Tuesday, November 20, 2012

CHUO CHA UASIBU ARUSHA CHAFANIKISHA MALENGO KWA KUKUSANYA MILIONI 2OO HADI KUFIKIA MILIONI 900


Na Queen Lema, Arusha

CHUO cha Uasibu Arusha kimefanikiwa kuongeza mapato yake kutoka kiasi cha Milioni 200 hadi kufikia milioni 900  kwa kila mwaka kutokana na kuongeza fani mbalimbali za masomo hasa katika Shahada za Uzamili ya Uongozi na Biashara katika Teknolojia ya Habari, Shahada ya Uzamili ya Uongozi na Biashara katika Ugavi pamoja na Shahada ya Uzamili ya Sayansi katika Fedha na Uwekezaji
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa chuo hicho Profesa Johanes Monyo katika maafali ya tatu ya chuo hicho yaliyofanyika Mapema jana Mjini hapa na kuhudhuriwa na watu mbalimbali

Aidha Profesa huyo alisema kuwa hapo awali mapato ya Chuo hicho yalikuwa yapo chini lakini mara baada ya kuongeza fani mbalimbali za elimu wamefanikiwa kukusanya kiasi cha Milioni 900 jambo ambalo limeweza kuwapa wadau mbalimbali wa Chuo hicho kuweza kutafuta Njia nyingine ya kuweza kuongeza fani mbalimbali huku fursa hizo nazo zikiwanufaisha watanzania walio wengi zaidi

“Hili ongezeko la fedha limetokana na fani hizi ambazo tunazitoa hapa lakini tunashirikiana na chuo kimoja cha uingereza ambacho kinajulikana kama Coventry cha Uingereza na kwa kweli tumeona matunda makubwa sana kwa kuwa wanafunzi waliopata elimu hii mbali na kuajiriwa katika sekta mbalimbali pia wataweza kujiajiri wao wenyewe na kuweza kushindana na soko la ajira hapa Afrika mashariki na duniani kote’aliongeza profesa Johanes.

Hataivyo alisema kuwa kutokana na ongezeko hilo chuo hicho bado kina mkakati wa hali ya juu sana wa kuhakikisha kuwa kinabuni mbinu mbadala za kuweza kuongeza mapato sanjari na kuhakikisha kuwa nao watanzania wananufaika hata kwakushirikiana na vyuo vya nje ya Nchi.

Katika hatua nyingine alisema kuwa nao wahitimu wa vyuo mbalimbali wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanajiwekea utaratibu wa kusoma kwa malengo ya kujiajiri toafuti na pale ambapo kwa sasa asilimia kubwa ya wasomi wanashindwa kufikia malengo yao kwa kuwa wanasoma kwa ndoto za kuajiriwa

Alifafanua kuwa endapo kama wasomi ambao ni vijana wa Taifa la Tanzania watasoma kwa ndoto za kujiajiri basi wataweza kuchangia sana hata kufanya mabadiliko ya hali ya juu sana katika soko la Ajira ambalo baadhi ya vijana wanashindwa kulipata kwa kuwa wana ndoto za kuajiriwa tena Serikalini.

“kama mhitimu wa  chuo chochote kile leo ataweza kujiwekea utaratibu wa kuhakikisha kuwa anasoma kwa malengo ya kujiajiri yeye mwenyewe basi ataongeza juhudi zaidi kuliko kusubiri kupewa ajira ambazo kwa sasa ni ndogo sana kwa kuwa kuna wimbi kubwa sana la wahitimu kutoka katika vyuo mbalimbali hapa nchini’aliongeza Profesa Johanes.

Kwa upande wa wahitimu ambao walikuwa 127 walisema kuwa bado kuna uitaji wa wataalamu katika nyanja mbalimbali hasa  kwa nchi ya Tanzania hivyo Serikali inatakiwa kuendelea kuwekeza zaidi katika vyuo ili kuweza kufikia malengo mbalimbali ya Milenia.
MWISHO

No comments:

Post a Comment