Sunday, November 11, 2012

WALTER AIBUKA NA MILIONI 50 KATIKA SHINDANO LA EBSS

WALTER CHILAMBO NDIYE MSHINDI WA EBSS 2012

Mshindi wa shindano la  Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS),Walter Chilambo (Dar) akikabidhiwa sanduku lake lenye kitita cha shilingi milioni 50 usiku huu ndani ya ukumbi wa Diamond jubilee,katika shindano hilo lililovuta hisia za wengi,mshindi wa pili ameibuka mwanadada Salma Abushiri  (Zanzibar) na watu ni Wababa Mtuka (Dar)
Mshindi wa shindano la  Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS),Walter Chilambo (Dar) akiwashukuru wapenzi na msahabiki wake waliompigia kura na hatimaye kuibuka mshindi wa shindano hilo,lililofanyika ndani ya ukumbi wa Diamond jubilee,usiku huu.
Baadhi ya mashabiki wa mshindi wa shindano hilo la EBSS,Walter Chilambo wakishangilia kwa shangwe na vifijo mara baada kutamkwa yeye ndiye kinara katika kilele cha shindano hilo lililovuta hisia za watu wengi
Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Productions Limited, na jaji mkuu wa Shindano la  Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS), akiwa amemkumbatia mshindi wa shindano hilo Walter Chilambo usiku huu ndani ya ukumbi wa Diamond,Chilamba ameibuka na kitita cha shilingi Milioni 50
Msanii Barnaba akiimba na mmoja wa washiriki wa shindano la Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS),
Mshiriki wa EBSS NshomaNg'hangasamala akiimba moja ya wimbo wake jukwaani.
Mwanadada Salma Albushiri akiimba kwa hisia huku akipiga gitaa mbele ya mashabiki wake waliofika kumshuhudia ndani ya ukumbi wa Diamond usiku huu.
Mapouda.! majaji hawaishi vituko
Mashabiki kama kawa.
Wasanii wa muziki wa kizazi kipya Linah na Amin wakiimbwa kwa pamoja wimbo mpya uitwa Mtima Wangu




 





Mwasiti akicheza na Wababa
  Mwasisi akitumbuiza jukwaani
  
 
WALTER CHILAMBO ndiye mshindi wa Shindano la Epic Bongo Star Search (EBSS)  2012. Kufuatia matokeo hayo Kalambo amejinyakulia kitita cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania kutoka kwa wadhamini wakuu wa shindano hilo kampuni ya Simu za Mkononi ya Zantel.

Chilambo ametwaa ubingwa huo baada ya kumwangusha mwana dada kutoka Zanzibar ambaye alikuwa ni mshindani wake wa karibu katika kinyang’anyoro hicho Salma Yusufu.
Salma Yusufu
Shindano la EBSS usiku huu limefikia patamu baada ya washiriki 3 walio ingia katika fainali hizo kutoka na sasa kubakia washiriki wawili ambao ni Walter Chilambo na Salama Yusufu mwakilishi pekee kutoka kisiwani Zanzibar.

Washiriki waliotoka usiku huu maridadi kabisa  na kuachia kitita chaa Shilingi Milioni 50, kikiwaniwa na Walter na Salama ni pamoja na Nsami Nkwabi, Nshoma Ng’hangasamala Wababa Mtuka.

Shindano la EBSS linafikia tamati yake usku huu katika ukumbi wa Diamond Jublee linapoendea kufanyika.
Kama kawaida nao hutoa burudani ....Chief Jaji na mratibu wa Shindano la Epiq Bongo Star Search (EBSS), Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Productions Limited, Ritha Poulsen a.k.a Madam Ritha, akifurahia jambo wakati washiriki wakitumbuiza jukwaani. Kulia ni Jaji mwingine Master Jay akionekana kama kukera na kicheko cha Madam Ritha.
Mashabiki na wapenzi wa shindano la Epiq Bongo Star Search (EBSS) waliofurika katika ukumbi wa Diamond Jubelee wakilipuka kwa shangwe baada ya mmoja wa washiriki ambao wanamkubali kumaliza kufanya show yake.
MC’s wa Show hii ya leo ni kijana mtanashati Caesar Daniel na mwana dada mrembo Vanessa Mdee ndio wanasongesha show nzima ya leo.
Huyu ni Salama Jabir  na hapa ni katiak yale ya Look ndani ya fainali za EBSS 2012
 Washiriki wa Washindano la EBSS 2012 ambao wamefanikiwa kuingia fainali ya shindano hilo wakiwa jukwaani usiku huu wakati wa kuanza kwa fainali hizo. Ni ndani ya Ukumbi wa Diamond Jijini Dar es Salaam. Mshindi kuondoka na kitita cha Shilingi Milioni 50 za kitanzania.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya simu za Mikononi ya Zantel, Awaichi Mawalla akiwa katika mahojiano na mmoja wa ma MC wa sho ya leo Caesar Daniel, wakati akingia katika zulia jekundu la Fainali za EBSS nadani ya  Diamond Jubilee. 

 Shindano la kutafuta vipaji la EBSS 2012 linataraji kufanyika usiku huu kuanzia majira ya saa 3:00 na kwa mujibu wa waandaaji litakuwa likionekana LIVE kupitia Luninga zenu hasa kupitia ITV. Father Kidevu Blog nayo itawapa yale yanayojiri katika tukio hilo.
Hawa ni baadhi ya mashabiki walikuwa wakiteta jambo kwa furaha baada ya wasanii mbalimbali kuweza kutumbuiza

No comments:

Post a Comment