Monday, January 2, 2012

MORANI WA KIMASAI WAVUNJA NA KUHARIBU KANISA, FAMILIA TANO ZAKIMBIA MAKAZI YAO KWA KOSA LA KUFANYA TOHARA KISASA, NA KUSALI



Katika hali isiyokuwa ya kawaida Vijana wa kundi la Kimasai wajulikano kama ‘Morani” wameamia kanisa la T.AG. oljoro Jerusalem na kuvunja kanisa hilo kwa madai kuwa sala pamoja na vitendo pamoja na Imani ambazo wanazo baadhi ya waumini wa kanisa hilo zina haribu Mila na Desturi ya kabila hilo la wamasai.

Hali hiyo ilitokea wiki iliyopita ambapo morani hao walivamia kanisa hilo na kuharibu sanjari na kuwatafuta baadhi ya waumini wa kanisa kwa malengo ya kuwatembeza mitaani uchi pamoja na kuwatoza faini ya pesa na faini ya Ngombe dume kwa kosa la kuharibu Mila na Desturi ya Kimasai.

Akiongea kijijini hapa msimamizi wa Makanisa ya T.A.G katika maeneo hayo Mchungaji Simion Vomo alisema kuwa kutokana na imani za morani hao, kanisa limelazimika kuchukua hatua kali na za kisheria juu ya Vurugu ambazo zinafanywa  na watu hao

Mchungaji Vomo alieleza kuwa Morani hao wamekuwa wakifanya hivyo kwa kuhofia kuwa baadhi ya waumini ambao wanajua madhara ya kuabudu na kukumbatia mila anbazo zinamchafua Mungu hivyo wanaamua kuwafuata watumishi  na kisha kuwatembeza uchi mitaani

Alisema kuwa mpaka sasa familia kama tano zimelazimika kukimbia kijijini hapo kwa kuhofia usalama wa maisha yao na familia zao kwa kuwa Morani hao wameshatangaza vita dhidi yao ya kuwatembeza mitaani wakiwa uchi kama fundisho kwa baadhi ya watu ambao watakaondelea na sala sanjari na kufanya tohara kwa njia za kisasa zaidi.

“tunayoongea sasa ndugu mwandishi ni kwamba mpaka sasa familia kama tano zimekimbia makazi yao ya kudumu kwa kuwa wanahofu ya hawa morani na kisa kikubwa ni imani zao katika kuomba , kukataa hii mila ya kufanya tohara kwa njia za kienyeji sana, na kukataa kuabudu Mila za kimasai”alieleza mchungaji Vomo.


Pia alisema kuwa mara baada ya kanisa kuona hali kama hiyo walilazimika kutumia njia na busara za kisasa zaidi za kuweza kuwaelimisha Morani hao, lakini morani hao walionekana kukiuka makubaliano hayo na ndipo walipovamia kanisa hilo pamoja na kumkamata muumini mmoja ambaye alirejea kijjini hapo mara baada ya kuwepo kwa muafaka

Alibainisha kuwa Morani hao walifanikiwa kuvunja mlango kwa muumini huyo ambaye yeye anatuhumiwa kwa kosa la kufanya ibada na kukiuka mila hizo za kimasai  majira ya usiku wa saa sita ambapo ilikuwa ni December 30 na kumtembeza umbali mrefu ambapo alitembea kwa masaa kama sita  jambo ambalo si sahihi hata mbele za Mungu.

“fikiria hali ya usiku ilivyokuwa alafu unamtembeza mtu akiwa amevaa gunia kisa ni imani yake ambayo inatoka katika biblia kisha unadai fedha na Ngombe kweli hii ni halali tutahakikisha kuwa tunapambana na hili mpaka tukomeshe hili tatizo’alisema mchungaji Vomo.

Katika hatua nyingine msimamizi wa makanisa hayo alisema kuwa ni lazima sheria ichukue mkondo wake ili kukomesha hali kama hiyo ambayo kwa sasa imeonekana kukua sana ndani ya mkoa wa Arusha kwa kuwa baadhi ya Masai wanataka Tohara kwa njia ya Kienyeji sanjari na kupinga makanisa yenye kukataa imani hiyo.

Awali Familia ambazo zimekimbia kutokana na kutafutwa na Morani hao zilisema kuwa kamwe hawataweza kukubaliana na wanachokitaka na kudai Morani hao kwa kuwa Biblia haijaonesha sehemu za kuabudu mila na desuri kama zao.

“hata kitokee nini sisi hatubadilishi msimamo wetu na badala yake tutazidi kumtangaza yesu kuwa mshindi wetu na pia kila kinachofanyika kimbilio letu ni Biblia na wala sio maagano, Mila, na Desturi”zilisema Familia hizo.

Nao Morani ambao walizunguka Kanisa hilo December 31 walisema kuwa ili mambo yaende vema wakati wkisubiri upatanishi baina ya familia hizo tano na kanisa, wanataka Kanisa hilo la T.A.G Oljoro Jerusalem Lifungwe hali ambayo Msimamizi wa Makanisa hayo alikataa na kusema kuwa ibada na taratibu zake itaendelea kawaida na kamwe hawatasitisha  kwa kosa la Mila.

Nae Kaimu Kamanda wa polisi kwa mkoa wa Arusha Bw Akili Mpwapwa alisema kuwa bado wanaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo ambapo watakaohusika kufanya fujo, kuchukua mali za watu au kuharibu kama walivyo fanya watafikishwa mahakamani kwani hayo ni makosa ya jinai.

MWISHO 

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA

ARUSHA 

0758907891.

ASKOFU URIO-WAKRISTO MSIWATEGEMEE ZAIDI WATABIRI TEGEMEENI BIBLIA



Askofu Fitiaely Urio wa makanisa ya Pentekoste Gospel Assemblies church ya mjini hapa amewataka wakristo kuhakikisha kuwa wanatumia zaidi maono ya kibiblia na wala sio maono ya tabiri kutoka kwa watu wanaotabiri kwa kuwa tabiri hizo zinachangia sana wengi wa wakristo kushindwa kukua kiroho na kiimani

Askofu Urio aliyasema hayo wakati wa ibada maalumu ya kuombea mwaka 2012 iliyofanyika katika kanisa la Usa Magadini wilayani Meru mkoani hapa.

Hataivyo Askofu Urio alisema kuwa wakristo wanapswa kuhakikisha kuwa wanatumia zaidi karama mbalimbali ikiwemo karama ya Roho mtakatifu na kuachana na tabia ya kupendelea zaidi Tabiri ambazo zinalenga kuwakatisha moyo.

Alisema kuwa endapo kama watatumia zaidi biblia kama mwongozo kwa mwaka 2012 ni wazi kuwa wataweza kufikia malengo yao mbalimbali ambayo walijiwekea na hata kufanya mabadiliko mbalimbali ambayo yatakuwa na faida kwa jamii na vizazi vyao.

“jamani hakikisheni kuwa mnaacha tabia ya kufuatilia tabiri mbalimbali ambazo zinatolewa hapa nchini juu ya mambo ya mwaka jiulieze biblia inatabiri mema na wao wanatabiri mabaya sasa nini maana yake mkabidhi mungu mizigo yako yote na yeye ataitatua”alisema Askofu Urio

Pia alianisha kuwa mbali na kutegemea zaidi tabiri mbalimbali kutoka kwa wanatabiri pia wapo baadhi ya wakristo katika jamii ambao kamwe hawaridhiki na neema ya mungu ambayo wanapewa hata kama ni kidogo na badala yake wanaanza kutoa malalamiko na lawama mbalimbali.

Alisema kuwa tabia hiyo haimfurashi mungu kwa kuwa mungu ndiye anayetoa na hivyo mungu anaanagalia zaidi kiwango cha imani ambacho mtu anacho hivyo kila mwenye tabia hiyo anapaswa kuacha mara moja ili afungulie zaidi baraka na Mafanikio katika Maisha yake.

“hili si jambo jema hata kidogo mjue mungu anapenda sana kurudishiwa shukurani sasa wewe unapopata halafu hutoi shukurani manaake ni nini asiye shukuru kwa kidogo hata kikubwa hataweza kushukuru hivyo nawasihi hakikisheni kuwa hamuendekezi hii tabia kwani ni mbaya sana’aliongeza Askofu Urio.

Alihitimisha kwa kusema kuwa wanadamu hawapaswi kuangalia kushindwa kwao katika mambo mbalimbali ambayo yanawakabili bali hata katika furaha na shida wanatakiwa kumuita mungu kwa kuwa ndiye kimbilio la kila mtu.

MWISHO

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA
ARUSHA 

0758 9078 91

CHANGAMOTO ZA MWAKA 2011 ZISIWAFANYE MKATEE TAMAA-MCHUNGAJI VOMO



IMEELEZWA kuwa pamoja na nchi kukabiliwa na majanga na changamoto mbalimbali hasa kwa mwaka 2011 wakristo hawapaswi kukata tamaa juu ya changamoto hizo bali wanatakiwa kuangalia imani na maitaji ya Mungu Kwa mwanadamu ili aweze kupunguza na kuondoa changamoto hizo.

Hayo yameelezwa mjini hapa na mchungaji Simion Vomo wakati akiongea na waumini wa kanisa la T.A.G Chrstian all  nation church lilopo katika manispaa ya mji wa arusha mapema wiki hii.

Aidha mchungaji Vomo alisema kuwa katika mwaka 2011 mambo mengi sana yalijitokeza hali ambayo iliwapelekea baadhi ya waumini kukata tamaa lakini katika mwaka huu mpya wa 2012 wanapaswa kumuangalia mungu zaidi kuliko matatizo yao binasi.

Alibainisha kuwa hata katika matatizo mungu yupo na kwa hali hiyo kila mwanadamu anapaswa kuangalia mpango na mikakati mbalimbali ya mungu na kuachana na tabia ya kuona wameshindwa mbele ya Macho ya wanadamu

“maandiko yanasema kuwa mwanadamu ataona yameshindikana lakini Mungu hatashindwa na pale Mwanadamu anapoonekana kuwa ameshindwa ndipo mungu anapoonekana kuwa anaweza nawasihi sana tuangalie imani zetu kwa kuwa ndicho chanzo pekee cha kufanikiwa’alieleza Bw Vomo.

Awali alisema kuwa nao waliofanikiwa wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanatangaza zaidi utukufu wa mungu kuliko mafanikio yao kwa kuwa ndicho chanzo pekee cha kufanikiwa katika maitaji mbalimbali ambayo yanamzunguka mwanadamu wa leo.

Alibainisha kuwa endapo kama wataweza kufanya hivyo ni wazi kuwa mafanikio yatakuwa ni makubwa sana ukilinganisha na mafanikio ambayo hayana utukufu wowote hapa duniani.

“Mungu ana makusudi na kila mmoja wetu na kwa hali hiyo mungu anapswa kupewa utukufu kwa kila jambo hata kama ni dogo kwa kuwa yeye ndiye anayetutoa kutoka ushindi kwenda ushindi, na kwa maana hiyo hatupaswi kukata tama wala kuangalia masuala ya mambo ya hapa duniani tukasahau ya Mungu Wetu”alisema Mchungaji Vomo.


Alimalizia kwa kusema kuwa kwa wale ambao hawajafanikiwa kwa msimu wa mwaka uliopita wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanaongeza kiwango cha imani katika maisha yao kwa kuwa Pia Mungu anapenda na kuthamini zaidi Mtu mwenye Imani.

MWISHO 

CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA
ARUSHA 

O758907891

Sunday, January 1, 2012

WALAZIMIKA KUKIMBIA MAKAZI KISA SALA, NA TOHARA, MORANI WAHARIBU KANISA


Familia tano zenye watoto zaidi ya ishirini zimelazimika kukimbia makazi yao ya kudumu kwa kipindi cha wiki tano sasa kwa kuhofia kutembezwa uchi na kupigwa na vijana wa kabila la kimasai”Morani”mara baaada ya kufanya ibada sanjari na kufanya tohara kwa njia za kisasa zaidi.

Familia hizo zimelazamika kufanya hivyo kwa kuhofia maisha yao pamoja na maisha ya watoto wao ambapo kundi kubwa la vijana wa kimasai wanawatafuta kwa makosa ya kuharibu na kuvunja mila zao kwa njia ya Sala pamoja na Kufanya tohara Mahospitalini.

Hayo yametokea katika eneo la Oljoro Mkoani hapa ambapo kwa muda wa wiki tano familia hizo zimelazimika kukimbia makazi yao kwa kuhofia kutembezwa mitaani Uchi, pamoja na kupigwa kipigo kikali.

Akiongea na “Upako wa habari za ufalme”mmoja wa wanafamilia waliolazimika kukimbia nyumba zao kwa hofu ya kutembezwa mitaani Uchi Bw Korduni Wilson, alisema kuwa Morani hao wamekuwa wakifanya vibaya sana kwa kuwa mila wanazozitaka zina madhara sana.

Bw Korduni alieleza kuwa wameamua kufikia uamuzi huo wa kukimbia nyumba zao kwa kuwa wao tayari wameshajua na kufahamu madhara ya kufanya tohara kwa njia ya kienyeji sanjari na kuabudu mila ambazo Morani hao wanazitaka.

“kati ya hizi familia tano nyinginezo hazijakimbia kwa kuwa wamefanya tohara kwa watoto wao bali Morani hao wamekuwa wakidai kuwa wanaharibiwa mambo ya Kimila hasa pale wanaposali kwa maana hiyo wanakataa hata makanisa kwa kuhofia Matambiko, na Mila”aliongeza Bw Korduni.

Pia aliongeza kuwa mara baada ya Morani hao kuona kuwa Kanisa linakubali na kusisitiza waumini wake kufanya Tohara kwa njia ya kisasa sanjari na kukataa Mila ambazo zina madhara kwa Mtanzania Morani hao waliktaa amri hiyo na kuvunja Kanisa la T.A.G  oljoro hali ambayo ilisababisha hasara kubwa sana.

Katika hatua nyingine Msimamizi  na Muangalizi  wa makanisa ya T.A.G mkoani hapa Bw Simion Vomo alisema kuwa wao kama kanisa hawataweza kuwasikiliza Morani hao kwa kuwa madai yao hayana Msingi Kisheria.

Aliongeza kuwa Kanisa litalazimika kuchukua hatua kali na za kisheria,kwa kuwa Morani hao wanasababisha amani ndani ya miji na Maboma ya wananchi kukosekana hali ambayo kama haitaweza kuchukuliwa tahadhari basi itazaa matatizo makubwa sana katika jamii.

Awali Kaimu Kamanda wa  Polisi mkoa wa Arusha Bw Akili Mpwapwa alisema kuwa bado polisi wanaendelea na Upelelezi,hivyo familia hizo tano ambazo zimelazimika kukimbia makazi yao kwa kuwahofia Morani hao, wanatakiwa kutoa Taarifa ili Sheria ichukue mkondo wake kwa kuwa wanachokifanya Morani hao ni Makosa.

MWISHO
 
CHANZO CHA HABARI NA QUEEN LEMA

ARUSHA 

0758907891.