Sunday, September 30, 2012

WENYE UELEWA FINYU, WASIOJUA KUSOMA NA KUANDIKA WAPENI MUDA WA ZIADA ILI WAFIKE KWENYE KIWANGO BORA CHA ELIMU



Na Queen Lema, MERU

MBUNGE wa Jimbo la Arumeru Mashariki Bw Joshua Nassari, ameishauri Serikali hasa kwa Mkoa wa Arusha kuhakikisha kuwa inaweka mikakati zaidi hasa kwa wanafunzi ambao wanakabiliwa na changamoto ya kuwa na uelewa mdogo, pamoja na kushindwa kusoma na kuandika kupewa muda wa ziada na fursa nyingi zaidi za muda wa masomo ili kuweza kupunguza idadi hiyo ambayo itapunguza changamoto hiyo ambayo inaikabili shule nyingi sasa.


Alisema kuwa kwa sasa wanafunzi ambao hawajui kusoma na kuandika pamoja na wale wenye uelewa mdogo huwa wanaachwa kama walivyo huku muda wa masomo nao ukiwa unaendelea hali ambayo ndiyo inayochangia hata maendeleo hafifu ya Elimu kwa baadhi ya wilaya hapa nchini

Bw Nassari aliyasema hayo wakati wa maafali  tisa ya darasa la saba katika shule ya Fikiria Kwanza  Usa river  wilayani Meru Mkoani hapa mapema jana ambapo pia alisema kuwa ipo haja ya Serikali kuendelea kuwekeza zaidi katika masuala ya Elimu hasa kwa wanafunzi ambao wanakabiliwa na changamoto kama hiyo mkoani hapa.

“tusilie kila siku elimu elimu bali  tunapaswa kuangalia changamot ambazo zinaikabili sekta hiyo tena hasa katika wasiojua kusoma na kundika pamoja na wale wenye uelewa finyu lakini kama wanafunzi hawa tutakuwa tunawaacha kama hasara ya mzazi basi tutakuwa tunaongeza idadi ya Mambumbu ila kama tutaweka  Nia hata kwa kuwapa walimu kazi ya ziada ya kuwafundisha hawa watoto basi kiwango cha elimu kitakuwa kwa kiwango kikubwa sana’aliongeza

Alisema kuwa mbali na changamoto ambazo zinaonekana kuwa chanzo cha kusababisha elimu hasa ya Mkoa wa Arusha kuwa chini pia Serikali inatakiwa kuhakikisha kuwa inaangalia zaidi shule za Kata kwani nazo zimekuwa shule ambazo zinasahaulika sana na kusababisha hata aina ya elimu ambayo inatolewa ndani ya shule hizo kuwa ni elimu duni sana huku asilimia kubwa ya watanzania wakiwa wanategemea elimu kutoka ndani ya shule hizo

“kwa upande wa Vijijini shule hizi ni tegemeo kubwa sana kwa jamii lakini sasa hapa inaonekana baadhi ya watendaji wa Serikali kukwepa  majukumu yao na kusababisha mfumo wa elimu hizi kuwa chini lakini kama wangekuwa wanazitatua kero mbalimbali basi hata idadi ya watoto wenye uelewa finyu na wale wasiojua kusoma na kuandika nayo ingepungua sana na hivyo kukuza hata kiwango cha elimu ya Meru na Mkoa wa Arusha kwa Ujumla”aliongeza  Bw Nassari

Hataivyo Mkurugenzi mtendaji wa shule hiyo ya Fikiria kwanza Bi Necta Lema alisema kuwa ili kuboreesha suala zima la elimu hapa nchini kwa ujumla nazo shule mbalimbali zinatakiwa kutatua kero za elimu ambazo zipo sanjari na kuhakikisha kuwa wanajiwekea taratibu za kuwapa Motisha walimu mara kwa mara ili kuongeza hata kiwango cha ufaulu kwa haraka sana

Bi Lema alibainisha kuwa kwa sasa zipo baadhi ya shule ambazo zinawasahau sana walimu katika kuwapa Motisha hali ambayo inawafanya walimu wa shule hizo kuweza kufundisha kwa njia ya mazoea tofauti na pale ambapo walimu watakapotangaziwa Motisha kuweza kufundisha  kwa ufanisi wa hali ya juu ili kuwa mfano mzuri kwa shule na hata mbele ya wanafunzi.

“Motisha kwa walimu ni jambo jema sana kwani sisi tayari mpaka hapa tumeshajaribu kuweza kufanya hivyo na matunda tumeyaona hivyo ni jukumu la kila mkuu wa shule kuhakikisha kuwa mbalina kukazania elimu bora lakini kuwa mbunifu na ubunifu huo utachangia sana kuweza kuongeza hata idadi ya wanafunzi ambao wanafranya vema zaidi “aliongeza Bi Lema

No comments:

Post a Comment