Thursday, May 29, 2014

ILBORU YADAI KILICHOSABABISHA MIGOMO YA WANAFUNZI MARA KWA MARA NI WANASIASA OVYO


UONGOZI wa Shule ya Sekondari Ilboru iliopo Jijini hapa umeweka utaratibu maalumu wa kuwakataa wanasisasa shuleni hapo kwani tafiti mbalimbali zimeonesha kuwa wapo baadhi ya wanasiasa ambao wanatumia kofia zao za siasa na kuwavuruga wanafunzi
Hataivyo miezi michache iliopo shule hiyo ilipata misukosuko kutokana na migomo mbalimbali ambayo ilifanywa na wanafunzi huku vichocheo vikubwa vikiwa ni wanasisasa wa Jiji la Arusha ambao walikuwa wanataka wanafunzi hao waingine kwenye mifumo ya vyama vya kisiasa.
Akiongea na Gazeti hili mapema jana mkuu wa shule hiyo ya Ilboru Julius Shulha alisema kuwa kuanzia sasa uongozi wa shule hiyo umeweka mikakati ya kuwakataa wanasiasa kuwatumia wanafunzi hao.
"unajua kuwa migogoro ambayo ilionekana shuleni hapani kutokana na wanasiasa na kuanzia sasa tumewakataa na hatutataka waje ili wawavuruge wanafunzi wetu tena"aliongeza Shulha
Alidai kuwa hata hao wanasiasa ambao wanatumia mwanya wao kwa ajili ya kuweza kuwayumbisha wanafunzi wanatakiwa waache mara moja kwani wanapaswa kujua nakutambua kuwa wao tayari wana mwanagaza wa maisha ila wanafunzi hao badi hawana mwangaza wa kimaisha.
"unakuta mwana siasa ana taaluma lakini anaajira yake tayari lakini anamuweka mwanafunzi huyu katika kundi lake na akifukuzwa hapa anaanza tena kutangatanga kwanini tusiwaache wanafunzi wakasoma alafu badae ndio wakajiingiza kwenye siasa lakini wakiwa tayari na elimu yao tunabdidi sisi watanzania kuanzia sasa tubadilike tuwaache wanafunzi wajisomee"aliongeza Shulha.
Kutokana na hali hiyo ya wanasiasa kuyumbisha shule hiyo alisema kuwa mpaka sasa wameshachukuatahadhari kubwa sana ya kuweza kuwasaidia wanafunzi hao ikiwa ni pamoja na kuwaambia madhara ambayo yanaweza kujitokeza iwapo watajihusisha na siasa pindi wanapokuwa mashuleni
Alimalizia kwa kuwataka hata walimu wa shule nyingine nazo kuhakikisha kuwa wanapingana na siasa ambazo mpaka sasa zinaletwa mashuleni kwani hali hiyo ndiyo chanzo kikubwa sana cha wanafunzi kuingia kwenye migogoro na migomo ya kila siku.
MWISHO

SERIKALI YAOMBWA KUWAPATIA BIMA WATOTO

 NA JAMES STANLEY ARUSHA
SERIKALI  imeombwa kuwapatia Bima ya Afya watoto
wanolelewa katika kituo cha kulelea watoto  yatima
cha Samartan Villege,kilichoko Moshono,Mkoa ni Aru
sha.
   Mratibu wa kituo hicho,   Father Josephat Mumany,
akizungumza hivi karibuni wakati wakutoa taarifa fupi
yakituo hicho bkwa viongozi   na wanachama wa kiku
ndu cha uamsho cha Oldadai,waliotembelea kituo hich
o kwa ajili ya kutoa misaada mbalimbali,Alisema   bima
hizo zitwapunguzia adha watoto hao wanapougua.
   Alisema kutokana na watoto hao kutokuwa na Bima
ya Afya,hali hiyo imekuwa ikiupa shida kubwa viongozi
wa kituo hicho,pale unapopataka kuwapeleka  watoto
hao hospitalini.

  Father Mmanyi,alisema hiyo ni changamoto    kubwa
kwao,kutokana na kituo kukabiliwa na  uhabawafedha,
hali amabayo pia huwafanya watotowanaougua kukaa
na maradhi yao kwa muda mrefu pasipo kupata  matib
abu.
  Katika hatua nyingine  Mmanyi alisema watoto wanao
lelewa katika kituo hicho wanapelekwa na serikali baada
ya kuokotwa mitaani,kutokana na kutupwa na    wazazi
wao baada ya kujifungua.
  ''Watoto hawa wanaokotwa katika mazingira  magumu 
wengine wanavunjwa miguu na wazazi wao,    wengine
wanakutwa wametoboleatobolewa na wazazi wao kabla
ya kuwatupa,Inasikitisha sana unapoona mazingira amba
yo watoto hawa walikotoka.''Alisema
   Pamoja na serikali,aliitaka jamii na mashitika mbalimbali
ya kitaifa na kimataifa,kukisaidia kituo hicho kwa hali  na
mali,ili kiweze kumudu malezi ya watoto hao.Hivi sasa.ali
sema wana miradi waliyopewa na wahisani inayowasaidia
katika mambo madogomadogo.Nayo ni pamoja na bwawa
la samaki,shamba la mahindi,pamoja na migomba.
  Mweka Hazina wa kikundi cha Uamsho,kilichowatembele
a watoto hao,Be Marry Mayagila,Alisema wanaguswa  na
amahitaji ya watoto hao na kwamba kwa kuwa wao ni w
anawake wenye moyo wa huruma,ndiyo maana wameme
amua kuwatembea na kuwapatia misaada ya vyakula.

   Alitoa wito kwa wanawake,na vikundi mbalimbali kuwa
hurumia watoto hao kwa kuwapa misaada      mbalimbali
kwani hawawajui wazzi wao,ili nao wajione swa na wato
to wengine

Tuesday, May 27, 2014

HOSPITALI YA MT MERU ARUSHA YAENDELEA KUKABILIWA NA CHANGAMOTO

HOSPITALI ya Mkoa  wa Arusha, Mount Meru, inakabiliwa na upungufu wa
shuka 300 na blanketi 200, kutokana na ongezeko kubwa la wagonjwa kila
siku.

Akizungumzia upungufu huo jana hospitalini hapo, wakati akipokea
msaada wa shuka nyeupe 100 na blanketi 30 toka kwa Kanisa la Calvary
Temple la Kilombero Jijini Arusha,ambalo linaadhimisha miaka 75 tangu
lianzishwe, Mganga Mfawidi wa Hospitali hiyo, Dk. Josiah Mlay, alisema
upungufu ni mkubwa wa vitu hivyo ukizingatia wanakwenda kipindi cha
baridi kali.

Alisema kuwa shuka na blanketi walizonazo kwa sasa nyingi zimechakaa
kutokana na kemikali wanazotumia kufulia wakati zinapochafuka wodini,
hivyo wanahitaji shuka na blanketi zingine haraka kabla ya msimu wa
baridi haujaanza.

"Kwa nyie kutuletea hivi vitu tunashukuru sana na mtabarikiwa, kwani
bado tuna upungufu wa itu hivi mkubwa na tunaomba wadau wengine
wajitokeze kutusaidia kabla ya msimu wa baridi haujaanza,"alisema.

Dk. Mlay alisema kwa sasa hospitali hiyo inachangamoto kubwa ya
ongezeko la wagonjwa na huku mahitaji yao yakipungua, kutokana na
wingi wao, hivyo wanahitaji wasamaria wema wajitokeze kuwasaidia.
Mahitaji mengine wanayohitaji hospitalini hapo alitaja kuwa pamoja na
vifaa vya maabara navyo ni vichache,hivyo wanaomba msaada kwa
wasamaria wema na sio kuiachia serikali ambayo inamajukumu mengi.
Kwa upande wake Emmanuel Mbwiga ambaye ni Mzee wa  Kanisa la Calvary

Temple la Kilombero Jijini Arusha, akitoa msaada huo alisema mbali na
msaada huo pia kupitia vituo vyao mbalimbali wametoa msaada kwenye
vituo vya yatima vya Huruma Kwamurombo,Monduli,Esso.

Pia misaada mingine imetolewa shule za msingi Mwangaza, Olsinyai
Sombetini na Ngarenaro, lengo kubwa kusaidia watu wenye shida ili
wapate faraja nao katika kuadhimisha kilele cha kanisa hilo
kitakachofanyika Kitaifa Mbeya Julai mwaka huu.

Mbwiga alisema vitu walivyotoa maeneo hayo  ni Sabuni, ndoo za mafuta,
mchele, nguo, mahindi,daftari,soksi na vitu vingine vingi, ambavyo
vyote vina jumla ya shilingi milioni 3.

 Hata hivyo alitoa wito kwa watu wenye mapenzi mema kujitokeza
kusaidia hospitali hiyo na maeneo yenye uhitaji kama vitruo vya yatima
na shuleni, ili wabarikiwe zaidi.
Mwisho

UROHO, UPENDELEO WA UTOAJI WA MISAADA KUTOKA KWA WAFADHILI CHANZO KIKUBWA CHA WAFADHILI KUTOKOMEA GIZANI



NaBety Alex, Arusha

IMEELEZWA kuwa Tabia ya uroho na upendeleo unaofanywa na baadhi ya
Viongozi wa Dini, Serikali na Jamii kwa ujumla kwenye ugawaji wa
misaada kutoka kwa wafadhili ndio chanzo kikubwa sana cha Watoto wenye
mahitaji muhimu kutelekezwa na wafadhili.

Hataivyo pia tabia hizo zimekuwa chanzo na kisingizo kikubwa sana cha
makundi maalumu kuweza kusahaulika na hivyo kujikuta wakiwa
wanakabiliwa na hali ngumu sana ya maisha ikiwemo ukosefu wa mahitaji
muhimu.

Hayo yameelezwa na Mchungaji Nakembetwa Shakademasi kutoka katika
kanisa la T A G Kindness Chrstian Centre(KCC)lilopo Ungalmtd wakati
akikabidhi msaada wa ngyo kwa watoto 50 wa eeno hilo la ungalmtd
mapema jana.

Shakademasi alisema kuwa tabia hiyo kwa sasa imejaa kwa viongozi ambao
wapo kwenye sekta mbalimbali hali ambayo inakimbiza  wafadhili wa
ndani na hata wa nje ya nchi.

Alifafanua kuwa, jamii haipaswi kuwa na uroho dhidi ya msaada wowote
ule unaelekezwa kwehnye kundi maalumu wakiwemo watoto bali jamii
inapaswa kuwaunga mkono wafadhili hata kama wametoa vitu ambavyo ni
vizuri kuliko vile vya familia ambazo zina uwezo.

“katika miaka ya sasa inashangaza sana wafadhili wanaogopa kutoa
msaada kwa jamii kwa kuhofia kuchakachuliwa wakati watoto hasa wale
ambao wanatokea mazingira magumu wanakabiliwa na changamoto lukuki za
kimaisha , tunapswa kuwa waminifu hata kama misaada ni mizuri kuliko
ile ambayo tunayo”aliongeza

Katika hatua nyingine alisema kuwa ili wafadhili waweze kuongezeka
hapa nchini misaada inatakiwa kuwafikia walengwa ambao wamekusudiwa
jambo ambalo litaweza kuokoa maisha ya watu walioko kwenye makunid
maalumu.

Pia Mgeni Rasmi kwenye  Hafla hiyo Mchungaji Peter Kitila alisema kuwa
nao watanzania wana uwezo mkubwa wa kuwa wafadhili wa ndani,na kuacha
kutegemea ufadhili kutoka nje ya nchi.

Kitila alidai kuwa kama kila mtanzania akijitolea kuwasaidia watu
wenye maitaji maalumu basi umaskini ndani ya nchi utaweza kupungua kwa
kiwango kikubwa sana tofauti na sasa ambapo wengi bado hawana hamasa
ya kusaidia makundi maalumu yaliopo kwenye jamii.

MWISHO

Wanafunzi 125 kushiriki Riadha manyara



Wanafunzi 125 wa michezo ya riadha, mpira wa miguu, pete na wavu, wa shule za sekondari Wilaya ya Hanang’ wanatarajia kushiriki mashindano ya umoja wa michezo ya shule za sekondari (Umiseta) Mkoani Manyara.


Akizungumza na waandishi wa habari jana, mratibu wa umiseta wilayani humo, Caroline Marshali alisema wavulana na wasichana wa shule tofauti za sekondari wanashiriki michezo mbalimbali ya kutafuta wawakilishi wa wilaya hiyo.

Marshali alisema wanafunzi hao wa shule za sekondari watawakilisha wilaya hiyo kwenye kuruka juu, chini, kutupa mkuki, sahani, tufe, mbio ndefu na za mita 100, 200, 400, 800, 1,500 na mbio ndefu za marathoni.

“Pia kutakuwa na timu za mpira wa miguu za wasichana na wavulana, mpira wa wavu na mpira wa pete na wachezaji wetu wamejiandaa ipasavyo kwenye mashindano haya ili kuipa sifa wilaya yetu,” alisema.

Naye, Mwenyekiti wa umoja wa wakuu wa shule za sekondari (Tahosa) wilayani Hanang’ John Malley alisema wamewaandaa ipasavyo vijana wao ili washiriki kikamilifu michezo hiyo na kuleta ushindi katika wilaya yao.

“Pamoja na hayo tunamshukuru Mbunge wa jimbo letu Mary Nagu kwa kutuunga mkono kwenye maandalizi haya ya kwenda kushiriki mashindano ya mkoa kwa ikiwemo kutupa vyakula,” alisema Malley.

Nao baadhi ya wachezaji wa mpira wa miguu, wavu na kuruka juu, Nobert Aushak, Judith Mkilanya na Anna Aney walisema kupitia michezo wanajijenga kisaikolojia ili wafanikiwe katika masomo yao kwani hawana hofu ya mitihani.

Walidai kuwa zaidi kufahamiana na watu mbalimbali kupitia michezo, pia wanajenga afya zao kwa kuwa wakakamavu na wanajiamini zaidi pindi wakiwa masomoni hivyo wanatarajia kufanikiwa pia kimasomo.

MWISHO.

UKOSEFU WA UPENDO KWA WALIMU CHANZO CHA UTORO MASHULENI

UKOSEFU WA UPENDO KWA WALIMU CHANZO CHA UTORO MASHULENI

Arusha


IMEELEZWA kuwa ili wanafunzi wa shule mbalimbali hapa nchini waweze kupenda shule na kuthamini masomo walimu wanatakiwa kuwa na lugha pamoja na malezi yenye upendo wa hali ya juu tofauti na sasa ambapo zipo baadhi ya shule ambazo zina walimu wasiokuwa na upendo.
Aidha kwa sasa wanafunzi wengi watoro wanakwepa shule kwa kuwa wamekosa matumaini ya upendo toka kwa walimu wao hivyo basi walimu wanapaswa kubadilika.
hayo yameelezwa na Kanali Mstaafu John Mongi wakati akizindua rasmi kamati ya bodi ya shule ya St Benedict Meliyo Primary  iliopo maeneo ya Sekei jijini hapa mapema jana.
kanali Mongi alisema kuwa neno upendo linapaswa kutumika sana ipasavyo na walimu, wakuu wa bodi pamoja na wazazi na kama litaweza kutumika ipasavyo basi litachangia sana hamasa ya elimu hapa nchini .

aliendelea kwa kusema kuwa kwa kukosa upendo kwa baadhi ya walimu kumekuwa chanzo kikubwa sana cha wanafunzi kuona shule kama ni uwanja wa vita na sababu hiyo hiyo pia imechangia sana hata utoro.
"tujifunze kwenye hizi shule ambazo zinaongoza kitaifa jinsi ambavyo walimu, bodi za shule zinavyowapenda wanafunzi,kwa hali hiyo basi mimi nasisiiza kuwa ili elimu iweze kufika katika kiwango cha juu lazima kwanza walimu wawe na upendo na wanafunzi ambao wanawafundisha"aliongeza Kanali Mongi.
hataivyo aliwataka nao walimu mbali na kuhamasiaha upendo  kwa wanafuzni ili kuweza kuepukana na majanga ya utoro shuleni lakini pia muda ambao wanakuwa na wanafunzi wao wahakikishe kuwa wanawaambia juu ya madhara yaliopo hapa nchini kama vile mdondoko wa maadili ili kuweza kuokoa kizazi cha vijana ambacho kwa sasa kinaangamia.
Awali Mkurugenzi mtendaji wa shule hiyo Joseph Laiser alisema kuwa ili kufanya elimu hapa nchini iweze kufikia katika kiwango ambacho kinaitajika tayari shule hiyo imeweka mikakati ya kuwapa semina wazazi , pamoja na viongozi mbalimbali wa shule hiyo .
Laiser alifafanua kuwa kwa kuwapa semina wazazi, walezi, na viongozi wa shule kutaweza kusaidia walengwa wa watoto hao kujua majukumu yao kwani kwa sasa shule nyingi zinashindwa kutekeleza majukumu yake kwa kuwa wanakwamishwa na vitu mbalimbali likiwemo suala zima la wazazi pamoja na walezi .
MWISHO