Sunday, June 10, 2012

BREAKING NEWSSSSSSSSSSSS:PROFESA GEORGE SAITOTI AFARIKI KATIKA AJALI YA HELIKOPTA NCHINI KENYA



BREAKING NEWSSSSSSSSSSSS:PROFESA GEORGE SAITOTI AFARIKI KATIKA AJALI YA HELIKOPTA NCHINI KENYA


 Waziri wa Usalama wa ndani wa Kenya Profesa George Saitoti amefariki dunia kwa ajali ya Helikopta iliyotokea leo asubuhi katika eneo la Ngong Katika milima ya Magharibi mwa Nairobi nchini humo wakati akiwa katika safari ya kikazi akielekea Kisumu, Saitoti amefariki akiwa na Naibu Waziri wake Orwa Ojode.
Mbunge wa Kenya Najib Balala amethibitisha kutokea kwa kifo hicho katika mtandao wake wa Twitter, Serikali ya Kenya bado haijasema chochote kuhusu sababu za ajali hiyo iliyopoteza mawaziri hao pamoja na watu wengine wanne jumla yao wakiwa Sita, Profesa Saitoti alikuwa akitarajia kugombea urais katika uchaguzi wa Rais utakaofanyika baadae mwaka huu

No comments:

Post a Comment