Sunday, November 11, 2012

MKUU WA WILAYA AAGIZA VIONGOZI KUPANDA MITI

 MKUU WA WILAYA YA HAI,NOVATUS MAKUNGA

MKUU WA WILAYA AAGIZA VIONGOZI KUPANDA MITI

NA MWANDISHI WETU HAI


Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara,Brigedia Jenerali Cosmas Kayombo ameuagiza uongozi wa wilaya hiyo kutoa tuzo kwa watu wanaopanda miti ili kutunza mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Brigedia Jenerali Kayombo aliyasema hayo juzi mji mdogo wa Mirerani kwenye mdahalo wa mabadiliko ya tabia nchi na namna ya kupunguza athari zake uliondaliwa na mtandao wa asasi za kijamii mkoani humo Macsnet na The Foundation for Civil Society.
Alisema ili kuhakikisha jamii inapenda kutunza mazingira kwa kupanda miti uongozi wa wilaya hiyo unatakiwa kujipanga kutoa tuzo kwa washindi wa upandaji miti ili kuongeza hamasa ya kutunza mazingira wilayani humo.
Alisema mabadiliko ya tabia nchi ni suala ambalo hivi sasa linazungumzwa na wasomi,wanasayansi,wanasiasa na jamii kwa ujumla hivyo juhudi zinapaswa kufanyika ili kuhakikisha mabadiliko ya tabia nchi yanadhibitiwa.
“Juhudi za makusudi,elimu na sera ziendelee kutolewa kwa jamii kwani uelewa mdogo na dhamira ya wenye dhamana ni ya mashaka katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi hivi sasa,” alisema Brigedia Jenerali Kayombo.
Mtoa mada Jackson Muro alisema madhara ya mabadiliko ya tabia nchi ni ukame,magonjwa ya binadamu,mifugo,wanyama na mimea,mafuriko yasiyotegemewa,sunami  theluji kuyeyuka,kukosekana mvua na kina cha bahari au ziwa kupungua.

Alisema namna ya kupambana na mabadiliko ya tabia nchi ni kutunza uoto wa asili,kupunguza uzalishaji wa hewa na gesi,kupanda miti ili inyonye hewa ukaa inayopanda angani na kuchanganya mazao ya kawaida na misitu.

“Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na shirika la chakula duniani FAO mwaka 2005 ulionyesha kiwango cha ukataji misitu duniani umefikia hekta milioni 7.3 milioni kwa mwaka hivyo hewa ya ukaa kushindwa kufyozwa,” alisema Muro.

Naye,mmoja kati ya washiriki wa mdahalo huo,Kaanael Minja alimuuliza mkuu huyo wa wilaya nani anatoa kibali cha kukatwa mkaa wilayani humo kwani hivi sasa uuzwaji wa mkaa umeenea na hakuna hatua inayochukuliwa.
Hata hivyo,Brigedia Jenerali Kayombo alisema hakuna kibali kinachotolewa na mtu cha kukata mkaa kwenye wilaya hiyo,hivyo ushirikiano baina ya viongozi na jamii uongezwe ili kukomesha hali hiyo kwani kijiografia Simanjiro ni kubwa. 

No comments:

Post a Comment