Friday, June 15, 2012

MHARIRI WA GAZETI LA RAI AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUOMBA RUSHWA YA SHILINGI MILIONI 1NA NUSU


MHARIRI WA GAZETI LA RAI AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUOMBA RUSHWA YA SHILINGI MILIONI 1NA NUSU

Na Queen Lema,ARUSHA


MHARIRI wa gazeti la Rai bw Masiaga Matinyi pamoja na watuhumiwa wengine wawili wamefikishwa katika mahakama ya Arusha kwa kosa la kuomba Rushwa kutoka kwa afisa wa Shirika la Tanesco wilayani Monduli mkoani hapa.

Akisomewa mashitaka pamoja na watuhumiwa wengine wawili ambao ni  bi Bora  Bidiga (36)na  Mwita Chomote (32) walitenda kosa hilo wilayani Monduli

Aidha iliendelea kudaiwa mahakamani hapo mbele ya hakimu mkazi bw Yohana miombo na mwendesha mashitaka wa Serikal bw Amidu Msimbana  kuwa watuhumiwa hao wote walitenda kosa hilo kati ya June 13 na 14 majira ya saa kumi jioni wilayani Monduli Mkoani Arusha

Pia ilidaiwa kuwa watuhumiwa wote hao watatu walimlazimisha kwa nguvu afisa wa shirika la Tanesco ambaye amejulikana kwa majina ya Andew Mahamudu  kutoa Rushwa kwa kuwa hakuwa na vigezo vya kufanya kazi ndani ya shirikan hilo 

“baada ya kufanya hivyo watuhumiwa wote hawa walimshawishi awape kiasi cha shilingi Milioni 5 ili wasitangaze lakini baada ya hapo walipokea kiasi cha shilingi laki mbili ambapo walikamtwa na vyombo vya usalama”aliongeza bw Amidu.

Aidha iliendelea kudaiwa kuwa Mshitakiwa wa pili ambaye ni dereva wa mhariri huyo naye anakabiliwa na mashitaka mawili ambapo shitaka la kwanza ni pamoja na kushawishi kupokea rushwa wakati shitaka la pili ni kupokea rushwa kiasi cha shilingi laki mbili

“inadaiwa kuwa huyu ndiye alieenda kupokea kiasi cha shilingi Laki mbili kwa niaba ya Masiaga ambapo kwa kufanya hivyo ni kosa la kisheria hivyo anakabiliwa na mashitaka mawili ya kujibu’aliongeza mwendesha mashitaka huyo

Hataivyo watuhumiwa wote watatu walipewa masharti ya dhamana ambapo walitakiwa kuwa na mdhamini  ambaye anafanya kazi katika kampuni inayofahamika pamoja na kusaini hati ya kiasin cha shilingi laki tano ambapo wadhamini walifanikiwa kuweka kukidhi matakwa ya mahakama hiyo.

MWISHO

No comments:

Post a Comment