Monday, December 3, 2012

mwandishi wa habari arusha ashirkiana na watanzania wenye asili ya asia kutoa damu




WATANZIA wenye asili ya Kiasia 300,akiwemo na mwakilishi wa radio uhuru mkoa wa Arusha, wamejitokeza kuchangia damu kwenye mpango wa taifa wa damu salama kanda ya kaskazini katika zoezi liliofanyika hospital ya Shree Hindu Union Tample   jijini Arusha iliyoandaliwa na Patel Commonity na Koja Ithinasheri .

Zoezi hilo linafuatia kuwepo uhaba wa damu katika hospital ya mkoa wa Arusha, ambayo inakabiliwa na wagonjwa wengi hasa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano wenye mahitaji ya damu

Mgeni rasmi katika zoezi hilo ,mkuu wa mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, aliyewakilishwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mnasa Deusi Sabhi,amesema uchangiaji huo ni kuunga mkono juhudi za rais Kikwete za kuokoa maisha ya wajawazito, watoto wakati wa kujifungua pia  majeruhi wa pikipiki wanaohitaji kuongezewa damu wakati wa matibabu.

Mulongo amesema kuwa hospital ya mkoa inahitaji 80 % ya damu lakini imekuwa ikipokea asilimia 30 hadi 40 tu hivyo mahitaji ya damu bado ni makubwa  akawaomba wananchi kujitokeza  kwa wingi ili kuchangia damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano na wanaopata ajali za pikipiki.

“Damu hii inayotolewa na wananchi haiuzwi na ole wake mtumishi wa hospital atakayejihusisha na kuiuza ata shughulikiwa mara moja, damu haina mbadala wala haizalishwi kutoka popote” ,alisema mkuu wa mkoa .

Amesema mpango huo wa kuchangia damu ni kuunga mkono juhudi za rais Kikwete ambae ni mwenyekiti wa mpango wa Umoja wa mataifa wa kuhusu afya ya uzazi duniani


Nae mwenyekiti wa jumuia ya Patel ,Kanu Patel, amesema wamefikia uamzi huo wa kuchangia damu kwa sababu katika hospital ya mkoa wa Arusha watu wanapoteza maisha kutokana na kukosa damu

Amesema jumuia ya Patel inakusudia kuendesha zoezi lingine la kuchangia damu Januari 15 hadi 17 mwakani  litakalofanyika mjini Arusha hivyo akawaomba wananchi kujitokeza kuchangia damu ili kuokoa maisha ya watu.


Mganga mkuu wa mkoa wa Arusha, Dakta Frida Mokiti, amesema kuwa vifo vng vinavyotokea katika hospiotal ya mkoa husababishwa na upungufu wa damu.

Amesema upungufu wa damu unashikilia nafasi ya pili kwa vifo vya wagonjwa wanaolazwa katika hospital ya mount Meru,hasa wajawazito wanaotokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua na watoto wachanga chini ya umri wa miaka mitano  ambapo ugonjwa wa Ukimwi ndio unashika nafasi ya kwanza kwa vifo .Ameipongeza jumuia hizo za Patel na Koja Ithinasheri, kwa kuendesha zoezi hilo la kuokoa maisha ya wananchi ambao wanakosa damu wakati wa matibabu .



No comments:

Post a Comment