Monday, December 3, 2012

KUSHINDWA KUFUATILIA MAENDELEO YA WANAFUNZI MASHULENI CHANZO CHA WANAFUNZI KUPEWA ALAMA ZA JUU HUKU WAKIWA HAWANA SIFA ZA KUPATA ALAMA HIZO

wanfunzi wa shule moja wakiwa zaidi ya 100 kwenye darasa moja


Na Queen Lema,Arusha

KUSHINDWA KUFUATILIA MAENDELEO YA WANAFUNZI MASHULENI CHANZO CHA WANAFUNZI KUPEWA ALAMA ZA JUU HUKU WAKIWA HAWANA SIFA ZA KUPATA ALAMA HIZO


IMEELEZWA kuwa kutokana na tabia ya baadhi ya wazazi pamoja na walezi kushindwa kufuatilia maendeleo ya watoto wao mashuleni kumesababisha kukithiri kwa wizi wa mithiani kwenye baadhi ya shule binafsi,huku wanafunzi wengine wakiwa wanapewa alama za juu wakati hawana uwezo wa kupata alama hizo.

Hayo yameelezwa na  Bw Wilson Shange ambaye ni mkurugenzi mkuu wa shule ya Sotwa iliopo maeneo ya Ilboru katika maafali ya tatu ya shule hiyo yaliyofanyika mapema jana.

Bw Shange alisema kuwa zipo baadhi ya shule ambazo msimamo wake ni kuwapa alama za juu wanafunzi huku wanafunzi hao wakiwa hawana uwezo wa kupata alama za juu hali ambayo inachangia sana kukithiri kwa wingi wa Mambumbu ingawaje wazazi wanajisifia kuwa watoto wanasoma

Alisema kuwa mbali na hiyo kuweza kuongeza idadi ya mambumbu tena wanaolipiwa ada pia inachangia sana hata kiwango cha elimu ndani ya Nchi ya Tanzania kupungua kwa kiwango kikubwa ingawaje Serikali inalia na kiwango cha elimu kinachotolewa kwa shule binafsi.

Alifafanua kuwa hali hiyo inachangiwa sana na baadhi ya wazazi au walezi ambao wanawapeleka watoto wao shule za binafsi kwa kuwa baadhi yao wana mila potofu kuwa mwanafunzi wa shule binafsi hana haja ya kufuatiliwa maendeleo yake

Bw Shange aliongeza kuwa hali hiyo inasababisha kukithiri kwa changamoto kubwa sana ndani ya shule hizo binafsi kwa kuwa baadhi ya shule na walimu ambao hawana maadili ndio wanapata fursa pekee ya kuanza kufanya udanganyifu wa kuwapa wanafunzi alama za juu huku wanafunzi hao wakiwa hawana uwezo huo

Aliongeza kuwa endapo kama wazazi na walezi wangekuwa na tabia ya kufuatiliwa maendeleo ya watoto wao shuleni basi wasingeweza kupewa alama za juu hivyo wangechangia sana maendeleo ya wanafunzi tofauti na sasa ambapo baadhi ya wazazi wanashindwa kufika mashuleni kwa kisingizio kuwa ni shule binafsi.

“inakuwa ni ngumu sana kwa baadhi ya shule hata kufanya maamuzi ya kitaaluma kwa kuwa wazazi na walezi hawaonekani kabisa wanajua ukishalipa ada umemaliza mchezo wa elimu kwa kweli tunakabiliwa na changamoto hiyo na kama wazazi na walezi wataendelea hivi ni wazi elimu ya hapa nchini itaendelea kushuka  badala ya kupanda”aliongeza Bw shange

Awali aliongeza kuwa ndani ya Shule hiyo ya Sotwa wameweka msimamo mbalimbali wa kuhakikisha kuwa wanafukuza wanafunzi ambao wazazi wao hawana mila na desturi za kufuatilia maendeleo ya watoto wao kwani kwa kuwafukuza watasababisha taaluma kupanda sanjari na maadili ambayo yamepotea sana tofauti na kuaacha kujua maendeleo ya mwanafunzi.

MWISHO



No comments:

Post a Comment