Monday, June 11, 2012

CHUO KIKUU UDSM CHAFANYA KONGAMANO LA WANATAALUMA


Mwanataalum mkonge Profesa Goran Hyden akijibu hoja na maswali mbalimbali yalitolewa na wahadhiri na wanataalum mbalimbali kutoka ndani na nje ya Tanzania leo mjini Dar es salaam wakati wa kongamano la siku moja la wanataalum liloandaliwa maalum na Chuo Kikuu cha Dar es salaam la kutambua mchango wake kitaalum. 
Picha na Tiganya Vincent- MAELEZO- Dar e salaam.
Waziri Mkuu Mstaafu wa Uganda Profesa Apolo Nsibambi(kulia) akichangia mada jana mjini Dar es saam wakati wa kongamano la siku moja la wanataalum liloandaliwa maalum na Chuo Kikuu cha Dar es salaam la kutambua mchango wa Profesa  Goran Hyden alioutoa ndani na nje Tanzania. Wengine ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma George Yambesi(katikati) na Profesa Goran Hyden(kushoto)
Katibu Mkuu zamani wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Balozi Juma Mwapachu akichangia mada jana mjini Dar es saam wakati wa kongamano la siku moja la wanataalum liloandaliwa maalum na Chuo Kikuu cha Dar es salaam la kutambua mchango wa Profesa  Goran Hyden alioutoa ndani na nje Tanzania.Kulia ni Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es  salaam Profesa Rwekaza Mukanda. 
Profesa Bernadeta Killian wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam akitoa mada jana mjini Dar es salaam kuhusu kitabu cha Profesa Goran Hyden cha Beyond Ujamaa in Tanzania wakati wa kongamano la siku moja la wanataalum liloandaliwa maalum na Chuo Kikuu cha Dar es salaam la kutambua mchango wake kitaalum.
Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es  salaam Profesa Rwekaza Mukanda (kulia) akibadilishana mawazo na Waziri Mkuu Mstaafu wa Uganda Profesa Apolo Nsibambi (katikati) na Balozi wa Zambia nchini Judith Kangoma( kushoto) leo mjini Dar es salaam wakati wa kongamano la siku moja la wanataalum liloandaliwa maalum na Chuo Kikuu cha Dar es salaam la kutambua mchango wa Profesa  Goran Hyden alioutoa ndani na nje Tanzania 

No comments:

Post a Comment