Thursday, November 16, 2017

WAZIRI AISHAURI SERIKALI JINSI YA KUPINGA RUSHWA KUANZIA NGAZI YA CHINI KABISA

 Na Queen Lema, Arusha

Waziri wa nchi,ofisi ya rais na utumishi George Mkuchika ameishauri wizara ya elimu kutoa elimu dhidi ya mapambano ya rushwa kwa wanafunzi kuanzia shule za msingi hadi chuo kikuu ili kuwawezesha kutambua madhara yanayotokana na rushwa.

Mkuchika aliyasema hayo  alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa nchi za umoja wa Afrika zinazopambana na rushwa unaoendelea jijini hapa

Alisema kuwa endapo kama elimu ya rushwa itaweza kutolewa mashuleni kuanzia ngazi za awali itawezesha kupunguza kasi ya rushwa kwa nchi husika na hivyo taifa husika kupata haki zake za msingi

Aliongeza kuwa watu wengi wanatoa rushwa kwa kushindwa kufahamu haki zao za msingi hivyo elimu hiyo ikitolewa kuqnzia ngazi za chini itapunguza vitendo vya rushwa ambavyo vimekithiri kwa baadhi ya nchi.
Alitolea mfano nchi za Norway na Sweden ambazo zimekuwa zikitoa elimu ya rushwa kuanzia ngazi za chini mpaka vyuo vikuu ambapo imesaidia kila mtu katika nchi hizo  rushwa kuwa adui wao.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Takukuru  hapa nchini Valentine Mlowola alisema kuwa kutokana na rushwa kukithiri hapa tanzania wamefanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi bilioni 14 kwa kipindi cha mwaka huu ambazo zilikuwa zikitumika kwenye rushwa.

Alidai kuwa kwa sasa rushwa imekuwa tatizo la kimataifa hivyo kupitia mkutano huo wa umoja wa nchi za afrika wataweza kupanga mikakati ya kupunguza tatizo la rushwa katika nchi hizo.

Ameongeza kuwa nchi za afrika hazitaweza kujikwamua kiuchumi bila kumaliza tatizo hilo kutokana na maliasili nyingi zinazopotea kwenye bara hili zimekuwa zikipotea kutokana na rushwa.

Friday, November 3, 2017

WAFANYAKAZI WA EXIM WAHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 27 JELA KWA KOSA LA UTAKATISHAJI NA UHARIBIFU WA NYARAKA


WAFANYAKAZI wa Benki Ya exim waliokuwa wanakabiliwa na makosa 318 ikiwa ni pamoja na kugushi,kuharibu nyaraka,na utakatishaji fedha haramu na wizi wa dola za kimarekani 521,000 wamehukumiwa kifungo cha miaka 27 jela huku wafanyakazi wengine saba wakiachiliwa huru kutokana na mahakama kushindwa kudhibitisha makosa yao


Aidha wafanyakazi hao wamehukumiwa mapema leo kwenye MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha/Arumeru ambapo wamekutwa na hatia mbalimbali kinyume cha sheria.


Akisoma hukumu hiyo kwa zaidi ya masaa 5 kuanzia saa 4.30 asubuhi hadi saa 9.07 Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Deusdedit Kamugisha aliwataja aliowatia hatiani ni pamoja na mshitakiwa namba mbili Liliani Mgeye{33},Daudi Nhosha{39},Doroth Cjijanja{50},Genes Massawe{32},Christopher Lyimo{34} na DeusdediT Chacha{35}.


Alisema watuhumiwa wengine waliokutwa na makosa ya kugushi nyaraka na kuharibu nyaraka ambao ni pamoja na Nhosha Massawe na lyimo wamehukumiwa kwenda jela miaka minne kila mmoja kwa kosa hilo.

Hakimu Kamugisha aliwataja walioachiwa huru na mahakama baada ya upande wa jamhuri kushindwa kuthibitisha katika ushahidi wao kuwa watuhumiwa hao walitenda makosa hayo ni pamoja na mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo ambaye alikuwa meneja Mkuu wa  Exim Benki{T} ltd tawi la Arusha Bimel Gondaili.

Wengine ni pamoja na Livingstone Mwakihaba{37} maarufu kwa jina la ‘’stone’’,Joyce Kimaro{36},Evance Kashebo{40},Tutufye Agrey{32},Joseph Neki{30} na mfanyabiashara Gervas Lubuva{54}.

MWISHO WSA








NA WAANDISHI WETU,ARUSHA


KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mbunge wa jimbo la Arusha mjini Goodbless Lema, amesema kuwa yeye pamoja na chama chake wanatarajia kuwa wapole sana katika chaguzi za madiwani zinazotarajia kufanyika mapema mwezi huu lakini pia watakuwa wa Mwisho kuonewa na kunyimwa haki kwenye chaguzi mbalimbali

lema aliyasema hayo mapema leo kwenye kata ya Murieth iliopo jijini Arusha wakati akimtambulisha rasmi mgombea wa udiwani wa kata hiyo ya Murieth bw Mosses Mollel  ambaye atapeperusha bendera ya chama cha demokrasia na maendeleo

Lema alisema kuwa kusema kuwa wao wanatarajia kuwa wapole haimanishi kuwa watakubali kuibiwa kura au kuteswa kwa namna yoyote bali watatembeza upole pamoja na ustaarabu kama wanavyofanya kwenye kampeni mbalimbali

"sisi tutaongoza kampeni zetu kwa njia ya ustarabu lakini pia tunatarajia hapa Murieth kuwa wamwishio kabisa kuonewa kwa namna yoyote ile na kamwe hatutakubali kudhalilishwa endapo kama upole wetu hautaweza kujidhirisha'aliongeza lema

alisema kuwa mgombea wao amekidhi viwango vyote vya uchaguzi na hivyo basi wanamleta kwennye jamii waweze kumdhibitisha na kumpa nafasi ya kushinda katika uchaguzi ujao

Awali mgombea udiwani wa kata hiyo ya Murtieth kupitia chama cha demokrasia na Maendeleo, Mosses Mollel alisema kuwa wananchi wa kata hiyo wanatakiwa kumchagua na kumpa kura za ndio kwa sababu yeye  ni kiongozi wa wananchi na sio tajiri wa wananchi

Mollel alibainisha kuwa wananchi wanatakiwa waweze kumpitisha kwenye chaguzi hizo kwani anatarajia kufanya mabadiliko makubwa sana ukilinganisha na vipaumbele ambavyo anavyo mpinzani wake kutoka CCM

jamii yatakiwa kuwakumbuka wajane

Jamii kwa kushirikiana na viongozi mbali mbali wameombwa kujitoa kwa hali na mali  kumsaidia mjane aliyeunguliwa na nyumba yake katika kitongoji cha kanisani kata ya  Imbaseny katika halmashauri ya Meru ili kumwezesha aweze kurudia katika hali yake ya kawaida.

Wito huo umetolewa na mhadhiri mwandamizi chuo  kikuu cha  tumaini makumira ambae pia ni mjumbe wa mkutqno mkuu  ccm taifa dr danieli mirisho palangyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari  mara baada ya kukabidhi misaada ya mabati na mchele kwa mjane huyo aliyeunguliwa na nyumba yake hivi karibuni  katika kitongoji cha imbaseny .

Dr Palangyo amesema kuwa kufuatia janga kubwa alilopata mjane huyo ambae aliunguliwa  na nyumba yake hivi karibuni kutokana na chanzo ambacho hadi sasa hakijajulikana jamii,na viongozi mbali mbali ndani ya wilaya ya arumeru wanapaswa kuungana kwa pamoja na jamaa wanaojitolea kumsaidia mjane huyo ili aweze kujengewa nyumba yake na kuweza kurudi katika hali yake kwani kwa sasa anaishi mazingira magumu sana.

Amedai kuwa akiwa kama kiongozi amewiwa kufika kwa mjane huyo na kuweza kutoa bati 23   pamoja na mchele kg 25   kwani mama huyo pamoja na watoto wake wapo katika hali ngumu ambayo bila michango hataweza kurejea katika hali yake.

Akizungumza mara baada ya kupokea kwa misaada hiyo mjane huyo aliyetambulika kwa majina ya Maria Kimario mkazi wa imbaseny alisema kuwa nyumba yake iliungua tarehe 29 mwezi uliopita na kusababisha kupata hasara ya milioni 16 kwani vifaa vyote viliteketea kwa moto huo huku chanzo cha awali kikiwa bado hakijajulikana kwani alikuwa anatumia umeme unaotokana na Mobisol.

Aidha bi maria aliwaomba wadau mbali mbali kujitokeza na kumsaidia ili aweze kurejea katika hali yake kwani kwa sasa anaishi mazingira magumu pamoja na watoto wake huku akiwa hana chochote ikiwemo nguo,chakula ,na mahala pa kuishi
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limeunga mkono juhudi za Umoja wa Boda Boda Jiji la Arusha (UBOJA) za kutaka kuanza kusajili wanachama wake pamoja na vituo vyote kwa njia ya kisasa katika mfumo wa kompyuta kama hatua ya kuweka kumbukumbu itakayosaidia watambulike haraka kwa sura, majina yao, vyombo vyao vya usafiri na maeneo yao wanayoishi kuanzia ngazi ya kata hadi wilaya.

Akizungumzia nia ya kufanya hivyo na namna itakavyotekelezwa jana katika ukumbi wa bwalo la Polisi ulilopo jijini hapa, Mwenyekiti wa UBOJA Bw. Maulid Makongoro alisema kwamba wameamua kufanya hivyo ikiwa ni mkakati wa kuliunga Jeshi la Polisi katika kutokomeza uhalifu.

Bw. Makongoro alieleza ili kufanikisha suala hilo la usajili, kila kituo kitatakiwa kwanza kilipe ada ya mwaka mzima lakini pia kitatakiwa kulipia gharama ya Shilingi 20,000 ambapo wanachama wake bila kujali idadi waliyonayo wote watapigwa picha na taarifa zao zitapelekwa kwa viongozi wa wilaya likiwemo Jeshi la Polisi lakini pia kila mmoja atakuwa na kitambulisho.

“Usajili wa awali ulikuwa wa kibubu bubu kwa mfano baaadhi ya vituo vilikuwa vinamsajili mwanachama bila kumpiga picha lakini kumbukumbu zilikuwa hazifiki ngazi ya juu lakini wa sasa utakuwa wa Kidijitali kwa kuwa ofisi ya UBOJA itakuwa na kumbukumbu hizo kwenye vitabu na kwenye mfumo wa kumbukumbu wa Kompyuta”. Alifafanua Bw. Makongoro.

Alisema wameamua kufanya hivyo ili kuwadhibiti watu wanaofanya uhalifu kwa mgongo wa waendesha boda boda jambo ambalo linaweza kuwaletea taswira ambayo si nzuri machoni mwa watu.

Naye mgeni rasmi wa mkutano huo, Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo alisema kwamba, Jeshi la Polisi linaunga mkono moja kwa moja wazo hilo la UBOJA kwani hatua hiyo itasaidia kudhibiti uhalifu.

Alisema hatua hii inaonyesha nia njema walionao UBOJA kwa Jeshi la Polisi katika kushirikiana na kudhibiti vitendo vya uhalifu katika jiji la Arusha lakini pia mbali ya kuonyesha taswira nzuri kwa jamii itawasaidia kwa usalama wao.

Kamanda Mkumbo alisema kwa hivi sasa ushirikishwaji wa jamii katika kudhibiti uhalifu ni muhimu sana na kuwataka waendelee kuliunga mkono Jeshi hilo kwa kutoa taarifa mbalimbali za uhalifu hasa unaotokea maeneo yao ya kazi.

“Kwa hivi sasa wezi wengi wanapenda kuwatumia kwa kuwakodi waendesha pikipiki; kukagua eneo la kufanya uhalifu lakini pia baada ya kufanya uhalifu wanatoroka kwa pikipiki hivyo ukimgundua mtu wa namna hiyo toa taarifa haraka kwa askari yeyote unayemuamini au kwa viongozi ili tumkamate”. Alisisitiza Kamanda Mkumbo.

Aliwaasa katika utendaji wao wa kazi kutoweka mbele sana pesa bali waangalie uhai wao kwanza hasa wanapoona baadhi ya abiria wanawakodisha kwa pesa nyingi na kuwapeleka maeneo tete hasa usiku kwani wengine hawana nia nzuri.

Kwa upande wake Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Arusha Mrakibu wa Polisi (SP) Joseph Charles Bukombe, aliwataka wananchi wote wa mkoa huu wafuate sheria za usalama barabarani kwani kwa kufanya hivyo hakuna mtu atakayewakamata.

Mkuu huyo wa Usalama Barabarani alisisitiza suala la kuvaa kofia ngumu “Helmet” kwa dereva na abiria na kusema hatakuwa na msamaha kwa mtu yeyote atakayekaidi hilo awe mtumishi wa serikali au mwendesha pikipiki za abiria na kuongeza kwamba endapo vyombo vya usafiri vitaendeshwa salama basi vitabaki salama na watu watakuwa salama na kutaja kauli mbiu ya mwaka huu ya wiki ya nenda kwa Usalama Barabarani inayosema “ENDESHA SALAMA HATUTAKI AJALI TII SHERIA TUNATAKA KUISHI”.

Mkutano huo uliohudhuriwa na Mkuu wa kitengo cha Polisi Jamii mkoani hapa Mrakibu Msaidizi (ASP) Edith Makweli na msaidizi wake Mkaguzi wa Polisi Shabani Shabani ulihudhuriwa na washiriki 220 toka kanda tano ambao ni viongozi wa kata na vituo vya waendesha pikipiki ambapo Jiji la Arusha linakadiriwa kuwa na jumla ya vituo vya bodoa boda 400.


VIJANA 50 WAPEWA ELIMU YA KUTAMBUA SERA NA FURSA KWENYE JAMII


na mwandishi wetu, Arusha

VIJANA zaidi ya 50 kutoka katika kata tano za jiji la Arusha wamefanikiwa kupewa elimu ya matumizi na fursa za sera mbalimbali za nchi ya Tanzania ili waweze kunufaika na sera zilizopo


Aidha mafunzo hayo yametolewa na asasi ya Intiative for youth(INFOY) kwa kushirikiana na asasi ya the Foundation for civil Society    yameweza kuwanufaisha vijana kutoka katika kata za Sombetini, Elerai, Sinon, Ngarenaro,  pamoja na Sokoni 1huku lengo likiwa ni kujua na kutambua umuhimu wa sera  za nchi
hataivyo mbali na vijana hao  kufanikiwa kufahamu sera za nchi kwa sasa asilimia kubwa ya vijana wa kitanzania hawajui sera na nchi na dunia hali ambayo wakati mwingine inasababisha kukosa fursa mbalimbali

 Akiongea kwenye mafunzo hayomapema jana mratibu wa asasi ya INFOY  Bw Laurent Sabuni  alisema kuwa ukosefu wa elimu ya sera umekuwa ni kikwazo kikubwa sana kwa vijana wa sasa

Sabuni alisema kuwa kutokana na ukosefu wa elimu hiyo ya sera umekuwa sababu mojawapo ya vijana kushindwa kutambua fursa mbalimbali ambazo zipo kwenye jamii hali ambayo inachangia umaskini mkubwa kwenye maisha yao

Aliongeza kuwa kwenye mataifa yalioendelea duniani vijana wake huwa wanakuwa na desturi ya kuchambua na kufuatilia sera zao na za nchi jirani hali ambayo inawafanya waibue mambo mbalimbali kwenye jamii


katika hatua nyingine alibainisha kuwa vijana hao 50 ambao wamefanikiiwa kupewa elimu ya kutambua sera na faida zake pia wataweza kuunda mabaraza mbalimbali ambayo nayo yatalenga kuibua fursa za vijana kwenye jamii

Sabuni alidai kuwa kwa sasa ndani ya mkoa wa Arusha  hakuna mabaraza ya vijana kitu ambacho wakati mwingine vijana wanakosa sehemu ya kujadilia mambo yao kama ilivyo kwenye nchi ambazo zimeendelea barani Afrika.



Alimalizia kwa kusema kuwa vijana sasa wanatakiwa kujumuika kwenye mabaraza ya kata na hata wilaya na kuachana na tabia ya kukwepa vikundi au umoja kwani umoja unaweza kuleta mabadiliko makubwa sana kwa nchi ya Tanzania

MWISHO

Wednesday, November 12, 2014

Mkutano wa TCRA na wamiliki wa Blogs (Bloggers) Tanzania wafanyika jijini Dar


 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),Prof. John Nkoma akitoa hotuba yake wakati wa ufungumzi wa Mkutano wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini na wamiliki wa Blogs (Bloggers) Tanzania wenye lengo la kutoa mafunzo ya namna ya kutoa taarifa mbali mbali wakati wa Chaguzi mbali mbali hapa nchini,uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City,Jijini Dar es Salaam.Picha na Othman Michuzi.
Inginia Andrew Kisaka akitoa Mada katika  Mkutano wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini na wamiliki wa Blogs (Bloggers) Tanzania wenye lengo la kutoa mafunzo ya namna ya kutoa taarifa mbali mbali katika wakati wa Chaguzi mbali mbali hapa nchini.
Sehemu ya Maafisa wa TCRA wakiwa kwenye Mkutano huo.
Moja ya Mada zinazoendeleo kutolewa katika Mkutano huo.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO),Assah Mwambene akitoa hotuba yake wakati  akifunga Mkutano wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini na wamiliki wa Blogs (Bloggers) Tanzania uliokuwa na lengo la kutoa mafunzo ya namna ya kutoa taarifa mbali mbali wakati wa Chaguzi mbali mbali hapa nchini,unaoendelea kufanyika hivi sasa katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City,Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Wanablog waliohudhulia Mkutano huo uliofanyika leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City,Jijini Dar es Salaam.
Afisa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),Mabel Masasi akizungumza katika Mkutano huo.
Baadhi ya Wanalibeneke wakiendelea kuuliza maswali mbali mbali katika mkutano huo.
Mdau Josephat Lukaza na Dada Shamim Mwasha wakiwa mkutanoni hapo.
Prof. John Nkoma akijibu maswali ya wanablog.

Mdau Fred Njeje akidaka taswira.
Mkutano ukiendelea.
Mdau Henry Mdimu akitoa hoja.
Mdau akitafakari kabla ya kuuliza swali.
Wanablog kazini.


Monday, July 7, 2014

MWANA WA MFALME WA JAPAN PRINCE AKISHINO AFURAHIA NGOMA ZA KIMASAI,NA WA BARBAIG

Mwana wa mfalme wa Japan Prince Fumihito Akishino akipewa maelezo  mbalimbali
Mwana huyo wa mfalme wa Japan akipewa maelezo
kuhusu shughuli za uhifadhi ndani ya mamlaka ya Ngorongoro katika kutuo cha habari
cha Loduare Gate,


Mwana wa mfalme wa Japan Prince Fumihito Akishino na mkewe Kiko,
wakifurahia ngoma za makabila la Wadatoga (Barbaig) na ile ya Wamasai,
katika eneo la mlango wa Loduare kwenye hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro,
pamoja nao wapo pia maafisa wa mamlaka hiyo, Bruno Kawasange na Adam Akyoo
pamoja na Mkuu wa wilaya ya Karatu, Felix Daudi Ntibenda. PICHA ZOTE NA MALKIA WA MATUKIO ARUSHA

Thursday, May 29, 2014

ILBORU YADAI KILICHOSABABISHA MIGOMO YA WANAFUNZI MARA KWA MARA NI WANASIASA OVYO


UONGOZI wa Shule ya Sekondari Ilboru iliopo Jijini hapa umeweka utaratibu maalumu wa kuwakataa wanasisasa shuleni hapo kwani tafiti mbalimbali zimeonesha kuwa wapo baadhi ya wanasiasa ambao wanatumia kofia zao za siasa na kuwavuruga wanafunzi
Hataivyo miezi michache iliopo shule hiyo ilipata misukosuko kutokana na migomo mbalimbali ambayo ilifanywa na wanafunzi huku vichocheo vikubwa vikiwa ni wanasisasa wa Jiji la Arusha ambao walikuwa wanataka wanafunzi hao waingine kwenye mifumo ya vyama vya kisiasa.
Akiongea na Gazeti hili mapema jana mkuu wa shule hiyo ya Ilboru Julius Shulha alisema kuwa kuanzia sasa uongozi wa shule hiyo umeweka mikakati ya kuwakataa wanasiasa kuwatumia wanafunzi hao.
"unajua kuwa migogoro ambayo ilionekana shuleni hapani kutokana na wanasiasa na kuanzia sasa tumewakataa na hatutataka waje ili wawavuruge wanafunzi wetu tena"aliongeza Shulha
Alidai kuwa hata hao wanasiasa ambao wanatumia mwanya wao kwa ajili ya kuweza kuwayumbisha wanafunzi wanatakiwa waache mara moja kwani wanapaswa kujua nakutambua kuwa wao tayari wana mwanagaza wa maisha ila wanafunzi hao badi hawana mwangaza wa kimaisha.
"unakuta mwana siasa ana taaluma lakini anaajira yake tayari lakini anamuweka mwanafunzi huyu katika kundi lake na akifukuzwa hapa anaanza tena kutangatanga kwanini tusiwaache wanafunzi wakasoma alafu badae ndio wakajiingiza kwenye siasa lakini wakiwa tayari na elimu yao tunabdidi sisi watanzania kuanzia sasa tubadilike tuwaache wanafunzi wajisomee"aliongeza Shulha.
Kutokana na hali hiyo ya wanasiasa kuyumbisha shule hiyo alisema kuwa mpaka sasa wameshachukuatahadhari kubwa sana ya kuweza kuwasaidia wanafunzi hao ikiwa ni pamoja na kuwaambia madhara ambayo yanaweza kujitokeza iwapo watajihusisha na siasa pindi wanapokuwa mashuleni
Alimalizia kwa kuwataka hata walimu wa shule nyingine nazo kuhakikisha kuwa wanapingana na siasa ambazo mpaka sasa zinaletwa mashuleni kwani hali hiyo ndiyo chanzo kikubwa sana cha wanafunzi kuingia kwenye migogoro na migomo ya kila siku.
MWISHO

SERIKALI YAOMBWA KUWAPATIA BIMA WATOTO

 NA JAMES STANLEY ARUSHA
SERIKALI  imeombwa kuwapatia Bima ya Afya watoto
wanolelewa katika kituo cha kulelea watoto  yatima
cha Samartan Villege,kilichoko Moshono,Mkoa ni Aru
sha.
   Mratibu wa kituo hicho,   Father Josephat Mumany,
akizungumza hivi karibuni wakati wakutoa taarifa fupi
yakituo hicho bkwa viongozi   na wanachama wa kiku
ndu cha uamsho cha Oldadai,waliotembelea kituo hich
o kwa ajili ya kutoa misaada mbalimbali,Alisema   bima
hizo zitwapunguzia adha watoto hao wanapougua.
   Alisema kutokana na watoto hao kutokuwa na Bima
ya Afya,hali hiyo imekuwa ikiupa shida kubwa viongozi
wa kituo hicho,pale unapopataka kuwapeleka  watoto
hao hospitalini.

  Father Mmanyi,alisema hiyo ni changamoto    kubwa
kwao,kutokana na kituo kukabiliwa na  uhabawafedha,
hali amabayo pia huwafanya watotowanaougua kukaa
na maradhi yao kwa muda mrefu pasipo kupata  matib
abu.
  Katika hatua nyingine  Mmanyi alisema watoto wanao
lelewa katika kituo hicho wanapelekwa na serikali baada
ya kuokotwa mitaani,kutokana na kutupwa na    wazazi
wao baada ya kujifungua.
  ''Watoto hawa wanaokotwa katika mazingira  magumu 
wengine wanavunjwa miguu na wazazi wao,    wengine
wanakutwa wametoboleatobolewa na wazazi wao kabla
ya kuwatupa,Inasikitisha sana unapoona mazingira amba
yo watoto hawa walikotoka.''Alisema
   Pamoja na serikali,aliitaka jamii na mashitika mbalimbali
ya kitaifa na kimataifa,kukisaidia kituo hicho kwa hali  na
mali,ili kiweze kumudu malezi ya watoto hao.Hivi sasa.ali
sema wana miradi waliyopewa na wahisani inayowasaidia
katika mambo madogomadogo.Nayo ni pamoja na bwawa
la samaki,shamba la mahindi,pamoja na migomba.
  Mweka Hazina wa kikundi cha Uamsho,kilichowatembele
a watoto hao,Be Marry Mayagila,Alisema wanaguswa  na
amahitaji ya watoto hao na kwamba kwa kuwa wao ni w
anawake wenye moyo wa huruma,ndiyo maana wameme
amua kuwatembea na kuwapatia misaada ya vyakula.

   Alitoa wito kwa wanawake,na vikundi mbalimbali kuwa
hurumia watoto hao kwa kuwapa misaada      mbalimbali
kwani hawawajui wazzi wao,ili nao wajione swa na wato
to wengine

Tuesday, May 27, 2014

HOSPITALI YA MT MERU ARUSHA YAENDELEA KUKABILIWA NA CHANGAMOTO

HOSPITALI ya Mkoa  wa Arusha, Mount Meru, inakabiliwa na upungufu wa
shuka 300 na blanketi 200, kutokana na ongezeko kubwa la wagonjwa kila
siku.

Akizungumzia upungufu huo jana hospitalini hapo, wakati akipokea
msaada wa shuka nyeupe 100 na blanketi 30 toka kwa Kanisa la Calvary
Temple la Kilombero Jijini Arusha,ambalo linaadhimisha miaka 75 tangu
lianzishwe, Mganga Mfawidi wa Hospitali hiyo, Dk. Josiah Mlay, alisema
upungufu ni mkubwa wa vitu hivyo ukizingatia wanakwenda kipindi cha
baridi kali.

Alisema kuwa shuka na blanketi walizonazo kwa sasa nyingi zimechakaa
kutokana na kemikali wanazotumia kufulia wakati zinapochafuka wodini,
hivyo wanahitaji shuka na blanketi zingine haraka kabla ya msimu wa
baridi haujaanza.

"Kwa nyie kutuletea hivi vitu tunashukuru sana na mtabarikiwa, kwani
bado tuna upungufu wa itu hivi mkubwa na tunaomba wadau wengine
wajitokeze kutusaidia kabla ya msimu wa baridi haujaanza,"alisema.

Dk. Mlay alisema kwa sasa hospitali hiyo inachangamoto kubwa ya
ongezeko la wagonjwa na huku mahitaji yao yakipungua, kutokana na
wingi wao, hivyo wanahitaji wasamaria wema wajitokeze kuwasaidia.
Mahitaji mengine wanayohitaji hospitalini hapo alitaja kuwa pamoja na
vifaa vya maabara navyo ni vichache,hivyo wanaomba msaada kwa
wasamaria wema na sio kuiachia serikali ambayo inamajukumu mengi.
Kwa upande wake Emmanuel Mbwiga ambaye ni Mzee wa  Kanisa la Calvary

Temple la Kilombero Jijini Arusha, akitoa msaada huo alisema mbali na
msaada huo pia kupitia vituo vyao mbalimbali wametoa msaada kwenye
vituo vya yatima vya Huruma Kwamurombo,Monduli,Esso.

Pia misaada mingine imetolewa shule za msingi Mwangaza, Olsinyai
Sombetini na Ngarenaro, lengo kubwa kusaidia watu wenye shida ili
wapate faraja nao katika kuadhimisha kilele cha kanisa hilo
kitakachofanyika Kitaifa Mbeya Julai mwaka huu.

Mbwiga alisema vitu walivyotoa maeneo hayo  ni Sabuni, ndoo za mafuta,
mchele, nguo, mahindi,daftari,soksi na vitu vingine vingi, ambavyo
vyote vina jumla ya shilingi milioni 3.

 Hata hivyo alitoa wito kwa watu wenye mapenzi mema kujitokeza
kusaidia hospitali hiyo na maeneo yenye uhitaji kama vitruo vya yatima
na shuleni, ili wabarikiwe zaidi.
Mwisho

UROHO, UPENDELEO WA UTOAJI WA MISAADA KUTOKA KWA WAFADHILI CHANZO KIKUBWA CHA WAFADHILI KUTOKOMEA GIZANI



NaBety Alex, Arusha

IMEELEZWA kuwa Tabia ya uroho na upendeleo unaofanywa na baadhi ya
Viongozi wa Dini, Serikali na Jamii kwa ujumla kwenye ugawaji wa
misaada kutoka kwa wafadhili ndio chanzo kikubwa sana cha Watoto wenye
mahitaji muhimu kutelekezwa na wafadhili.

Hataivyo pia tabia hizo zimekuwa chanzo na kisingizo kikubwa sana cha
makundi maalumu kuweza kusahaulika na hivyo kujikuta wakiwa
wanakabiliwa na hali ngumu sana ya maisha ikiwemo ukosefu wa mahitaji
muhimu.

Hayo yameelezwa na Mchungaji Nakembetwa Shakademasi kutoka katika
kanisa la T A G Kindness Chrstian Centre(KCC)lilopo Ungalmtd wakati
akikabidhi msaada wa ngyo kwa watoto 50 wa eeno hilo la ungalmtd
mapema jana.

Shakademasi alisema kuwa tabia hiyo kwa sasa imejaa kwa viongozi ambao
wapo kwenye sekta mbalimbali hali ambayo inakimbiza  wafadhili wa
ndani na hata wa nje ya nchi.

Alifafanua kuwa, jamii haipaswi kuwa na uroho dhidi ya msaada wowote
ule unaelekezwa kwehnye kundi maalumu wakiwemo watoto bali jamii
inapaswa kuwaunga mkono wafadhili hata kama wametoa vitu ambavyo ni
vizuri kuliko vile vya familia ambazo zina uwezo.

“katika miaka ya sasa inashangaza sana wafadhili wanaogopa kutoa
msaada kwa jamii kwa kuhofia kuchakachuliwa wakati watoto hasa wale
ambao wanatokea mazingira magumu wanakabiliwa na changamoto lukuki za
kimaisha , tunapswa kuwa waminifu hata kama misaada ni mizuri kuliko
ile ambayo tunayo”aliongeza

Katika hatua nyingine alisema kuwa ili wafadhili waweze kuongezeka
hapa nchini misaada inatakiwa kuwafikia walengwa ambao wamekusudiwa
jambo ambalo litaweza kuokoa maisha ya watu walioko kwenye makunid
maalumu.

Pia Mgeni Rasmi kwenye  Hafla hiyo Mchungaji Peter Kitila alisema kuwa
nao watanzania wana uwezo mkubwa wa kuwa wafadhili wa ndani,na kuacha
kutegemea ufadhili kutoka nje ya nchi.

Kitila alidai kuwa kama kila mtanzania akijitolea kuwasaidia watu
wenye maitaji maalumu basi umaskini ndani ya nchi utaweza kupungua kwa
kiwango kikubwa sana tofauti na sasa ambapo wengi bado hawana hamasa
ya kusaidia makundi maalumu yaliopo kwenye jamii.

MWISHO

Wanafunzi 125 kushiriki Riadha manyara



Wanafunzi 125 wa michezo ya riadha, mpira wa miguu, pete na wavu, wa shule za sekondari Wilaya ya Hanang’ wanatarajia kushiriki mashindano ya umoja wa michezo ya shule za sekondari (Umiseta) Mkoani Manyara.


Akizungumza na waandishi wa habari jana, mratibu wa umiseta wilayani humo, Caroline Marshali alisema wavulana na wasichana wa shule tofauti za sekondari wanashiriki michezo mbalimbali ya kutafuta wawakilishi wa wilaya hiyo.

Marshali alisema wanafunzi hao wa shule za sekondari watawakilisha wilaya hiyo kwenye kuruka juu, chini, kutupa mkuki, sahani, tufe, mbio ndefu na za mita 100, 200, 400, 800, 1,500 na mbio ndefu za marathoni.

“Pia kutakuwa na timu za mpira wa miguu za wasichana na wavulana, mpira wa wavu na mpira wa pete na wachezaji wetu wamejiandaa ipasavyo kwenye mashindano haya ili kuipa sifa wilaya yetu,” alisema.

Naye, Mwenyekiti wa umoja wa wakuu wa shule za sekondari (Tahosa) wilayani Hanang’ John Malley alisema wamewaandaa ipasavyo vijana wao ili washiriki kikamilifu michezo hiyo na kuleta ushindi katika wilaya yao.

“Pamoja na hayo tunamshukuru Mbunge wa jimbo letu Mary Nagu kwa kutuunga mkono kwenye maandalizi haya ya kwenda kushiriki mashindano ya mkoa kwa ikiwemo kutupa vyakula,” alisema Malley.

Nao baadhi ya wachezaji wa mpira wa miguu, wavu na kuruka juu, Nobert Aushak, Judith Mkilanya na Anna Aney walisema kupitia michezo wanajijenga kisaikolojia ili wafanikiwe katika masomo yao kwani hawana hofu ya mitihani.

Walidai kuwa zaidi kufahamiana na watu mbalimbali kupitia michezo, pia wanajenga afya zao kwa kuwa wakakamavu na wanajiamini zaidi pindi wakiwa masomoni hivyo wanatarajia kufanikiwa pia kimasomo.

MWISHO.

UKOSEFU WA UPENDO KWA WALIMU CHANZO CHA UTORO MASHULENI

UKOSEFU WA UPENDO KWA WALIMU CHANZO CHA UTORO MASHULENI

Arusha


IMEELEZWA kuwa ili wanafunzi wa shule mbalimbali hapa nchini waweze kupenda shule na kuthamini masomo walimu wanatakiwa kuwa na lugha pamoja na malezi yenye upendo wa hali ya juu tofauti na sasa ambapo zipo baadhi ya shule ambazo zina walimu wasiokuwa na upendo.
Aidha kwa sasa wanafunzi wengi watoro wanakwepa shule kwa kuwa wamekosa matumaini ya upendo toka kwa walimu wao hivyo basi walimu wanapaswa kubadilika.
hayo yameelezwa na Kanali Mstaafu John Mongi wakati akizindua rasmi kamati ya bodi ya shule ya St Benedict Meliyo Primary  iliopo maeneo ya Sekei jijini hapa mapema jana.
kanali Mongi alisema kuwa neno upendo linapaswa kutumika sana ipasavyo na walimu, wakuu wa bodi pamoja na wazazi na kama litaweza kutumika ipasavyo basi litachangia sana hamasa ya elimu hapa nchini .

aliendelea kwa kusema kuwa kwa kukosa upendo kwa baadhi ya walimu kumekuwa chanzo kikubwa sana cha wanafunzi kuona shule kama ni uwanja wa vita na sababu hiyo hiyo pia imechangia sana hata utoro.
"tujifunze kwenye hizi shule ambazo zinaongoza kitaifa jinsi ambavyo walimu, bodi za shule zinavyowapenda wanafunzi,kwa hali hiyo basi mimi nasisiiza kuwa ili elimu iweze kufika katika kiwango cha juu lazima kwanza walimu wawe na upendo na wanafunzi ambao wanawafundisha"aliongeza Kanali Mongi.
hataivyo aliwataka nao walimu mbali na kuhamasiaha upendo  kwa wanafuzni ili kuweza kuepukana na majanga ya utoro shuleni lakini pia muda ambao wanakuwa na wanafunzi wao wahakikishe kuwa wanawaambia juu ya madhara yaliopo hapa nchini kama vile mdondoko wa maadili ili kuweza kuokoa kizazi cha vijana ambacho kwa sasa kinaangamia.
Awali Mkurugenzi mtendaji wa shule hiyo Joseph Laiser alisema kuwa ili kufanya elimu hapa nchini iweze kufikia katika kiwango ambacho kinaitajika tayari shule hiyo imeweka mikakati ya kuwapa semina wazazi , pamoja na viongozi mbalimbali wa shule hiyo .
Laiser alifafanua kuwa kwa kuwapa semina wazazi, walezi, na viongozi wa shule kutaweza kusaidia walengwa wa watoto hao kujua majukumu yao kwani kwa sasa shule nyingi zinashindwa kutekeleza majukumu yake kwa kuwa wanakwamishwa na vitu mbalimbali likiwemo suala zima la wazazi pamoja na walezi .
MWISHO

Tuesday, April 29, 2014

ASKOFU ISANGYA ANENA NA VIJANA

IMEELEZWA kuwa ongezeko la vijana maeneo ya mijini chanzo chake kikubwa ni kuwa asilimia kubwa ya vijana hasa wa vijijini bado hawajaweza kutambua fursa za uchuni  walizonazo hali ambayo nayo inasababisha wimbi kubwa la watu mijini ambao hawana ajira za kutosha


Vijana wanaokimbilia mijini kutoka vijijini ni kutokana na kuwa kule vijijini hawahapata muongozo wa kutambua na kisha kutumia fursa za mali zilizopo jambo ambalo kwa sasa wadau ikiwemo serikali inatakiwa kuchukua tahadhari juu ya hilo.

Kauli hiyo imetolewa na askofu Dkt Eliud Isangya wa kanisa la Intenational evangelism Church  wakati akiongea na waandshi wa habari kuhusiana na fursa za vijana pamoja na changamoto ambazo zinawakabili vijana.

Aidha alidai kuwa inashangaza sana kuona kuwa wimbi kubwa la vijana wanakimbilia mijini wakati huko vijijini kuna fursa za kutosha na hazitumimiki wakati mijini fursa za ajira hazipatikani

Kutokana na hilo alisema kuwa kinachosabbisha waje mijini ni kuwa hawajaweza kutambua fursa zilizopo huku baadhi ya watumishi wa serikali wenye dhamana na vijana nao wakiwa wamesahu wajibu wao kwenye jamii wa kusaidia kundi hilo.

“hawa watendaji wa serikali wakati mwingine wanasahu wajibu wao hata wa kuweza kutangaza fursa za ajira kwa vijana na inasababisha vijana waweze kuona kuwa wapo pekee yao na hivyo wanaona bora waje mjini”aliongeza Dkt Isangya.

Hataivyo alidai kuwa kutokana na hilo asilimia kubwa ya vijana wanaokuja mijini wanasababisha madhara makubwa sana kwani wengi wao wajikuta wakiwa wanaangukia katika matukio ya kihalifu na matukio mabaya ya uharibifu wa amani ya nchi kwa hali hiyo ni changamoto kubwa sana kwa serikali, kwa vijana na hata wadau wa dini’aliongeza Dkt Isangya.
MWISH

NYUMBA ZAIDI YA 300 ZILIZOBOLEWA ARUSHA ZALETA DALILI YA WAWEKEZAJI WA KIMATAIFA

NYUMBA ZAIDI YA 300 ZILIZOBOLEWA ARUSHA ZALETA DALILI YA WAWEKEZAJI WA KIMATAIFA

Arusha

JIJI la Arusha limefanikiwa kuvunja nyumba zaidi ya 300 katika oparesheni maalumu ya kusafisha  jiji huku pia likiweza kuweka mikakati mbalimbali ya kuendelea kuboresha sehemu ambazo zimebomolewa nyumba hizo  huku pia Viongozi nao wakidai kuwa kuanzia kubomolewa kwa nyumba hizo kumeanza kuongeza idadi ya wawekezaji wenye nia ya kuwekza katika maeneo hayo.

Aidha nyumba hizo zilibomolewa siku chache zilizopita ambapo pia zoezi hilo liliweza kwenda sanjarai na ukamataji wa bidhaa ambazo zilikuwa zinauzwa nje bila mipangilio.

Hayo yamelelezwa na Mkuu wa Wilaya ya Arusha John Mongela wakati akiongea na viongozi wa Majiji mbalimbali hapa nchini wakati akielezea mpango wa kuboresha jiji la Arusha

Mongelea alisema kuwa hapoa wali nyumba zilizobomelewa zilikuwa  katikati ya Jiji na zilikuwa zinalipa kodi ndogo sana ukilinganisha na hadhi yenyewe ya Jiji la Arusha hali ambayo ilisababisha waweze kuchukua hatua hiyo.

Hatiavyo Monngela alisema kuwa kabla ya hapo walilazimika kuburutwa mahakani ambapo wenye nyumba hzio walidia kuwa Jiji limewaonea na hivyo hawapaswi kuondolewa katika nyumba hizo.

“hawa walituburuza mahakamani na kudai kuwa tunawaonea sasa sisi tulishinda katika kesi hiyo na tuliweza kubomoa nyumba hizo ambazo walikuwa wanalipa kiasi cha kati ya elfu sita mpaka kumi kama kodi wakati kwenye majumba mengine watu wanalipa mpaka kiasi cha Mamilioni kwa ajili ya nyumba za biashara na nyumba za kuishi”aliongeza Mongela

Hataivyo Mkurugenzi mtendaji wa Jiji Juma Iddi alisema kuwa kwa sasa kuna mpango wa kuweza kuendeleza maeneo hayia mbayo yalikuwa kwanza na ujenzo holela lakini pia yalikuwa hayaingizi faida kubwa kwa Jiji

Iddi alisema kuwa toka nyumbha hizo kubomolewa Jiji la Arusha limekuwa katika taswira tofauti sana kwani kwa sasa hata wawezekaji nao wameanza kujitokeza tofauti na hapo awali ambapo kulikuwa na nyumba hizo

“hapo awali tulikuwa hatufanikiwi kwa lolote hata kodi yao kwetu ilikuwa ni ndogo sana lakini kwa sasa tumeweza kubomoa na sisi tutawekeza kwenye majengo makubwa yenye hadhi zake na wala sio yale”aliongeza Iddi.

Pia alisema kuwa mbali na kuwekeza majengo yenye hadhi ya Jiji na kimataifa kwenye maeneo ambayo nyumba hizo zimebomolewa lakini pia wanampango endelevu wa kuhakikisha kuwa nyumba za Jiji la Arusha zinajengwa kwenye hadhi ambayo inakubalika na wala sio ujenzi holela.

MWISHO

MANYARA WAPEWA CHANGAMOTO YA MABWENI

ILI kupambana na changamoto za elimu kwa watoto wa kike Mkoani Manyara, imeelezwa suluhisho ni kuwajengea mabweni ya kulala kwani hivi sasa wanasoma kwenye mazingira mabovu kutoka na mazingira ya mkoa huo.
 
Wito huo umetolewa Wilayani Mbulu na Mwenyekiti wa Mtandao wa asasi za kiraia mkoani Manyara, (Macsnet) Asia Lembariti, wakati akizungumza juzi kwenye Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo.
 
Lembariti alisema ili kuboresha elimu kwa mtoto wa kike shirika la WEGCC limejikita kufanya utafiti kwenye sekta ya elimu hasa ubora wa mazingira ya upatikanaji wa elimu kwa watoto wa kike katika shule za sekondari.
 
Alisema shule nyingi zipo mbali na kaya nyingi wanakotoka wanafunzi na uhaba wa miundombinu unachangia wanafunzi kutembea umbali mrefu mpaka kilometa 16 hadi 32 kwa siku, kwenda shule na kurudi nyumbani.
 
“Hii ni hatari zaidi kwa watoto wa kike na suluhisho ni mabweni, kwani huchangia mahudhurio hafifu, kuacha shule, kuchochea ubakaji na ujauzito kwani toka mwaka 2004 hadi 2010 watoto 45,256 waliacha masomo,” alisema.
 
Alisema ili kukabiliana na changamoto zote hizo zisababishwazo na kutembea umbali mrefu kwenda na kutoka shule, ujenzi wa mabweni ni muhimu, tofauti na kupanga kwenye magheto na matatizo kwenye vyombo vya usafiri kila siku.
 
Alisema Macsnet inatekeleza miradi minne kwa kushirikiana na wanachama wake ndani ya mkoa huo ikiwemo kuboresha elimu kwa watoto wa kike kuwajengea uwezo wa uandishi wa miradi, kuboresha ufugaji wa asili na kuboresha lishe.
 
“Katika kufanikisha miradi hiyo Wegcc imejikita kufadhili mradi wa kuboresha elimu kwa watoto wa kike na pia tunashirikiana na Usaid katika lishe, Care International kwa ufugaji na FCS utekelezaji miradi,” alisema Lembariti.
 
MWISHO.

WAFANYABIASHARA WAPEWA MBINU YA MABOMU

NA MWANDISHI WETU, ARUSHA


jeshi la polisi mkoa wa Arusha limewaomba wafanyabiashara pamoja na wanachi wote ambao wanakuwa kwenye mikusanyiko mara kwa mara kuhakikisha kuwa wanatumia camera aina ya CCTV ili kuweza kujiepusha na majanga hasa ya mabomu.

Hataivyo kauli hiyo inakuja siku moja mara baada ya kutokea kwa mlipuko wa bomu ambalo linadhani kuwa ni bomu la kienyeji na kisha kulipuka katika baa moja ijulikanayo kama Arusha Night  Park
Kauli hiyo imetolewa Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya Jinai Isaya  Mngulu wakati akiongea na waandishi wa habari juu ya hatua ambazo wamezichukua mpaka sasa juu ya matukio hayo ya mabomu kwa mkoa wa Arusha.


Kamanda Isaya alisema kuwa watu wakichukua tahadhari basi wataweza kuwasaidia wengine kuepukana na vifo ambavyo sio vya lazima kwani kwa sasa magaidi wanaitesa sana jiji la Arusha.

Alidai kuwa kupitia camera hizo tahadhari inaweza kuchukuliwa tofautri na sasa ambapo kwa sasa asilimia kubwa ya mabomu ya kienyeji yanarushwa sana hasa kwenye mikusanyiko ya watu.


Hataivyo alishauri uongozi wa mkoa wa Arusha kuweka mikakati mbalimbali ya kuweka Camera hizo pande zote za Jiji kwani pia hilo nalo litaweeza kusaidia sana kupunguza uhalifu .


Kamanda Isaya alisema kuwa pamoja na kuwa wameweka mikakati mbalimbali ya kuweza kupunguza na kutokomeza uhalifu hasa wa mabomu katika maeneo ya mikusanyiko Polisi wanatarajia kufanya uchunguzi wa tukio hilo ambalo liliweza kujerui watu 15 ingawaje pia watatoa kitita cha Milioni 10 kwa mtu yeyote ambaye ataweza kutoa taarifa na kisha kufanikisha kukamtwa kwa mtuhumiwa.



Alimalizia kwa kusema kuwa katika tukio hilo la kurushwa kwa bomu la kienyeji katika nyumba hiyo ya kulala wageni hali za majerui zinaendelea vizuri na kwa sasa majerui nane wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya mkoa wa Arusha.

Mbali na hayo Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas amewataka wananchi wa Jiji la Arusha wasiwe na hofu juu ya mikusanyiko ila wachukue tahadhari ingawaje kwa sasa wamejipanga kulinda ipasavyo hasa msimu huu wa majira ya sikukuu ya Pasaka.

sabas alidai kuwa wanatarajia kufanya ulinzi wa kutosha kwa kutumia vifaa mbalimbali kama vile Mbwa, Farasi, pamoja na Polisi wenyewe ili kuweza kuwafanya wananchi waweze kusherekea siku hiyo ya Pasaka.

MWISHO

DAWA YA NJAA YAINISHWA

IMEELEZWA kuwa ili nchi ya Tanzania iweze kuepukana na majgana hasa ya baa
la njaa Nchi inapaswa kuzalisha kilimo kwa asilimia zaidi ya sita ambapo
chakula kinachozalishwa kitaweza kuwekwa hadi akiba tofauti na sasa ambapo
uzalishaji wa kilimo ni kwa asilimia 4 pekee.

Hataivyo uzalishaji huo wa asilimia sita pia utaweza kuongeza ufanisi wa
kilimo na kitakuwa ni cha kisasa zaidi hivyo majnga hasa ukosefu wa
chakula,umaskini nao utaweza kupungua kwa kiwango kikubwa sana .

Hayo yameelezwa na Bi Nkuvililwa Simkanga ambaye ni mkurugenzi wa sera na
mipango kutoka katika Wizara ya kilimo na ushirikia wakati akiongea kwa
niaba ya wizara hiyo mara baada ya kukabidhiwa kwa Jengo la kuhifadhia
mazao ambalo limejengwa chini ya uzamini wa  TAHA

Mkurugenzi huyo alidai kuwa kwa sasa Tanzania bado inazalisha Kilimo kwa
kiwango cha Asilimia 4 pekee hali ambayo bado inahitajika kuongezewa nguvu
zaidi kwani uwezekano wa kuendelea kuzalisha kwa wingi sana bado upo endapo
kama kutakuwa na umoja baina ya wakulima na wadai wengine wa Kilimo.

"tukizalisha kilimo chenye ubora na kiwango ambacho kinahitajika basi
tutaweza kupunguza tatizo la uhaba wa chakula na hata umaskini nao
utapungua kwani uwezo wa kufanya hivyo tunao kabisa ila changamoto bado
zinashindwa kutufikisha"aliongeza Bi Simkanga.

Mbali na hayo alisema kuwa Kilimo kinachangia uti wa mgongo wa taifa kwa
asilimia 24.7 huku wananchi nao wakiwa wanategemea kama ajira kwa asilimia
75 ambapo pia asilimia 95 ya chakula kinachotumika hapa nchini kinatokana
na kilimo

"Takwimu zinaonesha kuwa hali si mbaya sana na kilimo kinaendelea vizuri
sana ingawaje pia wakulima wana uwezo mkubwa sana wa kuzalisha chakula
kingi na hata kikaweza kupelekwa nje ya nchi hivyo jitiada za makusudi
zinahitajika kwa haraka sana"aliongeza

Wakati huo huo Mwenyekiti wa TAHA Erick Ngmario    erick alisema kuwa ili
wakulima waweze kufikia malengo yao ya kila siku wanatakiwa kuachana na
mila ambazo zimepitwa na wakati kwani wakati mwingine zinasababisha waweze
kulima kilimo cha umaskini

Erick alidai kuwa moja ya mila hizo amnazo zimepitwa na wakati ni pamoja na
mila za kulima kwa mazoea bila kulima kilimo cha kisasa hali ambayo wakati
mwingine husababisha umaskini ingawaje wanatumikia Kilimo kila mara

"kwa sasa wakulima wanatakiwa kujifunza kulima kilimo ambacho kinatija na
kamwe wasikubali kulima ili waweze kuonekana kama wamelima bali sheria,
taratibu na mbinu za kilimo zinaitajika kufuatwa"aliongeza Erick

Alimalizia pia kwa kuwataka wakulima hasa wa Eneo hilo la Midawi
wahakikishe kuwa wanatumia vyema jengo hilo kwa ajili ya kuhifadhi mazao na
kisha kuondokana na changamoto ya kuharibika kwa mazao.

MWISHO

SHULE YATOA UFADHILI WA MILIONI 90 KWA WANAFUNZI 90 KWA KILA MWAKA


SHULE YATOA UFADHILI WA MILIONI 90 KWA WANAFUNZI 90 KWA KILA MWAKA

SHULE ya Sekondari Edmund iliopo Sinon Mjini Arusha imetenga kiasi cha zaidi Milioni 90 kwa wanafunzi 90 kila mwaka kwa ajili ya kuwasaidia watoto wanaotokea katika mazingira magumu huku lengo likiwa ni kuwaepusha na mimba za utotoni lakini pia uvunjifu wa amani kwenye jamii
hataivyo fedha hizo zinatolewa na wafadhili wa nje ya nchi pamoja na mfuko wa shule hiyo ujulikanao kama Mfuko wa Edmund ambao pia huo unalenga kuhamasisha ufadhili wa ndani
Hayo yameelezwa na Mkwabi Francis ambaye ni mkuu wa shule hiyo wakati akiongea na wanafunzi, wazazi pamoja na walezi wa shule hiyo kwenye maafali ya nane ambapo jumla ya wanafunzi 240 wanatarajia kuhitimu katika shule hiyo.
Mkwabi alisema kuwa mpango huo wa kuwasidia watoto wanaotokea katika mazingira magumu umeweza kuwanufaisha watoto wanaotokea katika vijiji vya Murieth, Mkono,Nadosoito,Ungalmtd, na Sinoni ambapo walengwa ni wale wenye maitaji muhimu
alifafanua kuwa walengwa hao ni wale watoto wanaotokea katika familia ambazo hazina uwezo,na mayatima ambapo watoto hao huweza kukupewa ufadhili maalumu kwa ajili ya kusoma na kupata elimu ya Sekondari.
"wafadhili wetu wakubwa wanatokea katika Nchi za Ausralia, Newzeland,Iland, na Marekani na hawa wanatufanikikishia hawa watoto 90 kuweza kupata elimu yao bora sana ya Sekondari ingawaje na sasa sisi tumejipanga kuhakikisha kuwa na sisi hapa hapa shuleni tunatoa ufadhili kwa watoto wetu ili siku hata kama tukikosa wafadhili basi tunaweza kusaidia jamii'aliongeza Mkwabi
Pia alisema kuwa nao wazazi wanapaswa kujua na kutambua kuwa nao wana nafasi kubwa sana ya kuweza kuwasaidia watoto hasa wale ambao hawana uwezo wa kupata elimu ya sekondari kwani kupitia njia ya ufadhili wa ndani inawezekana kabisa
"kama wazazi, na walezi wakiwa na tabia ya kuchangia sekta ya maendeleo ya shule hasa mifuko ya shule  basi wataweza kusaidia jamii na hatutaweza kuwategemea zaidi wafadhili ambao wanatokea nje ya nchi kwani wakati mwingine wanapokatisha ufadhili wao wanasababisha watoto wawe kwenye hali ya uoga'aliongeza Mkwabi.
Wakati huo huo Wanafunzi wa shule hiyo ambao ni wahitimu waliwashauri walimu wa shule hiyo lakini pia wale wa shule nyingine kuachana na tabia ya kuwatenganisha wanafunzi wa kidato cha kwanza mpaka cha nne dhidi ya wale wa kidato cha tano na sita kwani kwa kufanya hivyo kunasababisha wale wa vidato vya chini kutopata hamasa ya kujiunga au kufanya vema ili kuweza kujiunga na kidato cha tano na sita.
MWISHO

TAASISI ZA FEDHA ZAPEWA CHANGAMOTO

TAASISI  za kifedha zimetakiwa kangalia umuhimu  wa kwawezesha
wakulima  kuwakopesha mikopo kwa kutumia dhamana ya hatimiliki za
kimila ili waweze kulima kilimo cha biashara kwa kuwa ndio dhamana
pekee wakulima waliyo nayo.

Hayo yalisemwa jana  na mkuu  wa wilaya ya arumeru Munasa Nyerembe
alipokuwa akifungua maonyesho ya kilimobiashara ya  kuwaunganisha
wakulima na taasisi  kifedha  yanayofanyika katika viwanja vya AVRDC
tengeru mjini Arusha.

Munasa alisema kuwa asilimia kubwa ya ya wakulima wa vijijini
wanategemea dhamana ya hati miliki za kimila katika kujipatia mikopo
na hivyo taasisi zinapaswa kuhakikisha kuwa zinawawezesha wakulima hao
kwa kuwapatia mokopo ili waweze kuendeleza kilimo chao kiweze kuwa cha
manufaa zaidi.

Alieleza kuwa taasis zinazokataa kukopesha wakulima mikopo kwa kupitia
dhamana ya hati miliki za kimila zinachangia sana kuwanyima wakulima
kutofikia malengo yao ya kilimo cha biashara ambacho ndicho
kinachotegemewa kwa sasa.

Aliongeza kuwa taasisi zozote za kifedha zinazokataa kuwawezesha
wakulima kwa kupitia hati miliki za kimila zinavunja sheria na kwamba
watakaobanika kukataa dhamana hiyo watakchukuliwa hatua za kinidhamu.

“naombeni sana ninyi taasisi za kifedha wapeni wakulima mikopo kwa
kutumia dhamana ya hatimiliki za kimila na ni makosa makubwa sana
kuwanyima mikopo kwa dhamana hii maana ndio dhamana waliyo
nayo”alisistiza

Awali meneja uchumi   benki kuu ya Tanzania tawi la arusha Wilfred
Mbowe akizungumza na wakulima  katika maonyesho  hayo alisema kuwa
benki kuu itaendelea kushirikiana na wakulima kwa kuwapatia mikopo
mbali mbali kwa kuwa ndio benki mama ambayo imezaa taasisi nyinginezo
ambazo zimekuwa bega kwa began a wakulima .

Mbowe alisema benki hiyo itahakikisha kuwa inaendelea kutoa elimu kwa
wakulima na hata pia kusisitizia taasisi nyinginezo umuhimu wa
kushirikiana na wakulima ili kuhakikisha kuwa kilimo cha hapa Tanzania
kinakuwa cha manufaa makubwa zaidi.

Nae mkurugenzi wa chama cha wakulima wa mboga mboga,maua matunda na
viungo(TAHA) Jaqline Mkindi alisema kuwa maonyesho hayo yanachangia
kuwapa wakulima fursa za kuwafanya waweze kukopa katika taasisi za
kifedha kwa kuwa wakulima wengi wameshindwa kufikia malengo ya kilimo
chao kutoka na kukosa mitaji ya biashara.

Alieleza kuwa kupitia maonyesho hayo wakulima watapata elimu na mbinu
ambazo zitawafnya kilimo chao kuwa cha manufaa zaidi huku wakiwa
wanapata hata pembejeo za kilimo chao kwa kupitia taasis hizo ambazo
zitakuwa zinatoa mikopo kwa kupitia dhamana walizo nazo .
mwisho

WAFUGAJI WAASWA


JAMII za wafugaji zimeaswa kuhakikisha kuwa zinajijengea tabia ya kutafuta na kutumia fursa nyingi za mikopo kwani tafiti zinaonesha kuwa wengi wana fursa ila wanashindwa kuzitumia na hivyo kusababisha umaskini kuongezeka kwa asilimia kubwa mwaka hadi mwaka.
Aidha kama jamii hizo za wafugaji zitaweza kutumia vema fursa za mikopo ambazo zipo kwenye taasisi za fedha basi zitachangia sana ongezeko la uchumi tofautiu na sasa ambapo bado wafugaji wengi wanakwepa mikopo hiyo

Hayo yameelezwa na Afisa Ushirika Wilaya ya Longido ,Reginald Lyakurwa wakati akiongea na Wananchi Kitombeine mara baada ya shirika la World Vision kwa kushirikiana na Shirika la Vision Fund kutanga rasmi mradi wa mikopo kwenye jamii ya wafugaji hasa wa eneo hilo mapema jana

Lyakurwa alisema kuwa wafugaji wa sasa wanatakiwa kuachana na mila potofu za kukwepa mikopo na kisha kujiunga kwenye vikundi na kisha kukopa kwa ajili ya kuweza kunenepesha hata mifugo yao ambayo wakati mwingine hufa kutokana na ukosefu wa malisho

Alidai kuwa kama watajiunga kwenye vikundi na kisha kukopa wataweza kufanya kazi ya ufugaji kuwa raisi sana na hivyo wataweza kufuraia kazi zao za ufugaji tofauti na sasa ambapo wengi wanatumikia mifugo

"leo tumeweza kuleta fursa za mikopo hapa Kitombeine kuna fursa nyingi sana za mikopo ila hazitumiki sasa tunaomba wafugaji muweze kukopa na kisha hata muweze kunenepesha mifugo yenu ambayo kama itakuwa kwenye hali nzuri soko lipo karibu tu hapa Kenya ila kama mkiendelea kulea mifugo alafu ni dhaifu kwa kuwa hamna namna ya kuwasaidia ni wazi kuwa mtakuwa mnasumbuka sana na umaskini kamwe hauwezi kuisha"aliongeza Lyakurwa.


Wakati huo huo alidai kuwa kitu kikubwa ambacho kinawafanya wafugaji wengi washindwe kukopa ni kutokana na kuwa wengi bado wanafikra potofu juu ya mikopo hali ambayo wakati mwingine inachochea umaskini.

wakati huo huo Kaimu Mratibu wa mradi huo wa Mikopo katika eneo hilo Bw George Banyenza alisema kuwa mradi huo ni wa maendeleo na lengo lake halisi ni kuhakikisha kuwa wananchi wanaepukana na umaskini

Banyenza alisema kuwa waliweza kufanya tafiti kwa miaka mingi iliyopita na kisha kuweza kugundua kuwa endapo kama eneo hilo la Kitombeine litapata  miradi ya kukopa basi litaweza kuwa  balozi mzuri sana wa maendeleo kwa nchi za jirani

Alimalizia kwa kusema kuwa mradi huo utaweza kuwanufaisha wananchi zaidi ya 500 ambapo wataweza kupata fursa za mikopo na kisha kujinufaisha wao wenyewe na hata mifugo yao ambayo wanaitumia kama ajira kwenye maisha yao ya kila siku.

MWISHO

Zaidi ya wakulima 500 kupewa elimu ya rasilimali fedha.

Zaidi ya wakulima 500 kupewa elimu ya rasilimali fedha.
 ,Arusha.

ZAIDI  ya wakulima 500 kutoka katika kanda ya kaskazini wanatarajiwa kupewa elimu ya Rasilimali fedha,na kuongeza ufahamu na uelewa juu ya huduma mbalimbali za kifedha zitolewazo na Mabenki.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi mtendaji wa chama cha wakulima wa mbogamboga,matunda na viungo(TAHA) JacKline Mkindi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na maonesho ya kuunganisha kilimo biashara na taasisi za kifedha yatakayofanyika April 25 na 26 mwaka huu katika viwanja vya AVDRC Tengeru.

Alisema kuwa,kwa sasa asilimia kubwa ya taasisi za kifedha zimekuwa zikiwakandamiza wakulima kwa kuwatoza riba kubwa kwenye mikopo hali ambayo imekuwa ikiwasababishia wakulima hao kupoteza imani na mikopo kutoka katika taasisi hizo.
Alidai kuwa hali hiyo imekuwa ni changamoto kubwa sana kwa wakulima hao,kwani wakati mwingine imewawia vigumu kushindwa kufikia malengo yao waliyojiwekea kutokana na ukosefu wa fedha za kutosha katika kuendesha miradi yao midogomidogo.

‘kutokana na changamoto hiyo sasa tumeamua kuandaa maonesho yatakayoweza kuwakutanisha taasisi za kifedha pamoja na wakulima ambapo hapo taasisi hizo zitaweza kutambua mahitaji ya wakulima,na jinsi ya kuweza kuwasaidia tofauti na hapo awali’alisema Jackline .

Pia alisema kuwa maonesho hayo yataenda sambasamba na uwasilishwaji wa mada mbalimbali ikiwemo uaandaji bora wa mipango biashara,umuhimu wa soko la hisa katika kuhakikisha upatikanaji wa mitaji wa muda mrefu,na matumizi bora ya mikopo katika biashara hususani za kilimo  ili walengwa waweze kujifunza zaidi juu ya mbinu bora za kufikia na kupata mitaji kwa kufanya biashara.
Kwa upande wake mratibu wa mtandao wa Agri-Hub Tanzania Bw Tom Ole Sikar alisema kuwa maonesho hayo yanalenga kuwawezesha wakulima pamoja na wamiliki wa biashara za kilimo kama vile wachuuzi,wauzaji wa pembejeo na wasindikaji kutambua fursa mbalimbali za mitaji pamoja na usalama wa kifedha zilizopo kwa biashara za kilimo.

Hata hivyo alisema kuwa wadau ambao wengi wao ni wakulima wataweza kupata fursa ya kutambua njia bora za kuboresha biashara na utoaji wa huduma kwa walengwa pamoja na kujifunza kutoka kwa wafanyabiashara wengine wa kilimo waliofanikiwa kutembelea maonesho yaliyopita.

MWISHO

VIJANA ZAIDI 1000 WA UVCCM MERU, WAFUNGA BARABARA, WAVAMIA OFISI ZA CCM MKOA WAKIDAI KUWA WAMECHOSHWA KUCHAGULIWA VIONGOZI NA MAKAO MAKUU

VIJANA ZAIDI 1000 WA UVCCM MERU, WAFUNGA BARABARA, WAVAMIA OFISI ZA CCM MKOA WAKIDAI KUWA WAMECHOSHWA KUCHAGULIWA VIONGOZI NA MAKAO MAKUU

Na Queen Lema, Arusha

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida vijana zaidi ya 1000 ambao ni wanachama wa umoja wa vijana chama cha mapinduzi (UVCCM)wilaya ya Meru mkoa wa Arusha wamevamia ofisi za chama hicho kuanzia ngazi ya Wilaya hadi mkoa huku wakidai kuwa Makao makuu ya chama hicho wamewaonea kwa kutangaza uamuzi wao wa kuwachagulia viongozi tofauti na matakwa yao ambapo wao walimchagua Kamanda wao ambaye Ni John Palangyo ila CCM makao makuu walitofautiana nao.
hataivyo maandamano hayo ambayo yaliratibiwa na wajumbe wa UVCCM Meru yaliweza kusababisha shuguli mbalimbali za chama hicho kuanzia ofisi ya Wilaya hadi Mkoa kusimama kwa kuwa wajumbe hao walilazimika kuingia kwa nguvu ndani ya ofisi hizo na kisha kushinikiza kusikilizwa kwa madai yao
Akiongea kwa niaba ya wajumbe hao mmoja wa wajumbe hao Joshua Mbwana "Mwarabu"alisema kuwa kilichosababisha waweze kufanya maandamano hayo ambayo yalianzia kuanzia eneo la Usa River Mpaka Arusha ni kuelezea umma kuwa wapo baadhi ya viongozi katika chama hicho ambao wanawachagulia viongozi wa kuwaongoza bila kuwauliza
"hivi juzi tulikuwa na tulimchagua kamanda wetu ambaye ni John Palangyo na tulimpitisha lakini baada ya jina kufika mkoani ghafa jina lilibadilishwa kama haitoshi makao makuu wakasema kuwa wana mtu wao sasa je wao ndio wanatuchagulia mtu wa kutuongoza au sisi kamwe hatutakubali na badala yake tutapigana hadi mwisho hii tabia imetucosha sana"aliongeza Joshua

wakati huo huo alidai kuwa endapo kama hali hiyo itaendelea kufanyika ambapo wananchi, wajumbe, na wanachama watachagua kiongozi alafu makao makuu pamoja na uongozi wa Mkoa wakakataa basi mapambano yatakuwa makubwa sana.
Kutokana na hilo mjumbe huyo alisema kuwa pamoja na kuwa wamevamia ofisi za CCM wakiwa wanachama zaidi ya 300 bado kama hawatapewa majibu yha kuridhisha juu ya kamanda wa vijana ambaye amechaguliwa kwa kura zote na wajumbe wa baraza hilo basi ndani ya siku nne kutoka sasa huenda wakaandamana hadi makao makuu ya ofisi za CCM
"tumesharatibu maandamano hayo na yataenda vizuri itakuwa ni histori a kwa CCM kuchagulia viongozi kwa maslahi yao binafsi na matakwa ya viongozi wa ngazi za juu hasa wale ambao wana malengo ya kugombea nafasi za ubunge katika majimbo kwani ujumbe wetu ni lazima tutauweka wazi na kila mtu aweze kuosoma lakini hata kuingia ndani ya ofisi hizo bila taarifa wala kibali cha aina yoyote ile"aliongeza Joshua.
Hataivyo Katibu wa chama hicho Wilaya ya Meru, Langaeli Akyoo alisema kuwa mchakato wa kumpata kiongozi ambaye vijana hao wanamtaka ulienda vizuri na majina matatu yalifikishwa Dar es saalam makao makuu lakini baadaye hayakurudi kama ilivyoratarjiwa
Akyoo alisema kuwa majina mawili yalirudi majina mawili ambayo yana utata mkubwa ambapo utata huo ndio uliosababisha maandamano makubwa kuanzia Meru hadi Arusha
"jamani maombi yenu nimeyapata na ninapenda kuwaambia kuwa majina ambayo yalienda Dar es saalam makao makuu yalirudishwa mawili ambayo yana utata na wao walisema kuwa mchakato unatakiwa kuanza moja jambo ambalo sisi hatukubalini nalo kabisa"aliongeza Akyoo

Awali mwenyekiti wa umoja wa vijana Wilaya hiyo Bw Elirehema Mbisse alisema kuwa mchakato wa kumpata Kamanda huyo unaendelea na hivyo amewataka wawe na subira ili waweze kuangalia namna ya kutatua tatizo hilo ambalo limesababisha ofisi za CCM  kusimamisha kazi kwa muda.

Hataivyo Uongozi wa Uvccm kupitia kikao chake cha kamati ya utekelezaji kilipendekeza majina matatu ambayo ni John .D.Palangyo, Sioi Solomoni Sumari, na Daniel Mirisho Palangyo,na baadaye mutsari uliweza kupelekwa mkoani ambapo Mkoa ulijiridhisha na majina hayo na uliweza kuhoji na hatimaye waliweza kumpata John.D.Palangyo kama Kamanda wa Vijana Wilaya ya Meru,lakini baadaye barua ilikuja na kudai kuwa kamanda wa Meru siyo huyo jambo ambalo si la kweli.

MWISHO