Friday, November 9, 2012

CHADEMA YADAKA VITONGOJI SITA KATI YA TISA NDANI YA MJI MDOGO WA USA RIVER

CHADEMA YADAKA VITONGOJI SITA KATI YA TISA NDANI YA MJI MDOGO WA USA RIVER

Na Queen Lema, MERU

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo mkoani hapa kimefanikiwa kuibuka
mshindi wa  vitongoji sita kati ya tisa vya mji mdogo wa usariver
wilyani Meru na kuahidi kufanya mabadiliko makubwa sana katika nyanja
za uchumi wa Mji huo

Akiongea na Majira mara baada ya kutangazwa kwa matokeo ya vitongoji
vyote katibu wa Chadema mkoa wa Arusha bw Amani Golugwa alisema kuwa
ushindi huo umetokana na mabadiliko mbalimbaliu ambayo yanafanywa na
chama hicho sanajari na kutoa Muongozo imara kwa maisha ya Mtanzania
hasa wa Eneo hilo la Usa River

Bw Golugwa aliongeza kuwa pamoja na kuwa wamefanikiwa kupata ushindi
kwa Vitongoji kama sita bado watafanya mabadiliko makubwa sana katika
Mji huo wa Usa River ambapo mabadiliko hayo ni pamoja na kukuza uchumi
wa mji huo katika halmashauri hiyo ambayo hapo awali palikuwa na
matatizo mbali mbali ya uchumi huku hali hiyo ikisababisha hata
umaskini mkubwa sana

‘leo tumeweza kupata Vitongoji kama sita huku vitatu tukivikosa na
sasa hii ni imara sana kwetu kwa kuwa sasa halamshauri itakuwa kama
ile ya Karatu kwa kuwa tutafanya mabadiliko makubwa sana na itafanya
kuchochea hata Umaskini kupoungua kwa kuwa tutaweza kuimarisha sana
mji huu mdogo wa Usa river na miji mingine nayo itaiga mfano mzuri wa
uongozi hasa katika nyanja za uchumi ambao unatekwa na baadhi ya
viongozi kwa manufaa yao wenyewe”aliongeza Bw Golugwa

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa taifa wa chama hicho bw Freeman
Mbowe alisema kuwa kupitia ushindi huo bado chama chake hasa kwa mkoa
wa Arusha kina nafasi kubwa sana ya kuweza kuboresha mabadiliko
makubwa sana ingawaje Vitongoji Vitatu vimechukuliwa na wapinzani wao.

“kushindwa kwa vitongoji vitatu sio sababu bali kutokana na hili sisi
tunaweza kusema kuwa huu ni ushindi imara na ushindi huu utaweza
kutufanya tuweze kuchapa kazi kwa kwenda mbele kwa hivyo tunaendelea
kupambana ma kuhakikisha kuwa tunafanya mabadiliko kulingana na chama
chetu:”aliongeza bw Mbowe

Hataivyo katika uchaguzi huo ambao ulishirikisha Vitongoji tisa
Chadema imechukua vitongoji vya Manyata
Kati,kisambare,Magadini,
Ngarasero, Nganana.Mji mwema    wakati kwa
upande wa  CCM wamechukua Vitongoji vya Magadirisho,Usa
madukani,pamoja na Mlima Sioni

MWISHO

No comments:

Post a Comment