Friday, September 28, 2012

WAMACHINGA WAGAWANA MAENEO KAMA NJUGU KILOMBERO

NA WAANDISHI WA UPAKO WA HABARI, ARUSHA

KUNDI la wa machinga mjini arusha leo wamevamia eneo la la
wazi lilopo ngarenaro na kujigawia tayari kwa kufanya biashara.

Kundi hilo la wamachinga limevamia eneo hilo ambalo lilikuwa
limezungushiwa mabati kwa kipindi cha
muda mrefu kilichopo ngarenaro jijini hapa wakidai kuwa eneo hilo ni la
serekali hivyo wanaenda hapo hapo kufanyia biashara maana wao wenyewe ni
serekali tosha.



Gazeti hili la nipashe lilifika eneo la tukio na kushughudia
wananchi hao wakiwa wanajigawia sehemu za biadhara huku wengine wakiwa wameanza
kuchimba kwa ajili ya kujenga vibanda vyao.

Wakiongelea tukio hilo baadhi ya wafanyabiashara hao
walisema wameamua kuchukuwa hatua hiyo kutokana na kukosa sehemu za
kwenda kufanyia biashara zao kwani eneo walilopewa
la uwanja wa NMC ni lidogo haliwatoshi wafanyabiashara wote.



Mmoja wa wafanyara
hao aliyejitambulisha kwa jina la Emanuel mushi alisema kuwa wao wamechukuwa
hatua hiyo kutokana na kitendo cha kukosa eneo la kufanyia biashara katika
kiwanja cha nmc huku mkandasi ambaye
amepewa tenda hiyo ya kuwagawia maeneo akiwa awazungusha.

Aidha alisema kuwa wameamua kufanya au kuchukuwa hatua hii
ili serekali ijue machinga arusha hawana mahala pa kwenda na wawaangalizie sasa
sehemu ya kuwaweka ili wafanyie biashara zao



Alisema kuwa wamesubiri kwa muda mrefu na tangu waambiwe
wanagawiwa eneo hilo hawajapatiwa na wamekuwa wakizungushwa tu bila ya
mafanikio yoyote hali ambayo inawafanya wao kuishi kama ndege.



,,leo asubuhi sisi tuliokuwa tumeweka vitu vyetu hapa nje ya
soko la ngarenaro tumefatwa tukafukuzwa kamamaubwa kibaya zaidi watufukuze
wakiwa wametupa sehemu ya kwenda lakini hawajatupa sehemu ya kwenda
wanatupeleka peleka na tulivyoona hivyo na ili eneo tunaliona wazi kila siku
tukaamua kuvamia ili tukae hapa,,alisema Mama rosemary mollel

Waliongeza kuwa sababu ingine ya kutoka katika uwanja huo ni
pamoja ya kuwa uwanja huo hauna miundo mbinu ya kutosha ikiemo choo kitu
ambacho ni tatizo kubwa sana kwa afya zao.

,,unajua eneo lile ni dogo kiukweli ni robo ya wamachinga tu
ndo wameingia katika eneo lile kibaya zaidi askari wanaotufata kutufukuza
tukiwauliza tuende wapi wanasema mtajua wenyewe kila tukaapo wanatufukuza
kibaya zaidi wanatuambia kuwa swali kama hilo msiniulize maana wakati mnakuja
kutoka vijijijini kwenu hamkututaarifu kwakua mlikuja kimnya kimnya basi
ondokeni ivyo ivyo kama ulivyokuja ,,alisema Lukas Seneu.



Machinga hao waliongeza kuwa serekali hii imekuwa ikifanya
kazi kwa kuwakomoa kwani wanadhani kuwa machinga wengi ni chadema hivyo
wanavyofanya hivi wanawakomoa kitu ambacho sio cha kweli na walibainisha kuwa
viongozi hao wa serekali wanawatesa hivi ili warudi kijijini lakini walisema
watapigana mpaka mwisho wake waone

Juhudi za kumpat a kaimu mkurugenzi wa jiji kuzungumzia swala hili
ziligonga mwamba kwani
ofisini hakuwepo na simu zake zote zilikuwa hazipo hewa.

No comments:

Post a Comment