Tuesday, May 22, 2012

STORY YA POLISI –WANANCHI WAUWA MAJAMBAZI WATATU




WANANCHI wenye hasira katika eneo la Ngusero Ndani ya manispaa ya Arusha wamewaua majambazi matatu kwa silaha za jadi mara baada ya majambazi hayo kubainika kuwa wanapanga mbinu mbalimbali za kuvunja nyumba

Akiongea na waandishi wa habari mapema leo kamanda wa polisi wa mkoa wa Arusha Bw Thobias Andengenye alisema kuwa tukio hilo lilitokea alfajiri ya saa kumi za asubui ambapo majambazi hayo yalifika katika eneo hilo huku yakiwa ndani ya gari

Kamanda Andengenye alisema kuwa mara baaada ya majambazi hayo kufika katika eneo hilo la tukio wakiwa na gari aina ya Corola lenye namba T830 AHU walianza kuzunguka zunguka katika eneo hilo ili kupanga nyumba ambayo wanaingia hali ambayo iliwashitua wananchi

Alifafanua kuwa mara baada ya wananchi kutilia shaka gari hilo ambalo lilikuwa na majambazi hao waliamua kuwaweka chini ya ulinzi na kukagua gari hilo ambapo walikutana na Silaha za jadi  pamoja na silaha nyingine ambazo ni za kuvunjia  nyumba hali ambayo ilisababisha waweze kupigwa sana na wananchi hao

“inavyosemekana ni kwamba hawa majambazi walikuwa wameshazunguka san a na gari lao kwa muda mrefu sana na sasa mara baada ya kuhisiwa wananachi waliamua kujichukulia sheria mkononi na kisha kuanza kuwapiga sana hali ambayo ilisababisha Mauti yao hapo hapo”alisema kamanda Andengenye.

Aliongeza kuwa mara baada ya Jeshi la Polisi kufika katika eneo hilo waliweza kugundua kuwa kati ya majambazi hayo matatu mawili yalikuwa yanatafutwa na jeshi hilo bila mafanikio kwa kuwa walikuwa wanatuhumiwa kwa makosa ya unyanganyi wa kutumia silaha ndani ya maeneo mbalimbali ya Mji wa Arusha

Pia alisema kuwa majambazi hayo yalifajhamika  kwa majina ya Philipho Naftari,huku jambazi mmoja amejulikana kwa jina la Utani ambalo ni shidaa na mwingine hajajulikana jina lake huku jitiada za kuwatafuta ndugu zake zikiwa zinaendelea.

Hataivyo kamanda huyo alisema kuwa pamoja na kuwa waliowawa walikuwa ni majambazi lakiniPolisi inatafuta chanzo halisi cha aliyeanzisha kipigo na kusababisha wengine kuwauwa majambazi hayo kwa kuwa wengeweza kusaidiasana  polisi katika upelelezi wao lakini kwa kuwa wameshawauwa hakuna upelelezi  tena
                                                       
Wakati huo huo Jeshi la Polisi mkoani Arusha linamshikilia mkazi mmoja wa longido kwa kosa la kumsukuma Rafiki yake na kisha  kudondoka na kupoteza maisha papo hapo katika baa moja iliyojulikana kwa jina laZebra.

Kamanda Andengenye alisema kuwa tukio hilo lilitokea  May 20 majira ya saa kumi za jioni ambapo mtu mmoja liyefhamika kwa jina la Abuu Msema alifariki dunia mara baada ya kusukumwa na rafiki yake ambaye aliyejulikana kwa majina ya Frank Mmasi  mkazi wa Longido mjini hapa

Alisema kuwa katika siku hiyo ya tukio  Marehemu akiwa na rafiki yake wakiwa ndani jya baa ya Zebra walikunywa pombe sana linaendelea na upelelezi zaidi kuhusiana na tukio hilo huku mtuhumiwa naye akiendelea kuhojiwa juu ya mauaji hayo na atafikishwa mahakamani upeleezi utakapokamilika.

lakini marehemu alikataa kuondoka huku rafiki yake akimtraka aondoke hali ambayo ilimfanya amnyanyue kwa nguvu huku akiwa amelewa na badaye alidondoka chini na kufariki dunia papo hapo

ADUMU NA UJAUZITO KWA MIAKA MINNE, AZAA MARA KUMI NA SABA



KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida Bi Chausiku Sulemani mkazi wa Maji ya chai wilayani Meru mkoani hapa amewaomba wataalamu mbalimbali wa afya pamoja na wachungji mbalimbali  kuweza kumsaidia kuchunguza kizazi chake kwa kuwa mpaka sasa ana uzao wa 17 huku mimba ya 17 ikiwa imedumu tumboni kwa miaka minne

Akiongea na UPAKO WA HABARI YA UFALME WA MUNGU wiki hii  bi Chausiku alieleza kuwa amekaa na Mimba hiyo kwa kipindi cha miaka minne sasa bila kujifungua huku kiumbe kikiwa kinaendelea kukua ndani ya Tumbo lake hali ambayo inamuweka katika njia panda na kusababisha kuomba msaada wa wachungaji  na watumishi wa Mungu kwa kuwa hali hiyo inamtesa  sana

Alifafanua kuwa hali hiyo ya kuwa na uzao wa 17 imewafanya watoto ambao wapo hai 13 kukosa maitaji yao ya Muhimu kama watoto hali ambayo wasamaria wema wanatakiwa kuiangalia kwa undani sana

Alieleza kuwa pamoja na kuweza kwenda kwa watalaamu mbalimbali wa afya katika hospitali za Arusha na Kilimanjaro lakini bado hali yake inaendeleea kuwa hiyohiyo ya kupata ujauzito wakati ni mzazi

Aliongeza kuwa kwa sasa kinachoitajika ili aweze kuoko maisha ya kiumbe ambacho kimo ndani ya Tumbo lake ni kupatiwa fedha za upasuaji (Oparesheni) hasa pale wakati utakapofika sanjari na kuweza kuwasaidia watoto wake katika mchakato wa Elimu

“Wakristo wenzangu naombeni mnisaidie jamani nina uzao wa kumi na saba sasa huku nikiwa bado nina mimba kubwa hivi sasa naishije watumishi wa Mungu kwa lolote lile nipo tayari kwa kuwa watoto nao wanaishi maisha ya shida sana baba yao hawezi kuwalea kwa kuwa ni wengi na watoto hawa pia wanalazimika hata kulala chini kwa ajili ya ukosefu wa vitanda”aliongeza Bi Chausiku

Naye diwani wa kata hiyo ya Maji ya Chai,bw Lotti Nnko alisema kuwa mama huyo ambaye kila mwaka anahistoria ya kuzaa bila kukutana na Mwanaume anaitaji msaaada wa hali ya juu kwa kuwa familia ambayo anailea nayo inamlemea kutokana na uhaba wa Kipato.

Bw Nnko alifafanua kuwa hali hiyo inachangia kwa kiwango cha hali ya juu sana watoto wake kukosa maitaji kama lishe hali ambayo nayo inachangia kwa kiwango kikubwa sana kushindwa kuendelea mbele na maisha ya kila siku hasa katika mchakato wa Elimu

Aliwataka Wasamaria wema kuhakikisha kuwa hawaachi watoto wa mama huyo kuendelea kupata shida ya uhaba wa lishe, maitaji muhimu ya shule, pamoja na sehemu ya kulala kwa kuwa hata nyumba wanayolala haina Milango wala Madirisha.


Diwani huyo aliwataka wakristo na watumishi wa Mungu kutumia Vipaumbele mbalimbali ambavyo vimo hata kwenye biblia kwa kuweza kumsaidia mama huyo hata kwa njia ya mambi pamoja na kuweza kupata kiasi cha Laki Tano ili aweze kufanyiwa upasuaji kwa mara nyingine tena 

KWA YEYOTE ATAKAYEGUSWA NA MAMA HUYO ASIISITE KUMSAIDIA KUPITIA NAMBA 0764650288
MWISHO

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA,ARUSHA

0758907891

Monday, May 21, 2012

VIONGOZI WA MAKAMPUNI YA ULINZI WATAKIWA KUWA NA TAARIFAA ZA MAFUNZO YA KAZI ZAO

VIONGOZI wa makampuni ya ulinzi  mkoani arusha yametakiwa kutoa taarifa za mafunzo yanayoendana na kazi zao kwa jeshi la polisi ili kuwawezesha wafanyakazi  wao  kupatiwa mafunzo ya  kuongeza ujuzi wa kufanya kazi  wawapo katika malindo yao.

Hayo yalisemwa na mkuu wa kitengo cha polisi jamii mkoani hapa bi Mary Lugola  alipokuwa akifungua kongamano la chama  cha wafanyakazi  walinzi(TUPSE) na wadau wa ulinzi binafsi  lililofanyiika mjini hapa.

Bi Mary alisema kuwa kwa sasa jeshi la polisi liko tayari kutoa mafunzo yanayoendana na kazi zao  kwa makampuni mbali mbali hivyo  viongozi wa makampuni hayo yahakikishe kuwa yamezingatia vigezo  ili kuwawezesha wafanyakazi hao kunufaika na mafunzo hayo.

  Aidha aliwataka askari kuwa na nidhamu na kuhakikisha kuwa huduma wanazozitoa kwa wananchi ni nzuri sio za kejeli kwa kuwa wapo baadhi ya askari ambao sio waaminifu wawapo katika kazi zao.

Kwa upande wake katibu wa chama cha wafanyakazi walinzi  kit aifa bw Godiwin Mariki alisema kuwa  katika chama chao kumekuwepo na changamoto lukuki ikiwemo   ya wateja kulazimisha rushwa ya fedha kutoka kwa waajiri walipotoa tenda ya ulinzi  na pale waajiri wanapokuwa hawatoi rushwa hizo basi wateja hao huvunja lindo na kuwapatia waajiri wengine.

Alisema kuwa kupitia jambo hili wanaiomba serikali ikemee vitendo hivyo na kuagiza malindo yatolewe kwa mkataba isiyopungua mika mitatu ili kuwezesha waajiri kuwa na uwezo wa kuwahudumia walinzi wake.

Pia alitaja changamoto ingine kuwa ni pamoja  na wanawake kuachishwa kazi pale wanapopata ujauzito na kutolipwa mishahara wakati wakiwa likizo ya uzazi kwa madai kuwa ni starehe yao na haimhusu mwajiri, hivyo kuitaka serikali kukemea na kuchukua hatua kwa kuwa huo ni uonevu.

Aidha TUPSE imependekeza kuwa sera na sheria ya ulinzi binafsi iharakishwe ili kuondokana na maonezi mengi yanayofanyiwa walinzi ,waajiri,wateja na jamii inayowazunguka .
Mwisho..


chanzo cha habari na Queen Lema,

ARUSHA

Sunday, May 20, 2012

PICHA ZA MATUKIO YA KUTOA SADAKA KWA MBUNGE WA JIMBO LA ARUMERU MASHARIKI

WAKWANZA  KUSHOTO NI MBUNGE KUTOKA MARA, BW KINGI LUGOLA  WAKATI WA PILI NA WATATU NI WABUNGE MACHACHARI SANA WA CHADEMA, WA KATIKATI NI MBUNGE JOSHUA NASSARI NA WA MWISHO NI PETER MSWIGWA WAKIWA MBELE ZA MADHABAU YA KANISA LA FPCT KILINGA MERU

 MAASKOFU NAO HAWAKUWA MBALI KUGAWA BARAKA WALIWAWEKEA MIKONO KAMA ISHARA YA KUKATAA RUSHWA NDANI YA TAIFA LA TANZANIA, PICHA NA QUEEN LEMA WA UPAKO WA HABARI ZA UFALME WA MBINGUNI

Mbunge Nassari arudi mbele za Mungu kwa ajili ya Shukurani

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida jana Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki Bw Joshua Nassari aliwakutanisha wapiga kura wake zaidi ya 4000 huku miongoni mwao wakiwa ni makada wa chama cha Mapinduzi pamoja huku Mgombea mwenza wa chama cha Mapinduzi Bw Sioi Sumari akishindwa kufika kwa kuwa amekosa usafiri wa haraka sana.

Hatua hiyo imekuja mara baada ya mbunge huyo kutoa sadaka mara baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo  ibada ambayo ilifanyika katika kanisa la FPCT Kilinga wilayani Meru Mkoani Arusha

Akiongea na Maelfu ya wananchi wa jimbo hilo katika kanisa hilo Bw Nassari alisema kuwa ameamua kutoa sadaka maalumu ya kushukuru mungu mara baada ya kumaliza vema uchaguzi huku wapiga kura wake wote wakiwa salama tofauti na pale ambapo wengi waliadhimia

Pia alisema kuwa kwa sasa Viongozi wa Vyama vingine ambao nao walishiriki katika uchaguzi hawapswi kukataana na badala yake wantakiwa kuwa wamoja kama walivyoshirriki makada wengine wa chama cha Mapinduzi ndani ya ibada hiyo ya shukurani

“leo nimetoa shukurani yangu ndani ya kanisa hili la Kilinga lakini ninafurai kuwa makada wa CCM tupo nao hapa lakini mbali na hayo mgombea wangu mwenza wakati wa kampeni naye alikuwa anatamani sana kuja ila kwa bahati mbaya alichelewa ndege , ingawaje kwa sasa tuna madiwani wengi sana wa CCM,  Mbunge wa Jimbo la Moibara na wengine wengi nah ii ndio inayotakiwa”alisema Bw Nassari

Awali aliongeza kuwa yeye hana shida yoyote na kiongozi hata kama ni wa chama chake ila ana shida na viongozi ambao wana mikakati na malengo mbalimbali ya kuteketeza  maslahi ya wananchi hasa wa jimbo la Arumeru Mashariki na kamwe kiongozi kama huyo hataweza kumvumilia  kwa kuwa hana msimamo na Taifa

Naye Kada maarufu wa chama cha mapinduzi ambaye ni Mbunge wa  Mwibara mkoani Mara, bw Kingi Lugora alisema kuwa ili kukabiliana na hali zote ndani ya nchi wapo baadhi ya viongozi ambao wanaharibu mpango wa Mungu hasa kwa nyakati za uchaguzi kwa kuwa wanatumia mabavu ya Rushwa na mara wanapopata uongozi bado wanaendeleza hali ya Rushwa  huku wananchi wa chini nao wakiwa wanazidi kuumia na hali ngumu ya maisha

“wapo wanasiasa ambao wanawapiga wananchi upofu wa Rushwa na ndio maaana uchumi wa leo umeyumba huku waumini wa leo wakiwa wanasuasua na kwa hili naomba makanisa ya sasa yaingie kwenye  maombi dhidi ya hawa watu ambao wanaomba rushwa hasa katika bunge, na pia napenda kuwatia Moyo hata wabunge ambao  wanajidhatiti na kisha kusema hadharani masuala ya Rushwa wasiogope hata kama ni makada kama mimi nilivyo  kwa kuwa wapo baadhi ya viongozi  ambao wanatamani kusema Rushwa lakini wanapata Kigugumizi kwa kuhofia maslahi ya vyama vyao”aliongeza Bw Lugora.

Pia alisema kuwa yeye kama yeye kamwwe hatasita kusema ukweli kwa kada yoyote  wa CCM  ambaye anachangia sana  uchumi wa Nchi kuyumba na badala yake atamuomba Mungu zaidi  ili aweze  kuwasema na kuwaweka hadharani kwa kuwa mpaka sasa Mungu anajibu Maombi juu ya mafisadi  ambao ndio chanzo kikubwa sana  cha umaskini ndani ya Nchi ya Tanzania


Katika hatua nyingine  Askofu Langaeli  Kahaya  naye alisema kuwa wananchi wanapswa kuhakikisha kuwa kamwe hawamchagui kiongozi yoyote kwa ajili ya maslahi ya Rushwa kwa kuwa wote wanaotoa rushwa  ndio wanaosababisha hata umaskini na umwagaji damu ndani ya  nchi

Kutokana na hali hiyo alisema kuwa ni mwiko kwa wananchi wma Jimbo la Arumeru  Mashariki kujihusisha na Rushwa kwa vipindi vyote vya uchaguzi kwa kuwa mpaka sasa Rushwa imeshaacha madhara makubwa sana ndani ya jimbo hilo na pia Rushwa ni dhambi kubwa sana.

“ukiangalia sana mtu anayetoa rushwa ni mtu mwenye elimu yake sasa kwa hili wananchi wanapswa kujua kuwa anayetoa na anayepokea rushwa anafanya dhambi na hiyo dhambi ndiyo inayotapakaa kwa jamii na vizazi vingine ambavyo navyo vinaibuka na  dhambi hiyohiyo”alisema Bw Kaaya

Mbali na hayo alisema kuwa pia taifa la Tanzania linatakiwa kuhakikisha kuwa kila mara linakuwa na maombi makubwa sana hasa ya baadhi ya watu ambao wanatekeleza  ahadi za Rushwa na Ufisadi hali ambayo nayo inachangia ka kiwango kikubwa sana umaskini wa watanzania wa Leo

Mwisho


chanzo cha habari na Queen Lema, arusha

Monday, May 14, 2012

MADUKA 10 YAMEUNGUA KATIKA MJI WA NGARAMTONI



Maduka 10 yenye thamani ya zaidi ya million 100 yameteketea kwa moto katika mji mdogo wa Ngaramtoni wilayaya Arusha vijijini ambapo chanzo halisi ni hitilafu ya Umeme

Akiongea na Majira katika eneo la Ngaramtoni  mmiliki wa maduka hayo Bw  Benjamini Mbayi alisema kuwa moto huo ulianza majaiara ya saa saba za mchana ambapo ulianza katika duka moja

Alisema kuwa wakati moto huo unaanza alilazimika kuingia kwenye chumba hicho na kuzima umeme katika kiunganisha cha umeme (SOCKET) lakini bado haikusaidia kabisa na moto huo uliendelea kutapakaa katikia vyumba bvingine vya biashara

“baada ya kuona moshi ukiwa unatapakaa kwenye paa ambapo  kwa kweli nilishindwa kuokoa kitu chochote ila nilifanya jitiada za kuhakikisha kuwa tunaomba msaada hasa kwa kikosi cha zima moto jambo ambalo lilifanikiwa ndani ya dakika 30”alisema Bw Mbayi

Pia aliongeza kuwa mara baada ya hapo kikosi hicho kilifanikiwa kuzima moto lakini vitu venye thamani ya Milioni 100 vilikuwa vimeshateketea kwa Moto lakini kutokana na zoezi hilo la uokoaji  hapakuwa na madhara yoyote yale ya kuunguwa kwa binadamu


Diwani wa kata ya Olmotony Bw David Kinisi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alisema kuwa kutokea kwa matukio hayo ya mara kwa mara ya moto katika mji mdogo wa Ngaramtoni kunatokana na ubovu wa mundombinu hasa ya maeneo ya biashara hali ambayo kila mara inasababisha matatizo makubwa sana

Bw Kinisi alifafanua kuwa tukio la Moto katika mji huo wa Ngaramtoni ni la Pili ambapo mwezi uliopita  maduka tisa nayo yaliteketea kwa moto huku maduka hayo yakiwa na gharama ya milioni 200 huku moja ya maduka yakiwa ni mali yake


”kama mnavyoona hapa ubovu wa miundo mbinu unachangia kwa kiwango kikubwa sana na kama halmashauri haoitaweza kuliangalia suala hili kwa undani zaidi basi itakuwa ni hatari sana kwani kuuungua kwa maduka haya  ni dalili kubwa snaa ya umaskini hasa Ngaramtoni”alisema Bw Kinisi

Alifafanua kuwa hali hiyo inatakiwa kuboreshwa sana hasa katika eneo la Umeme kwa kuwa ndio  chanzo kikubwa Sana cha kutokea kwa majanga ya moto kwa kuwa hata maeneo yaliongua ndio chanzo kikubwa sana  cha hasara  na umaskini katika mji mdogo wa Ngaramtoni.

Awali aliwataka wananchi hasa wafanyabiashara kuhakikisha kuwa wanafanya biashara kwa kuzingatia utaalamu wa mafundi wa umeme na wala sio kwa kuwatumia mafundi wa uchochoroni ambao ndio chanzo kikubwa  cha majanga ya Moto

Naye kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Bw Thobias Andengenye alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alisema kuwa bado wanaendelea na  uchunguzi wa tukio hilo na kujua thamani halisi ya maduka yaliyoangua katika janga hilo
MWISHO


CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA

0758907891

ARUSHA

MNAOTAKA ARDHI HAKIKISHENI KUWA INAKUWA NI KWA AJILI YA WAJANE NA YATIMA MERU

MBUNGE wa jimbo la arumeru mashariki Joshua Nasari amewataka wananchi wa jimbo hilo kuwa na maono mbali mbali juu ya  matumizi bora  ya ardhi iliyopo wanayoitaka kutoka kwa wawekezaji  kwa kuhakikisha kuwa ardhi hiyo inajengwa vyuo vya ufundi na mambo mengineyo ambayo yatawasaidia wao  na vizazi vyao vijavyo

Nasari aliyasema hayo alipokuwa akiongea na wakazi wa jimbo hilo  katika hafla ya kumuaga muhasisis wa kanisa la African Mission Evangelism Askofu Nickson Issangya iliyofanyika katika kituo cha kulea watoto yatima cha African Orphanag e kilichopo Sakila wilayani arumeru

Alisema kuwa pamoja na kuwa wana arumeru wanahitaji ardhi yao  kutoka kwa wawekezaji ,lakini  wanapaswa  wawe   na maono juu ya matumizi yake kwa kuwa wako ambao wakipewa ardhi hiyo  wanakimbilia kuuza ili wapate  fedha.

“Arumeru tuna matatizo mengi hatuna vyuo vya ufundi ,mji mdogo  ,wa usa river hauna hata viwanja vya kuzikia ndugu waliofariiki,hakuna hata viwanja vya michezo ila endapo mtakuwa na maono mazuri juu ya ardhi hiyo ni wazi kuwa  mtaifanyia mambo makubwa sana ya maendeleo”alisema Nasari

Aidha akielezea mikakati aliyonayo  alisema kuwa ni pamoja na kuhakikisha anawasaidia watoto yatima na wajane kwa kuwa makundi haya mawili yametekelezwa bila kukumbukwa  hivyo kuwafanya waonekane wametengwa na jamii.

Hata hivyo alitumia fursa hiyo kuwasihi vijana kuachana na makundi ya kupotoshana na badala yake  wahakikishe wana kuwa na nidhamu ,maono . na uwajibikaji mzuri wa kazi kwa kuwa endapo watazingatia mambo hayo yatawafanya kufanikiwa katika maisha yao.

Nae mhasisisi huyo Nickson Issanya aliwataka wananchi wa jimbo hilo kuweka itikadi za kisiasa pembeni na badala yake wawe na umoja kwa kuhakikisha kuwa wanampa mbunge wao ushirikiano ili aweze kutimiza malengo aliyojiwekea.

Issangya alisema kuwa endapo wataendeleza itikadi za kisiasa katika jimbo hilo ni wazi kuwa makundi hayatavunjika jambo ambalo litasababisha kurudisha nyuma maendeleo ya jimbo hilo.
mwisho



CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA


0758907891

Saturday, May 12, 2012

Meru yajipanga kuhakikisha kuwa inafanyamabadiliko ya hali ya juu sana hasa katika kuibua vipaji






mkurugenzi wa Meru Trisias Kagenzi akifanya mahojiano na mwandishi  wa  Upako wa ufalme wa Mungu hayupo pichani kuhusiana na mikakati mbalimbali ya halmashauri hiyo hivi karibuni

WAPO WATU AMBAO HAWATAONA UFALME WA MUNGU KISA SIMU


Wakristo wametakiwa kuwa makini sana na matumizi ya simu za mikononi kwa kuwa asilimia kubwa ya wakristo wanadanganya watu bila kujua na kutambua kuwa wana muasi mungu wao

Asilimia kubwa ya watu wanadanganya na kisha wanakuja makanisani wakijua kuwa wapo sawa lakini hakuna dhambi ndogo hata kidogo

Hayo yameelezwa na mchungaji Joseph moto wa kanisa la antiokia reviaval church liliopo sombetini jijini hapa wakati akiongea na waumini wa kanisa hilo hivi karibuni

Mchungaji Moto alisema kuwa kila mahala wakristo wanajiwekea utaratibu wa kuongea uongo wakati wa kiwa wanaongea na simu na badala yake wanashindwa kujua kuwa kwa mungu hakuna dhambi ambayo ni ndogo

Alieleza watu hao wanaongea uongo kwa njia ya simu mara nyingi sana huwa wanadhamiria huku wakiwa makanisani mwao wanaonesha kuwa wanapinga dhambi ya uongo

‘napenda kuwasihi wakristo kuhakikisha kuwa duniani hakuna dhambi ndogo na badala yake wajue kuwe mungu hapendi na wakicheza wapo baadhi ambao hawataweza kuona ufalme wa mungu ktokana na simu”alisema mchungaji huyo

Katika hatua nyingine aliwatahadharisha wakristo kuhakikisha kuwa wanajua matumizi ya simu kwa kuhakikisha kuwa wanakuwa na ukweli hasa kwa wenza wao

Aliongeza kuwa hakuna jambo jema kwenye simu kama kuongea kwa mwenza wako au ndugu yako wa karibu ukweli kwa kuwa hali hiyo itachangia kwa kiwango kikubwa sana hata kujenga jamii

‘leo  unakuta watoto wetu wan waangalia masuala mbalimbali na wananakili sana wazazi wao wanchokifanya sasa kwa hali hii kama wazazi wataangalia zaidi kuongea uongo wanawafundisha nini watoto wao"aliongeza mchungaji huyo
 MWISHO

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA

ARUSHA 

0758907891

WENYE HOFU YA MAISHA NA WASIOJIAMINI WATAKIWA KUWA CHINI YA UTAWALA WA MUNGU NA WALA SIO WA SHETANI WAONYWA


,ARUSHA

ASILIMIA kubwa ya watu ambao wanakuwa na hofu ya Maisha na kushindwa kujiamini ni wale watu ambao wapo chini ya utawala wa Shetani huku kwa wale ambao wapo chini ya utawala  wa Mungu wanakuwa majasiri hata wanapopita kwenye mapito ya nguvu za giza.


Hayo yamesemwa Wilayani Meru katika kanisa la E.A.G.T Nkure na Mchungaji Raphael Nanyaro wakati akiongea na Waumini wa kanisa hilo mapema wiki hii

Mchungaji huyo alisema kwa mtu ambaye yupo chni ya utawala wa nguvu za giza mara zote anakuwa na hali ya uoga mkubwa sana wakati kwa ailiye chini ya utawala wa Mungu muda wote anakuwa na imani hata kama anapita katika mapito makubwa sana

Alifafanua kuwa utawala wa nguvu za giza una madhara makubwa sana na kwa mtu yoyote ambaye anaongozwa na utawala huoi anapaswa kujua kuwa mwisho wake uo karibu sana wakati kwa anayekuwa chini ya utawala wa Mungu kila kinachomtokea ni kwa ajili ya mapenzi ya Mungu


Aliongeza kuwa ili utawala huo wa Shetani uweze kukaa vema ni pale unapokuta mkristo anakimbia Neno la Mungu katika Mahubiri yake, Nyimbo za Sifa na hata Nyimbo za Kuabudu kwa kuwa hata naye Shetani analijua vema Neno la Mungu

“ukishakuwa wa kukimbia Neno la mungu basi wewe  ni wa utawala wa shetani na mtu yeyote ambaye  anataka mungu afanye mabadiliko hata ya kiutawala ni lazima matendo na imani na Neno viweze kuambatana kwa pamoja”alisema Mch Raphael


Pia alibainisha kuwa mtu anapokuwa chiuni ya utawala wa milele ambao ni utawala wa mungu basi mtu huyo anaweza kumpinga shetani na kazi zake kwa uraisi sana kwa kuwa silaha zote zimeanishwa vema katika maaandiko matakatifu

Hataivyo alitaja nyenzo mbalimbali za kutumia hasa pale ambapo mtu anapotaka kupigana na utawala wa nguvu za giza ambapo nyenzo hizo ni pamoja na Maombi ya dhamira ya Nafsi, kulijua vema neon la bwana,na pia sifa na kuabudu ambapo ndipo mungu anapotaka

Mchungaji Raphael alisema kuwa hata hizi ni Nyakati za Mwisho kwa hali hiyo ni vema kwa kila mtu kuhakikisha kuwa anatumia vema Nyenzo hizo kila baada ya Dakika ili kuwa na uhakika wa Unyakuo hasa pale ambapo muda utakapofika.


MWISHO


WENYE HOFU YA MAISHA NA WASIOJIAMINI WATAKIWA KUWA CHINI YA UTAWALA WA MUNGU NA WALA SIO WA SHETANI
WAONYWA.

NA BETY ALEX,ARUSHA

ASILIMIA kubwa ya watu ambao wanakuwa na hofu ya Maisha na kushindwa kujiamini ni wale watu ambao wapo chini ya utawala wa Shetani huku kwa wale ambao wapo chini ya utawala  wa Mungu wanakuwa majasiri hata wanapopita kwenye mapito ya nguvu za giza.


Hayo yamesemwa Wilayani Meru katika kanisa la E.A.G.T Nkure na Mchungaji Raphael Nanyaro wakati akiongea na Waumini wa kanisa hilo mapema wiki hii

Mchungaji huyo alisema kwa mtu ambaye yupo chni ya utawala wa nguvu za giza mara zote anakuwa na hali ya uoga mkubwa sana wakati kwa ailiye chini ya utawala wa Mungu muda wote anakuwa na imani hata kama anapita katika mapito makubwa sana

Alifafanua kuwa utawala wa nguvu za giza una madhara makubwa sana na kwa mtu yoyote ambaye anaongozwa na utawala huoi anapaswa kujua kuwa mwisho wake uo karibu sana wakati kwa anayekuwa chini ya utawala wa Mungu kila kinachomtokea ni kwa ajili ya mapenzi ya Mungu


Aliongeza kuwa ili utawala huo wa Shetani uweze kukaa vema ni pale unapokuta mkristo anakimbia Neno la Mungu katika Mahubiri yake, Nyimbo za Sifa na hata Nyimbo za Kuabudu kwa kuwa hata naye Shetani analijua vema Neno la Mungu

“ukishakuwa wa kukimbia Neno la mungu basi wewe  ni wa utawala wa shetani na mtu yeyote ambaye  anataka mungu afanye mabadiliko hata ya kiutawala ni lazima matendo na imani na Neno viweze kuambatana kwa pamoja”alisema Mch Raphael


Pia alibainisha kuwa mtu anapokuwa chiuni ya utawala wa milele ambao ni utawala wa mungu basi mtu huyo anaweza kumpinga shetani na kazi zake kwa uraisi sana kwa kuwa silaha zote zimeanishwa vema katika maaandiko matakatifu

Hataivyo alitaja nyenzo mbalimbali za kutumia hasa pale ambapo mtu anapotaka kupigana na utawala wa nguvu za giza ambapo nyenzo hizo ni pamoja na Maombi ya dhamira ya Nafsi, kulijua vema neon la bwana,na pia sifa na kuabudu ambapo ndipo mungu anapotaka

Mchungaji Raphael alisema kuwa hata hizi ni Nyakati za Mwisho kwa hali hiyo ni vema kwa kila mtu kuhakikisha kuwa anatumia vema Nyenzo hizo kila baada ya Dakika ili kuwa na uhakika wa Unyakuo hasa pale ambapo muda utakapofika.


MWISHO
CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA

0758907891

ARUSHA

MAOMBI YASABABISHA KAKA MTU KUVUNJA PAA LA NYUMBA

MAOMBI YASABABISHA KAKA MTU KUVUNJA PAA LA NYUMBA

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mke mmoja wa  muinjilisti wa makanisa ya Anglican Bi Elizabeth  Bakari amejikuta katika wakati mgumu sana mara baada ya kufanya maombi ya kuvunja malango ya kuzimu ambapo baada ya muda mfupi  kaka wa dada huyo alipoamua kuvunja  paa la nyumba yake kwa madai kuwa hamtambui

Akiongea na Nyakati mapema  wiki hii Bi Elizabeth alisema kuwa kilichofanya kaka yake ambaye anatambulika kwa majina ya Shabani Bakari ni malango ambayo yeye alikuwa akiyapinga wakati wa kuomba kwake

Alisema kuwa jumamosi iliyopita majira ya usiku alijikuta akiwa anapambana na maroho mbalimbali ambapo hali hiyo ilifanya kaka yake mzazi kutafuta ulimwengu mwingine na kisha kumshambulia ambapo pia hata zoezi hilo la kumnshambulia katika ulimwengu wa roho nao ulikwama

Alifafanua kuwa baada ya mapambano hayo ya muda mrefu sana  hayakuishia hapo na badala yake siku inayofuta ambayo ni jumapili iliyopita majira ya saa nne za asubui kaka huyo alivamia nyumba ya dada yake ambayo wanaishi na kisha kutoa mapaa kwa kisingizo kuwa hamtambui

“mimi nilishangaa sana kwa hali ya juu na kuona kuwa  ni jambo la ajabu sana kwa kuwa kaka yangu tena wa kuzaliwa nae anafanya vitu kama hivi lakini ninachojua ni kuwa  maombi ya vita niliyoyaomba ndio chanzo nah ii ni changamoto hata kwa wengine ambao wanafanya maombi ya kila siku hasa kwa maadui zao”alisema Bi Elizabeth

Alisema kuwa mara baada ya kutokea kwa tukio hilo ambalo liliwavutia watu wengi sana ambapo baada ya muda alilazimika kwenda kwenye ofisi ya kijiji ili kupata haki yake ya msingi kwa kuwa kila mara baada ya maombi kaka huyo anamfanyia vituko vikali sana

Alifafanua kuwa mara baada ya kufika katika ofisi ya kijiji walimtaka afike kwenye kituo cha Polisi Kaloleni ili hatua za juu ziweze kuchukuliwa hali ambayo ilimfanya amtafute kaka yake chini ya uangalizi mkubwa sana wa jeshi la polisi

‘nililazimika kumtafuta chini ya jeshi la polisi kwa RB No KAL/RB/792/2012  ambapo alifanikiwa kukamatwa majira ya Jioni na kisha kuwekwa katika kituo kidogo cha Polisi ambapo  Jumatatu alifikishwa mahakamani na kujibu mashitaka ambayo yalikuwa yanamkabili

Alifafanua kuwa kutokana na hali hiyo kilichomfanya ampeleke katika mahakama ya mwanzo ya Maromboso ili aweze kujifunza kwa undani wake kwa kuwa Neno msamaha limetakiwa kuwasemehe sasa kwa hali hiyo amemsamehe ili anachokitaka ni aweze kujifunza na anachokitaka ni maombi zaidi kwa kuwa inavyoonekana kaka yake ana matatizo makubwa hasa ya ulimwengu wa  roho

MWISHO 

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA 

ARUSHA

0758907891

KANISA LATAKIWA KUWAKUMBATIA ZAIDI VIJANA KATIKA MCHAKATO WA UJASIAMALI

MAKANISA mbalimbali hasa ya kanda ya kaskazini yametakiwa kuhakikisha kuwa yanasoma alama za nyakati kwa kuhakikisha yanasaidia sana vijana hasa katika mchakato wa ajira ambao unaanzia kwenye suala zima la Ujasiamali

Kwa sasa kama makanisa mengi yatahakikisha kuwa yanajiwekeza zaidi hata kwa kuhubiri na kuwapa moyo vijana walio wengi kuhusu umuhimu wa kuwa wajasiamali hata kama wameajiriwa basi watajiokoa kutoka matatizo mbalimbali zikiwemo anasa za dunia

Kauli hiyo imetolewa mjini Arusha na Mwenyekiti wa kanisa la Morovian jimbo la Kaskazini Tanzania,Mchungaji Peter Malema wakati alipokuwa akizundua kikundi cha wajasimali cha jijini hapa kijulikanacho kama SEMENS GROUP  wiki iliyopita

Mchungaji Malema alisema kuwa endapo  kama kanisa litasoma alama za nyakati na kuweza kujua hilo basi kwa kiwango kikubwa sana litakuwa limeweza kuwaokoa maelfu ya vijana ambao wengine wanateketea kwa kuwa hawana elimu hata ya ujasiamali

Aliongeza kuwa kwa muda huu ni vema kanisa likahakikisha kuwa linawaboreshea vijana bila kujali changamoto yopyote mafundisho hata ya ujasiamali ambayo yatalenga kuwaokoa na hivyo kama wataondokana na umaskini basi jamii nayo itakuwa imetua mzigo mkubwa

“kwa sasa ni vema kwa kila kijana wa kikristo kuhakikisha kuwa anakuwa mjasiamali kwa kuhakikisha kuwa anatafuta sana kwa kuwa hata maaandiko nayo yamewataka watafute na kama watafanya hivyo umaskini ndani ya nchi yetu utapungua kwa kiwango kikubwa sana”alisema mchungaji Malema

Awali mkurugenzi wa kampunin hiyo ya Semens Group  Bw Elias Semens alisema kuwa amejipanga kuhakikisha kuwa anawakomboa wakrisro hasa vijana na wanawake kwa kuwa wao ndio wenye mzigo mkubwa sana katika jamii

Alifafanua kuwa  kwa upande wa wanawake wanapopata elimu ya ujasiamali na kuwezeshwa kufanya kazi mbalimbali faida hiyo huenda kwenye jamii zao hali ambayo ni moja ya malengo ya makanisa mengi hasa kanisa la Morivian hapa nchini

Aliwataka viongozi wa makanisa mbalimbali kuhakikisha kuwa wanatumia kikiundi hicho ambacho kinahusika na usafi wa maofisini,na pia upishi kwenye halaiki kubwa ya watu ambapo hali hiyo nayo itaweza kuongeza hata chachu ya maendeleo ya kanisa na wajasiamali mbalimbali hapa nchini

MWISHO

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA

0758907891

ARUSHA

TANZANITE ONE YAIKUMBUKA WILAYA YA SIMANJIRO


TANZANITE Foundation ambayo ni kampuni tanzu ya TanzaniteOne ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara imechangia maendeleo ya jamii kwenye kijiji cha Naisinyai kwa kujenga shule mbili,zahanati,visima vya maji na kituo cha jamii.
 
Akizungumza wakati akigawa vifaa vya shule na michezo kwa wanafunzi wa shule ya msingi New Vision ya mji mdogo wa Mirerani,Mkurugenzi wa Tanzanite Foundation Hayley Henning alisema lengo lao ni kusaidia jamii na siyo kupata faida.
 
Henning aliongoza na wageni kutoka nchini Marekani wakiwemo waandishi wa habari Robert Weldan Weldo wa Gia na Steve Bennett wa Gems Tv alisema wapo kwa ajili ya kuimarisha na kudumisha imani na uadilifu wa Tanzanite.
 
Alisema walijenga baadhi ya madarasa ya shule ya msingi na sekondari Naisinyai,kliniki na visima vya maji kwa ajili ya kuboresha afya ya watoto wa eneo hilo walioathirika baada ya kutumia maji yenye floride nyingi.
 
“Tuliamua kuchimba visima hivyo baada ya watoto wengi wa Naisinyai meno yao kuwa na rangi ya hudhurungi hivyo hivi sasa maji hayo hayana tatizo hilo na wanatumia jamii pamoja na mifugo yao,” alisema Henning.

Naye,Mkurugenzi Mtendaji wa American Gem Trade Association (AGTA) Doug Hucker alisema wamefurahia fursa ya kutembelea kampuni ya TanzaniteOne na kufahamu shughuli mbalimbali za madini ya Tanzanite zinazofanyika.
 
“Safari yetu baada ya maonyesho ya Arusha Internation Gem imetusaidia kuona hazina kubwa ya migodi ya Tanzanite na namna mnavyoijali jamii inayowazunguka kwa kuboresha hali ya maisha ya watoto wa Tanzania,” alisema Hucker.
 
Wageni hao walitembelea eneo hilo baada ya kutoka kwenye maonyesho ya kimataifa ya madini ya Arusha International Gem Fair yaliyofanyika wiki iliyopita na kuhusisha wafanyabiashara mbalimbali wa kimataifa.




0758907891