Friday, November 9, 2012

MBOWE ASEMA KUWA YUPO TAYARI KUACHA CHADEMA KAMA HAKITAANGALIA MAHITAJI MUHIMU YA MAISHA YA MTANZANIA

MBOWE ASEMA KUWA YUPO TAYARI KUACHA CHADEMA KAMA HAKITAANGALIA
MAHITAJI MUHIMU YA MAISHA YA MTANZANIA


Na Queen Lema, MERU

MWENYEKITI  wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA)Bw Freeman
Mbowe amesema kuwa yupo  tayari kuacha chama chake endapo kama chama
hicho  hakitaweza kufuata sheria taratibu na kanuni za maisha bora kwa
mtanzania kwa kuwa kwa sasa wapo baadhi ya watu ambao wamefunga ndoa
na vyama vya siasa hali ambayo inasababisha hata shuguli za maendeleo
kukwama

Bw Mbowe aliyasema hayo wilayani Meru mkoani hapa  katika harambee ya
shule ya ufundi ya Olokii iliyo chini ya kanisa la Kiinjili la
kilutheri dayosisi ya kaskazini kati, wakati alipokuwa mgeni rasmi
mapema jana

Bw Mbowe alisema kuwa endapo kama chama chake hakitaweza kutumia vema
nafasi yake katika kutetea haki za mtanzania hususani katika sekta ya
elimu basi ni bora kuachia ngazi kwa kuwa chama cha siasa sio baba
wala mama bali ni mpango wa kupingana kwa hoja ingawaje kwa sasa wapo
baadhi ya watu ambao wamefunga ndoa na vyama vya siasa na kusababisha
hata kukitihiri kwa mgawanyo mkubwa sana ndani ya Jamii

“utakuta mtu akiona kuwa eti Mbowe yupo kanisani na anafanya harambee
haingii kwa kuwa ni Chadema nay eye ni CCM sasa hali itaenda mpaka
lini wakati Chadema ni mali ya wananchi na CCM pia ni mali ya wananchi
na kutokana na hali kama hii ndiyo inayochangia sana hata baadhi ya
watu wanashindwa kufuata sheria na kanuni za maisha bora kwa mtanzania
na wengine wanateseka kiasi cha kufa sasa mimi sijafunga ndoa na
Chadema kwa kuwa sio baba yangu wala Mama yangu’aliongeza bw Mbowe

Katika hatua nyingine alisema kuwa bado anailaumu sana Serikali ya
sasa kwa kushindwa kutekeleza sera ya elimu na kusababisha hata elimu
ya Tanzania kuwa hafifu tofauti na nchi nyingine ambazo zinaendelea
huku kundi kubwa sana la wanafunzi  wakiwa bado wanaendelea kuzorota
Mitaani hili hali Serikali inauwezo mkubwa sana wa kuwasomesha
kutokana na Rasilimali ambazo zipo.

Aliongeza kuwa kundi kubwa sana la vijana ambalo linaachwa mitaani
hasa wale ambao wamekosa nafasi kwa darasa la Saba,kidato cha Nne,
kidato cha Sita ndio wanaosababisha hata umaskini kukitihiri kwa kuwa
baadhi yao wanakosa mahitaji muhimu huku kwa nchi zilizoendelea vijana
kama hao wanapewa kipaumbele kwa kuhakikisha kuwa wanapata fursa
mbalimbali za elimu na ajira imara.

‘Sasa hivi unakuta baadhi ya watu eti wanaawacha hawa wanafunzi ambao
wameitimu madaraja mbalimbali alafu nchi inadai kuwa inapambana na
Umaskini sasa kama sio uongo ni nini utapambana na umaskini ilihali
watu hawana elimu na ndio maana Nchi jirani yetu ya Kenya inatuzidi na
idadi ya watoto wa vigogo wanaosoma Kenya na Uganda ni kubwa kuliko
ile ya watoto wa vigogo kutoka katika nchi hizo wanaokuja Tanzania
kusoma tuamke watanzania na tuangalie hili kwa undani sana’aliongeza
Mboye.

Awali Askofu wa kanisa la kiinjili la kilutheri mkoani hapa(
KKKT)dayosisi ya Kaskazini Kati Dkt Thomas Laizer alisema kuwa ni
jambo la ajabu sana kwa wanasiasa kuchukiana ovyo kwa kuwa siasa
inaenda kama mchezo wa mpira ambao kamwe hautabiriki na hivyo
wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanajijengea tabia ya kupenda na
kuthaminiana wao kwa wao hasa kwenye majukumu ya msingi ya
Kimaendeleo.

Dkt Thomas alisema kuwa wapinzani kuwakataa watawala na watawala
kuwakataa wapinzani si jambo jema na halitakiwi kuendelezwa kwa sasa
kwani wote wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanakuwa kitu kimoja na kutatua
matatizo mbalimbali ambayo yanaikabili jamii kwa  sasa likiwemo suala
zima la uvunjifu wa amani ndani ya Nchi.

“leo mtu wa CCM hampendi huyu wa Chadema ambaye ni mpinzani wake
wakati kesho 2015 bado haujajua na kutambua kuwa atakayeongoza nchi
atakuwa ni ninani je akiwa ni Chadema ndiye kiongozi itakuwaje hivi
vyama vinatakiwa kufikiria na wanatakiwa kuwa na umoja na wala sio
kulumbana kwa vitu ambavyo havina maana kabisa shuguli za maendeleo
zipo nyingi sana na huo muda unaopotea bure utumike hasa kwenye
shuguli kama zetu za maendeleo ya jamii’aliongeza Dkt Laizer

Katika Harambee hiyo ambayo ni kwa ajili ya Mabweni ya wanafunzi wa
Shule hiyo ya ufundi ya Olokii zaidi ya Milioni kumi zilipatikana
ambapo iliongozwa na Bw Mbowe pamoja na wadau wengine wa elimu hapa
nchini.

MWISHO

No comments:

Post a Comment