Thursday, September 20, 2012

KIFO CHA BABA MZAZI WA TUNDU LISU,NA ALUTE MUGWAI AMBAYE NI MAWAKILI KATIKA KESI YA LEMA CHASABABISHA KESI KUHARISHWA


KIFO CHA BABA MZAZI WA TUNDU LISU,NA ALUTE MUGWAI AMBAYE NI MAWAKILI KATIKA KESI YA LEMA CHASABABISHA KESI KUHARISHWA

Kesi ya Rufaa iliyokuwa inamkabili Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Bw Goodbless Lema imeharishwa mpaka October 2 kutokana na Mawakili wawili ambao ni Alute Mugwai na Tundu Lisu kufiiwa na baba yao mzazi na mazishi kufanyika Kesho kutwa

Kesi hiyo ya Rufaa ambayo inaendeshwa na Majaji watatu ambao ni Othaman Chande,Natalia Kimaro,na Salum Masati pia  mahakama imeamuru baadhi ya walengwa kuhakikisha kuwa wanakamilisha taratibu zote ili kesi hiyo iweze kusikilizwa

Aidha ilidaiwa mahakani hapo mbele ya Jaji Mkuu Othaman Chande ambaye alitoa ufafanuzi huo kwa niaba ya majaji wenzake alidai kuwa kesi hiyo itasikilizwa October 2 ambapo Wajibu rufaa nao wanatakiwa kuhakikisha kuwa walete hoja zao zote ili kuraisisha masuala mbalimbali ndani ya kesi hiyo ya Mbunge wa Arusha Mjini

“hawa mawakili ambao ni ndugu na wapo pande zote mbili ni ndugu na kwa maana hiyo wamempoteza baba yao mzazi kwa hali hiyo watamzika siku ya Jumamosi lakini pamoja na hayo yote taratibu mbalimbali nazo zinazohusu hii kesi zinatakiwa kuboreshwa na kuwasilishwa hapa October 2 mwaka huu nah ii ni kwa wahusika wote”aliongeza Jaji Chande

Hataivyo Jaji huyo aliamuru mahakama kuhakikisha kuwa Mahakama ihakikishe kuwa wajibu rufaa wawasilishe hoja zao za awali kabla ya September  26 mwaka huu,huku naye muomba Rufaa na Mwanasheria wa Serikali naye anatakiwa kuhakikisha kuwa wanaleta majibu kabla ya September 29.

Katika hatua nyingine ilidaiwa mahakamani hapo naye Mwanasheria  wa upande wa walamikaji wa naye alete hoja zake kuhusu rufaa kabla ya September 28 ili kuweza kuruhusu  kesi hiyo kusikilizwa kwa uraisi hapo October 2 ndani ya Mahakama hiyo.

Hataivyo kwa upande wa mawakili wa Serikali atawakilishwa na wakili Timothy Vitalisi ambapo kwa upande wa Majaji wataongozwa na Jaji Othmani  Chande

Katika hatua nyingine mara baada ya Kesi hiyo kuharishwa mamia ya wananchi wa mji wa Arusha walilazimika kutembea miguu na kufunga baaadhi ya barabarani za mji wa Arusha kutoka katika eneo hilo la mahakama hadi kufikia katika Ofisi za chama hicho zilizopo katika eneo la Makao Mapya.

MWISHO

No comments:

Post a Comment