Friday, November 3, 2017

jamii yatakiwa kuwakumbuka wajane

Jamii kwa kushirikiana na viongozi mbali mbali wameombwa kujitoa kwa hali na mali  kumsaidia mjane aliyeunguliwa na nyumba yake katika kitongoji cha kanisani kata ya  Imbaseny katika halmashauri ya Meru ili kumwezesha aweze kurudia katika hali yake ya kawaida.

Wito huo umetolewa na mhadhiri mwandamizi chuo  kikuu cha  tumaini makumira ambae pia ni mjumbe wa mkutqno mkuu  ccm taifa dr danieli mirisho palangyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari  mara baada ya kukabidhi misaada ya mabati na mchele kwa mjane huyo aliyeunguliwa na nyumba yake hivi karibuni  katika kitongoji cha imbaseny .

Dr Palangyo amesema kuwa kufuatia janga kubwa alilopata mjane huyo ambae aliunguliwa  na nyumba yake hivi karibuni kutokana na chanzo ambacho hadi sasa hakijajulikana jamii,na viongozi mbali mbali ndani ya wilaya ya arumeru wanapaswa kuungana kwa pamoja na jamaa wanaojitolea kumsaidia mjane huyo ili aweze kujengewa nyumba yake na kuweza kurudi katika hali yake kwani kwa sasa anaishi mazingira magumu sana.

Amedai kuwa akiwa kama kiongozi amewiwa kufika kwa mjane huyo na kuweza kutoa bati 23   pamoja na mchele kg 25   kwani mama huyo pamoja na watoto wake wapo katika hali ngumu ambayo bila michango hataweza kurejea katika hali yake.

Akizungumza mara baada ya kupokea kwa misaada hiyo mjane huyo aliyetambulika kwa majina ya Maria Kimario mkazi wa imbaseny alisema kuwa nyumba yake iliungua tarehe 29 mwezi uliopita na kusababisha kupata hasara ya milioni 16 kwani vifaa vyote viliteketea kwa moto huo huku chanzo cha awali kikiwa bado hakijajulikana kwani alikuwa anatumia umeme unaotokana na Mobisol.

Aidha bi maria aliwaomba wadau mbali mbali kujitokeza na kumsaidia ili aweze kurejea katika hali yake kwani kwa sasa anaishi mazingira magumu pamoja na watoto wake huku akiwa hana chochote ikiwemo nguo,chakula ,na mahala pa kuishi

No comments:

Post a Comment