Friday, November 9, 2012

SERIKALI YA TANZANIA YAHIDI KUBORESHA SEKTA YA AFYA


Na Joseph Ngilisho,ARUSHA

RAIS  Jakaya Kikwete amesema kuwa serikali ipo kwenye mchakato wa kuhakikisha vituo vya afya na zahanati hapa nchini vinajengwa kwenye vijiji, kata ,wilaya na kwamba hospitali za mkoa zinakuwa na hadhi ya rufaa.

Rais Kikwete ameyasema hayol eo wakati akizindua hospitali teule ya Olturumenti kuwa ya wilaya, ambapo hapo awali ilikuwa kituo cha Afya katika halimashauri ya wilaya ya Arusha,na kutoa wito kwa vituo vya afya na zahanati zilizopo kuboreshwa ili ziwe na hadhi ya kulaza wagonjwa.

Aidha alisema utekelezaji wa mpango wa mpango huo umeanza na  unalengo la kuwasogezea  huduma za Afya  wananchi kwa ukaribu na kuondokana na  adha inayowakabili ya kufuata huduma hiyo umbali mrefu .

Alisema katika kukamilisha mpango huo serikali imeongeza mara sita bajeti yake kutoka shilingi bilioni 271 ya mwaka 2005 na kufikia kiasi cha shilingi Trioni 6.2 ,ambapo lengo ni kuhakikisha kuna kuwepo na vituo vya Afya na zahanati za kutosha hapa nchini.

Hata hivyo aliwataka viongozi husika akiwemo waziri wan chi ofisi ya rais dkt Hawa Ghasia kuzifanyia kazi changamoto zote zinazozikabili hospitali vituo vya Afya na zahanati ili kuhakikisha vinatoa huduma iliyo bora itakayo saidia kupunguza kero kwa wananchi.

Kikwete aliongeza kwa kusema kuwa serikali imefanikiwa kupunguza vifo vinavyotokana na maambukizi ya malaria kutoka asilimia 14 na kufikia asilimia 2 ,sanjari na kuweka mipango mikakati mbalimbali ambayo inalenga kuimarisha zaidi afya ya Mtanzania dhidi ya maambukizi ya ugonjwa huo
 
Alitaja Mikakati hiyo ambayo inaendelea kutekelezwa ili kuepusha jamii na maambukiz mapya ya ugonjwa wa Malaria kuwa ni pamoja na kugawa vyandaru viwili  kwa kaya,ambapo hadi sasa  Jumla ya Vyandarua Milioni 13 vimeshagawiwa,huku mkakati mwingine ambao unafuatwa ni kupuliza dawa kwa kila kaya,na mkakati mwingine  ni kujenga na kuimarisha zaidi kiwanda ambacho kinazalisha Viluilui ambao wataweza kushambulia wadudu wa Malaria.

Awali mganga mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Arusha Thobias Mkina alisema kuwa pamoja na kuwa Ujenzi wa hospitali hiyo ya Oltument umegarimu kiasi cha  zaidi ya Milioni 924 lakini bado kuna changamoto lukuki ndani ya Hospitali hiyo ambayo inatarajia kuhudumia maelfu ya wakazi wa wilaya hiyo na nyingine za jirani.

Dkt Thobias alitaja changamoto kubwa sana ndani ya hospitali hiyo kuwa wa majengo ya kutosha hasa wadi za wamama wajawazito, watoto , chumba cha X ray, pamoja chumba cha kupimia magonjwa ya VVU hali ambayo inatakiwa kuangaliwa kwa haraka sana ili kuweza kuboresha afya za wananchi wa wilaya hiyo

No comments:

Post a Comment