Friday, November 9, 2012

HALMASHAURI YA ARUSHA VIJIJINI INAKABILIWA NA UHABA WA MAPATO

Na  MWANDISHI WETU


HALMASHAURI YA ARUSHA VIJIJINI INAKABILIWA NA UHABA WA MAPATO

HALMASHAURI ya Arusha Vijijini Mkoani hapa inakabiliwa na uhaba wa mapato kutokana na baadhi ya watendaji wa halamshauri hiyo kushindwa kufuatilia kwa undani sana baadhi ya vyanzo vya mapato hali ambayo kama haitaweza kutatuliwa kwa haraka sana basi itasababisha madhara makubwa hasa kwenye malengo ya halmashauri hiyo kwenye jamii

Hayo yamebainishwa Wilayani humo na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo bw Khalifa Idda mapema juzi wakati akiongea katika baraza la madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baraza hilo pia liliwashirikisha wananchi wa maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.

Bw Idda alisema kuwa kwa sasa bado kuna upungufu mkubwa sana wa  mapato ya kutosha katika halmashauri hiyo ingawaje ina vyanzo vingi sana vya mapato hali amnbayo inasababisha kuonekane taa ya hatari hususani katika shuguli za maendeleo ya wananchi wa wilaya hiyo

Aliongeza kuwa ingawaje wilaya hiyo ina vyanzo vingi sana vya mapato bado kuna uitaji mkubwa sana wa watendaji wa halamshauri hiyo kuhakikisha kuwa wanaongeza nguvu zaidi katika kusaka na kubuni aina mpya ya vyanzo sanjari na kuhakikisha kuwa vyanzo ambavyo vipo vinatoa mapato kwa mujibu wa sheria na kanuni za Halmashauri hiyo

‘tuna upungufu mkubwa sana wa masuala ya fedha ndani ya halmashauri yetu nah ii ni kutokana na kuwa  na mapato madogo katika vyanzo vyetu  na hili suala kwa kweli halitupendezi kabisa kwani kama hali itaendelea hivi ni wazi kuwa hata ,mipango yetu kwa wananchi itakwama sana na tutasababisha madhara makubwa sana’aliongeza Bw Idda

Pia alisema kuwa kutokana na hali hiyo ya uhaba wa mapato kutoka kwenye vyanzo vya kudumu vya Halmashauri hiyo wantarajia kuhakikisha kuwa kila mkuu wa Idara anatumia vema taaluma yake huku akifuatilia kwa ukaribu sana vyanzo vyote kwani kama watafanya hivyo basi watachangia kwa kiwango kikubwa sana maendeleo ya mapato

Hataivyo alifafanua kuwa mara baada ya kukaa chini na wakuu wa idara pamoja na wachumi wa halmashauri hiyo hivi karibuni wataweza kuweka kipaumbele kikubwa sana na kuhakikisha kuwa wanabuni vyanzo vipya na kuimarisha vile vya zamani ambapo kama mtendaji wa halmashauri hiyo hataweza kufanya kazi yake kikamilifu basi watachukuliwa hatua kali na za kisheria.

Katika hatua nyingine madiwani wa baraza hilo walisema kuwa suala hilo la uhaba wa vyanzo vya mapato sio suala dogo kabisa kwani linatakiwa kuchukuliwa hatua za haraka ili kuweza kunusuru Halmashauri hiyo dhidi ya Majanga mbalimbali ingawaje nao wakuu wa idara nao wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanawajibika kwa haraka sana.

Madiwani hao walisema kuwa ni aibu kubwa sana kwa halmashauri hiyo kukosa mapato huku ikiwa na vyanzo vingi sana vya mapato na aibu hiyo inatakiwa kufutwa na wakuu wa idara hasa Mweka hazina wa Halmashauri ambapo wanatakiwa kutembea mitaani na kuangali hali ilivyo na kuachana na tabia ya kudai kuwa halmashauri haina fedha huku vyanzo vingine vikiwa vinateketea  na watendaji wasio wahaminifu

‘Mweka hazina hapaswi kukaa ofisini na kusubiria taarifa anatakiwa kutumia taaluma yake vema na kuanza kubuni vyanzo lakini sio hilo pekee bali anatakiwa pia hata kwenda kwenye vyanzo vya mapato na kama ataweza kutembelea vyanzo vya mapato kila mara hata watendaji wazembe watajulikana na wale wanaokula fedha za halmashauri kwa madai kuwa mapato hakuna basi na wao wataweza kujulikana na hapo tutarudisha vyanzo vyetu jamani tuache kukaa ofisini na kusubiri kudanganywa na baadhi ya watu “waliongeza madiwani hao

MWISHO

No comments:

Post a Comment