwa Kituo hicho kina umuhimu mkubwa sana hasa kwenye Kilimo kwanza na Changamoto mbalimbali ambazo zinaikabili kituo hicho zitasikilizwa ili kuendelea kuimarisha zoezi zima la Kilimo kwanza hasa kwa Mkoa wa Arusha ambao bado unaitaji sana nguvu ya watalaamu wa Kilimo bora

“Nitakuja katika kituo chenu cha utafiti tutaongea ili tuweze kuona juu ya hili suala ambalo limeongelewa hapa ingawaje na kituo hiki kinatakiwa kuhakikisha kuwa kila kitu ambacho wanakizalisha kinatakiwa kuwepo kwenye mitaa yote ya kanda ya kaskazini ili kuboresha Kilimo kwanza ndani ya Mikoa hiyo husika”aliongeza Bw Mulongo.


MWISHO

NMB YAAHIDI KUWASAIDIA WAKULIMA WADOGO WADOGO

BI VICKY AMBAYE NI MENEJA WA BENKI YA NMB KWA KANDA YA KASKAZINI AKIPOKEA CHETI KAMA ISHARA YA USHINDI KATIKA MAONESHO YA NANENA NE AMBAPO MGENI RASMI ALIKUWA NI MIZENGO PINDA





NMB YAHIDI KUBORESHA KILIMO CHA WAKULIMA WADOGO WADOGO KWA KANDA YA KASKAZINI

BENKI ya NMB  kanda ya kaskazini imesema kuwa ina mikakati mbalimbali ya kuweza kuimarisha kilimo hasa kwa wakulima wadogo wadogo sanjari na kutoa mikopo mbalimbali kama vile Pembejeo kwa wakulima hao wadogo wadogo ili kufanya Kilimo chao kuwa cha Kisasa zaidi


Hayo yameelezwa na Bw Ally Jamali ambaye ni afisa uhusiano kilimo katika benki hiyo wakati alipokuwa akiongea na Waziri Mkuu Bw Mizengo Pinda ambaye alitembelea banda la NMB katika viwanja vya Nane nane (TASO)mapema juzi

Aidha bw Jamali alisema kuwa ili kumkomboa Mkulima wa sasa Benki hiyo imejidhatiti kuhakikisha kuwa  wakulima wadogo wadogo wanapata huduma za msingi ili nao waweze kufikia malengo yao mbalimbali ambayo wamejiwekea

Alifafanua kuwa kwa sasa kupitia mfum wa Stakabadhi ya mazao ghalani (WRS) wwakulima wa kanda ya kaskazini wameweza kupata mikopo ya aina mbalimbali ambapo lengo ni kukomboa zaidi Kilimo kwanza

“huu mfumo na mingine inayokuja itaweza kusaidia sana kushamiri na kustawi kwa mazao mbalimbali ambayo yana tegemewa ndani ya kanda yetu ambapo kwa sasa tuna mazao kama vile Kahawa,Mbaazi, Mahindi, pamoja na Korosho huku mpaka sasa matunda na mafanikio mbalimbali yameshaonekana kupitia mfumo huu”aliongeza Bw Jamali.

Pia alisema kuwa ili kuendelea kuboresha zaidi hali ya Kilimo wamefanikiwa kufanya majaribio ya pembejeo kwa ajili ya wakulima wa mbogamboga ambapo Kama zoezi hilo nalo litakamilika basi litachangia sana kukuza na kuimarisha hata uchumi wa wakulima hao.

Aliongeza kuwa Pembejeo hizo za wakulima wadogo wadogo zitakuwa na faida kubwa sana kwenye kilimo chao kwani hapo awali wakulima hao walikuwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali hali ambayo ilifanya washindwe hata kukopesheka na Taasisi mbalimbali za Fedha nchini lakini kupitia Pembejeo hizo wataweza kuzalisha kwa nguvu kubwa hivyo kukopesheka kwa Uraisi sana.

“kwa hapo awali wakulima hawa ambao ni wadogo wadogo walikuwa wanashindwa kuaminika kwa uraisi sana lakini kama watafanikiwa kuuungana nasi katika mikopo na mazoezi kama haya watachangia kwa kiwango kikubwa kubadilisha hata aina ya kilimo ambacho wanalima kwa sasa na kuwa kilimo cha kisasa zaidi”aliongeza bw Jamali

Katika hatua nyingine aliwataka wakulima hasa wadogo wadogo kuhakikisha kuwa wanaachana na dhana ya kuogopa Taasisi mbalimbali za fedha na kuhakikisha kuwa wanafuatilia kwa ukaribu kwani hata wao wana nafasi kubwa sana ya kuweza kukopa na kufikia ndoto zao mbali mbali ambazo wanazo katika kilimo