Friday, November 9, 2012

CHAMA CHA KIJAMII CHATOA TAMKO DHIDI YA VIONGOZI WA KIISLAMU

Na Queen Lema,Arusha

CHAMA CHA KIJAMII CHATOA TAMKO DHIDI YA VIONGOZI WA KIISLAMU


CHAMA cha Kijamii  hapa nchini (CCK)kimeipinga kauli ya Kiongozi wa Dini ya Kiislamu Shehe Ponda Isa Ponda ambayo ilikuwa inamtaka Raisi Kikwete atoe amri ya kuwafungulia waislamu wote walioshikiliwa na jeshi la polisi kwa makosa ya kufanya maandamano bila kibali na kufanya uharibifu wa makanisa mbalimbali Jijini Dar es salaam

Akiongea na waandishi wa habari mapema jana mjini hapa Katibu mkuu wa chama hicho Bw Renatus Muabhi alisema kuwa kauli hiyo ni kauli ya uchochezi na uharibifu wa amani hasa kwa mkoa wa Dar es  salaam ambapo mpaka sasa madhara mbalimbali yameshatokea

Alisema kuwa Kiongozi huyo wa dini ya kiislamu hakutoa kauli nzuri kwani kauli hiyo imechangia sana baadhi ya waumini wa dini hiyo kupata vichwa na kufanya vurugu huku kama angeweza kutumia vema nafasi yake aliyonayo katika jamii basi angeweza kurudisha amani hata kwa kiwango kidogo sana .

Aliongeza kuwa viongozi hao wa dini wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanatumia vema nafasi yao katika kuleta amani na badala yake wasitoe matamko mbalimbali ambayo ndiyo yanayofanya na kusababisha uvunjifu wa amani kwa ajili ya itikadi mbalimbali na za watu tofautitofauti.

“Hivi karibuni Raisi Kikwete alitoa Tamko ambalo lilikuwa linaani matukio yalifanywa na baadhi ya watu lakini baada ya muda huyu kiongozi naye akatoa tamko lake ambalo lilifanya uchochezi mkubwa sana kwa waumini sasa anapaswa kujua na kutamnbua kuwa anatakiwa kutumia vema nafasi yake katika jamii kwani kama kiongozi wa dini hakupaswa kutoa tamko la kumuonya Raisi wa Nchi  na badala yake angetumia vema busara kwa jambo hilo “alisema

Pia alisema kuwa Naye Raisi wa kikwete kuhakikisha kuwa anawachukulia hatua wote waliohusika na kuamini kuwa yeye ndiye suluhisho la masuala kama hayo ambayo yanafanya amani ya nchi ya Tanzania kuweza kupotea kwa vyanzo vidogo vidogo.

Katika hatua nyingine alibainisha kuwa pamoja na kuwa CCK kinalaani sana matukio kama hayo lakini nayo Serikali inatakiwa kuhakikisha kuwa inawachukulia hatua kali na za kisheria  kwa wale wote ambao wamehusika kwa namna moja au nyingine katika kuvuruga amani ya Nchi hivi karibuni kutokana na Matukio ya itikadi za Kidini

Bw Renatus alifafanua kuwa endapo kama Serikali haitaweza kufanya hivyo basi amani ya Nchi ya Tanzania itayumba huku hali hiyo ikisababisha sana kuwepo kwa mdodoro mkubwa wa uchumi hasa kwa watu wa vipato vya chini kwa kuwa hawataweza kufanya kazi zao sanjari kukithiri kwa vifo ambavyo si vya lazima.

“Kwa  mfano kama juzi kumetokea vurugu kubwa sana hasa maeneo ya Kariakoo ambapo ndipo eneo la Uchumi mkubwa sana hasa kwa watu wa Dar  na walionekana kuathirika sana ni kina mama pamoja na watoto sasa kama hali nhii itaendelea hivi ni wazi kuwa tutakuwa tunaruhusu umaskini, lakini kama viongozi wa Dini watasimama na Serikali itawachukulia hatua basi haya matukio yatakuwa ni historia kubwa sana kwa jamii “aliongeza bw Renatus

Awali Bw Renatus alisema kuwa Watanzania wanatakiwa kuwa na Utii wa sheria pamoja na mamlaka ambazo zipo ndani ya nchi hasa vyombo vya dola kuwa ni wajibu wao kutambua kuwa jamii inaweza kuwa ni sehemu kubwa sana ya machafuko ya nchi kwa kufuatafuata mkumbo hasa kutoka kwa viongozi wa Kidini na Kisiasa kwa malengo ambayo hayajulikani,hivyo wasikubali kutumika kama kuni ili kuepusha madhara hasa kwa wananchi wa vipato vya chini.

MWISHO

No comments:

Post a Comment