Saturday, October 26, 2013

NYUMBA ZA ASKARI ZIMA MOTO ARUSHA ZAKABILIWA NA UCHAKAVU ULIODUMU KWA ZAIDI YA MIAKA 50


Na Queen Lema, Arusha.

Jeshi la zima moto na ukoaji mkoa wa Arusha linakabiliwa na changamoto
ya uchakavu wa nyumba uliodumu kwa miaka zaidi ya 50 ambapo pia
uchakavu huo wa nyumba unaenda sanajari na uahba wa Vyoo hali ambayo
inasababisha ongezeko la magonjwa ya Malaria kutokana na nyumba hizo
kugeuka kuwa makazi ya Mbu.

Aidha nyumba hizo zilijengwa mwaka 1954 ambapo mpaka sasa hazijaweza
kufanyiwa marekebisho ya aina yoyote ile hali ambayo inasababisha
nyumba hizo kugeuka magofu.

Hayo yamelezwa na Andrew James Mbate ambaye ni kamanda Zima moto na
uokoaji mkoa wa Arusha wakati akiongea na wafanyakazi wa jeshi hilo
mara baada ya kumuaga aliyekuwa kamanda wa jeshi hilo Bw Jesward
Ikonko mapema jana.

Kamanda Andrew alisema kuwa nyumba hizo za jeshi zilijengwa miaka
mingi iliyopita lakini toka kujengwa kwake mwaka 1954 mpaka sasa
hazijaweza kufanyiwa marekebisho ya aina yoyote ile jambo ambalo
linasababisha wafanyakazi pamoja na familia zao ziweze kuishi maisha
ya kuugua kila mara.

“tunaweza kusema kuwa nyumba hizi zimegeuka nyumba za mbu kwani kwa
juu hazijaweza kuzibwa na baridi yote inapita lakini pia hata kwa juu
kwa kuwa kuna uwazi mkubwa sana unasababisha mbu kukaa kama nyumbani
kwani sasa hali hiii kwa kweli inasababisha wafanyakazi wetu washindwe
kufanya kazi zao kwa kufuraia makazi’aliongeza hivyo.

Pia alisema kuwa mbali na nyumba hizo kugeuka chakavu sana lakini pia
hata suala la vyoo navyo ni chakavu kwa kiwango cha hali ya juu jambo
ambalo ni hatari kwa afya za watumiaji

“tunaweza kujiuliza kuwa choo kilichojengwa mwaka 1954 mpaka sasa
kitakuwaje na kinatumiwa na familia nyingi je kwa hali hii wafanyakazi
wataweza kufuraia maisha au ndo wataboreka “alihoji Kamanda huyo.

Kutokana na hali hiyo alisema kuwa ni vema kama mchakati wa nyumba
hizo za watumishi sasa zikageukia upande wa Wizara kutoka katika
mikono ya Jiji la Arusha kwani kama zitakuwa chini ya wizara zitaweza
kupata marekebisho makubwa ambayo yataongeza utendaji kazi mzuri wa
wafanyakazi.

Akiongelea suala zima la utendaji kazi wa kikosi hicho cha zima moto
mkoa wa Arusha alisema kuwa mkoa wa Arusha unakabiliwa na tatizo la
ujenzi holela hali ambayo inasababisha wakati mwingine washindwe
kuokoa baadhi ya nyumba ambazo zinateketea kwa Moto hivyo basi ni vema
kama kamati ya mipango miji wakati mwingine ikawa inatoa elimu kwa
wananchi wanaotaka kujenga nyumba zao.

MWISHO

IDADI YA WANAWAKE WABUNGE SADC IMEONGEZEKA

Na Gladness Mushi,Arusha

IDADI  ya wabunge wanawake  kwenye nchi wanachama wa mabunge ya nchi za kusini mwa Afrika (SADC) imeongezeka ingawaje kwa Tanzania bado baadhi ya wanawake wanahofu kubwa ya kushiriki katika chaguzi mbalimbali kutokana na changamoto zilizopo kwenye jamii

Hayo yameelezwa  na Anna Makinda ambaye ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akiongea na vyombo vya habari mapema leo kuhusiana na mkutano  wa 34 wa jukwaa la Mabunge ya Nchi wanachama wa jumuiya  ya maendeleo kusini mwa Afrika unaotarajiwa kufunguliwa na Makamu wa Raisi dkt Gharib Bilali mapema jumapili ijayo.

Aidha Makinda alisema kuwa kuongezeka kwa wabunge wanawake katika mabunge ya SADC kunatokana na juhudi mablimbali ambazo zinafanywa na jumuiya hiyo hali ambayo nayo imefanya mabadiliko makubwa sana kwenye baadhi ya nchi.

Alisema kuwa pamoja na ongezeko kubwa la idadi ya wabunge wanawake katika jumuiya hiyo lakini kwa Tanzania bado baadhi ya wanawake wanauoga na hofu ya kushiriki katika chaguzi kuu jambo ambalo wanatakiwa kulipinga.

"hapa tunaona kuwa hii idadi ya wanawake ni kubwa katika jumuiya hii ya SADC lakini kupitia ongezeko hili ni muhimu sana kwa wanawake wa Tanzania nao wakahakikisha kuwa wanajitokeza kwenye chaguzi mbalimbali na kushiriki kwani uwezo wa wao kuwa wabunge upo na wasiogoope wala kujiwekea udhaifu wa changamoto”aliongeza Makinda

Wakati huo huo alidai kuwa wanawake wa Tanzania hawapaswi kukatishana tamaa wao kwa wao na badala yake wanatakiwa kupena moyo hasa pale wagombea wanawake wanapokutana na changamoto kubwa ambazo wakati mwingine zinasababisha baadhi yao kukimbia nafasi za uongozi

Awali akiongelea mkutano huo wa 34 alisema kuwa Nchi ya Tanzania imepewa nafasi ya kuwa mwenyeji mkuu wa mkutano huo ambao utaweza kuwashirikisha viongozi wa Mabunge mbalimbali kutoka SADC na hivyo kupitia mkutano huo wataweza lkujadili mambo mbalimbali

Makinda alisema kuwa mkutano huo utaaangalia vitu muhimu kwa nchi wananchama kama vile  vigezo vya kusimamia na kutathimini mwenendo wa chaguzi za nchi wanachama wa jumuiya hiyo.

“Kauli mbiu ya mkutano huu ni  vigezo vya kuendesha na kutathimini chaguzi kwa nchi za kusini  mwa Afrika hivyo basi hapa tutaweza kuangalia na kukagua hilo hivyo tutaweza kupata hata majibu ambayo yatasaidia nchi zetu”aliongeza Makinda.

MWISHO

WAFADHILI KUTOKA UJERUMANI WATOA MSAADA WA VITABU WENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 9


MERU

WAFADHILI kutoka Ujerumani wamefanikiwa kutoa msaada wa vitabu venye thamani ya Milioni tisa kwa shule ya sekondari Leguruki iliopo Wilayani Meru mkoani Arusha kwa lengo la kuongeza ufanisi wa elimu zaidi kwenye shule hiyo.

Akiongea na wanafunzi shuleni hapo mapema jana mara baada ya kupokea msaada huo Mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Arusha John Palangyo alisema kuwa msaada huo utasaidia sana shule hiyo ya sekondari ambayo pia ipo chini ya Chama cha mapinduzi.

Palangyo alisema kuwa wafadhili hao wameamua kutoa msaada huo wa vitabu venye thamani ya milioni tisa lakini ni wajibu wa wanafunzi kuhakikisha kuwa wanavisoma na kuvifanyia kazi vitabu hivyo kwani vina mitaala ya nchi ya Tanzania

Pia alsiema kuwa kama wanafaunzi wa shule ya sekondario yoyote ile hapa nchini watakuwa na tabia ya kujisomea vitabu mbalimbali basi watachangia kwa kiwango kikubwa uelewa tofauti na sasa ambapo bado wapo wanafunzi wanaosoma kwa kufundishwa na walimu pekee.

Alibainisha kuwa kuna umuhimu mkubwa sana wa walimu wenyewe kuhakikisha kuwa wanawasisitiza wanafunzi kujisomea vitabu na kuachana na tabia ya kujidanganya kuwa hata wasiposoma watakuwa na maisha mazuri tena yenye mvuto wa hali ya juu jambo ambalo nalo linachangia sana kuongeza idadi ya wanaofeli katika shule za Sekondari pamoja na Vyuo vikuu hapa nchini

“mimi napenda kuwaambia kuwa msije kuona kuwa watu wana maisha mazuri mkadhani kuwa hawakujituma kusoma vizuri shuleni ni lazima kama mnataka maisha mazuri basi mjitume kusoma kwa bidii lakini pia msikubali kujiwekea fikra ambazo zinawapotosha kwani hizo ndizo zinazochangia ninyi mje kuwa na  maisha mabaya hapo baadae”aliongeza Palangyo

Katika hatua nyingine aliwataka hata walimu kuwatengenezea wanafunzi mazingira mazuri  na kuwapa motisha wanafunzi  hasa kwenye suala zima la usomaji wa vitabu kwani kwa kufanya hivyo kutaweza kuruhusu walio wengi kupenda kujisomea vitabu.

Awali mkuu wa shule hiyo ya Leguruki Emanuel Loi alisema kuwa msaada huo wa Vitabu umekuwa na tija kubwa sana shuleni hapo kwani hapo awali shule nzima ilikuwa na vitabu 52 na sasa wameweza kufanikiwa kupata vitabu zaidi ya elfu jambo ambalo litaweza kuwanufaisha wanafunzi shuleni hapo

Alimaliiza kwa kusema kuwa hata wazazi nao wana jukumu kubwa sana la kuhakikisha shule za sekondari zinakuwa na Vitabu vya kutosha ili kuweza kuharakisha maendeleo ya elimu

MSIWAACHIE WATOTO UHURU WA UTANDAWAZI NDIO CHANZO CHA KUFELI


Na gadness, Arusha

IMEELEZWA kuwa tabia ya wazazi kuwaachia watoto uhuru wa utandawazi hasa simu za mikononi kwa muda mrefu ndio chanzo kikubwa cha mdonodko wa elimu kwa nchi ya Tanzania kwani kwa sasa wapo baadhi ya wanafunzi ambao wanatumia muda mrefu sana kwenye utandawazi kuliko kwenye elimu

Kwa sasa hata mitandao ya kijamii ambayo ipo inatumiwa wakati mwingine vibaya na wanafunzi hali ambayo wazazi wanatakiwa kuchukulia tahadhari tena kwa haraka sana.

Hayo yameelezwa na Askofu Erick Mukwenda wakati akiongea na wazazi pamoja na walezi wa wanafunzi wa darasa la saba kwenye shule ya Maranatha iliopo jijini Arusha mapema jana katika maafali ya sita ya shule hiyo.

Askofu huyo alisema kuwa maana halisi ya utandawazi wakati mwingine imegeuzwa kabisa na wanafunzi na hivyo wengi wanadhubutu kuwekeza huko kuliko kuwekeza zaidi kwenye masomo jambo ambalo ni hatari sana

Alisema kuwa ili kuikwepesha jamii na tabia hiyo ni lazima kwanza wazazi waangalie suala hilo kwa mapana zaidi kwani wakati mwingine  watawakemea watoto baasi wataogopa na hawatajihusisha sana na mitandao hiyo au utandawazi

Pia aliongeza nao wazazi wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanaepukana na tabia ya kufikiria zaidi ada kuliko kufikiria malezi ya watoto kwani kwa sasa walimu pekee ndio wanaoachia suala zima la malezi jambo ambalo wakati mwingine linakuwa gumu sana

“kama tunataka maendeleo ya elimu kwa nchi ya Tanzania ni lazima kwanza tuhakikishe kuwa tunashirikiana kwenye malezi kwani malezi ya wanafunzi sio ada bali hata maadili hivyo basi wazazi sasa mnatakiwa kubadilika”aliongeza Askofu huyo

Katika hatua nyingine aliwataka wazazi pia kuwapa elimu wanafunzi juu ya matumizi ya simu za mkononi lakini pia kuachana na tabia ya kuwapa simu pindi wanapokuwa mashuleni kwani pia jambo hilo pia linachangia sana wanafunzi kuwazia simu kuliko  masomo.

MWISHO

SERIKALI YATAKIWA KUBORESHA MAZINGIRA YA WAFUGAJI ILI WASIKONDE WAO NA MIFUGO YAO


|Serikali imetakiwa kuboresha mazingira ya wafugaji wan chi ya
Tanzania pamoja na miundombinu yake kwani kwa sasa wapo baadhi ya
wafugaji ambao hawanufaiki na ufugaji na badala yake wanakonda wao
pamoja na mifugo yao

Hayo yameelezwa Jijini hapa na Naibu waziri wa mawasiliano sayansi na
Teknolojia January Makamba wakati akiongea na wataalamu wa mifugo
Tanzania mapema jana kwenye mkutano wa 36 unaondelea jijini hapa.

Makamba alisema kuwa inaskitisha kuona kuwa wafugaji na mifugo yao
imekondeana kwa kuwa haina mazingira mazuri hivyo kuna umuhimu mkubwa
sana wa Serikali kuwekeza kwenye sekta hiyo ambayo bado inakabiliwa na
changamoto kubwa

Alisisitiza kuwa kama mazingira ya wafugaji wa Tanzania yataweza
kuboreshwa kwa asilimia 100 ni wazi kuwa hata mazao yanayotokana na
mifugo nayo yatakuwa ya hali ya juu sana hivyo kuruhusu kuweza kuingia
hata kwenye soko la dunia.

“katika nchi ya Tanzania wapo baadhi ya wafugaji ambao wanafuga
ilimradi waonekane nao wamefuga sasa hili si jambo jema ni muhimu sana
kwa Serikali kuweza kuboresha mazingira na miundombuni lakini pia
kuweza kuwapa misaada muhimu kwa ajili ya kuhimiza uzalishaji na
ufugaji bora zaidi”aliongeza Makamba

Pia alisema kuwa tabia ya kubaki na idadi ya mifugo hususani ngombe
kwenye takwimu za nchi bado haitoshi na wala haijengi bali Nchi
inatakiwa kuwa na takwimu nzuri sana za uzalishaji na ufugaji bora
kama ilivyo kwa nchi zilizoendelea katika sauala zima la mifugo.

Naye mwenyekiti wa chama cha wataalamu wa mifugo Tanzania Stella
Bitende alisema kuwa bado kuna umuhimu mkubwa sana wa Serikali
kuhakikisha kuwa hata wananchi wa Vijijini nao wanapata huduma za
wataalamu wa mifugo kwani idadi ya wataalumu hao(Maafisa Ugani)ni
ndogo sana ukilinganisha na uitaji

Bitende aliongeza kuwa kama Serikali itaweza kuongeza idadi ya
wataalumu wa ugani hasa katika maeneo hayo ya vijijini basi ufugaji
utaweza kuwanufaisha wananchi wengi sana tofauti na sasa ambapo katika
maeneo ya vijijini bado wanatumia mbinu na njia za zamani sana

Alimalizia kwa kusema kuwa pamoja na kuwa chama hicho kimeweza
kujipanga hasa katika masuala ya tafiti mbalimbali lakini bado zipo
changamoto kubwa kama vile nyenzo za uzalishaji ,ambazo zinawanyima
kufanikiwa katika uzalishaji kwenye sekta ya mifugo.

MWISHO

Wafanyakazi wa hoteli hawana ujuzi na elimu ya kutosha.


,Arusha.
IMEELEZWA kuwa asilimia kubwa ya watanzania wamekuwa  hawapati nafasi mbalimbali za ajira kwenye mahoteli kutokana na wengi wao kutokuwa na elimu  ya kutosha na hivyo kuchangia wageni kutoka nje ya nchi kupata ajira kwa urahisi .

Aidha hali hiyo imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa sana vijana wengi kukosa ajira katika mahoteli kutokana na wengi wao kutokuwa na elimu ya  vitendo na hivyo kuishia kutumia elimu ya darasani.

Hayo yalisemwa jana na  Meneja wa programu  wa shirikisho la vyama vya utalii Tanzania (TCT)  Fatma Mabrouk  alipokuwa akizungumza na wamiliki wa mahoteli jijini Arusha wakati wa kuutambulisha programu ya mafunzo  kazini ambayo itawanufaisha vijana wenye umri wa miaka 17-25.

Alisema kuwa, programu hiyo kwa sasa ipo katika hatua ya majaribio  kwa miaka miwili ambapo wameanzia jijini Dar es Saalamu kwa kuzungumza na wamiliki  wa  mahoteli kwa lengo la kuitambulisha programu hiyo ili waweze kuitumia kwa wafanyakazi  wao na kuongeza ufanisi na utendaji kazi zaidi.

Fatma aliongeza kuwa,programu hiyo itasaidia kuwaongezea wafanyakazi wa mahoteli ujuzi zaidi katika utendaji kazi wao kwani wengi wao hawana ujuzi  huo hali inayochangia wengi wao kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

‘kwa sasa hivi wengi wao wanajifunza masomo ya darasani kwa asilimia 70 huku makazini wakitumia asilimia 30 tu, hali ambayo inaadhiri utendaji kazi wao kwa kiasi kikubwa kutokana na kutumia muda mwingi darasani badala  ya makazini’alisema Fatma.
Naye Mkurugenzi mtendaji wa chama cha mahoteli  Tanzania(HAT) ,alisema kuwa,Lathifa Sykes alisema kuwa,baada ya muda majaribio kumalizika programu hiyo itapitishwa kuwa sheria na hatimaye kuweza kutumika katika vyuo mbalimbali vya utalii hapa nchini .

Sykes aliongeza kuwa,kwa sasa vyuo vingi vya utalii vimekuwa vikitoa elimu hiyo kwa njia tofauti tofauti na hivyo kupitia programu hii itasaidia kufundisha kitu kimoja kwa vyuo vyote na hivyo kuwawezesha wanafunzi hao kupata ujuzi unaohitajika katika soko la hoteli.

Alisema kuwa,programu hiyo inafadhiliwa na shirika la kazi duniani (ILO) ambapo lengo halisi ni kuhakikisha kuwa idadi ya wafanyakazi kwenye mahoteli inaongezeka .
Mwisho.

Tuesday, October 1, 2013

MBUNGE LEMA,AFUTIWA MASHITAKA





Na GLADNESS MUSHI, ARUSHA

Mahakama ya hakimu mkazi imefuta kesi iliyokuwa inamkabili mbunge wa jimbo la Arusha Goodbless Lema na kudai kuwa upande wa mashitaka hakuwa na nia ya kuendeleza kesi hiyo.

Aidha kesi hiyo iliyokuwa inamkabili mbunge huyo ilikuwa ni ya uchochezi  katika chuo cha uhasibu Arusha ambapo vurugu hizo zilisababisha chuo hicho kufungwa.

Pia kesi hiyo ilipangwa kuanza kusikilizwa leo  mbele ya Hakimu Devotha Msofe wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ili kuweza kuitolea ufafanuzi zaidi.

Hataivyio mara baada ya hakimu huyo pamoja na Jopo la mawakili kuingia mahakamani hapo, Wakili wa Serikali Elianenyi Njiro, aliiomba mahakama kesi hiyo ifutwe chini ya kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, kama ilivyorekebisha 2002.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa upande wa mashitaka uliona hauna haja wala tija ya kuendelea na kesi hiyo lakini pia ni vema kama kipengele cha sheria kikaangaliwa zaidi.

Pia mara baada ya ombi hilo mahakama iliridhia na kudai kuwa kuanzia sasa Mbunge huyo yupo huru kwa mujibu wa kifungu cha sheria.

Awali Akisoma maelezo ya awali Julai 10 mwaka huu mahakamani hapo, Wakili wa Serikali Elianenyi alidai Aprili 24 mwaka huu, Lema akiwa eneo la Freedom Square la IAA alifanya kosa la uchochezi wa kutenda kosa kinyume na Sheria ya Kanuni ya Adhabu.

Akifafanua shtaka hilo, Elianenyi, alidai kuwa Lema aliwaeleza wanafunzi wa chuo hicho ambao walikuwa wamekusanyika kufuatia kuuawa kwa mwenzao na watu wasiojulikana kuwa;

Upande wa mashtaka tayari ulikuwa umewaleta mashahidi watano ambao ni Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Arusha, Giles Mroto, Naibu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha, Faraji Kasidi, Inspekta wa Polisi Bernard Nyambalya, Jane Chibuga na Mwadili wa Wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha, John Joseph Nanyaro.

MWISHO