Monday, May 6, 2013

Bilion 9.8 zatengwa kwa ajili mikopo kwa wachimbaji wadogo

Na Wankyo Gati,arusha

Serikali imetenga  sh.bilioni 9.8 kwa ajili ya mikopo ya vifaa kwa wachimbaji wadogo nchi nzima ili kuboresha uchimbaji wao na watakopeshwa kupitia vikundi watakavyojiunga na itakuwa mkopo endelevu ili kuinua sekta hiyo ya madini kupitia wachimbaji hao.
Hayo yalisemwa leo na Kamishna wa madini wa kanda ya kaskazini Eng.Benjamini Mchwampaka  wakati wa mahojiano na waaandishi wa habari yaliyofanyika katika ofisi za kanda hiyo zilizoko mkoani arusha.

Alisema kuwa kupitia mikopo hiyo itatoa fursa mbalimbali kwa wachimbaji hao kupata vifaaa hivyo ili kuweza kuinua uchimbaji wao na kuwa wa kisasa zaidi ili kuongeza uzalishaji wa madini nchini ambapo hivi sasa wamekuwa wakikwamishwa na ukosefu wa vifaa vya kisasa hali ambayo wanachimba ila hawapati madini ya kutosha.

Ameongeza kuwa wachimbaji wadogo wa kanda ya kaskazini  bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali  katika uzalishaji madini ikiwemo  kutokuwa na vifaa vya uchimbnaji vya kisasa ,bei kubwa ya milipuko na elimu ndogo ya uchimbaji madini hayo  hali ambayo inakwamisha jitihada zao za kuchimba madini hayo na kuwarudisha nyuma katika kujikwamua kiuchumi
.
Alisema kuwa hivi sasa wachimbaji wadogo walio wengi wanachimba kwa mazoea na vifaa duni ambapo elimu ya utambuzi madini  sehemu yalipo ni ndogo hali ambayo inasababisha kutopata madini yakutosha na kutumia gharama kubwa zaidi.

Eng.Mchwampaka alisema kuwa katika kanda hii wachimbaji wamekuwa wakichimba kiholela bila lessen hali ambayo inaweza kuhatarisha usalama wa maisha yao na hata kusababisha kifo na madhara mbalimbali ambapo  maeneo hayo yanachimbwa kwa kesi sana  hali ambayo ni hatari kwa  badala yake wachimbaji wafate taratibu za kuchimba eneo tengefu kwa madini kwa maendeleo yao na usalama wa maisha yao kuepuka kupoteza nguvu kazi ya taifa.

Aidha aliongeza kuwa hivi sasa ofisi ya kanda imejiwekea mkakati mbalimbali ikiwemo kusogeza huduma karibu na wachimbaji katika kanda hii hususan kutoa elimu ,ya uchimbaji wa madini kitaalamu zaidi,hali ya masoko ,afya migodini  ,ajira na kutoa mafunzo kwa vitendo ya namna ya ulipuaji  mogodini sambamba na watatoa fursa ya namna ya uchimbaji salama na wenye tija na maendeleo kwa maslahi yao na taifa kwa ujumla.

Eng.Mchwampakka alisema kuwa hivi sasa wako kwenye mchakato wa kuandaa maonyesho ya vito ,na madini mbalimbali  yatakayofanyika oktoba 28 hadi 30 mwaka huu mkoani hapa  ambapo watahiusisha wafanyabiashara wote ncnini na nchi jiran ikiwemo Kenya ,DRC kongo ,Zambia ,Madagascar ,Malawi ,Ethiopia ,Afrika ya kusini na Msumbiji ili kuweza kubadilishana uzoefu na kuweza kuongeza ushindani katika sekta ya madini nchini.
Mwisho.

WANANCHI WALALAMIKA KIJIJI KUKOSA MAPATO KWA MIAKA MITANO MWENYEKITI ADAI KUWA ANAONEWA VWIVU NA WANANCHI

Na Queen Lema,ARISHA

WANANCHI WALALAMIKA KIJIJI KUKOSA MAPATO KWA MIAKA MITANO MWENYEKITI ADAI KUWA ANAONEWA VWIVU NA WANANCHI

Wanananchi wa Kijiji cha Ilikirioti Kata ya Moivo Wilaya ya Arusha wamemuomba Mkuu wa wilaya  Munasa Nyirembe  kuingilia kati kwenye uongozi wa kijiji hicho kwa kuwa uongozi huo unadai kuwa toka mwaka 2009 mpaka sasa hawajafanikiwa kupata mapato ya aiana yoyote ile.

Wananchi hao waliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw Prosper Steven ili kujadili ili kuweza kusoma matumizi ya kijiji hicho.

Wananchi hao walidai kuwa ni aibu kubwa sana kuona kuwa kila siku ndani ya kijiji hicho wanapata asilimia kumi ya mashamba yanaouzwa lakini pia hata michango lakini uongozi wa kijiji unadai kuwa hauna fedha yoyote ile toka mwaka 2009

Aidha walidai kuwa kwa kukosa kijiji kukosa mapato huku wananchi wakiwa wanashangishwa fedha mbalimbali kunaashiria harufu ya Rushwa lakini pia harufu ya ukandamizaji wa hali ya juu jambo amblo kama Mkuu wa Wilaya hataingilia kati basi huenda liksababisha matatizo makubwa sana

“tunamuomba Mkuu wa wilaya hii pamoja na mkurugenzi waje hapa Kijijini waje wajione hali ilivyo hatuna hata barabara lakini tunaambiwa kuwa eti mapato hayapo na sisi tunachanga kila siku na mtu akija kununua shamba ni lazima atoe asilimia kumi sasa kama hali itaendelea hivi je mwisho wake utakuwa ni upi kama sio kudodondosha damu?walihoji wananchi hao.

Lakini mbali na hayo walidai kuwa ndani ya Kijiji hicho hakuna ulinzi pamoja na usalama wa mali zao kutokana na kituo cha polisi kuwa mbali na makazi yao hali ambayo inatakiwa kutatuliwa kwa haraka sana

Walifafanua kuwa umbali ambaop upo ndani ya Kijiji hicho unasababisha baadhi ya waahalifu kuiba huku wakiwa wanajiamini kabisa kwa kile ambacho wanakifanya kwa kuwa mpaka polisi watoke mjini na kufika katika eneo hilo watakuwa wameshamaliza kuiba wananchokitaka jambo ambalo wakati mwingine linasababisha Umaskini wa kutisha.

Awali Mwenyekiti wa Kijiji ghicho Prosper Steven alidai kuwa kinachoendelea kijijini hapo wivu kwa kuwa amejenga nyumba kubwa nay a kifahari lakini kijiji hakina mapato ya iana yoyote ile hivyo wananchi hawapswi kukosa imani nae

“nawashangaa sana hawa wananchi wanaosema kuwa kijiji hakina mapato kwa miaka mimi najua kuwa hii ni roho ya wivu kwa kuwa nimejenga nyumba ya kifahari kuliko wao na ndio maana wanaongoza kwa kudai kuwa ningatuke kwa kuwa ninachakachua mapato ya Kijiji”alisema Prosper.

Mwisho

BALOZI WA VATIKAN ALIPUKIWA NA BOMU,MMOJA AFA WENGINE ZAIDI YA THELATHINI WAJERULIWA VIBAYA KANISANI. Katika hali isiyokuwa ya kawaida kundi la watu wasiofahamika wametupa bomu katika kanisa la Roman Katoliki la Mt Joseph mfanyakazi liliopo Olasiti Mjini hapa na kusababisha mtu mmoja kufariki dunia huku wengine thelathini wakiwa majerui Bomu hilo lilirushwa na watu wasiojulikana majira ya saa nne za asubuhi ambapo kanisa hilo lilikuwa linazinduliwa na a balozi wa Vatikan nchini, Fransisko Padika Akidhibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas alisema kuwa tukio hilo lilitokea asubuhi wakati balozi huyo akijiandaa kukata utepe wa kanisa hilo jipya Sabas alisema kuwa wakati balozi huyo anakata utepe huo ghafla mtu asiojulika alirushwa bomu ambalo liliweza kuwajerui watu huku likisababisha mauti ya mtoto mmoja "huyu balozi alikuwa hapa Arusha toka siku ya alhamisi lakini leo sisi tulikuwa na ulinzi wa kutosha juu yake lakini wakati anakata utepe ghafla alilipukiwa na bomu hali ambayo ilisababisha vurugu kubwa sana katika kanisa hilo jipya"alisema Sabasi Pia aliongeza kuwa mpaka sasa polisi inamshikilia mtu mmoja ambaye hajajulikana makazi yake lakini uchunguzi unaendelea huku jeshi hilo likiomba msaada wa wananchi lakini pia msaada wa majeshi mengine ili kuweza kuchunguza tatizo hilo. wakati huo huo Mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo akiongea kwa niaba ya Serikali alisema kuwa wananchi wa jiji la Arusha hawapaswi kujiuliza chanzo na kuhusisha tukio hilo na imani za kidini bali wanatakiwa kutoa ushirikiano alisema kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa majerui wote wanapata matibabu ingawaje bado kuna ukosefu wa vifaa katika hospitali ya mkoa wa Arusha (Mt Meru) "kazi ya uchunguzi tunatakiwa kuachia vyombo vya usalama pekee tuwe watulivu na tutoe taarifa kwa Polisi lakini pia tunaomba msaada wa madaktari wa ziada katika hospitali kwani hawa majerui wameumia vibaya sana"alifafanua Magesa Wakati huohuo Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Goodbless Lema alisema kuwa matukio ya uharibifu wa makanisa ni mwendelezo wa kile kilichotokea Zanzibar, na Dar es Saalam lakiniSerikali bado haiskii wala kuona mpaka idadi kubwa sana ya watu wafe. Lema alisema kuwa lazima mambo kama hayo yatatokea kwa kuwa wanasiasa wa sasa wanatafuta umaarufu kwenye makanisa hususani uzinduzi bila kujua na kutambua kuwa kuna hatari kama hiyo. Aliyataka makanisa kuachana na tabia ya kuwa karibu na wanasiasa na badala yake wahakikishe kuwa wanajitegemea kwa michango yao wao wenyewe kwan kuwa siasa haziendi kabisa kwenye makanisa. Hataivyo Waumini waliojeruhiwa katika tukio hilo ambao wamelazwa katika hospital za mount Meru, na hospital teule ya jiji la Arusha ya St Elizabethi , wametambulika kuwa ni John Thadei,Regina Fredirik, Joram kisera, Novelt John, Rose pius, John James,Anna Kessy, Joan Temba, Neema kihisu, Regina Fredirik, Joram Kisela, Vovalt John, Gloria Tesha, Inocent Charles, Fatuma Haji, Fikiri Keya, John James, Anna Kessy, Simon Andrew, Anna Edward, . Wengine ni Lioba Osward , Ropse Pius, Philimon Gereza, Kisesa Mbaga, Neema Daud, Beata Cornel na Debora Joachim. Wakati huo huo jeshi la polisi limelazimika kutumia mabomu kumnusuru mwendesha boda boda mmoja katika eneo hilo anayedaiwa alimtorosha mtu anayesadikiwa alirusha bomu hilo lililoaangukia mbele ya kanisa hilo na kujeruhi waumini hao. MWISHO

picha ya kwanza ni jengo la kanisa la st joseph mfanyakazi mara baada ya baadhi ya waumini wake kupigwa na mabomu



baadhi ya majerui katika tukio hilo


majeruhi wengine tena katika tukio hilo


BALOZI WA VATIKAN ALIPUKIWA NA BOMU,MMOJA AFA WENGINE ZAIDI YA THELATHINI WAJERULIWA VIBAYA KANISANI.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida kundi la watu wasiofahamika wametupa bomu katika kanisa la
Roman Katoliki la Mt Joseph mfanyakazi liliopo Olasiti Mjini hapa na kusababisha mtu mmoja kufariki dunia huku wengine thelathini wakiwa majerui

Bomu hilo lilirushwa na watu wasiojulikana majira ya saa nne za asubuhi ambapo kanisa hilo lilikuwa linazinduliwa na
a balozi wa Vatikan nchini, Fransisko  Padika
Akidhibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas  alisema kuwa tukio hilo lilitokea asubuhi wakati balozi huyo akijiandaa kukata utepe wa kanisa hilo jipya

Sabas alisema kuwa  wakati balozi huyo anakata utepe huo ghafla mtu asiojulika alirushwa bomu ambalo liliweza kuwajerui watu huku likisababisha mauti ya mtoto mmoja

"huyu balozi alikuwa hapa Arusha toka siku ya alhamisi lakini leo sisi tulikuwa na ulinzi wa kutosha juu yake lakini wakati anakata utepe ghafla alilipukiwa na bomu hali ambayo ilisababisha vurugu kubwa sana katika kanisa hilo jipya"alisema Sabasi

Pia aliongeza kuwa mpaka sasa polisi inamshikilia mtu mmoja ambaye hajajulikana makazi yake lakini uchunguzi unaendelea huku jeshi hilo likiomba msaada wa wananchi lakini pia msaada wa  majeshi mengine ili kuweza kuchunguza tatizo hilo.

wakati huo huo Mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo akiongea kwa niaba ya Serikali alisema kuwa wananchi wa jiji la Arusha hawapaswi kujiuliza chanzo na kuhusisha tukio hilo na imani za kidini bali wanatakiwa kutoa ushirikiano

alisema kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa majerui wote wanapata matibabu ingawaje bado kuna ukosefu wa vifaa katika hospitali ya mkoa wa Arusha (Mt Meru)

"kazi ya uchunguzi tunatakiwa kuachia vyombo vya usalama pekee tuwe watulivu na tutoe taarifa kwa Polisi lakini pia tunaomba msaada wa madaktari wa ziada katika hospitali kwani hawa majerui wameumia vibaya sana"alifafanua Magesa

Wakati huohuo Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Goodbless Lema alisema kuwa matukio ya uharibifu wa makanisa ni mwendelezo wa kile kilichotokea Zanzibar, na Dar es Saalam lakiniSerikali bado haiskii wala kuona mpaka idadi kubwa sana ya watu wafe.

Lema alisema kuwa lazima mambo kama hayo yatatokea kwa kuwa wanasiasa wa sasa wanatafuta umaarufu kwenye makanisa hususani uzinduzi bila kujua na kutambua kuwa kuna hatari kama hiyo.

Aliyataka makanisa kuachana na tabia ya kuwa karibu na wanasiasa na badala yake wahakikishe kuwa wanajitegemea kwa michango yao wao wenyewe kwan kuwa siasa haziendi kabisa kwenye makanisa.

Hataivyo Waumini waliojeruhiwa katika tukio hilo ambao wamelazwa katika hospital z mount Meru, na hospital teule ya jiji la Arusha ya St Elizabethi , wametambulika kuwa ni John Thadei,Regina   Fredirik, Joram  kisera, Novelt  John, Rose  pius, John  James,Anna Kessy, Joan Temba, Neema kihisu, Regina Fredirik, Joram Kisela, Vovalt  John, Gloria Tesha, Inocent Charles, Fatuma Haji, Fikiri Keya, John James, Anna Kessy, Simon Andrew, Anna Edward, .

Wengine ni Lioba Osward , Ropse Pius, Philimon Gereza, Kisesa Mbaga, Neema Daud, Beata Cornel na Debora Joachim.



Wakati huo huo  jeshi la polisi limelazimika kutumia mabomu kumnusuru  mwendesha boda boda mmoja katika eneo hilo anayedaiwa alimtorosha mtu anayesadikiwa alirusha bomu hilo lililoaangukia mbele ya kanisa hilo na kujeruhi waumini hao.

MWISHO




Kamati ya maendeleo ya Mirerani yatembelea nyumba 26 zilizoharibika kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha


Diwani wa kata ya Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara,Justin Nyari akikagua nyumba ya mkazi wa mtaa wa Songambele,Katarina Selemani iliyoanguka kutokana na mafuriko yaliyotokea juzi na kuathiri baadhi ya nyumba na mazao ya wakazi wa kata hiyo.picha na Queen Lema,Simanjiro








                                     




Kamati ya maendeleo ya Kata ya Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, imetembelea maeneo yaliyoathirika na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha hivi sasa sehemu tofauti hapa nchini.

Akiongoza msafara huo juzi,Diwani wa kata ya Mirerani Justin Nyari aliwapa pole waathirika wa mafuriko hayo ambapo nyumba zaidi ya 26 na mazao mbalimbali yaliathirika kutokana na mafuriko hayo.

Akizungumza na baadhi ya waathirika hao,Nyari alisema ameshatoa taarifa kwa Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Simanjiro,Patrice Saduka kwa ajili ya hatua zaidi ya kutatua tatizo hilo.

“Hatua ya kwanza tuliyochukua na WDC yangu ni kutembelea na kubaini sehemu zilizoathirika na kutoa taarifa wilayani na watamtuma mhandisi Agai,lakini kubwa zaidi mji wa Mirerani unapaswa upimwe,” alisema Nyari.

Hata hivyo,Diwani wa kata hiyo Nyari alimkabidhi kifuta machozi cha fedha mmoja kati ya waathirika wa mafuriko hayo,Katarina Selemani mkazi wa Songambele ambaye nyumba aliyokuwa anashi ilibomolewa na mafuriko hayo.

Naye,mwathirika mwingine wa mafuriko hayo Boniface Mboya,akizungumza mbele ya kamati hiyo alisema mafuriko hayo yameathiri eneo analoishi kwani miti 750 ilichukuliwa na mafuriko,miche 1,300 na maua 250 na choo kubomoka.

Baadhi ya waathirika wa mafuriko hayo walidai kuwa,mvua kubwa zilizonyesha kwenye maeneo tofauti ya mkoa wa Arusha,yamesababisha mafuriko hayo yaliyopitia Msitu wa Mbogo,Mbuguni hadi eneo hilo na kuelekea Majengo.

MWISHO.





TANROAD ARUSHA YALAZIMIKA KUTUMIA MILION 700 KUKARABATI BARABARA ZILIZOHARIBIKA VIBAYA NA MVUA

Na gladness ,Arusha

TANROAD ARUSHA YALAZIMIKA KUTUMIA MILION 700 KUKARABATI BARABARA ZILIZOHARIBIKA VIBAYA NA MVUA

WAKALA  wa barabara mkoa wa Arusha (TANROAD)umelazimika kutumia kiasi cha zaidi ya Milion 700 kutokana na baadhi ya barabara kuharibiwa vibaya na mvua ambazo zinazoendelea kunyesha Jijini hapa

Akiongea na “Malkia wa matukio”mapema jana meneja wa Tanroad mkoa wa Arusha,Bw Deusdedit Kakoko alisema akuwa wamelazimika kutumia fedha hizo kwa ajili ya kukarabati baadhi ya barabara

Kakoko alisema kuwa kwa kipindi hiki baadhi ya barabara zimeharibika vibaya sana huku hali hiyo ikisababisha baadhi ya watumiaji wa barabara kushindwa kutumia kwa ajili ya shuguli za kila siku.
“hizi milioni 700 zimelazimika kutumika ili kuweza kurekebisha miundo mbinu tena kwa haraka sana na kama tusingefanya hivyo ni wazi kuwa wananchi wanaotumia barabara hizi wasingeweza kupata msaadawa haraka ingawaje bajeti yetu haikuwa hivyo”alisema Kakoko

Alitaja Barabara ambayo zimeharibika vibaya kutokana na mafuriko  pamoja na mvua ambazo zinaendelea kunyesha Jijini hapa ni pamoja na barabara ya Monduli Lokisare,barabara ya pili ikiwa ni Makuyuni Ngorongoro,Barabara ya Tatu ni Karatu Kilimapunda.

Mbali na hayo Kakoko alisema kuwa pamoja na kuwa wamelazimika kutumia kiasi hicho cha fedha lakini pia kuna umuhimu mkubwa sana wa Halmashauri za Mkoa wa Arusha kuhakikisha kuwa wanatenga maeneo ya maegesho ya magari

Alisema kuwa kwa sasa TANROAD inapata wakati mgumu sana kwa kuwa baadhi ya maeneo ya miji hakuna maegesho hali ambayo wakati mwingine inasababisha  magari makubwa ya mizigo kuegeshwa katikatati ya Mji hali ambayo wakati miwingine inasababisha vurugu kubwa sana


Amezitaka Halmashauri kuacha kuona suala la kutenga maegesho kama ni suala la utani badala yake wahakikishe kuwa hata kama hawana maegesho ya magari wanayatenga kwa haraka sana kwa kuwasasa wapo baadhi ya madereva wanaofanya makosa kwa visingizo kuwa hakuna maegesho ya magari

“ni vema kama halmashauri zikahakikisha kuwa kila halmashauri inakuwa na maegesho lakini kama maeneo ya maegesho yatakwepwa ni wazi kuwa malengo ya Tanroad hayatafikiwa na badala yake yatasababisha vurugu ingawaje Arusha ni Mji wa Kimataifa”alisema Kakoko.

ANDIKENI HABARI ZA UCHUNGUZI ZAIDI ACHANENI NA HABARI ZA SEMINA NA MIKUTANO- MWOLEKA

ANDIKENI HABARI ZA UCHUNGUZI ZAIDI ACHANENI NA HABARI ZA SEMINA NA
MIKUTANO- MWOLEKA

WAANDISHI wa habari hapa Nchini wameaswa kuhakikisha kuwa wanajiwekea
utatibu wa kuandika zaidi habari za uchunguzi kuliko kurtegemea habari
za semina na mikutano kwani habari za mikutano na semina bado hazitoi
majawabu na changamoto kwa jamii

Endapo kama waandishi wa habari wa Tanzania wataweza kujiwekea utaribu
wa kuandika habari ambazo zina uchunguzi wa kutosha basi watakuwa ni
chanzo kikubwa sana cha maendeleo ya Nchi

Hayo yalielezwa Jana na Anjelo Mwoleka ambaye ni Mkurugenzi wa Jambo
Arusha Publisher wakati  akiongea na wahitimu wa fani ya uandishi wa
habari katika chuo cha uandishi wa habari Arusha (AJTC) katika maafali
ya sita ya chuo hicho yaliyofanyika chuoni hapo.

Aidha Mwoleka alisema kuwa kwa sasa kuna wimbi kubwa la waandishi wa
habari a wanajihusisha zaidi na masuala ya habari za Semina na
kuachana na habari za kiuchunguzi hali ambayo wakati mwingine ina
nyima haki za msingi za jamii kwa kuwa waandishi wa habari wana nafasi
kubwa sana ya kuibua maovu yanaoendelea kwenye Jamii

Alifafanua kuwa habari za uchunguzi ndani ya Nchi ya Tanzania ni
muhimu sana kwa maendeleo ya nchi hivyo basi wana habari hawapswi
kukimbia na badala yake wanapswa kuzipa kipaumbele kikubwa ili kuweza
kuruhusu changamoto kwenye sekta zote kujilikana

“kuwa mwandishi wa habari sio lazima uwe unajua ratiba za mikutano za
kila siku bali kuna maana kuwa unapaswa kujua na kutambua kuwa
unatakiwa lkuwa mchunguzi na hapo ndio kazi yako itakuwa na manufaa
makubwa sana kwa jamii hivyo basi habari za muhimu zinatakiwa kupewa
kipaumbele tena kikubwa sana ili nchi ya Tanzania iweze kufika mahali
ambapo inatakiwa kufika kama zilivyo nchi nyingine ambazo zimeendelea
duniani”aliongeza Mwoleka

Pia alisema kuwa ili wana habari waweze kufika malengo yao mbalimbali
wanapaswa kujiepusha na rushwa pindi wanapokuwa kazini kwani Rushwa
husababisha sana baadhi ya wananchi kukosa haki ya habari hapa nchini
hivyo kuruhusu wimbi kubwa sana la udanganyifu

Alifafanua kuwa endapo kama watakimbia Rushwa basi watachangia hata
wale watenda maovu kwenye jamii kuweza kuonekana kwa haraka sana hivyo
mlengwa wa haki ataweza kupata tofauti na pale ambapo watajihusisha na
rushwa

Awali wahitimu wa mafunzo hayo ya uandishi wa habari katika ngazi ya
cheti, na shahada walisema kuwa pamoja na kuwa chuo hicho kimewalea
katika maadili mazuri lakini bado wanakabiliwa na uhaba wa vifaa kama
vile Kompyuta, na Kamera kwa ajili ya mazoezi.

UGONJWA WA MAHINDI KUTOKA KENYA WAWAATHIRI WANANCHI KATA YA KIKWE MERU

Na Queen Lema, MERU

UGONJWA WA MAHINDI KUTOKA KENYA WAWAATHIRI WANANCHI KATA YA KIKWE MERU

ZAIDI ya Hekari 300 kutoka katika kata ya Kikwe Wilayani Meru mkoania
Arusha zimeharibiwa vibaya na ugonjwa mahindi kutoka Nchini Kenya
unaojulikana kama ugonjwa wa kusinyaa kwa mahindi hali ambayo itafanya
wakulima washindwe kupata mahindi wakati wa mavuno

Akiongea na “patapata”mapema jana diwani wa kata hiyo bw Emanuel
Silayo alisema kuwa hali hiyo ya ugonjwa ambayo imekumba kata hiyo ya
Kikwe inaashiria njaa kubwa sana kwa kuwa mazao ya mahindi shambani
hakuna huku wakulima wakiwa wameshapanda

Silayo alisema kuwa Miezi michache iliyopita wakulima waliweza kupanda
mazao ya nafaka hasa mahindi lakini baada ya mahindi kuchomoza
yalianza kushambuliwa na ugonjwa hadi kufa

Alisema kuwa pamoja na kuwa mahindi hayo yamekufa wakati wakulimna
wengi wamepanda kwa ajili ya mategemeo ya chakula katika eneo hilo la
Kikwe lakini mahindi machache sana yameweza kusalia hali ambayo bado
ni kiashirio kikubwa sana cha Njaa


Alifafanua kuwa kama tahadhari haitaweza kuchukuliwa kwa haraka sana
basi huenda wakati wa mavuno ndani ya mwaka huu kusiwe na mavuno
kabisa hivyo baa la njaa kuweza kutawala katika Wilaya hiyo ya Meru.

Akiongelea Ugonjwa huo wa mahindi kutoka nchini Kenya Afisa Kilimo
Wilaya ya Meru,Grace Solomoni alisema kuwa ugonjwa huo ni hatari sana
kwa kuwa unashambulia zao la mahindi hadi kufa lakini bado mkulima
anaweza kupata angalau kiasi kidogo

Grace alisema kuwa kwa mujibu wa taararibui za kilimo mara baada ya
shamba kuathiriwa na ugonjwa huo shamba linapswa kupumzishwa kwa
kipindi cha miaka mitatu ili vijidudu vife lakini kama wakulima
wataendelea kulima basi watasababisha  vijidudu hivyo kuzaliana kwa
wingi sana

TAASISI BINAFSI INAYOENDESHA MAFUNZO YABUNI UZIO WA KIENYEJI WA KUZUIA TEMBO KUINGIA MASHAMBANI UTAKAOGHARIMU MILIONI 400

TAASISI BINAFSI INAYOENDESHA MAFUNZO YABUNI UZIO WA KIENYEJI
WA KUZUIA TEMBO KUINGIA MASHAMBANI UTAKAOGHARIMU MILIONI 400

,Arusha

TAASISI binafsi inayoendesha mafunzo kwa kushirikiana na vyuo vya nje
(University Times Training Insititute )iliyopo mjini hapa imebuni mradi wa
kutengeneza uzio  wa kiasili  utakaogharimu  kiasi cha shilingi milioni mia
nne wa kuzuia tembo kutoharibu mazao ya binadamu mashambani.

Akizungumza na” MALKIA WA MATUKIO “  mkurugenzi wa taasisi hiyo bw Solomon Njiamoja
alisema kuwa mkakati huo  wa kuweka uzio huo utaanza kutekelezeka julai
mwaka huu katika maeneo ya vijiji  vya Serengeti.

Alisema kuwa chuo hicho kimeweza kubuni njia hiyo ya uzio wa kiasili ambayo
itakuwa tofauti na fensi ya umeme ambayo haitaweza kuathiri tembo
wanaozunguka hayo maeneo husika.


Aliongeza kuwa mara nyingi tembo wanapovamia mashamba ya watu ni bunduki
zinatumika kuwaua au kuwafukuza hali ambayo inafanya kupungua kwa idadi ya
tembo hao ambapo kupitia mradi huo utapunguza kwa kiwango kikubwa kwani
tembo hawataweza tena kupita mashambani na kuleta madhara kwa jamii.

 Alitaja faida zitakazotokana na uzio huo wa kienyeji kuwa ni pamoja na
kuokoa chakula ambacho kinaharibiwa na tembo pindi wanapoingia
mashambani,kuokoa maisha ya wakazi walioko maeneo hayo ,kuepusha migogoro
kati ya jamii na tembo pamoja na kuokoa fedha ambazo serikali ingetoa kama
fidia kwa wale walioathiriwa na tembo.

Aidha vijiji vitakavyonufaika na mradi huo ni pamoja na Nata,Mtakuja
,Biafra,Ruhamchanga na Bihonchugu  ambapo uzinduzi wa uzio huo utatangazwa
rasmi katika kongamano litalofanyika mapema nchini Marekani

SIMANJIRO YATAKIWA KUTUNGA SHERIA AMBAZO ZITAWALZIMISHA MIFUGO KUOGESHWA

SIMANJIRO YATAKIWA KUTUNGA SHERIA AMBAZO ZITAWALZIMISHA MIFUGO KUOGESHWA

Na Queen Lema,Simanjiro

Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara,imetakiwa kutunga
sheria ndogo zitakazowalazimisha wafugaji kuogesha mifugo yao kwenye
majosho ili kuiepusha na vifo vinavyotokana na magonjwa ya kupe.

Hayo yalielezwa juzi na Mkurugenzi wa shirika la Cedesota,Jackson Muro
kwenye mafunzo ya kuwajengea uwezo,kusimamia mipango na ufufuaji wa
majosho,madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara.

Muro alisema endapo sheria hiyo ndogo ikipitishwa na halmashauri ya
wilaya hiyo,wafugaji watayatumia majosho hayo ambayo yapo kwenye
maeneo mengi lakini hayatumiki kwa kuoshea mifugo.



Alisema kwenye wilaya ya Simanjiro kuna majosho mengi ya kuoshea
mifugo lakini wafugaji hawayatumii ipasavyo,hivyo wanapaswa
kuwashinikiza ili wayatumie majosho yao kwa kuoshea mifugo yao.



“Bila hivyo itakuwa kazi kubwa kwani wafugaji wengine watakuwa
wanaogesha mifugo yao na inapokuwa kwenye malisho inachanganyana na
isiyoogeshwa hivyo kuambukizana na watakuwa wanawapa hasara wenzao,”
alisema Muro.



Hata hivyo,Diwani wa kata ya Shambarai Alais Edward alisema tayari
Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo wameshapitisha azimio
la kupitisha sheria ndogo ya kuwataka wafugaji waogeshe mifugo yao.



“Tumeshapitisha azimio hilo na kutoa maagizo kwa maofisa watendaji
wote wa vijiji kuhakikisha mchakato wa kupitishwa sheria hizo ndogo
kwenye mikutano ya vijiji ili wafugaji wetu watumie majosho yaliyopo,”
alisema Edward.

ALIYEUWA ASKARI AKAMATWA MANYARA

Na Gladness Mushi,Arusha

Jeshi la polisi Mkoani Manyara linamshikilia mfanyabiashara wa madini
ya Tanzanite,Lawi Abayo (33) kwa kudaiwa kumuua kwa kumpiga risasi
askari polisi wa kituo cha Mirerani Wilayani Simanjiro G.7037 Joseph
Tairo (28).

Akithibitisha kushikiliwa kwa mfanyabiashara huyo,Kamanda wa polisi wa
mkoa wa Manyara,Kamishna Msaidizi Akili Mpwapwa alisema jana kuwa
Abayo alijisalimisha juzi kwenye kituo cha polisi wilayani Babati.

Kamanda Mpwapwa alisema baada ya mfanyabiashara huyo kujisalimisha
mwenyewe hivi sasa wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo kabla ya
kumfikisha mtuhumiwa huyo Mahakamani ili kujibu shtaka la mauaji.

Hata hivyo,Kamanda Mpwapwa alithibitisha kushikiliwa kwa bastola
inayodaiwa kutumiwa na mfanyabiashara huyo kumuua Tairo na pia
wanalishikilia gari aina ya Prado alilotumia kutorokea mara baada ya
tukio hilo.

Askari huyo PC Tairo alifariki dunia Aprili 15 mwaka huu,kwenye
hospitali ya Muhimbili (Moi) baada ya kupigwa risasi ya kichwa na
kujeruhiwa Aprili 7 akiwa kazini mjini Mirerani na kuzikwa kijijini
kwao Kaboro,Mkuu Rombo Aprili 19.

Chanzo cha tukio hilo ni PC Tairo akiwa na askari mwenzake G.8523 PC
Martin,kumkamata mhalifu mmoja na wakati wakimpeleka kituoni ndipo
mfanyabiashara huyo akazuia zoezi hilo kwa kumpiga risasi askari huyo.

MWISHO