Sunday, September 29, 2013

mamlaka ya hifadhi ya ngororo yatoa msaada wa mahindi

                                                  


Wakazi wa eneo la mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro wakipokea chakula cha msaada kutoka kwa uongozi wa Ngorongoro Conservation Are Authority (NCAA) ikiwa ni agizo kutoka kwa waziri mkuu mizengo pinda.

Tani 7000 zimegawiwa kwa familia 20,000 za jamii ya wamasai wanaoishi katika hifadhi hiyo. Idadi ya watu ndani ya NCAA kwa sasa ni zaidi ya 87,000 na wote wakiwa na mahitaji makubwa ya chakula kwani hawaruhusiwi kulima ndani ya eneo la NCAA.

Hivi karibuni wamasai hao wamejukuta wakikumbwa na baa la njaa baada ya ukame ulioathirini eneo lao kwa miaka mitatu mfululizo kuteketeza mifigo ambayo hasa ndiyo tegemeo lao la maisha.

Ugawaji wa chakula umeanza katika kata ya Olbalbal na utaendelea kwenye maeneo mengine huku NCAA ikijiandaa kununua tani zingine 29,000 za mahindi kutoka wilayani Karatu kwa ajili ya kuongeza mgawo huo wa chakula. picha na mwandishi wetu



MUSWADA WA MAREKEBISHO YA KATIBA WATARAJIA KUKABIDHIWA KWA JK

MUSWADA wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Katiba wa mwaka 2013 uliopitishwa na Bunge hivi karibuni, unatarajiwa kukabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete, wiki ijayo. Taarifa zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vyake vilivyoko serikalini zimeeleza kuwa Rais Kikwete atakabidhiwa muswada huo mara atakaporejea nchini akitokea katika ziara yake ya nchi za Marekani na Canada.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, jana alilieleza gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani kuwa Muswada huo utawasilishwa kwa Rais Kikwete na Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilillah, baada ya kuuandaa vizuri na rais atauperuzi kabla ya kufikia uamuzi wa kuusaini au kutousaini.

Taarifa hizi zimepatikana siku chache baada ya kusambaa kwa tetesi zinazoeleza kuwa Rais Kikwete alikutana na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba na baadhi ya maofisa walio katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kujadili baadhi ya vipengele vilivyo kwenye Rasimu ya Katiba Mpya, ambavyo vimeibua mvutano.

Hata hivyo, Jaji Werema aliliambia gazeti hili kuwa hana taarifa ni lini Dk. Kashilillah ataupeleka muswada huo Ikulu na hata alipoulizwa kuhusu tetesi zilizosambaa miongoni mwa jamii kuwa Rais alikutana na baadhi ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba pamoja na wale wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kujadili mwenendo na mwelekeo wa rasimu hiyo, alisema hafahamu chochote.

“Muswada ukishatoka bungeni, kama umepitishwa huo haumhusu tena Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali, anakuwa nao Katibu wa Bunge. Yeye sasa anakuwa na kazi ya kuuweka vizuri, akikamilisha anauchukua na kuupeleka Ikulu kwa Rais kwa ajili ya kusaini.

“Yeye Rais akishapewa naye anauangalia, ukimpendeza anausaini, vinginevyo hausaini anaurudisha. Sasa hivi sasa anao Katibu wa Bunge, jua kuwa anayejua kama umesaini au hapana ni yeye na rais tu, wengine wote tunasubiri taarifa ya Katibu wa Bunge. Hayo mengine ya ataupeleka kwa njia gani na lini siyajui,” alisema Jaji Werema.

Taarifa zilizopatikana kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, zimeeleza kuwa kuna wasiwasi umetanda iwapo Rais atasaini muswada kwa sababu Tume ya Jaji Warioba bado haijampelekea rasimu ya pili ya Katiba, ambayo ndiyo hutoa mwelekeo wa kuitishwa kwa Bunge la Katiba.

Mmoja wa maofisa wa juu wa wizara hiyo aliyezungumza na gazeti hili kwa sharti la kutotajwa jina lake, ameeleza kuwa mvutano ulioibuka baada ya Tume ya Jaji Warioba kutangaza rasimu ya kwanza ya Katiba Mpya unaweza kuchelewesha kutolewa kwa rasimu ya pili ambayo ni lazima Rais akabidhiwe na aipitie, ndiyo hatua ya kuitwa kwa Bunge itakapofuata.

Alisema, kwa sasa hali ni ya wasiwasi kwa sababu ipo hofu kuwa rais anaweza asisaini muswada huo, bali atakachofanya ni kuandika dokezo litakalokuwa na sababu za kutoweka sahihi yake kwenye muswada kisha ataurejesha kwa Katibu wa Bunge kwa ajili ya kuupeleka tena bungeni kujadiliwa.

“Na hii ni kwa sababu Bunge la Katiba haliwezi kuitishwa bila Tume ya Jaji Warioba kupeleka rasimu ya pili ya Katiba kwa Rais, na yapo mashaka kuwa hatapeleka kwa sasa kutokana na mwenendo wa mambo ulivyo.

“Sasa Jaji Warioba asipopeleka rasimu ya pili ina maana hata Bunge la Katiba halitakuwepo,” alisema.

Katibu wa Bunge, Dk. Kashilillah jana hakuweza kupatikana kuzungumzia suala hilo, baada ya simu yake ya kiganjani kutopatikana mara kadhaa alipopigiwa, lakini duru za habari kutoka Ofisi ya Bunge zimedokeza kuwa anatarajiwa kuuwasilisha muswada huo kwa Rais Kikwete siku ya Jumatano, Oktoba 2, 2013.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Dk. Kashilillah amekwishakamilisha maandalizi ya muswada na sasa anamsubiri rais arejee nchini ili amkabidhi.

Imeelezwa kuwa hatua ya Rais Kikwete ya kutosaini muswada huo utakuwa ni mtego kwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walioupitisha kwa sababu watalazimika kukubaliana na mabadiliko yanayoshinikizwa na makundi mbalimbali ya jamii, ambayo yanadai kuwepo kwa kasoro ndani ya muswada.

Mabingwa wa mambo ya kibunge ambao wamekuwa wakizungumza na gazeti kwa nyakati tofauti, huku wakisisitiza majina yao kuhifadhiwa kwa kile wanachoeleza kuwa suala la Rasimu ya Katiba sasa ni nyeti, wameeleza kuwa uamuzi wa Rais Kikwete ndio utakaowaongoza wabunge wa CCM wanachopaswa kufanya na iwapo watapingana nao, ipo hatari ya Bunge kuvunjwa.

Kwa mujibu wa kanuni na taratibu za Bunge, iwapo Rais Kikwete hatasaini muswada huo na kuurejesha bungeni na iwapo wabunge nao wataupitisha tena bila kuufanyia marekebisho, Rais atalivunja Bunge.

GAZETI LA MTANZANIA LAFUNGIWA KWA SIKU 90 MWANANCHI SIKU 14

SERIKALI kupitia Idara ya Habari (MAELEZO) imelifungia Gazeti la MTANZANIA kwa muda wa siku 90 kupitia Tangazo la Serikali namba 332 la tarehe 27 Septemba, 2013 kwa kile inachodai kuwa limekuwa likiandika habari za kichochezi. Sambamba na MTANZANIA, pia imelifungia gazeti la MWANACHI kwa muda wa siku 14 kwa madai hayo hayo.

Uamuzi huo wa serikali ulitangazwa jana na Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO, Assah Mwambene, kwa vyombo vya habari vichache vilivyotumiwa wito wa kuwepo kwa mkutano baina yake na vyombo hivyo.

Taarifa hiyo iliyotolewa na Mwambene, ilisambazwa pia katika mitandao ya kijamii na ilieleza kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya serikali kulionya mara nyingi MTANZANIA kuacha kuandika habari za uchochezi lakini halikuonyesha kuzingatia maelekezo ya Msajili wa Magazeti.

Ilizitaja habari inazodai kuwa za uchochezi kuwa ni pamoja na iliyochapishwa katika toleo namba 7262 la Machi 20 mwaka huu iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho ‘URAIS WA DAMU,’ na makala ya uchambuzi iliyochapishwa Juni 12 katika toleo namba 7344 iliyokuwa na kichwa cha maneno ‘MAPINDUZI HAYAEPUKIKI.’

Habari nyingine iliyolalamikiwa na serikali ni iliyochapishwa Jumatano ya Septemba 18 mwaka 2013 katika ukurasa wa mbele wa toleo namba 73414 iliyobebwa na kichwa kisemacho ‘SERIKALI YANUKA DAMU.’

Taarifa ya Mwambene inadai kuwa habari hiyo ilikolezwa na picha zilizounganishwa kwa ustadi mkubwa kwa kutumia kompyuta na kutapakaza rangi nyekundu mithili ya damu nyingi kumwagika.

Aidha, taarifa hiyo inaeleza kuwa habari hiyo haikuwa na uthibitisho na ililituhumu Jeshi la Polisi kuhusika na wahanga walioumizwa na watu wasiojulikana kwa kumwagiwa tindikali na waliyovamiwa na kujeruhiwa vibaya na pia kuishitumu serikali kwa ugoigoi katika kushughulikia matukio yenye sura ya kigaidi.

Kwa upande wa Gazeti la MWANANCHI, serikali imeeleza kuwa imechukua uamuzi wa kulifungia kwa sababu ya kuandika habari zenye mwelekeo wa uchochezi na uvunjifu wa amani na imetoa mfano wa habari iliyokuwa na kichwa kisemacho MISHAHARA MIPYA SERIKALINI 2013 na nyingine iliyokuwa na kichwa kilichosomeka ‘WAISLAM WASALI CHINI YA ULINZI MKALI.’

Saturday, September 28, 2013

WATANZANIA WATAKIWA KUACHANA NA DHANA YA KULALAMIKA OVYO JUU YA CHANGAMOTO ZAO BADALA YAKE WATUMIE FURSA WALIZONAZO KUTATUA CHANGAMOTO HIZO




IMEELEZWA kuwa dhana ya ulalamishi juu ya changamoto mbalimbali kwa
watanzania imesababisha watanzania wenyewe kushindwa kuwajibika huku
wengine wakiendelea kukosa mahitaji yao ya msingi na kisha kusingizia
Serikali.

Kwa sasa asilimia kubwa ya watanzania wamebaki wakiwa wanalalamikia
baadhi ya viongozi kwa kushindwa kutimiza na kutatua changamoto zao
bila kujua na kutambua kuwa kila mtanzania anapaswa kutatua kero
mbalimbali

Hayo yameelezwa na Waziri wa  waziri wa Nchi ofisi ya waziri mkuu
uwekezaji na uwezeshaji Dkt Mary Nagu wakati mapema wiki hii wakati
akiongea na wanafunzi wa shule ya Haradali katika maafali ya tatu ya
shule hiyo

Dkt Nagu alisema kuwa dhana hiyo ya kulalamikia siyo dhana nzuri kwani
haijengi Nchi badala yake inabomoa kwa kuwa kila mtanzania ana uwezo
mkubwa sana wa kuweza kusaidia maendeleo ya Nchi ya Tanzania

Alifafanua kuwa umefika wakati wa watanzania kubadilika na kujiuliza
maswali kabla ya kuanza lawama na mara baada ya kujiuliza maswali pia
wanatakiwa kubuni aina na mbinu mbadala ambazo zinaweza kuiokoa nchi.

“ni kweli tunao viongozi wa aina mbalimbali lakini hawawezi kusikiliza
kero,shida, na changamotoo za kila mmoja wetu hivyo basi kama kila
mtanzania atawajibika kutatua kero leo nchi ya Tanzania itaweza
kusonga mbele zaidi na malalamishi yataisha”aliongeza Dkt Nagu

Pia alisema hata viongozi wa Serikali nao wanatakiwa kuhakikisha kuwa
wanawajibika tena kwa kiwango ambacho kinahitajika kwani kama wao
watawajibika vizuri basi watachangia kuharakisha maendeleo ya Nchi
ambayo bado yapo chini sana.

“ukiwa kama kiongozi wa Serikali katika Ngazi yoyote ile unapswa
kuhaakikisha kuwa unawajibika kwa kiwango cha asilimia 100 usilale na
usichague kazi ya kufanya wewe fanya zote ili uweze kuppunguza dhana
hii ya kulalamika ambayo wakati mwingine ndio chanzo cha umaskini
katika maisha yawatanzania wengi”alifafanua zaidi Dkt Nagu

Wakati huo huo mkurugenzi mtendaji wa shule hiyo ya Haradani,Bw Simon
Kaaya alisema kuwa ili kukuza na kuwekeza kwenye sekta hiyo ya elimu
hapa nchini Changamoto mbalimbali zinatakiwa kutatuliwa kwa haraka
sana kwani bado kuna umuhimu mkubwa wa elimu.

Bw Kaaya alisema kuwa mbali na hayo hata wamiliki wa shule mbalimbali
wanatakiwa kuangalia zaidi suala la mahitaji kuliko suala la maslahi
ambalo wakati mwingine linasababisha baadhi ya watoto kukosa elimu
kabisa.

“nikisema hivyo nina maana kuwa kwa mfano kabla haujaanzisha shule ni
lazima uangalie mahitaji ya eneo lile lakini pia uhakikishe kuwa hata
ada ambayo unaitoza nayo inaendana na uwezo wa wazazi wa maeneo yale
kwani kama utaweka kiwango kikubwa na eneo lile lisipate watoto
utakuwa umefanya kazi ya bure kabisa’aliongeza Bw Kaaya

WAFADHILI WATOA MSAADA WA MILIONI 90 KWA AJILI YA MRADI WA WATOTO




Shule ya Ngorika Happy watoto School iliopo katika kitongoji cha Ngorika Tarafa ya Kingori Wilayani Meru mkoani Arusha imefanikiwa kupewa Mradi wa shamba lenye hekari nane huku likiwa na tahamani ya Milioni 90 kwa ajili ya kuwasaidia watoto yatima waliopo katika shule lakini pia kuachana na tabia ya kuwa tegemezi.

Aidha Mradi huo wa shamba upo katika eneo  Lerai Kati ambapo mradi huo umetolewa na wafadhili wa Kitanzania (Friends of Tanzania)hivi karibuni ili ikuwajengea uwezo wa kuwasiaida yatima lakini pia kujiimarisha zaidi

Akiongelea mradi huo katika maafala ya kwanza ya shule hiyo wiki iliyopita mkuu wa shule hiyo Edward Mwololo alisema kuwa wafadhili hao waliamua kukunua mradi huo ili kuweza kusaidia shule hiyo dhidi ya ukosefu wa mahitaji ya chakula

Aidha alidai kuwa mpaka sasaivi mradi huo umeweza kuwasaidia sana wanafunzi ambao wengine ni Yatima wale wanaotokea katika mazingira magumu kwa kuweza kupata vyakula mbalimbali kama vile mboga kwa uraisi sana tofauti na hapo awali ambapo shule hiyo ilikuwa haina mradi huo

Wakati huohuo amedai kuwa ni vema kama baadhi ya shule ambazo zipo chini ya wafadhili mbalimbali lakini pia ambazo zinawahudumia Yatima na wale waliotoka katika mazingira kuhakikisha kuwa wanakuwa wabunifu lakini pia miradi ambayo wamepewa waweze kuitumia vizuri

Alidai kwa kufanya hivyo kutaweza kuruhusu hata watoto yatima wenyewe kuepukana na tabia ya kuwa tegemezi na badala yake watahakikisha kuwa wanaweza kujishugulisha kwa maslahi ya maisha yao ya hapo baadaye lakini pia kwa maslahi ya taifa zima

“tunapswa kujua na kutambua kuwa ipo siku masuala ya ufadhili yatakoma lakini kama yatakoma na miradi ambayo tumepewa tunaiweza kuihudumia vizuri basi tutaweza kupiga hatua ya hali yajuu sana na pia ni muhimu hata kuwajengea hawa yatima pamoja na wale ambao wanatokea katika mazingira magumu kuannza kujitegemea na kuacha kutegemea zaidi misaada’aliongeza hivyo

Awali akielezea changamoto ambazo zinaikabili shule hiyo ambayo asilimia kubwa ya wanafaunzi wake ni Yatima alidai kuwa mpaka sasa wanafunzi katika shule hiyo hawana uhakika wa kupata maji safi na salama kwa kuwa eneo hilo limekosa maji kwa muda mrefu sasa.

“kwa kipindi cha miaka mitatu sasa tumekosa maji safi na salama kwa ajili ya matumizi hapa shuleni hivyyo basi tunaomba serikali iweze kushirikiana na sisis katika kuhakikisha kuwa tunapata maji kwani maji tunayotumia sasa ndio hayo yanwasababishishia watoto wetu magonjwa kwani floride iliopo katika maji hayop ni kubwa sana”aliongeza mkuu huyo.


ASILIMIA 30 YA WATANZANIA WAISHIO VIJIJINI KUPATA UMEME IFIKAPO MWAKA 2015





SERIKALI imesema kuwa mpaka ifikapo mwaka 2015 asilimia 30 ya
watanzania  waishio vijijini watakuwa wamepata huduma ya umeme kwani
kwa sasa asilimia saba tu ya wananchi waishio vijijini ndio wanapata
huduma hiyo ya umeme.

Kauli hiyo imetolewa jana (leo) jijini hapa na Naibu waziri wa Nishati
na madini hapa nchini Steven Massele wakati akiongea na wadau wa
mashirika yazilishayo umeme katika nchi za kusini mwa jangwa la
sahara(PIESA).

Masele alisema kuwa asilimia 21 ya watanzania ndio wanapata huduma ya
umeme ambapo kati yao asilimia saba ndio wanaishi vijiijini lakini
kupitia mpango wa wakala wa umeme Vijijini (REA)watahakikisha wilaya
zote na vijiji vyote vinapata umeme kwani ni haki yao ya msingi.

“tunataka kuona kuwa kila familia hata kama ni ya kijijini inapata
umeme na pia kama watapata umeme ni wazi kuwa hata maendeleo yatakuja
kwa haraka tofauti na pale ambapo hakuna umeme wala huduma
hizo”alisema Masele

Katika hatua nyimgine aliwataka wakala wa umeme vijijini kuhakikisha
kuwa wafanya kazi kwa haraka sana ikiwa ni pamoja na kutatua
changamoto ambazo zipo kijijini kwani asilimia kubwa ya wananchi wa
vijijini bado hawajaweza kupata huduma hiyo ya umeme lakini pia
hawajatambua umuhimu wake.

Awali mwenyekiti wa PIESA ambaye pia ni Kaimu mkurugenzi wa shirika la
Tanesco hapa nchini Mhandisi Felchesmi Mramba alidai kuwa lengo halisi
la kukutana maeneo hayo ni pamoja na kuhakikisha kuwa wanajadili namna
ya kutumia matumizi ya Teknolojia katika kupata umeme

Mhandisi Mramba alidai kuwa kama watafanya hivyo basi wataweza
kuruhusu kwa kiwango kikubwa sana upatikanaji wa umeme hasa maeneo ya
Vijijini lakini pia kuangalia namna ya matokeo ya tafiti ambazo
walizifanya na nchi zilizoendelea Duniani.

Ametaja nchi ambazo zitajadili namna ya upatikanaji wa umeme hasa
vijiijini kuwa ni pamoja na Marekani, Mexico,Ausralia, India, Canada,
China, Indonesia,Japani,Kenya ,Malawi Uganda, Botswana , Lesotho
pamoja na Afrika ya kusini.

MWISHO

Sunday, September 22, 2013

WAZIRI KABAKA AZINDUA RASMI MCHAKATO WA MAANDALIZI YA USHIRIKI WA WAJHASIRIA MALI .....

WAZIRI KABAKA AZINDUA RASMI MCHAKATO WA MAANDALIZI YA USHIRIKI WA WAJHASIRIA MALI .......





Waziri wa Kazi na Ajira  Mhe. Gaudentia  Kabaka  leo  tarehe  19/09/2013, amezindua  rasmi  mchakato wa  maandalizi ya ushiriki wa Wajasiria mali wa Tanzania  katika Maonesho ya 14 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yajulikanayo  kama  Nguvu kazi/Jua kali.

Maonesho hayo yaliyoanza kufanyika  mwaka  1999 jijini Arusha  Tanzania wakati wa kusainiwa mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yameendelea kufanyika kila mwaka kwa mzunguko katika nchi ya wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Dhumuni kuu la maonesho haya ni kuwezesha sekta  isiyo rasmi kukua na kurasimisha shughuli zao katika ukanda wa Afrika Mashariki kwa kuwapatia fursa Wajasiriamali wa sekta hii kuonesha bidhaa zao, kukutana na wenzao, kubadilishana taarifa, ujuzi, kukuza masoko ya bidhaa na huduma pamoja na kuwezesha kupanuka kibiashara.

Jumla ya Wajasiriamali 1,070 kutoka nchi tano za  Jumuiya ya Afrika Mashariki wanategemewa kushiriki na Tanzania inatarajiwa kupeleka washiriki 250.

Mhe. Waziri Kabaka amesema,ili kurahisisha na kuharakisha ushiriki wa Wajasiriamali wa Tanzania katika maonesho hayo, kuna swala la usajili, na fomu za usajili pamoja na vigezo vya kuangalia kabla ya kujaza fomu ambavyo vinapatikana kwenye  Tovuti ya Wizara ambayo  ni www.kazi.go.tz
IMETOLEWA
Ridhiwan.M.Wema
Msemaji

HASARA NYINGI ZA WAKRISTO ZINATOKANA NA UBAGUZI WA HUDUMA ZA KANISA

HASARA NYINGI ZA WAKRISTO ZINATOKANA NA UBAGUZI WA HUDUMA ZA KANISA

Na Mwandishi wetu. Arusha


Wakristo wanakabiliwa na changamoto ya ubaguzi wa ibada hali ambayo wakati mwingine ndiyo chanzo cha wao kwenda makanisani kwa mazoea bila kufanikiwa katika maisha yao huku wengine wakiwa wnaaambulia hasara za mali na hali zao kila siku

Asilimia kubwa ya wakristo wana ubaguzi wa huduma za ibada kama vile Maombi,utoaji wa mafungu ya kumi,harambee za kila siku na michango ya hiari hali ambayo ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya kanisa.

Hayo yameelezwa na Mchungaji Steven Laizer  wa kanisa la Bethel  Kishore  lilopo maeneo ya Kishore Ngaramtoni jijini Arusha mapema wiki iliyopita.

Mchungaji Steven alidai kuwa tabia hyo imekuwa na kustawi sana kwenye baadhi ya maksanisa huku baadhi ya wakristo wakiona kuwa makanisa hayo pamoja na wachungaji hawawombei kwa kutosha bila kujua na kutambua kinachowafanya wasiweze kusonga mbele ni uchoyo na ukaataaji wa huduma mbalimbali ndani ya makanisa.

Alisema kuwa wengi wanajidanganya kuwa huduma ambazo zinaweza kuwakomboa kwenye maisaha yao ni huduma za kusifu na kuabudu pekee jambo ambalo sio la kweli kwani huduma zote Mungu yupo pamoja na wanadamu

“ndani ya kanisa ukiita huduma ya kusifu na kuabudu watuw ataalikana lakini ita huduma ya maombi hata ya kufunga na kuomba uone kama utaona watu wengi watu wanashindwa kujua na kutamvbua kuwa ubaguzi wa huduma ndani ya makanisa haufai kabisa na badala yake unaddiimiza maslahi ya kanisa’aliongeza Mchungaji huyo

Wakati huo huo aliseama kuwa ndani ya makanisa wapo baadhi ya watu ambao wanaona shida kutoa sadaka kwa madai kuwa hakuna anayewaona na kisha kuingia mitini jambo ambalo ndilo chanzo cha hasara kwenye maisah yao

“chunguza sana mtu anayeshidwa kutoa sadaka kwa mungu maisaha yaklle yakoje utakuta kila siku analia mara ugonjwa, mara hasara, mara wizi sasa kama utakuwa unatoa sadaka ni wazi kuwa utakuwa unajilinda dhidi ya vitu kama hivi ambavyo vinacheza kwenye malango ya shetani’aliongeza mchungaji huyo.

Alimalizia kwa kuwataka hata Viongozi wa dini nao wahakikishe kuwa kamwe hawaoni aibu kuhubiri juu ya vitu mbalimbali ambavyo vinaweza kuwatenganisha wakristo na huduma za Mungu kwa kuhofia jambo Fulani kwenye maisha ya kibinadamu ya kila siku.

MWISHO

MAASKOFU NCHINI WASHAURIWA KUSEMA UKWELI JUU YA MADAWA YA KULEVYA

MAASKOFU NCHINI WASHAURIWA KUSEMA UKWELI JUU YA MADAWA YA KULEVYA



Na Bety Alex, Arusha



Viongozi wa dini hasa maaskofu wameshauriwa kuhakikisha kuwa kamwe
hawaogopi kusema ukweli juu ya biashara ya madawa ya kulevya ambayo
inaendelea hapa nchini na kama hawatasema ukweli na kisha kuelezea
umma juu ya madhara ya kujihusisha na biashara hiyo basi Tanzania
itaweza kuyumba sana



Kwa sasa wapo baadhi ya watanzania ambao wanasingizia umaskini na
kisha kujihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya bila kujua
na kutambua kuwa wanaweka nchi kwenye sifa mbaya



Hayo yameelezwa na Askofu Mstaafu wa kanisa la Angikan Jijini
Arusha,Simon Makundi wakati wa kuwaingiza rasmi Viongozi wa dayosisi
ya Arusha katika Kanisa la Tanzania Methodist Church lilopo njiro
jijini Arusha mapema jana.



Askofu Makundi alisema kuwa inasahangza sana kuona kuwa wimbi kubwa la
watanzzania bado wanaendelea kukabiliwa na changamoto ya biashara
haramu ya madawa ya kulevya ingawaje viongozi wa dini wapo hapa nchini



Alisema, viongozi wa dini wana nafasi kubwa sana ya kuhakikisha kuwa
wanakemea masuala hayo kwani wao wana nafasi nzuri sana ya kukuytana
na wananchi kila siku na kila juma tofauti na viongozi wa serikali
ambao ni mara chache sana.



“kwa sasa hii biashara inaonekana kufanywa na watu wengi sana na kama
viongozi wa dini hasa ninyi mnaoitwa maaskofu mtaendelea kukaa kimya
mtakuwa hamtendi haki kabisa kwenye jamii na badala yake hii biashara
itazidi kushamiri hapa nchini’alisema Askofu Makundi



Wakati huohuo Askofu Mteule wa kanisa hilo la Tanzania Methodist
Church jimbo la Arusha Dkt Izack Sarakikya alisema kuwa uwepo wa
kanisa hilo kwa mkoa wa Arusha utaweza kuraisisha shuguli mbalimbali
za kidini lakini pia za kijamii kwani bado jamii inakabiliwa na
changamoto nyingi sana



Alifafanua kuwa Kanisa hilo lina huduma maalumu ya kungalia majanga
ndani ya Nchi ya Tanzania hasa yale ambayo yanawakumba viongozi wa
dini mbalimbali lakini pia hata yatima na wajane



Alimalizia kwa kusema kuwa huduma ya kanisa hilo ambayo itawafikia
watu wenye mahitaji mbalimbali pia itaweza kuwakumbuka hata viongozi
mbalimbali wa dini ambao wakati mwingine wanasahulika kwa kuwa tayari
ni wastaafu au ni wazee jambo ambalo sio hazina ya taifa la Tanzania


CHAMA CHA WAFANYAKAZI MASHAMBANI NA KILIMO TANZANIA CHAANZISHA KAMPENI YA KUONDOA BUGHUDHA SEHEMU ZA KAZI

CHAMA CHA WAFANYAKAZI MASHAMBANI NA KILIMO TANZANIA CHAANZISHA KAMPENI
YA KUONDOA BUGHUDHA SEHEMU ZA KAZI



Na Queen Lema, Arusha



Chama cha wafanyakazi mashambani na kilimo Tanzania(TPAWU)kimezindua
kampeni ya kuweka mazingira huru yasiyo nnughudha za kijinsia mahala
pa kazi huku lengo likiwa mi kutokomeza kabisa unyanyasaji



Akizundua Kampeni hiyo mapema jana naibu Katibu mkuu wa chama hicho
hapa nchini Bw John vahaya alisema kuwa kampeni hiyo italenga
wafanyakazi wa maeneo mbalimbali hapa nchini



Bw Vahaya alisema kuwa lengo halisi la kampeni hiyo ni kuhakikisha
kuwa inatokomeza kabisa masuala ya unyanyasaji hasa mahala pa kazi
kwani unyanyasaji wakati mwingine umesababisha madhara mengi sana hasa
kwa wafanyakazi wa kike



“chama hiki kinatamani kuona kuwa suala la unyanyasaji hasa ule wa
kijinsia linakuwa ni ndoto kabisa kwani pia tulikuwa na tafiti
mbalimbali ambazo zinaonesha mazingira mabaya sana kwa wanawake ambapo
mpaka sasa suluhu ya mambo haya kupitia kampeni hii
yatagundulika”aliongeza bw Vahaya



Vile vile alisema kuwa utafiti ambao umezaa kampeni hiyo uliweza
kufanywa kwenye mikoa ya Mbeya, Iringa,Kilimanjaro na Arusha ambapo
umeweza kubaini mambo mbalimbali ambayo wakati mwingine ndio chanzo
kikubwa cha umaskini hasa kwa maisha ya wanawake



Akiongelea matokeo ya tafiti hiyo alisema kuwa ni pamoja na wanawake
wengi kushindwa kusema hadharani jinsi ambavyo wanafanyiwa na wanaume
hasa wale wenye madaraka huku hali hiyo ikichangia kuongezeka kwa
akina mama wa majumbani



Pia alidai kuwa tafiti hiyo imeweza kugundua kuwa bado wafanyakazi wa
mashambani na viwandani bado nao wanakabiliwa na changamoto ya ngono
mahala pa kazi huku hali hiyo pia ikipunguza kasi ya utendaji kazi
hasa kwa jinsia ya kike



Kutokana na hali hiyo alitoa wito kwa wamiliki wa viwandani lakini pia
wale wa mashamba ya maua kuhakikisha kuwa wanapinga vikali tabia hiyo
lakini wanawachukulia hatua kali wakuu wa idara ambao wataonekana
kujihusisha na unyanyasaji mahala pa kazi kwa visingizio vya Jinsia ya
kike au ya Kiume.



MWISHO

WAZIRI NAGU ATAKA MCHANGO WA WALIMU KWENYE TAIFA LA TANZANIA UJULIKANE

dkt Mary Nagu

Serikali imetakiwa kuhakikisha kuwa inatambua na kuthamini zaidi kazi za walimu hapa nchini lakini pia kuwajengea mazingira mazuri ya kazi kwani kama watabaguliwa na kisha kuachwa nyuma ni wazi kuwa sumu mbaya itatembea kwenye maisha ya wanafunzi

Kauli hiyo imetolewa mjini Arusha na waziri wa Nchi ofisi ya waziri mkuu uwekezaji na uwezeshaji Dkt Mary Nagu katika maafali ya nne ya shule ya Msingi haradali iliopo Wilayani Meru mkoani Arusha mapema leo.

Dkt Nagu alisema kuwa Serikali lakini hata nao wanachi wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanawajengea walimu mazingira mazuri ya kufanya kazi kwani wao wanamchango mkubwa sana kwenye taifa

Alisema kuwa kama wadau mbalimbali lakini pia Serikali itafanya hivyo ni wazi kuwa walimu watafundisha kwa moyo bila kujali aina ya shule na changamoto ambazo wanakabiliana nazo mabazo wakati mwingine ndio chanzo kikubwa cha mdondoko wa elimu

Alifafanua kuwa kama walimu wa nchi ya Tanzania watakuwa wanafanya kazi bila kupewa kipaumbele cha hali ya juu sana basi wao watakuwa mabalozi wazuri wa kupandikiza mbegu mbaya kwa wanafunzi na hatimaye madhara yatajionesha muda usio mrefu.


Wakati huo huo mkurugenzi mtendaji wa shule hiyo ya Haradani,Bw Simon Kaaya
alisema kuwa ili kukuza na kuwekeza kwenye sekta hiyo ya elimu hapa nchini Changamoto mbalimbali zinatakiwa kutatuliwa kwa haraka sana kwani bado kuna umuhimu mkubwa wa elimu.

Bw Kaaya alisema kuwa mbali na hayo hata wamiliki wa shule mbalimbali wanatakiwa kuangalia zaidi suala la mahitaji kuliko suala la maslahi ambalo wakati mwingine linasababisha baadhi ya watoto kukosa elimu kabisa.