Friday, November 3, 2017








NA WAANDISHI WETU,ARUSHA


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mbunge wa jimbo la Arusha mjini Goodbless Lema, amesema kuwa yeye pamoja na chama chake wanatarajia kuwa wapole sana katika chaguzi za madiwani zinazotarajia kufanyika mapema mwezi huu lakini pia watakuwa wa Mwisho kuonewa na kunyimwa haki kwenye chaguzi mbalimbali

lema aliyasema hayo mapema leo kwenye kata ya Murieth iliopo jijini Arusha wakati akimtambulisha rasmi mgombea wa udiwani wa kata hiyo ya Murieth bw Mosses Mollel  ambaye atapeperusha bendera ya chama cha demokrasia na maendeleo

Lema alisema kuwa kusema kuwa wao wanatarajia kuwa wapole haimanishi kuwa watakubali kuibiwa kura au kuteswa kwa namna yoyote bali watatembeza upole pamoja na ustaarabu kama wanavyofanya kwenye kampeni mbalimbali

"sisi tutaongoza kampeni zetu kwa njia ya ustarabu lakini pia tunatarajia hapa Murieth kuwa wamwishio kabisa kuonewa kwa namna yoyote ile na kamwe hatutakubali kudhalilishwa endapo kama upole wetu hautaweza kujidhirisha'aliongeza lema

alisema kuwa mgombea wao amekidhi viwango vyote vya uchaguzi na hivyo basi wanamleta kwennye jamii waweze kumdhibitisha na kumpa nafasi ya kushinda katika uchaguzi ujao

Awali mgombea udiwani wa kata hiyo ya Murtieth kupitia chama cha demokrasia na Maendeleo, Mosses Mollel alisema kuwa wananchi wa kata hiyo wanatakiwa kumchagua na kumpa kura za ndio kwa sababu yeye  ni kiongozi wa wananchi na sio tajiri wa wananchi

Mollel alibainisha kuwa wananchi wanatakiwa waweze kumpitisha kwenye chaguzi hizo kwani anatarajia kufanya mabadiliko makubwa sana ukilinganisha na vipaumbele ambavyo anavyo mpinzani wake kutoka CCM

No comments:

Post a Comment