Tuesday, June 5, 2012

SHIRIKA LA HOPE FOR TANZANIA LAFANIKIWA KUTOA KOMPYUTA 92



Shirika lisilo la kiserikali la Hope For Tanzania limetoa computer 92 zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 15 kama mchango wa kuinua kiwango cha elimu katika shule nne jijini Arusha.

Wakurugenzi wa shirika hilo hapa Tanzania Felex Masenge  na Naomi Masenge wamesema kuwa msaada huo unatokana na wafadhili wa shule isiyo ya kiserikali ya Tuishime ambao waliahidi kuzisaidia shule 10 jijini arusha vifaa hivyo  ili wanafunzi waweze kujifunza somo la Tehama.

Felex amesema kuwa zoezi hilo la kupatiwa computer  linaendelea hali ambayo itatoa fursa kwa shule hizo kufanya vizuri kielimu katika ulimwengu wa sasa wa sayansi na teknolojia.

Akikabidhi computer  hizo kwa wakuu wa shule hizo ambazo ni shule ya msingi uhuru,ukombozi,kijenge na tuishime mgeni rasmi  katika  hafla hiyo Afisa elimu vielelezo Godfrey Augustino amesema kuwa vifaa hivyo vimekuja wakati muafaka na amewataka kuvilinda na kuvitunza vizuri.

Pia amesema kuwa shule nyingi za serikali zinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa fedha  hali ambayo inapelekea kushindwa  kununua computer  na wanafunzi kushindwa kufanya mitihani ya Tehama kama ilivyo kwa  shule  zinazomilikiwa na watu binafsi.

Aidha Augustino ametoa wito kwa wakuu hao wa shule kuzitunza na kuzilinda  na kuwa hatokuwa tayari kupokea taarifa ya  kupotea ama kuibiwa kwa vifaa hivyo   bali hatua kali za kisheria zitachuliwa dhidi ya mwalimu husika.

Lakini hata hivyo amewataka walimu kwenda shule na kwenda kujifunza alimu ya computer ili waweze kuwafundisha wanafunzi somo hilo la Tehama na hatimaye waweze kufanya vizuri katika mitihani yao.

Akiongea kwa niaba ya wakuu wa shule diwani wa kata ya sokon one Michael Kivuyo amesema kuwa ni vyema watanzania wakaiga mfano huo kwa kuchangia kuinua elimu katika shule za msingi na sio kuchangia ama kutoa msaada kwa mambo yasiyo ya msingi katika jamii.

Mwisho.

Chanzo cha habari na Ashura Mohamed Arusha

No comments:

Post a Comment