Friday, June 15, 2012

WAONESHENI WAHALIFU UPENDO NA PIA WAPENI ELIMU


Na Queen Lema,ARUSHA


WAONESHENI WAHALIFU UPENDO NA PIA WAPENI ELIMU

IMEELEZWA kuwa machafuko ndani ya jamii nyingi yanazidi kuongezeka kwa kuwa asilimia kubwa ya wanajamii waliowengi wanawatenga wahalifu mbalimbali badala ya kuwapa elimu ambayo itawafanya waweze kuacha uhalifu wao

Kauli hiyo imetolewa na Mchungaji Steve Robert Kutoka Tanga wakati alipokuwa akiongea na wananchi wa kijiji cha kwa Muorombo Kata ya Terrat Mkoani Arusha mapema jana

Bw Robert alisema kuwa kwa sasa hakuna elimu yoyote ambayo inatolewa kwa watu ambao wanahasi jamii hali ambayo inawafanya hata baadhi yao kutengwa huku uhalifu ukiwa unakithiri sana

Alifafanua kuwa endapo kama jamii ingekuwa na Muongozo imara hasa katika eneo hilo la Kwa Muorombo basi hata idadi ya uhalifu nayo ingepungua sana kwa kuwa kila mara wahalifu wa matukio mbalimbali wangeweza kupatiwa mafunzo pamoja na madhara ya uhalifu

Alisema kuwa mtu ambaye ni muhalifu hapaswi kutengwa na jamii yake na badala yake jamii inatakiwa kuonesha na kuimarisha zaidi upendo ili waweze kufikia katika hatua za kuacha uhalifu ambao ndio chanzo kikubwa sana cha umaskini

“leo hii unakuta eti mtu ni muhalifu lakini badala ya kupewa elimu mbalimbali ya kumsaidia jinsi ya kuepukana na tabia hiyo anatengwa na jamii na wakati nafasi mbalimbali zinatakiwa kutumikan ikiwemo nafasi ya mashirika na Taasisi za Dini”aliongeza bw Robert

Pia aliongeza kuwa wananchi wanapswa kujua mbinu pekee ya kuweza kukinzana na uhalifu wa aina mbalimbali ndani ya jamii husika ni kuhakikisha kuwa wanatoa elimu kuanzia ngazi za familia kwa kuwa nazo familia nyingi hazina utaratibu wa kuwaelezea watoto wao madhara ya kuwa waharibifu na wavunjifu wa amani

Awali alitataja madhara ya kukithiri kwa uhalifu hasa wizi mdogo mdogo kuwa ni pamoja na kuwepo kwa majanga makubwa sana ya umaskini ndani ya jamii wakati taifa lina buni mbinu mbalimbali za kupambana na Umaskini.

MWISHO

No comments:

Post a Comment