Monday, December 16, 2013

VIJANA WA MERU WATAKAOKIUKA MAADILI NA KUIGA TAMADUNI ZA NJE YA NCHI KUCHAPWA VIBOKO 60 HADHARANI

VIJANA WA MERU WATAKAOKIUKA MAADILI NA KUIGA TAMADUNI ZA NJE YA NCHI KUCHAPWA VIBOKO 60 HADHARANI
 
Na Queen Lema, Meru
 
UONGOZI wa Kimila ujulikanao kama Rika la Kilovio kutoka katika kabila la Kimeru
 umepitisha sheria kali ya kudhibiti maadili kwa vijana wa kike na wa kiume hasa wale ambao wanaiga tamaduni  za mataifa ya nje ya nchi ambapo kwa kijana atakayebainika kuiga au kukiuka maadili ya Kitanzania basi atalazimika kuchapwa viboko 60 hadharani
 
Hatua hiyo inakuja mara baada ya baadhi ya vijana katika eneo hilo la Meru kuanza tabia ya kuiga tamaduni lakini hata madili ya mataifa ya nje hali ambayo inachangia kwa kiwango kikubwa maadili kuendelea kuporomoka.
 
Hayo yameelezwa na Bw Akundaely Mbisse ambaye ni kiongozi wa marika ya vijana katika kabila hilo wajulikao kama “Kilovio”wakati wakimsimika na kumuingiza rasmi kiongozi wa vijana katika eneo hilo la Mareu Bw Herieli Mafie mapema jana.
 
Mbisse alisema kuwa utaratibu huo wa kuwapa vijana adhabu ya viboko 60 utaweza kurudisha maana halisi ya kijana wa kabila hilo ambapo kwa sasa jamii ya Mkoa wa Arusha bado inaonekana kuendelea kulelemewa na tatizo la vijana wengi kuiga tamaduni za nje ya nchi huku hali hiyo nayo ikichangia sana hata ubaribifu wa amani ya Kaya,hadi mkoa.
 
Alifafanua kuwa adhabu hiyo ya viboko 60 hadharani itaenda sanjari na vijana wote wenye tabia mbalimbali ambazo hazina tija kwenye jamii hiyo ya Meru kama vile Uzinzi, ulevi wa kupindukia saa za kazi, wizi, Mavazi yanaonesha maumbile,ukosefu wa adabu pamoja na makosa mengine ambayo chanzo chake ni kuiga maadili yasiyokuwa na tija kwennye jamii.
 
“tumejipanga kuhakikisha kuwa wilaya hii ya Meru inakuwa na utofauti wa hali ya juu sana kwani tunao uwezo wa kuwaweka vijana wetu wawe katika maadili mazuri, na masuala kama vile uvaaji wa nguo za ajabu utaisha na kwa hali hiyo jamii itaweza kupungza hata ujinga unaofanywa na baadhi ya vijana wachache huku wakisingizia umaskini’aliongeza Mbisse.
 
Hataivyo Mgeni rasmi katika sherehe hizo ambaye ni Mjumbe wa kamati ya siasa ya mkoa wa Arusha John Palangyo alisema kuwa kuna umuhimu mkubwa sana wa maadili ya kila kabila kurudiwa ili kuweza kuwajengea vijana uwezo wa kufanikiwa zaidi kwenye maisha yao ya kila siku.
 
Palangyo alisema kuwa suala hilo la ulindaji wa maadili lina manufaa sana sio kwa vijana kwani hata kwa taifa kwani kwa sasa wapo baadhi ya vijana ambao wanaharib na kuvunja amani ya Nchi kwa kuwa hawana maadili ambayo yanaanzia ngazi za marika hadi taifa.
 
‘hili jambo la kuweza kuwaweka vijana katika mazingira mazuri ya kimaadili linawezekana kabisa na sisi watanzania tunatakiwa kuondokana na dhana potofu kuwa eti vijana wa sasa hawana maadili wa kuwafundisha maadili ni sisi wazee wa ukoo,rika, na hata wana siasa hivyo basi kila mtu anatakiwa kuzingatia hili lakini pia kuona kuwa kijana wa mwenzake ni wa kwake na hata kama ataharibikiwa basi atachangia uharibifu bila kujali anaharibu kwa nani”aliongeza Palangyo.
 
MWISHO

`WIVU WA KIMAPENZI WASABABISHA MWALIMU KUMWAGIWA MAJI YA MOTO MITHILI YA KUKU

PICHANI NI MWALIMU NEEMA AKIWA AMELALA KWENYE CHUMBA CHA MAJERUI KWENYE HOSPITALI YA MKOA WA ARUSHA MT MERU,PICHA NA QUEEN LEMA

MWALIMU AMWAGIWA MAJI YA MOTO NA KUUNGUWA VIBAYA KWA KUHOFIWA KUWA ANAMAHUSIANO NA MUME WA MTU

Na Queen Lema, Arusha

KATIKA hali isiyokuwa ya awaida Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Neema Teti ambaye pia ni mwalimu,mkazi wa Shangarai mkoa wa Arusha amepata majeraha makubwa sana mara baada ya kumwagiwa maji ya moto sehemu zote za mwili wake mara baada ya kuhofiwa kuwa anatembea na mume wa mtu

Aidha tukio hilo lilitokea December tisa majira ya asubui katika eneo la Shangarai ambapo  Bi Neema alimwagiwa maji ya moto na rafiki yake kwa kuhofiwa kuwa anatembea na mume wake

Akiongea na “MALKIA WA MATUKIO ”mapema jana katika hospitali ya Mt Meru ambapo anapatiwa matibabu Bi Neema alisema kuwa siku hiyo ya December tisa rafiki yake ambaye bi Tatu  Msuya alienda nyumbani kwake na kumuomba kuwa waweze kwenda kwa pamoja kwani kuna matatizo na hivyo yeye ndio anatakiwa kusimamia familia yake.

Neema alidai kuwa mara baada ya kufika nyumbani kwa rafiki yake  kwa malengo ya kumsaidia shida aliyonayo ambayo alidai ni msiba lakini walipofika mambo hayakuwa hivyo

Aliongeza kuwa mara baaada ya hapo rafiki yake ambaye ni Bi Tatu alimtaka aingie ndani ili waweze kupanga mambo yao ya jinsi ya kusaidia familia kwa kipindi hicho cha msiba jambo ambalo hakuwa na wasiwasi nalo kwa kuwa walikuwa wanaaminiana sana

“baada ya hapo nilishangaa sana kwani alifunga milango yote na kuongeza makofuli jambo ambalo lilinipa shida kwa haraka kwani niliwaza labada anataka mazungumzo yawe siri”aliongeza Neema

Alidai kuwa mara baada ya tukio hilo la kufungwa milango,yote ya nyumba ya rafiki yake ndipo alipomtaka aweze kunywa soda lakini alikataa kwani ilikuwa ni asubui sana  lakini pia soda hiyo ilikuwa na chupa ndogondogo jambo ambalo halikuwa na ishara nzuri

“niloishangaa kwa kuwa aliniletea soda ambayo ilikuwa na chupa ndogondogo ndani lakini nilijiuliza kwanini huyu rafiki yangu ananilazimisha zaidi ninywe soda asubui na inaonekana inasumu machale yalinicheza lakini sikuweza kutoka kwa kuwa alikuwa tayari ameshafunga milango yote huku baadhi ya watu wa familia yake nao wakiwa wamefungiwa ndani”aliongeza zaidi Neema

Pia alidai baaada ya muda  mfupi rafiki yake alikuja na maji ya moto ambayo yamechemka sana na kuanza kumwagia bila kujali kuwa ni rafiki yake jambo ambalo pia lilifanya ashindwe kupata msaada wa haraka kwa kuwa milango yote alikuwa ameifunga

“alinimwagia maji ya moto kama kuku bila hata kunionea huruma huku akidai kuwa analipiza kwa kuwa ameambiwa mimi natembea na mume wake na nina mimba ya mume wake jambo ambalo sio kweli na alidai anachotaka ni kunitoa roho”aliongeza Neema

Alidai kuwa baada ya tukio hilo alifungua mkilango na kisha kuchukua mizigo yake haraka na kisha kukimbia kusikojulikana jambo nalo liliwafanya majirani wa eneo hilo kuweza kukusanyika na kisha kumpa msaada wa kwenda kituo cha polisi kwa ajili ya kutoa taarifa lakini pia kumfikisha hospitalini

Awali Muuguzi wa zamu katika hospitali hiyo ya Mte Mt Meru  ambaye ni Bi Neema Baya alisema kuwa hali ya mgonjwa huyo inaendelea vizuri japokuwa bado ana maumivu makali na pia ametoa wito kwa wanawake wengine kuacha tabia ya ukatili kama hiyo kwani inaweza kusababisha vifo.

Wakati huohuo Jeshi la polisi mkoa wa Arusha kupitia Kitengo cha dawati la jinsia limedai kuwa bado linamtafuta Bi Tatu kwa kosa ambalo amelifanya kwani tukio hilo ni la kinyama na nituykio ambalo halipaswi kutokea tena kwenye jamii

Akiongea kwa niaba ya Jeshi hilo Maria  alisema kuwa kwa kuwa jeshi hilo lina mkono mrefu basi litahakikisha kuwa linamtafuta Bi tatu na kisha kumfikisha mahakamani kwa kuwa amefanya kitendo kibaya sana kwa mwenzake baada ya kumuhisi kuwa anamahusiano ya kimapenzi na Mume wake

MWISHO


UKOSEFU WA HUDUMA ZA MAJI ZA UHAKIKA CHANZO CHA NDAO NYINGI KUVUNJIKA, PIA CHANZO CHA MIMBA ZA UTOTONI





IMELEZWA kuwa ukosefu wa huduma za uhakika za maji hasa maeneo ya vijijini ni chanzo mojawapo cha ongezeko la mimba  za utotoni lakini pia uvunjikaji wa ndoa nyingi huku hali hizo zikisababisha pia ongezeko la watoto mitaani ndani ya mji wa Arusha

Pia hali hiyo ya ukosefu wa maji kwenye kaya pia inasababisha umaskini wa hali ya juu sana ingawaje Serikali kwa sasa inaweka mikakati mbalimbali ya kupambana nao.

Hayo yameelezwa na Bi Asha Shabani ambaye ni Katibu wa Mradi wa maji ujulikanao kama Mangole uliopo maeneo ya Kisongo jijini hapa,wakati akielezea mradi huo lakini pia umuhimu wa miradi ya uhakika ya maji hasa kwa maeneo ambayo yapo nje ya miji

Asha alisema kuwa ukosefu wa maji ya uhakika hasa katika maeno ambayo yapo nje kidogo ya miji ni changamoto kubwa sana kwa wanawake kwa kuwa asilimia kubwa huambulia uchovu lakini pia hata kipigo kutoka kwa wenza wao kwa kuwa hutumia muda mrefu kwa ajili ya kusaka maji

Mbali na hayo alisema kuwa ukosefu huo hauathiri pekee wanawake bali hata mabinti wadogo ambao baadhi ya vijana hutumia mwanya huo katika kuwadanganya ili waweze kuwapa maji au kuwasaidia kubeba maji kwa uraisi jambo ambalo nalo ni chanzo kikubwa cha mimba za utotoni lakini pia mdondoko wa elimu kwa watoto wa kike

Akiongelea Mradi huo wa MANGOLE ambao unawasaidia wananchi kutoka katika kata za Matevesi,Ngorobobu, na Lemguru alisema kuwa umekuwa ni faida kubwa sana kwenye jamii hiyo kwani hapo awali kulikuwa na matatizio mengi sana

Alitaja matatizo hayo ni pamoja na baadhi ya wanawake kukosa ndoa,huku wengine wakiambulia wajukuukabla ya wakati kutokana na udanganyifu ambao ulikuwa uanendelea kwa watoto wa kike na vijana pia.

“hapo awali tulikuwa tunalazimika kwenda kilomita mpaka 20 kwa siku ili kutafuta maji lakini toka mradi huu uletwe kwa hisani ya Word Vision umekuwa na faida kubwa sana na hivyo tunataka tuhakikishe kuwa hata wanawake wa maeneo mengine ndani ya mkoa wa Arusha nao wanaweza kufaidika na miradi kama hii ili waweze kuepukana na changamoto za uhaba wa maji”aliongeza Asha

Wakati huohuo Mwenyekiti wa Mradi huo ambaye ni Profesa Calvin Marealle alisema kuwa pamoja na kuwa mradi huo umekuwa ni faida kubwa sana kwa jamii lakini bado unakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile Ukosefu wa umeme wa uhakika hali ambayo wakati mwingine inasababisha baadhi ya wananchi kutoka katika vijiji hivyo vitatu kukosa maji ya uhakika

Profesa Marealle aliongeza changamoto nyingine ni pamouja na baadhi ya wananchi kuiba na kuharibu miundombinu ya maji hali ambayo ni chanzo kikubwa sana cha hasara kwenye miradi hiyo.

MWISHO

WATENDAJI 17 KUTOKA KATIKA KATA 17 MERU HAWANA SIFA ZA KUWA NA CHEO HICHO

WATENDAJI 17 KUTOKA KATIKA KATA 17 MERU HAWANA SIFA ZA KUWA NA CHEO HICHO


IMEELEZWA kuwa watendaji wa kata 17 kutoka katika Wilaya ya Meru mkoa
wa Arusha hawana sifa za kuwa watendaji kutokana na kuwa na elimu
chini ya kiwango hivyo wanatakiwa kuacha kukaidi amri ya Serikali
iliyowataka waende shule kwa ajili ya kujiendeleza



Aidha Serikali ilishatoa waraka toka July mosi mwaka 2003 kuwa
watendaji wanatakiwa kwenda shule lakini mpaka sasa watendaji hao
hawajaweza kwenda shule kutokana na sababu mbalimbali



Hayo yameelezwa na Afisa utumishi wa Wilaya hiyo Anord bureta wakati
akielezea kazi mbalimbali za watendaji hao kwenye baraza la madiwani
wa Halmashauri hiyo kwa malengo ya kuelezea changamoto mbalimbali
ambazo zinawakabili watendaji hao mapema jana


Bureta alisema kuwa July Mosi 2013 Serikali iilitoa tamko ambalo
liliwataka watumishi hao kuweza kwenda mashuleni lakini mpaka sasa
tunaweza kusema kuwa agizo hilo halijaweza kutimizwa jambo ambalo ni
madhara makubwa kwa ajili ya utendaji kazi lakini pia hata kwa ajili
ya maslahi ya umma



Pia alisema kuwa ili kuweza kukabiliana na hali hiyo kwa sasa wameweka
utaratibu wa watendaji hao kuweza kwenda kusoma ili kuweza kukidhi
matakwa ya sheria hiyo ambayo inawataka kuwa na elimu lakini kuweza
kwenda sanjari na mpango wa serikali wa sasa yaani Big Result


Akiongelea suala hilo kwa niaba ya madiwani wa halmashauri hiyo Makamu
Mwenyekiti Frida Kaaya alisema kuwa  ni lazima watendaji hao waweze
kwenda shule lakini pia hata Halmashauri ihakikishe kuwa inasimamia na
kutatua changamoto zao ambazo zinajali maslahi


‘hapa ni lazima tujiulize kuwa hawa watendaji walikosa fedha au fursa
za kwenda kusoma au walikaidi agizo hilo lakini pia kuanzia sasa
maslahi ya watendaji yawekwe hadharani na pia waweze kupewa kwa
wakati ili nao pia waweze kupata moyo wa kufanya kazi”aliongeza Frida



Pia  Bi Frida alidai kuwa kama Halmashauri lakini pia Serikali
itashindwa kuwajali watendaji ni wazi kuwa lawama zitakuwa nyingi sana
kwani wao ndio wapo na wananchi kila siku ingawaje kwa sasa zipo
changamoto lukuki ambazo zinasababishwa na watendaji hao.



MWISHO

WANAWAKE 200,WATOTO 1000 WAFANIKIWA KUPEWA ELIMU PAMOJA NA UWEZESHWAJI KIUCHUMI KWA AJILI YA KUPAMBANA NA UMASKINI



Na Queen Lema, Arusha

ZAIDI  ya watoto elfu pamoja na wanawake mia mbili kutoka jijini
Arusha wamefanikiwa kuwezeshwa kiuchumi pamoja na kupatiwa elimu
mbalimbali ili kupunguza kasi ya ongezeko la watoto mijini lakini pia
kwenye vituo vya kulelea watoto yatima

Hataivyo watoto hao pamoja na wanawake hao wamefanikikiwa kupatiwa
elimu pamoja na uwezeshwaji hali mabyo mpaka sasa imeweza kuonesha
mafanikio ya hali ya juu sana.

Wanawake hao pamoja na watoto wamewezeshwa na Kijiji kinachotoa malezi
mbadala ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu(SoS)chini ya mradi
wa kuimarisha familia(FSP)unaotekelezwa sehemu mbalimballi nchini.

Hayo yamelezwa na Mratibu wa utetezi kutoka katika kijiji hicho cha
SOS ambaye ni John Batista wakati akiongea kwenye maazimisho ya
ukatili wa kijinsia kwa wanwake na watoto yaliyofanyiika katika eneo
la Kimnyaki Jijini Arusha mapema wiki hii

Batista alisema wanawake hao 200 pamoja na watoto elfu moja wameweza
kusaidiwa kutokan ana kampeni ambayo inaendeshwa chini ya SOS ya
kupinga nakutokomeza suala zima la unyanyasaji kwenye kwenye jamii.


Alisema kuwa kwa kuwawezesha wanawake hao pamoja na watoto kutasaidia
sana kupungua kwa umaskini kwenye jamii kwani umaskini unapokithiri
basi unachangia hata suala zima la malezi nalo kuwa duni sana.


Mbali na hayo Batista pia alitoa wito kwa jamii kuhakikisha kuwa
wanachana na ukatili dhidi ya wanawake lakini pia kwa watoto kwani
hali hiyo ndiyo chanzo cha ongezeko la watoto wa mitaani

SHULE ZA SEKONDARI AMBAZO ZINA MAABARA KUPEWA HUDUMA YA INTERNET BURE

SHULE ZA SEKONDARI AMBAZO ZINA MAABARA KUPEWA HUDUMA YA INTERNET BURE

Na Queen Lema, Arusha

KAMPUNI ya Smile ya mawasiliano ya Smile imeweka mikakati ya kusaidia
shule za Serikali ambazo zina maabara kwa kutoa huduma ya
mawasiliano(internet)bure itakayowawezesha wanafunzi waweze kusoma kwa
kupitia mitandao.

Hayo yameelezwa na Deo Ndejembe ambaye ni meneja kitengo cha mauzo
katika kampuni hiyo wakati akiongea kwenye uzinduzi wa mtandao wa
smile kwa mkoa wa Arusha mapema leo.

Deo alisema kuwampango huo unalenga kuimarisha huduma za maabara
katika shule za sekondari za serikali kwani wanafunzi wakiwa na huduma
hizo wataweza kusoma na kwenda pamoja na soko la dunia ambalo
linategemea zaidi huduma za mitandao.

Alidai kuwa mpango huo utaweza kuwanufaisha zaidi shule ambazo zina
maabara pamoja na kompyuta hivyo basi hata kwa shule ambazo hazina
maabara zinatakiwa kuweka mara moja ili ziweze kunufaika na mpango huo
ambao umeshaanza

“tunataka kuona kuwa lile lengo la serikali ambalo lililenga shule
ziwe na maabara linatimia lakini pia maabara ziwe za kisasa zaidi na
ziweze kupata teknolojia ya mawasiliano bure kwani itasaidia hata
ufaulu wa masomo kama sayansi kuweza kuongezeka’alisisitiza Deo

Wakati huo huo alidai kuwa mpango huo wa kutoa huduma za Tekonlojia
umeshaanza kwa shule 10 ndani ya Jiji la Dar es saalam lakini kwa mkoa
wa Arusha shule ya Arusha School tayari imeshanufaika na mpango huo
ambao ni bure

Naye Afisa mawasiliano wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania
(TCRA)Innocent Mongi alidai kuwa bado mkoa wa arusha unahitaji huduma
za mawasiliano zaidi kutokana na mwingiliano wa huduma kama vile
uchumi, na utalii

Mongi alidai kuwa uwepo wa mtandao huo wa Smile kwa mkoa wa arusha pia
utachangia wafanyabiashara  wakubwa na wadogo kuweza kufanya biashra
kutoka katika masoko mbalimbali duniani .

“napenda kuwasihi wakazi wa Arusha kuhakikisha kuwa wanatumia vema
mtandao huo ili kuraisisha shuguli mbalimbali za maendeleo kwa mkoa wa
arusha na kutokana na hili tunaamini kuwa Arusha itapata mabadiliko
makubwa”alisema Mongi

WAZIRI AZITAKA NCHI ZA AFRIKA ZIUNGANE ILI KUPAMBANA NA RUSHWA


WAZIRI wa nchi ofisi ya rais anayeshughulikian utawala bora George
Mkuchika amezitaka nchi za Afrika  kujenga umoja na kupeana uzoefu
katika vita vya kupambana na rushwa huku  nchi hizo z ikitakiwa
kujenga sera za uwazi kwenye sekta nzima ya rasilimali ili waweze
kunufaika nazo ikiwa ni pamoja na kupaza sauti moja kuomba kurejeshwa
kwa fedha zilizoko nje ya bara la afrika.

Mkuchika alitoa kauli hiyo jana  alipokuwa akifunga na kusherehekea
maadhimisho ya siku ya umoja wa mataifa ya mapambano dhidi ya rushwa
yaliyofanyika jini hapa

Alisema kuwa umoja una  nguvu katika kupambana na rushwa hivyo ili
kuhakikisha kuwa swala hilo linatokomezwam nchi za afrika zinapaswa
kutekelza kwa vitendo mkataba wa umoja wa afrika dhidi ya rushwa kwa
kila nchi kujiunga moja kwa moja kwa kutoa uzoefu juu ya mapambano
dhidi ya rushwa ambayo yameonekana kurudisha nyuma maendeleo ya bara
la afrka.

Alieleza kuwa pamoja na chi za Ulaya kuwa mstari wa mbele katika
mapambano dhidi ya rushwa lakini nchi hizo zimekuwa zikikumbatia
Uhamishaji wa fedha kutoka bara la afrika na kukaa kimya
kilawanapotakiwa urejeshwaji wa fedha zilizopo kwenye mataifa hayo


Aidha alifafanua kuwa nchi 30  zimesaini mkataba wa umoja wa mataifa
wa mapambano dhidi ya rushwa kati ya nchi 44 zinazotakiwa kusain
mkataba huo hivyo kuzitaka nchi zilizobaki kujiunga na umoja huo ili
kuliletea maendeleo bara la afrika na kuwa na sauti moja ya mapambano
dhidi ya rushwa huku akizitaka nchi za bara la afrika kutambua kuwa
mapambano si ya rushwa si ya mtu moja bali ya watu wote.

Nae mkurugenzi wa takukuru nchini Drt Edward Hosea alisema kuwa bara
la afrika bado lina safari ndefu katika mapambano ya vita vya rushwa
kwani kati ya nchi za afrika 34 kati ya 44 ndizo amabzo zimesaini
mkataba wa mapambano ya rushwa huku akidai kuwa mikataba mingi
inaingia kwenye rasilimali za nchi za bara la afrka haina uwazi na
sheria zinazotumika  hazimnufaishi mwananchi wa kawaida dhidi
yamapambano ya rushwa.

Aidha aliitaka serikali kuweka sera ya uwazi kwenye mikataba ya
wawekezaji wa rasilimali ya gesi ili iweze kuwanufaisha watanzania na
sheria zitakazotungwa iwe ya uwazi na yenye faida kwa watanzania
hukuakizishawishi nchi ambazo hazijatakeleza mkataba wa umoja wa
mataifazifanye hivyo mara moja kwani bara la afrka ndilo linalohitaji
maendeleo makubwa hivyo bila kuungana hawataweza kufanikiwa.

MWISHO.

KIKUNDI CHA OLGILAI CHANGAMKENI YOUTH GROUP CHAFANIKIWA KUTOA MSAADA WA MADAWATI,NA VIFAA VYA SHULE YA OLGILAI


KIKUNDI CHA OLGILAI CHANGAMKENI YOUTH GROUP CHAFANIKIWA KUTOA MSAADA WA MADAWATI,NA VIFAA VYA SHULE YA OLGILAI

Na Queen Lema, Arusha


KIKUNDI cha Olgilai Changamkeni Youth Group kilichopo maeneo ya Olgilai mkoani Arusha kwa kushirikiana na wadau wengine wa elimu wameweza kutoa msaada wa madawati zaidi ya 50 pamoja na vifaa vingine kama vile meza, kabati, na viti  kwa shule ya msingi Olgilai huku lengo likiwa ni punguza changamoto za kielimu shuleni hapo

Hataivyo msaada huo ambao ulitolewa mapema jana ulienda sanjari na uzinduzi wa kikundi hicho ambacho kimelenga kutatua changamoto mbalimbali katika kijiji hicho cha Olgilai na Mkoa wa Arusha kwa ujumla.

Akiongea mara baada ya kukabidhi msaada huo kwa shule ya msingo Olgilai Mwenyekiti wa kikundi hicho Benjamini Justin alisema kuwa wameamua kuchangia zoezi zima la elimu ili kwenda sanjari na mpango wa serikali wa matokeo ya haraka(BRN)

Benjamini alidai kuwa hapo awali shule hiyo ilikuwa inakabiliwa na changamoto kubwa sana ya ukosefu wa madawati na vifaa vingine hali ambayo ilifanya wazazi wa eneo hilo ambao ni wanakikundi kuhakikisha kuwa wanatafuta mbinu ya kukabiliana na changamoto hiyo.

Alifafanua kuwa baada ya kuweka mikakati mbalimbali waliweza kuwashirikisha wadau wengine ambao nao waliweza kuungamkono na kuhakikisha kuwa wanapunguza tatizo la uhaba wa madawati kwenye shule hiyo ya Olgilai.


Wakati huo huo alidai kuwa pamoja na kuwa wameweza kufanikisha kutoa msaada huo wa madawati, meza,viti, madaftari, na kalamu lakini bado wanakabiliwa na changamoto lukuki ambazo wakati mwingine zinakwamisha jitiada zao

Alitaja changamoto hiyo kuwa ni pamoja na baadhi ya fursa za mikopo ni finyu kwa kuwa taasisi hizo hazitoi mikopo kwa vikundi jambo ambalo linakwamisha jitiada za maendeleo ya vikundi hasa vile vya mitaa.

“pamoja na kuwa leo tumeweza kutoa msaada huu kwa shule hii pamoja na kuzindua rasmi kikundi chetu bado changamoto hii tunaifikiria sana hivyo basi tunaomba taasisi za Fedha kuhakikisha kuwa zinatuangalia ili nasi tuweze kusaidia jamii kama tulivyofanya leo”aliongeza Benjamini

Wakati huo huo akiongea kwa niaba ya wanafunzi ambao ndio walengwa wa msaada huo Irene Peter alidai kuwa msaada huo wa madawati utasaidia sana kuongeza ufanisi wa elimu kwani hapo awali wanafunzi shuleni hapo walikuwa wanalazimika kuandika Miandiko mibaya kwa kuwa hawakuwa na madawati.

WAZEE ARUSHA WAPATIWA MSAADA


Asasi ya Informal Sector team(INSERT)imefanikiwa kutoa msaada wa Mablanketi yenye thamani ya zaidi ya milioni moja na nusu kwa Jukwaa la wazee wa mkoa wa Arusha (JUWA)huku lengo halisi likiwa ni kuhakikisha kuwa wazee wote wanaendelea kusihi maisha ya upendo na amani

Akiongea na wazee hao mara baada ya kuwapa msaada mratibu wa asasi hiyo ya INSERT,Japhet Saruni alisema kuwa msaada huo unalenga kuhakikisha kuwa afya za wazee zinaendelea kuboreka zaidi

Aidha Saruni alisema kuwa kwa sasa wazee wengi sana wamekuwa wakisahulika kwenye maslahi yao hali ambayo inachangia sana kuzorotesha hata afya zao ingawaje sera za wazee bado zipo

Alifafanua kwa kusema kuwa hali hiyo imechangia kwa kiwango kikubwa sana wazee wengi kupoteza maisha kabla ya siku zao hivyo basi ndio maana Asasi hiyo ya INSERT ikaweza kuona kuwa kuna umuhimu wa kuwasaidia wazee

Pia alisema kuwa kuna umuhimu wa jamii kuhakikisha kuwa wanatatua kero za jamii kila mara kwani kwa sasa jamii imeacha kabisa kuwasaidia wazee huku wazee nao wakikabiliwa na changamoto kubwa sana

Hataivyo alifafanua kuwa kama jamii itaweza kuwakumbuka wazee kila mara basi kasi ya ongezeko la vifo visivyo vya lazima hasa vya wazee vitaweza kupungua kwa kiwango kwani takwimu zinaonesha kuwa wazee wengi wanakufa kutokana na kuwa hawana msaada wa kuwasaidia.


Awali wazee waliopewa msaada walisema kuwa pamoja na kuwa wamepewa msaada huo bado kuna umuhimu wa sera za wazee kuweza kutekelezwa hasa kwenye sekta muhimu kwani sera hizo zipo lakini hazitekelezwi na baadhi ya watendaji tena wwa Serikali.

MWISHO

WASANII ARUSHA WAHIDIWA NEEMA


KAMPUNI ya Mkundi Production yenye makao makuu Jijini Arusha imeahidi kuibua lakini pia kuwezza kuendeleza vipaji vya  mbalimbali vya vijana ikiwa ni pamoja na kuweza kuwasaida kurekodi na kusambaza kazi zao

Aidha kwa sasa asilimia kubwa ya vijana wenye vipaji vya uimbaji wanashindwa kufikia malengo yao mbalimbali kwa kuwa hawana uwezo wa kuingia studio lakini pia kutoa na kughramikia baadhi ya gharama hali ambayo inachangia sana kupoteza vipaji vingi

Hayo yameelzezwa na mkurugenzi jmtendaji wa kampuni hiyo Carlos Mkundi mapema jana mara baada ya kuzindua Album ijulikanayo kama “NIMETOKA  MBALI”ambayo imejumuisha vijna mbalimbali wa mkoa wa Arusha

Mkundi alisema kuwa kampuni yakeimejidhatiti kuhakikisha kuwa kila msanii mwenye uwezo wa kuimba aweze kunufaika na kipaji chake na kamwe kisingizo kuwa ghrama ni chanzo kisiwepo

Aidha alidai kwa sasa wasanii wa nyimbo mbalimbali ndani ya mkoa wa Arusha wanashindwa kuimba na kutoa album zao kwa kuwa kuna changamoto lukuki sana ambazo ndizo chanzo kikubwa cha wao kushindwa kufanya vema zaidi

Wakati huo huo alisema kuwa kwa kipindi cha mwaka huu Kampuni yake tayari imeshwaweza kuwasaidia wasanii saba kuweza kurekodi album zao na hivyo mikakati zaidi bado itaendelea kuwekwa

Pia alidai kwa kila mwaka wasanii saba kutoka Jijini Arusha wataweza kurekodi kwa msaada wa kampuni hiyo lakini hata wale ambao bado hawajaweza kurekodi basi watapewa misaada mbalimbali ambayo inalenga kuinua vipaji vyao zaidi

MWISHO

Wednesday, December 4, 2013

HALMASHARI YAURARUSHA VIJIJINI WAFANIKIWA KUKUSANYA MILIONI 682 KUTOKA KATIKA VYANZO VYAKE VYA MAPATO


Wilaya ya Arusha Vijijini imefanikiwa kukusanya kiasi cha Milioni 682
sawa na asilimia 31.8 kutoka katika vyanzo vyake vya mapato ingawaje
kwa kipindi cha mwaka 2013,2014 wanatarajai kukusanya kiasi cha zaidi
ya bilioni mbili sanjari na kuibua vyanzo vya mapato ambavyo
vitaimarisha zaidi uchumi wa wananchi wake.

Hayo yamelezwa mapema jana na Kaimu mweka wa Halmashauri hiyo bw
Munguabela Kakulima wakati akielezea Vyanzo vya mapato ambavyo
vitakwenda sanjari na mpango wa matokeo makubwa (Big Result Now)kwenye
wilaya hiyo

Kakulima alidai kuwa kupatikana kwa fedha hizo kunatokana na jitoada
mbalimbali ambazo zinafanywa na idara yake ambapo ndipo zilipochangia
mafanikio hayo

Aidha alidai mpaka mwaka wa fedha wa sasa uweze kuisha wanatarajia
kuvuka hata lengo ambalo walikuwa wameliweka na hivyo kukusanya fedha
nyingi zaidi hali ambayo itachangia shuguli mbalimbali za maendeleo
kuweza kufanyika kwa haraka

Mbali na hayo alidai kuwa kwa sasa wanamikakati mbalimbali ya
kuhakikisha kuwa wanaweka uwezekano wa kubaini vyanzo vipya vya mapato
ambavyo navyo vitaweza kuweka halmashauri hiyo kwenye kiwango cha juu
sana

Mkakati mwingine ambao nao aliweza kuutaja ni pamoja na kuweza kuwapa
wananchi elimu ya kuweza kulinda vyanzo vya mapato lakini kuweza
kuonesha umoja baina ya watendaji wa halmashauri hiyo ili kuweza
kuharakisha shuguli mbalimbali za ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri

Awali alisema kuwa pamoja na mikakati na jitiada ambazo zinafanywa na
idara ya fedha katika Halmashauri hiyo zipo changamoto ambazo nazo
zinachangia kukwamisha malengo mbalimbali ya ukusanyaji wa mapato
kutoka katika vyanzo

Kakulima alidai kuwa changamoto hizo ni pamoja na baadhi ya wanasiasa
kuingilia shuguli pamoja na vyanzo vya mapato hali ambayo wakati
mwingine inasababisha waone kuwa halmashauri hiyo inachangia sana
kuwadidimiza.

Naye mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo alisema kuwa ili matokeo ya
haraka yaweze kuja katika Halmashauri hiyo vyanzo vya mapato
vinatakiwa kulindwa lakini nao watendaji wa idara ya fedha wanatakiwa
kufuata wajibu wao wa kulinda na kuitetea halmashauri hiyo.

MWISHO

ACHENI UKIRITIMBA USIOKUWA WA LAZIMA

MKUU wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, amewataka watumishi wa
serikali na taasisi zake kuondoa ukiritimba usio wa lazima katika
kutoa huduma kwa wadau wa maendeleo, hususani, wanaowafundisha
wakulima wadogo wadogo  kilimo cha kibiashara ili waweze kujipatia
maendeleo.




Alitoa maagizo hayo wakati akifungua maonesho ya vikundi vya wakulima
zaidi ya 21 kutoka mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, yaliyoandaliwa na
Shirika lisilo la kiserikali la Farm Concern International (FCI)
wakishirikiana na World Vision Tanzania, World Vision Canada na
Shirika la Maendeleo la Canada (CIDA), jijini hapa jana.




Mkurugenzi wa FCI Afrika, David Richiu, alisema shirika lake ambalo ni
wakala wa masoko kwa wakulima wadogo wadogo, limejikita kuwafundisha
kilimo cha kibiashara, uongozi katika vikundi kupitia mfumo kijiji
biashara, wanawapa mbinu za kutafuta masoko ya mazao, utunzaji wa
mazingira, elimu ya lishe bora kwa familia, uhifadhi wa mazao,
huwaunganisha na watu wa pembejeo na huduma za ugani.



Alisema maonesho hayo ya kilimo yenye kauli mbiu, “Jua mahitaji ya
soko zalisha kibiashara,” yamedhaminiwa na mradi wa SMART (Sustainable
Market led Agriculture Resource) na wanafanya kazi katika wilaya za
Arusha, Monduli, Siha, Arumeru na Hai.



Baadhi ya miradi ambayo shirika lake linatekeleza nchini ni pamoja na
kukuza uzalishaji na ulaji wa mboga mboga za kiasili unaotekelezwa
katika wilaya za Arusha, Arumeru, Hai, Siha, Same na Karatu, lishe kwa
wakulima wa kahawa unaotekelezwa wilaya za Arusha, Arumeru, Siha na
Hai.



Mingine ni mradi wa muhogo ulioanzia kijiji cha Mbuguni wilayani
Arumeru, mradi wa ndizi na viazi vitamu hasa viazi lishe vyenye
asilimia nyingi ya vitamin A ambao wanatarajia kuupanua kwenye mikoa
mingine nchini.



Kwa upande wake, Kiongozi mkazi wa FCI nchini, Wiston Mwombeki,
alisema ili mkulima aweze kupata soko yampasa kwanza ajue mahitaji ya
soko kama vile mazao yanayohitajika sokoni, ubora, mahali walipo
wanunuzi, kiwango kinachotakiwa, ufungashaji, uhifadhi na usafirishaji
wa mazao, kilimo bora na pembejeo bora.


MWISHO.

OFISI ZA CHADEMA ARUSHA ZACHOMWA MOTO NA WATU WASIOFAHAMIKA

Na Queen Lema, Arusha



KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida watu wasiofahamika jana(leo)wamevamia ofisi ya Chadema Kanda ya kaskazini iliopo Jijini Arusha na kisha kuanza kuwasha moto ambao ulisababisha hasara kubwa sana.

Akizungumza na “Majira”katibu wa kanda ambaye pia ni katibu wa mkoa wa Arusha Chadema, Amani golugwa alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya asubuhi katika ofisi za kanda zilizopo eneo la Ngarenaro mjini Arusha.

Golugwa alisema kuwa watu hao waliingia mara baada ya mlinzi kutoka zamu ya kulinda usiku ambapo walilazimika kuvunja kioo kikubwa na kisha kuingia ndani ili kufanya lile walilolikusudia.

Aliendelea kwa kusema kuwa baada ya kuingia ndani walipanda kwenye dari la nyumba hiyo ambapo walianza kutafuta uwiano wa chumba ambacho kinahifadhi nyaraka mbalimbali za Chama na kisha kuwasha moto

Alidai kuwa wakati wanawasha moto huo ghafla uliweza kulipuka hivyo lengo halisi halikuweza kutimia kwa haraka na badala yake walishuka na kuanza kukimbia wakati jingo letu likiwa linateketea kwa moto
Pia alisema baada ya watu hao kuona kuwa hawawezi kuchoma chumba hicho walitengeza shoti kubwa ya umeme ambayo iliweza kusababisha vyumba vya choo na bafu kuunguwa na hatimaye walishuka wakiwa wanakimbia huku moto ukiendelea kutapakaa kwenye jingo la ofisi hiyo.

“kilichofanya tuweza kusema kuwa walikuwa na lengo la kuchoma chumba hiki ambacho kinahifadhi nyaraka muhimu za chama ni baada ya kuona kuwa wameacha maeneo yote na kisha kuingia hapa na inavyoonekana lengo lao ni kupoteza ushahidi wa vitu mbalimbali ambavyo tunapambana navyo”aliongeza Golugwa

Katika hatua nyingine Golugwa alisema kuwa tukio hilo la kuchoma ofisi linaonesha kuwa wapo baadhi ya watu ambao wanatumia muda na fikra zao nyingi kuwawinda viongozi wa Chadema na kuingilia hata kwenye maisha yao ya kila siku

Aidha aliwataja watu ambao wanawindwa sana kwa ajili ya kujeruliwa ni pamoja nay eye ,mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Goodbless Lema, pamoja na mwenyekiti wa wilaya ambaye ni Ephata Nanyaro
‘mpaka sasa tunawahisi watu watatu katika sakata hili na kwa maana hiyo tumesharipoti polisi ili waanze mara moja upelelezi wao lakini jingo letu tumeliwekea ulinzi mkubwa sana na kumbukumbu zote zipo ingawaje mpaka sasa bado hatujaweza kujua kwanza ni hasara ya shilingi ngapi tumeipata’aliongeza Golugwa

POLISI ARUSHA WASHIKILIA SILAHA ILIYOKUWA IKITUMIKA KWENYE MATUKIO YA UHALIFU



JESHI la Polisi mkoani Arusha,linashikilia silaha aina ya short gun
WINCHESTER  yenye namba za usajili c.056900 pamoja na mmiliki wake
ambaye alikuwa anaitumia kwenye matukio mbalimbali ya uhalifu kwa mkoa
wa Arusha na nje ya mkoa wa Arusha

Pia Polisi mkoa wa Arusha ilifanikiwa kumkamata mmiliki wa silaha hiyo
ambaye ni Jumanne Abadlaha(25) maarufu kama babu G

Akiongea na vyombo vya habari mapema leo kamanda wa polisi mkoa wa
Arusha Liberatus Sabas alisema kuwa silaha hiyo pamoja na jambazi
huyo walifanikiwa kumkamata September 27 majira ya asubuhi.

Sabas alisema kuwa Polisi waliokuwa katika doria waliweza kumkamata
jambazi huyo na silaha yake  katika eneo la Ungalmtd ambapo ndipo
makazi ya jambazi huyo mara baada ya kupewa taarifa na raia wema kuwa
anamiliki silaha kinyume cha sheria lakini pia anatumia kwenye matukio
mbalimbali ya uhalifu.

Aidha alidai kuwa mara baada ya kumkamata jambazi huyo na silaha yake
waliweza kugundua kuwa silaha hiyo tayari ilikuwa imeshakatwa kitako
lakini ndani ilikuwa na risasi 13

Sabasi aliendelea kwa kusema kuwa mara baada ya kumkamata jambazi huyo
pamoja na silaha yake waliweza kumuhoji na alikiri kuwa amehusika na
matukio mbalimbaliya uhalifu kama vile unyanganyi wa kutumia nguvu na
silaha, lakini pia anamiliki silaha hiyo kiyume cha sheria.

Pia alidai kuwa mbali na kuweza kugundua kuwa anamiliki silaha hiyo
kinyume cha sheria lakini pia silaha hiyo imekuwa ikitumika kwenye
matukio mbalimbali  ya uhalifu ambayo yameweza kutokea katika mkoa wa
Arusha na nje ya mkoa wa Arusha.

Hataivyo kamanda huyo amedai kuwa upelelezi zaidi bado unaendelea na
mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika.

Wakati huohuo kamanda huyo aliwataka wakazi wa mkoa wa Arusha
kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa za siri hasa za wale wananchi wasio
waaminifu wanaojihusisha na matukio ya uhalifu kwani matukio hayo ya
ualifu yamechangia sana kushuka kwa amani ya nchi ya mkoa wa Arusha.
Mwisho.

SHULE ZA SEKONDARI AMBAZO ZINA MAABARA KUPEWA HUDUMA YA INTERNET BURE



Na Queen Lema, Arusha

KAMPUNI ya Smile ya mawasiliano ya Smile imeweka mikakati ya kusaidia
shule za Serikali ambazo zina maabara kwa kutoa huduma ya
mawasiliano(internet)bure itakayowawezesha wanafunzi waweze kusoma kwa
kupitia mitandao.

Hayo yameelezwa na Deo Ndejembe ambaye ni meneja kitengo cha mauzo
katika kampuni hiyo wakati akiongea kwenye uzinduzi wa mtandao wa
smile kwa mkoa wa Arusha mapema leo.

Deo alisema kuwampango huo unalenga kuimarisha huduma za maabara
katika shule za sekondari za serikali kwani wanafunzi wakiwa na huduma
hizo wataweza kusoma na kwenda pamoja na soko la dunia ambalo
linategemea zaidi huduma za mitandao.

Alidai kuwa mpango huo utaweza kuwanufaisha zaidi shule ambazo zina
maabara pamoja na kompyuta hivyo basi hata kwa shule ambazo hazina
maabara zinatakiwa kuweka mara moja ili ziweze kunufaika na mpango huo
ambao umeshaanza

“tunataka kuona kuwa lile lengo la serikali ambalo lililenga shule
ziwe na maabara linatimia lakini pia maabara ziwe za kisasa zaidi na
ziweze kupata teknolojia ya mawasiliano bure kwani itasaidia hata
ufaulu wa masomo kama sayansi kuweza kuongezeka’alisisitiza Deo

Wakati huo huo alidai kuwa mpango huo wa kutoa huduma za Tekonlojia
umeshaanza kwa shule 10 ndani ya Jiji la Dar es saalam lakini kwa mkoa
wa Arusha shule ya Arusha School tayari imeshanufaika na mpango huo
ambao ni bure

Naye Afisa mawasiliano wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania
(TCRA)Innocent Mongi alidai kuwa bado mkoa wa arusha unahitaji huduma
za mawasiliano zaidi kutokana na mwingiliano wa huduma kama vile
uchumi, na utalii

Mongi alidai kuwa uwepo wa mtandao huo wa Smile kwa mkoa wa arusha pia
utachangia wafanyabiashara  wakubwa na wadogo kuweza kufanya biashra
kutoka katika masoko mbalimbali duniani .

“napenda kuwasihi wakazi wa Arusha kuhakikisha kuwa wanatumia vema
mtandao huo ili kuraisisha shuguli mbalimbali za maendeleo kwa mkoa wa
arusha na kutokana na hili tunaamini kuwa Arusha itapata mabadiliko
makubwa”alisema Mongi

KANISA LATANGAZA NEEMA KWA WAHUDMU,WAHADIWA KUPEWA MASAMBA YA KILIMO KWA AJILI YA MSIMU MPYA WA KILIMO UJAO

NA BETY ALEX, ARUSHA


HUDUMA ya Maisha ya Yesu iliopo maeneo ya Kisongo jijini Arusha imesema kuwa kwa kutambua mchango wa wahudumu lakini pia wazee wa kanisa hilo wanatarajia kuwagawia mashamba ya kulima ili waweze kujiendeleza kwenye maisha yao ya kila siku na kuachana na tabia ya kuwa tegemezi

Aidha mpango huo unakuja mara baada ya kanisa hilo kuanza kutoa na kusisitiza masomo ya upendo ambayo yanalenga kumuinua zaidi Mungu kuliko mwanadamu

Akitangaza msimamo huo wa kuwasaidia wahudumu hao mchungaji kiongozi wa huduma hiyo Eliakimu molel”Channel”alisema kuwa mpango huo utasaidia sana kuongeza ufanisi wa kazi za kila siku lakini hata za kanisa

Alisema kuwa kwa kufanya hivyo wahudumu hao hasa wale ambao hawana kazi wataweza kuepukana na dhambi mbalimbali ambazo zinasababishwa na ukosefu wa kazi za kufanya

“ukiwa kama muhudumu hapa kanisani kwangu nilazima nihakikishe kuwa mnatoka siwezi kutoboa mimi mwenyewe halafu ninyi mkabaki mkiwa hamna lolote nasema nitagawa mashamba ya kulima na kila atakayweze akulima katika mashamba hayo ni lazima atoke”aliongeza Channel

Pia alisema kwa kanisa lolote lile ili liweze kusimama vema wahudumu lakini pia hatawazee wa kanisa wanapaswa kuwa makini kuanzia kiroho hadi kimwili hivyo ni wajibu wa viongozi wa makanisa kuhakikisha kuwa wanawaangalia makundi hayo

Alidai kuwa kama wakiwa dhaifu kwenye nyanja yoyote ile ni lazima kuwepo na kasoro kwenye huduma hiyo na badala yake badala ya kusonga mbele kwenye wokovu basi hata waumini watakuwa wanarudi nyuma kwenye wokovu

“wahudmu, wazee wa kansiani watu muhimu sana kwenye maendeleo ya kanisa la leo tusiwaache wakawa legelege bali tuwainue juu hata hali zao za maisha ziweze kubadilika ni faraja sana kama mhudumu wa kanisa akapanda daraja kwenye kiwango cha juu alafu pia akawa na imani basi hata mimi mchungaji nitafanya kazi yangu bila shaka ila kama akiwa legelege pepo likija linaanza nay eye kwanza”aliongeza Channel

Wakati huo huo alisema kuwa pia kanisa hilo limejiwekea hata utaratibu wa kuweza kuwasaidia wale wasiojweza kwa kuwa msaada wa vyakula ili wasiwe wakrisro wenye imani lakini pia wawe na uwezo kuamini kuwa hata kama hawana kitu bado mchungaji wao anawapenda na anaweza kufunga na kuomba juu yao ili hali za maisha ziweze kubadilika.

MWISHO

Saturday, October 26, 2013

NYUMBA ZA ASKARI ZIMA MOTO ARUSHA ZAKABILIWA NA UCHAKAVU ULIODUMU KWA ZAIDI YA MIAKA 50


Na Queen Lema, Arusha.

Jeshi la zima moto na ukoaji mkoa wa Arusha linakabiliwa na changamoto
ya uchakavu wa nyumba uliodumu kwa miaka zaidi ya 50 ambapo pia
uchakavu huo wa nyumba unaenda sanajari na uahba wa Vyoo hali ambayo
inasababisha ongezeko la magonjwa ya Malaria kutokana na nyumba hizo
kugeuka kuwa makazi ya Mbu.

Aidha nyumba hizo zilijengwa mwaka 1954 ambapo mpaka sasa hazijaweza
kufanyiwa marekebisho ya aina yoyote ile hali ambayo inasababisha
nyumba hizo kugeuka magofu.

Hayo yamelezwa na Andrew James Mbate ambaye ni kamanda Zima moto na
uokoaji mkoa wa Arusha wakati akiongea na wafanyakazi wa jeshi hilo
mara baada ya kumuaga aliyekuwa kamanda wa jeshi hilo Bw Jesward
Ikonko mapema jana.

Kamanda Andrew alisema kuwa nyumba hizo za jeshi zilijengwa miaka
mingi iliyopita lakini toka kujengwa kwake mwaka 1954 mpaka sasa
hazijaweza kufanyiwa marekebisho ya aina yoyote ile jambo ambalo
linasababisha wafanyakazi pamoja na familia zao ziweze kuishi maisha
ya kuugua kila mara.

“tunaweza kusema kuwa nyumba hizi zimegeuka nyumba za mbu kwani kwa
juu hazijaweza kuzibwa na baridi yote inapita lakini pia hata kwa juu
kwa kuwa kuna uwazi mkubwa sana unasababisha mbu kukaa kama nyumbani
kwani sasa hali hiii kwa kweli inasababisha wafanyakazi wetu washindwe
kufanya kazi zao kwa kufuraia makazi’aliongeza hivyo.

Pia alisema kuwa mbali na nyumba hizo kugeuka chakavu sana lakini pia
hata suala la vyoo navyo ni chakavu kwa kiwango cha hali ya juu jambo
ambalo ni hatari kwa afya za watumiaji

“tunaweza kujiuliza kuwa choo kilichojengwa mwaka 1954 mpaka sasa
kitakuwaje na kinatumiwa na familia nyingi je kwa hali hii wafanyakazi
wataweza kufuraia maisha au ndo wataboreka “alihoji Kamanda huyo.

Kutokana na hali hiyo alisema kuwa ni vema kama mchakati wa nyumba
hizo za watumishi sasa zikageukia upande wa Wizara kutoka katika
mikono ya Jiji la Arusha kwani kama zitakuwa chini ya wizara zitaweza
kupata marekebisho makubwa ambayo yataongeza utendaji kazi mzuri wa
wafanyakazi.

Akiongelea suala zima la utendaji kazi wa kikosi hicho cha zima moto
mkoa wa Arusha alisema kuwa mkoa wa Arusha unakabiliwa na tatizo la
ujenzi holela hali ambayo inasababisha wakati mwingine washindwe
kuokoa baadhi ya nyumba ambazo zinateketea kwa Moto hivyo basi ni vema
kama kamati ya mipango miji wakati mwingine ikawa inatoa elimu kwa
wananchi wanaotaka kujenga nyumba zao.

MWISHO

IDADI YA WANAWAKE WABUNGE SADC IMEONGEZEKA

Na Gladness Mushi,Arusha

IDADI  ya wabunge wanawake  kwenye nchi wanachama wa mabunge ya nchi za kusini mwa Afrika (SADC) imeongezeka ingawaje kwa Tanzania bado baadhi ya wanawake wanahofu kubwa ya kushiriki katika chaguzi mbalimbali kutokana na changamoto zilizopo kwenye jamii

Hayo yameelezwa  na Anna Makinda ambaye ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akiongea na vyombo vya habari mapema leo kuhusiana na mkutano  wa 34 wa jukwaa la Mabunge ya Nchi wanachama wa jumuiya  ya maendeleo kusini mwa Afrika unaotarajiwa kufunguliwa na Makamu wa Raisi dkt Gharib Bilali mapema jumapili ijayo.

Aidha Makinda alisema kuwa kuongezeka kwa wabunge wanawake katika mabunge ya SADC kunatokana na juhudi mablimbali ambazo zinafanywa na jumuiya hiyo hali ambayo nayo imefanya mabadiliko makubwa sana kwenye baadhi ya nchi.

Alisema kuwa pamoja na ongezeko kubwa la idadi ya wabunge wanawake katika jumuiya hiyo lakini kwa Tanzania bado baadhi ya wanawake wanauoga na hofu ya kushiriki katika chaguzi kuu jambo ambalo wanatakiwa kulipinga.

"hapa tunaona kuwa hii idadi ya wanawake ni kubwa katika jumuiya hii ya SADC lakini kupitia ongezeko hili ni muhimu sana kwa wanawake wa Tanzania nao wakahakikisha kuwa wanajitokeza kwenye chaguzi mbalimbali na kushiriki kwani uwezo wa wao kuwa wabunge upo na wasiogoope wala kujiwekea udhaifu wa changamoto”aliongeza Makinda

Wakati huo huo alidai kuwa wanawake wa Tanzania hawapaswi kukatishana tamaa wao kwa wao na badala yake wanatakiwa kupena moyo hasa pale wagombea wanawake wanapokutana na changamoto kubwa ambazo wakati mwingine zinasababisha baadhi yao kukimbia nafasi za uongozi

Awali akiongelea mkutano huo wa 34 alisema kuwa Nchi ya Tanzania imepewa nafasi ya kuwa mwenyeji mkuu wa mkutano huo ambao utaweza kuwashirikisha viongozi wa Mabunge mbalimbali kutoka SADC na hivyo kupitia mkutano huo wataweza lkujadili mambo mbalimbali

Makinda alisema kuwa mkutano huo utaaangalia vitu muhimu kwa nchi wananchama kama vile  vigezo vya kusimamia na kutathimini mwenendo wa chaguzi za nchi wanachama wa jumuiya hiyo.

“Kauli mbiu ya mkutano huu ni  vigezo vya kuendesha na kutathimini chaguzi kwa nchi za kusini  mwa Afrika hivyo basi hapa tutaweza kuangalia na kukagua hilo hivyo tutaweza kupata hata majibu ambayo yatasaidia nchi zetu”aliongeza Makinda.

MWISHO

WAFADHILI KUTOKA UJERUMANI WATOA MSAADA WA VITABU WENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 9


MERU

WAFADHILI kutoka Ujerumani wamefanikiwa kutoa msaada wa vitabu venye thamani ya Milioni tisa kwa shule ya sekondari Leguruki iliopo Wilayani Meru mkoani Arusha kwa lengo la kuongeza ufanisi wa elimu zaidi kwenye shule hiyo.

Akiongea na wanafunzi shuleni hapo mapema jana mara baada ya kupokea msaada huo Mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Arusha John Palangyo alisema kuwa msaada huo utasaidia sana shule hiyo ya sekondari ambayo pia ipo chini ya Chama cha mapinduzi.

Palangyo alisema kuwa wafadhili hao wameamua kutoa msaada huo wa vitabu venye thamani ya milioni tisa lakini ni wajibu wa wanafunzi kuhakikisha kuwa wanavisoma na kuvifanyia kazi vitabu hivyo kwani vina mitaala ya nchi ya Tanzania

Pia alsiema kuwa kama wanafaunzi wa shule ya sekondario yoyote ile hapa nchini watakuwa na tabia ya kujisomea vitabu mbalimbali basi watachangia kwa kiwango kikubwa uelewa tofauti na sasa ambapo bado wapo wanafunzi wanaosoma kwa kufundishwa na walimu pekee.

Alibainisha kuwa kuna umuhimu mkubwa sana wa walimu wenyewe kuhakikisha kuwa wanawasisitiza wanafunzi kujisomea vitabu na kuachana na tabia ya kujidanganya kuwa hata wasiposoma watakuwa na maisha mazuri tena yenye mvuto wa hali ya juu jambo ambalo nalo linachangia sana kuongeza idadi ya wanaofeli katika shule za Sekondari pamoja na Vyuo vikuu hapa nchini

“mimi napenda kuwaambia kuwa msije kuona kuwa watu wana maisha mazuri mkadhani kuwa hawakujituma kusoma vizuri shuleni ni lazima kama mnataka maisha mazuri basi mjitume kusoma kwa bidii lakini pia msikubali kujiwekea fikra ambazo zinawapotosha kwani hizo ndizo zinazochangia ninyi mje kuwa na  maisha mabaya hapo baadae”aliongeza Palangyo

Katika hatua nyingine aliwataka hata walimu kuwatengenezea wanafunzi mazingira mazuri  na kuwapa motisha wanafunzi  hasa kwenye suala zima la usomaji wa vitabu kwani kwa kufanya hivyo kutaweza kuruhusu walio wengi kupenda kujisomea vitabu.

Awali mkuu wa shule hiyo ya Leguruki Emanuel Loi alisema kuwa msaada huo wa Vitabu umekuwa na tija kubwa sana shuleni hapo kwani hapo awali shule nzima ilikuwa na vitabu 52 na sasa wameweza kufanikiwa kupata vitabu zaidi ya elfu jambo ambalo litaweza kuwanufaisha wanafunzi shuleni hapo

Alimaliiza kwa kusema kuwa hata wazazi nao wana jukumu kubwa sana la kuhakikisha shule za sekondari zinakuwa na Vitabu vya kutosha ili kuweza kuharakisha maendeleo ya elimu

MSIWAACHIE WATOTO UHURU WA UTANDAWAZI NDIO CHANZO CHA KUFELI


Na gadness, Arusha

IMEELEZWA kuwa tabia ya wazazi kuwaachia watoto uhuru wa utandawazi hasa simu za mikononi kwa muda mrefu ndio chanzo kikubwa cha mdonodko wa elimu kwa nchi ya Tanzania kwani kwa sasa wapo baadhi ya wanafunzi ambao wanatumia muda mrefu sana kwenye utandawazi kuliko kwenye elimu

Kwa sasa hata mitandao ya kijamii ambayo ipo inatumiwa wakati mwingine vibaya na wanafunzi hali ambayo wazazi wanatakiwa kuchukulia tahadhari tena kwa haraka sana.

Hayo yameelezwa na Askofu Erick Mukwenda wakati akiongea na wazazi pamoja na walezi wa wanafunzi wa darasa la saba kwenye shule ya Maranatha iliopo jijini Arusha mapema jana katika maafali ya sita ya shule hiyo.

Askofu huyo alisema kuwa maana halisi ya utandawazi wakati mwingine imegeuzwa kabisa na wanafunzi na hivyo wengi wanadhubutu kuwekeza huko kuliko kuwekeza zaidi kwenye masomo jambo ambalo ni hatari sana

Alisema kuwa ili kuikwepesha jamii na tabia hiyo ni lazima kwanza wazazi waangalie suala hilo kwa mapana zaidi kwani wakati mwingine  watawakemea watoto baasi wataogopa na hawatajihusisha sana na mitandao hiyo au utandawazi

Pia aliongeza nao wazazi wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanaepukana na tabia ya kufikiria zaidi ada kuliko kufikiria malezi ya watoto kwani kwa sasa walimu pekee ndio wanaoachia suala zima la malezi jambo ambalo wakati mwingine linakuwa gumu sana

“kama tunataka maendeleo ya elimu kwa nchi ya Tanzania ni lazima kwanza tuhakikishe kuwa tunashirikiana kwenye malezi kwani malezi ya wanafunzi sio ada bali hata maadili hivyo basi wazazi sasa mnatakiwa kubadilika”aliongeza Askofu huyo

Katika hatua nyingine aliwataka wazazi pia kuwapa elimu wanafunzi juu ya matumizi ya simu za mkononi lakini pia kuachana na tabia ya kuwapa simu pindi wanapokuwa mashuleni kwani pia jambo hilo pia linachangia sana wanafunzi kuwazia simu kuliko  masomo.

MWISHO

SERIKALI YATAKIWA KUBORESHA MAZINGIRA YA WAFUGAJI ILI WASIKONDE WAO NA MIFUGO YAO


|Serikali imetakiwa kuboresha mazingira ya wafugaji wan chi ya
Tanzania pamoja na miundombinu yake kwani kwa sasa wapo baadhi ya
wafugaji ambao hawanufaiki na ufugaji na badala yake wanakonda wao
pamoja na mifugo yao

Hayo yameelezwa Jijini hapa na Naibu waziri wa mawasiliano sayansi na
Teknolojia January Makamba wakati akiongea na wataalamu wa mifugo
Tanzania mapema jana kwenye mkutano wa 36 unaondelea jijini hapa.

Makamba alisema kuwa inaskitisha kuona kuwa wafugaji na mifugo yao
imekondeana kwa kuwa haina mazingira mazuri hivyo kuna umuhimu mkubwa
sana wa Serikali kuwekeza kwenye sekta hiyo ambayo bado inakabiliwa na
changamoto kubwa

Alisisitiza kuwa kama mazingira ya wafugaji wa Tanzania yataweza
kuboreshwa kwa asilimia 100 ni wazi kuwa hata mazao yanayotokana na
mifugo nayo yatakuwa ya hali ya juu sana hivyo kuruhusu kuweza kuingia
hata kwenye soko la dunia.

“katika nchi ya Tanzania wapo baadhi ya wafugaji ambao wanafuga
ilimradi waonekane nao wamefuga sasa hili si jambo jema ni muhimu sana
kwa Serikali kuweza kuboresha mazingira na miundombuni lakini pia
kuweza kuwapa misaada muhimu kwa ajili ya kuhimiza uzalishaji na
ufugaji bora zaidi”aliongeza Makamba

Pia alisema kuwa tabia ya kubaki na idadi ya mifugo hususani ngombe
kwenye takwimu za nchi bado haitoshi na wala haijengi bali Nchi
inatakiwa kuwa na takwimu nzuri sana za uzalishaji na ufugaji bora
kama ilivyo kwa nchi zilizoendelea katika sauala zima la mifugo.

Naye mwenyekiti wa chama cha wataalamu wa mifugo Tanzania Stella
Bitende alisema kuwa bado kuna umuhimu mkubwa sana wa Serikali
kuhakikisha kuwa hata wananchi wa Vijijini nao wanapata huduma za
wataalamu wa mifugo kwani idadi ya wataalumu hao(Maafisa Ugani)ni
ndogo sana ukilinganisha na uitaji

Bitende aliongeza kuwa kama Serikali itaweza kuongeza idadi ya
wataalumu wa ugani hasa katika maeneo hayo ya vijijini basi ufugaji
utaweza kuwanufaisha wananchi wengi sana tofauti na sasa ambapo katika
maeneo ya vijijini bado wanatumia mbinu na njia za zamani sana

Alimalizia kwa kusema kuwa pamoja na kuwa chama hicho kimeweza
kujipanga hasa katika masuala ya tafiti mbalimbali lakini bado zipo
changamoto kubwa kama vile nyenzo za uzalishaji ,ambazo zinawanyima
kufanikiwa katika uzalishaji kwenye sekta ya mifugo.

MWISHO

Wafanyakazi wa hoteli hawana ujuzi na elimu ya kutosha.


,Arusha.
IMEELEZWA kuwa asilimia kubwa ya watanzania wamekuwa  hawapati nafasi mbalimbali za ajira kwenye mahoteli kutokana na wengi wao kutokuwa na elimu  ya kutosha na hivyo kuchangia wageni kutoka nje ya nchi kupata ajira kwa urahisi .

Aidha hali hiyo imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa sana vijana wengi kukosa ajira katika mahoteli kutokana na wengi wao kutokuwa na elimu ya  vitendo na hivyo kuishia kutumia elimu ya darasani.

Hayo yalisemwa jana na  Meneja wa programu  wa shirikisho la vyama vya utalii Tanzania (TCT)  Fatma Mabrouk  alipokuwa akizungumza na wamiliki wa mahoteli jijini Arusha wakati wa kuutambulisha programu ya mafunzo  kazini ambayo itawanufaisha vijana wenye umri wa miaka 17-25.

Alisema kuwa, programu hiyo kwa sasa ipo katika hatua ya majaribio  kwa miaka miwili ambapo wameanzia jijini Dar es Saalamu kwa kuzungumza na wamiliki  wa  mahoteli kwa lengo la kuitambulisha programu hiyo ili waweze kuitumia kwa wafanyakazi  wao na kuongeza ufanisi na utendaji kazi zaidi.

Fatma aliongeza kuwa,programu hiyo itasaidia kuwaongezea wafanyakazi wa mahoteli ujuzi zaidi katika utendaji kazi wao kwani wengi wao hawana ujuzi  huo hali inayochangia wengi wao kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

‘kwa sasa hivi wengi wao wanajifunza masomo ya darasani kwa asilimia 70 huku makazini wakitumia asilimia 30 tu, hali ambayo inaadhiri utendaji kazi wao kwa kiasi kikubwa kutokana na kutumia muda mwingi darasani badala  ya makazini’alisema Fatma.
Naye Mkurugenzi mtendaji wa chama cha mahoteli  Tanzania(HAT) ,alisema kuwa,Lathifa Sykes alisema kuwa,baada ya muda majaribio kumalizika programu hiyo itapitishwa kuwa sheria na hatimaye kuweza kutumika katika vyuo mbalimbali vya utalii hapa nchini .

Sykes aliongeza kuwa,kwa sasa vyuo vingi vya utalii vimekuwa vikitoa elimu hiyo kwa njia tofauti tofauti na hivyo kupitia programu hii itasaidia kufundisha kitu kimoja kwa vyuo vyote na hivyo kuwawezesha wanafunzi hao kupata ujuzi unaohitajika katika soko la hoteli.

Alisema kuwa,programu hiyo inafadhiliwa na shirika la kazi duniani (ILO) ambapo lengo halisi ni kuhakikisha kuwa idadi ya wafanyakazi kwenye mahoteli inaongezeka .
Mwisho.

Tuesday, October 1, 2013

MBUNGE LEMA,AFUTIWA MASHITAKA





Na GLADNESS MUSHI, ARUSHA

Mahakama ya hakimu mkazi imefuta kesi iliyokuwa inamkabili mbunge wa jimbo la Arusha Goodbless Lema na kudai kuwa upande wa mashitaka hakuwa na nia ya kuendeleza kesi hiyo.

Aidha kesi hiyo iliyokuwa inamkabili mbunge huyo ilikuwa ni ya uchochezi  katika chuo cha uhasibu Arusha ambapo vurugu hizo zilisababisha chuo hicho kufungwa.

Pia kesi hiyo ilipangwa kuanza kusikilizwa leo  mbele ya Hakimu Devotha Msofe wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ili kuweza kuitolea ufafanuzi zaidi.

Hataivyio mara baada ya hakimu huyo pamoja na Jopo la mawakili kuingia mahakamani hapo, Wakili wa Serikali Elianenyi Njiro, aliiomba mahakama kesi hiyo ifutwe chini ya kifungu cha 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, kama ilivyorekebisha 2002.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa upande wa mashitaka uliona hauna haja wala tija ya kuendelea na kesi hiyo lakini pia ni vema kama kipengele cha sheria kikaangaliwa zaidi.

Pia mara baada ya ombi hilo mahakama iliridhia na kudai kuwa kuanzia sasa Mbunge huyo yupo huru kwa mujibu wa kifungu cha sheria.

Awali Akisoma maelezo ya awali Julai 10 mwaka huu mahakamani hapo, Wakili wa Serikali Elianenyi alidai Aprili 24 mwaka huu, Lema akiwa eneo la Freedom Square la IAA alifanya kosa la uchochezi wa kutenda kosa kinyume na Sheria ya Kanuni ya Adhabu.

Akifafanua shtaka hilo, Elianenyi, alidai kuwa Lema aliwaeleza wanafunzi wa chuo hicho ambao walikuwa wamekusanyika kufuatia kuuawa kwa mwenzao na watu wasiojulikana kuwa;

Upande wa mashtaka tayari ulikuwa umewaleta mashahidi watano ambao ni Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Arusha, Giles Mroto, Naibu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha, Faraji Kasidi, Inspekta wa Polisi Bernard Nyambalya, Jane Chibuga na Mwadili wa Wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha, John Joseph Nanyaro.

MWISHO

Sunday, September 29, 2013

mamlaka ya hifadhi ya ngororo yatoa msaada wa mahindi

                                                  


Wakazi wa eneo la mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro wakipokea chakula cha msaada kutoka kwa uongozi wa Ngorongoro Conservation Are Authority (NCAA) ikiwa ni agizo kutoka kwa waziri mkuu mizengo pinda.

Tani 7000 zimegawiwa kwa familia 20,000 za jamii ya wamasai wanaoishi katika hifadhi hiyo. Idadi ya watu ndani ya NCAA kwa sasa ni zaidi ya 87,000 na wote wakiwa na mahitaji makubwa ya chakula kwani hawaruhusiwi kulima ndani ya eneo la NCAA.

Hivi karibuni wamasai hao wamejukuta wakikumbwa na baa la njaa baada ya ukame ulioathirini eneo lao kwa miaka mitatu mfululizo kuteketeza mifigo ambayo hasa ndiyo tegemeo lao la maisha.

Ugawaji wa chakula umeanza katika kata ya Olbalbal na utaendelea kwenye maeneo mengine huku NCAA ikijiandaa kununua tani zingine 29,000 za mahindi kutoka wilayani Karatu kwa ajili ya kuongeza mgawo huo wa chakula. picha na mwandishi wetu



MUSWADA WA MAREKEBISHO YA KATIBA WATARAJIA KUKABIDHIWA KWA JK

MUSWADA wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Katiba wa mwaka 2013 uliopitishwa na Bunge hivi karibuni, unatarajiwa kukabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete, wiki ijayo. Taarifa zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vyake vilivyoko serikalini zimeeleza kuwa Rais Kikwete atakabidhiwa muswada huo mara atakaporejea nchini akitokea katika ziara yake ya nchi za Marekani na Canada.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, jana alilieleza gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani kuwa Muswada huo utawasilishwa kwa Rais Kikwete na Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilillah, baada ya kuuandaa vizuri na rais atauperuzi kabla ya kufikia uamuzi wa kuusaini au kutousaini.

Taarifa hizi zimepatikana siku chache baada ya kusambaa kwa tetesi zinazoeleza kuwa Rais Kikwete alikutana na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba na baadhi ya maofisa walio katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kujadili baadhi ya vipengele vilivyo kwenye Rasimu ya Katiba Mpya, ambavyo vimeibua mvutano.

Hata hivyo, Jaji Werema aliliambia gazeti hili kuwa hana taarifa ni lini Dk. Kashilillah ataupeleka muswada huo Ikulu na hata alipoulizwa kuhusu tetesi zilizosambaa miongoni mwa jamii kuwa Rais alikutana na baadhi ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba pamoja na wale wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kujadili mwenendo na mwelekeo wa rasimu hiyo, alisema hafahamu chochote.

“Muswada ukishatoka bungeni, kama umepitishwa huo haumhusu tena Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali, anakuwa nao Katibu wa Bunge. Yeye sasa anakuwa na kazi ya kuuweka vizuri, akikamilisha anauchukua na kuupeleka Ikulu kwa Rais kwa ajili ya kusaini.

“Yeye Rais akishapewa naye anauangalia, ukimpendeza anausaini, vinginevyo hausaini anaurudisha. Sasa hivi sasa anao Katibu wa Bunge, jua kuwa anayejua kama umesaini au hapana ni yeye na rais tu, wengine wote tunasubiri taarifa ya Katibu wa Bunge. Hayo mengine ya ataupeleka kwa njia gani na lini siyajui,” alisema Jaji Werema.

Taarifa zilizopatikana kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, zimeeleza kuwa kuna wasiwasi umetanda iwapo Rais atasaini muswada kwa sababu Tume ya Jaji Warioba bado haijampelekea rasimu ya pili ya Katiba, ambayo ndiyo hutoa mwelekeo wa kuitishwa kwa Bunge la Katiba.

Mmoja wa maofisa wa juu wa wizara hiyo aliyezungumza na gazeti hili kwa sharti la kutotajwa jina lake, ameeleza kuwa mvutano ulioibuka baada ya Tume ya Jaji Warioba kutangaza rasimu ya kwanza ya Katiba Mpya unaweza kuchelewesha kutolewa kwa rasimu ya pili ambayo ni lazima Rais akabidhiwe na aipitie, ndiyo hatua ya kuitwa kwa Bunge itakapofuata.

Alisema, kwa sasa hali ni ya wasiwasi kwa sababu ipo hofu kuwa rais anaweza asisaini muswada huo, bali atakachofanya ni kuandika dokezo litakalokuwa na sababu za kutoweka sahihi yake kwenye muswada kisha ataurejesha kwa Katibu wa Bunge kwa ajili ya kuupeleka tena bungeni kujadiliwa.

“Na hii ni kwa sababu Bunge la Katiba haliwezi kuitishwa bila Tume ya Jaji Warioba kupeleka rasimu ya pili ya Katiba kwa Rais, na yapo mashaka kuwa hatapeleka kwa sasa kutokana na mwenendo wa mambo ulivyo.

“Sasa Jaji Warioba asipopeleka rasimu ya pili ina maana hata Bunge la Katiba halitakuwepo,” alisema.

Katibu wa Bunge, Dk. Kashilillah jana hakuweza kupatikana kuzungumzia suala hilo, baada ya simu yake ya kiganjani kutopatikana mara kadhaa alipopigiwa, lakini duru za habari kutoka Ofisi ya Bunge zimedokeza kuwa anatarajiwa kuuwasilisha muswada huo kwa Rais Kikwete siku ya Jumatano, Oktoba 2, 2013.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Dk. Kashilillah amekwishakamilisha maandalizi ya muswada na sasa anamsubiri rais arejee nchini ili amkabidhi.

Imeelezwa kuwa hatua ya Rais Kikwete ya kutosaini muswada huo utakuwa ni mtego kwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walioupitisha kwa sababu watalazimika kukubaliana na mabadiliko yanayoshinikizwa na makundi mbalimbali ya jamii, ambayo yanadai kuwepo kwa kasoro ndani ya muswada.

Mabingwa wa mambo ya kibunge ambao wamekuwa wakizungumza na gazeti kwa nyakati tofauti, huku wakisisitiza majina yao kuhifadhiwa kwa kile wanachoeleza kuwa suala la Rasimu ya Katiba sasa ni nyeti, wameeleza kuwa uamuzi wa Rais Kikwete ndio utakaowaongoza wabunge wa CCM wanachopaswa kufanya na iwapo watapingana nao, ipo hatari ya Bunge kuvunjwa.

Kwa mujibu wa kanuni na taratibu za Bunge, iwapo Rais Kikwete hatasaini muswada huo na kuurejesha bungeni na iwapo wabunge nao wataupitisha tena bila kuufanyia marekebisho, Rais atalivunja Bunge.