Saturday, June 9, 2012

WAMILIKI WA SHULE BINAFSI WAKUMBUSHWA KUWAKUMBUKA WATANZANIA KATIKA SUALA ZIMA LA AJIRA



HABARI NA UPAKO WA UFALME WA MUNGU


WAMILIKI wa shule binafsi wametakiwa kuacha kutoa ajira zaidi kwa walimu wa mataifa ya nje na badala yake wachukue walimu wa kitanzania ambao wanauwezo ili kuepusha shule zao na udanganyifu wa mithiani

Kauli hiyo imetolea mjini hapa na afisa elimu wa manispaa ya Arusha Bw Omary Mkombole wakati akiongea na wanachama wa Tamongsco ambao ni wamiliki pamoja namameneja wa shule mbalimbali jijii hapa

Bw Mkombloe alisema kuwa wamiliki hao wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanajiamini katika kazi zao ili waweze kufikia malengo mbalimbali ambayo wanayatka lakini kama wataendelea  kuwathamini zadii walimu wa mataifa ya nje basi hawataweza kufikia malengo

Alisema kuwa kuongeaz kingereza kwa mwalimu isiwe ni tija mojawapo ya kusababisha asilimia kubwa ya watu kuweza kuajiriwa bali wanatakiwa kuangalia sifa na vigezo vya mwalimu bora

Wakati huo huo mkaguzi wa elimu kanda ya kaskazini magharibi bw Victor Bwindiki aliwaambia walimu hao kuwa wanatakiwa kuwa wabiunifu dhidi ya shule zao za binafsi ili wali mu wasiwakambie ovyo

Bwindiki alisema kuwa endapo kama wamiliki wa shule wataboresha taasisi zao basi itasaidia kwa kiwango kikubwa sana hata kuweza kuongeza idadi ya wasomi ndani ya nchi ya Tanzania

Awali wamiiki hao wa shule pamoja na mameneja walisema kuwa wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa sana kuweza kuwafikia wananchi kwa kuwapa elimu iliyo baora lakini kinachowasumbua ni utozwaji wa kodi kubwa sana

Akiongea kwa niaba ya  wakuu hao mwenyekiti wa umoja huo jijini hapa Bi Ester Lema alisema kuwa Serikali inatakiwa kuaangalisa shuguli ambazo wanazifanya kwani ni shuguli kubwa sana ya kuweza kusadiia jamii lakini bado Serikali hiyohiyo imekuwa ni chanzo mojawapo cha kuwatoza ushuru.

Mwisho

No comments:

Post a Comment