Sunday, November 11, 2012

MWENYEKITI WA KIJIJI MONDULI,JIMBONI KWA LOWASA ANUSURIKA KIPIGO KITAKATIFU



Joseph Ngilisho,Arusha
 
MWENYEKITI wa kijiji cha Losirwa kata ya Esilalei wilayani Monduli,  George Arpakwa anatuhumiwa na wananchi wake kujihusisha na ufisadi wa uuzaji wa ardhi ya kijiji kiholela hali inayokwamisha shughuli za maendeleo  kijiji hapo.
 
Wananchi hao wakizungumza kwa masikitiko makubwa katika mkutano wa hadhara kijiji hapo wamedai kuwa wamechoshwa na uongozi wa mwenyekiti huyo kwa kushindwa kuonyesha uwadilifu wake kwa jamiii badala yake amegeukia maeneo ya kijiji ambayo amekuwa akiyauza kinyume na sheria.
 
Mwenyekiti huyo ambaye alinusulika kipigo cha wananchi wake waliokuwa na jazba katika mkutano huo,aliamua kuvunja mkutano huo ghafla baada ya kubaini kwamba miongoni mwa waliohudhulia mkutano huo walikuwemo waandishi wa habari.
 
‘’huu mkutano ni wa kijiji waandishi wa habari hawaruhusiwi kuhudhuria hapa ‘’alitamka maneno hayo huku akitokomea gizani na makablasha pasipo julikana.

Katika hali ya kushangaza mwenyekiti huyo aliamua kumkunja shati mmoja ya wazee wa ukoo Leigwanani aliyekuwa akiwatetea waandishi wa habari waendelee kuwepo katika mkutano huo kwa ajili ya kuijulisha jamii ,hali ambayo ilizua taflani kubwa kwa wananchi kutaka kumpiga mwenyekiti huyo.
 
Mmoja ya wanakijiji hao,Romeni ole Meiya alieleza kushangazwa na tukio la mwenyekiti huyo na kudai kuwa mkutano huo ni muhimu sana kwa kujua mustakabali wa maeneo yao ambayo huyatumia kwa ajili ya malisho ya mifugo yao kutokana na kuwepo dalili mbaya kwa kiongozi wao kucheza mchezo mchafu.
 
Alisema kuwa wameshangazwa kuona baadhi ya maeneo ya malisho na mapito ya mifugo pamoja na mabwawa kuwekewa uzio kuashiria kuwa mifugo hairuhusiwi kuingia eneo hilo licha ya maeneo hayo kutengwa kwa ajili ya kuhudumia mifugo yao.
 
Alisema hawana imani tena na mwenyekiti wao ambaye sasa ameonyesha udhaifu wake katika utendaji wake wa kazi  hivyo wanamtaka achie ngazi na kwasasa hawamtambui kama yeye nikiongozi wa jamii hiyo ya kifugaji .
 
Naye Kiteho  Richard alisema kuwa mwenyekiti wao ameonyesha dhahili udhaifu mkubwa alionao kwa kuogopa kufichuka kwa madhambi yake  baada ya kubaini kuwepo kwa waandishi wa habari,hata hivyo alisisitiza kuwa kijiji kimeamua kutomtambua tena na kunafanya mkakati wa kupata mwenyekiti wa muda.
 
‘’Kama mwenyekiti hahusiki na kuuza maeneo ya wananchi kwanini amekimbia mkutano hii inaonyesha kua anahusika kwa asilimia kubwa ndio mana alipowaona waandishi wa habari akakimbia akijua siri  inafichuka" Alisema Richard"
 
Wananchi hao waliandamana hadi ofisi ya mwenyekiti huyo nakuchukua jukumu kali la kuifunga ofisi hiyo wakiamini kuwa ninjia moja wapo ya kupata suluhisho la Ardhi yao kumilikiwa na wenye pesa wachache huku wakiomba serikali kushughulikia tatizo hilo likiwa bado halijaleta hadhari kubwa kwa jamii.
 
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Monduli ,Jowika Kasunga akizungumza kwa njia ya simu amekiri kupokea taarifa hizo za malalamiko ya wananchi nakuahidi kuwa anazifanyia kazi ilikubaini ukweli wa jambo hilo.
 
mwisho.
 

No comments:

Post a Comment