Sunday, December 23, 2012

Serikali ya Poland yakabithi miradi yenye thamani ya USD 360,000 kwa chuo cha Mifugo Kampasi ya LITA –Tengeru.

Serikali ya Poland yakabithi miradi yenye thamani ya USD 360,000 kwa chuo cha Mifugo Kampasi ya  LITA –Tengeru.

Happy Lazaro, Arusha.

SERIKALI  ya Poland imekabithi na kuzindua jumla ya miradi mitatu yenye thamani ya USD 360,000  iliyopo katika chuo cha mifugo Campus ya LITA   Tengeru , katika hafla iliyofanyika hivi karibuni chuoni hapo.

Aidha hafla hiyo ya makabithiano ilihudhuriwa na Mwakilishi kutoka wizara ya mambo ya nje (Poland)  ,Dr. Inveterinary and medicine PHD holder ,Dr. Maciej  klockiewicz ,na Mkurugenzi wa mradi huo, Dr.Eng.Wieslaw Ptach kutoka serikali ya Poland.

Akizungumzia miradi hiyo katika uzinduzi huo,Mkufunzi wa chuo hicho, David Malishi alisema kuwa awamu ya kwanza ya miradi hiyo ilianza rasmi mwaka 2009 ambapo wafadhili hao walianza kwa kununua vifaa mbalimbali vya kufundishia vikiwemo vya maabara.

Ambapo awamu ya pili mradi ulilenga kuimarisha matumizi mazuri ya maji ili kuboresha uzalishaji wa mazao katika malisho ya mifugo na chakula  ,pamoja na zana za kilimo ambapo waliweza kuchimba bwawa la kuhifadhia maji ya umwagiliaji na kujenga mifereji ili kuimarisha umwagiliaji.

Malishi alisema kuwa, mradi wa awamu ya tatu ulijikita zaidi katika umwagiliaji na ujenzi wa mitambo ya bioges na upandaji miti ambapo waliweza kukabithi pump za kumwagilia maji 2,pamoja na kukabithi visima 3 vya maji kila moja ikiwa na quibick mita 50 .

Aliongeza kuwa, katika bioges waliweza kukabithi jumla ya mitambo 2 ya bioges kila moja ikiwa na quibick mita 50 ,ikiwa ni pamoja na upandaji miti ambapo kwa msimu wa mwezi wa 3 hadi 6 jumla ya miti 4500 ilioteshwa kwa mchango wa serikali ya tanzania .

Alisema kuwa, katika miradi hiyo yote mitatu serikali ya Tanzania imeweza kuchangia asilimia 30 kama mchango wao .
Malishi alisema kuwa , kupitia miradi hiyo na kupatiwa vifaa mvalimbali hivi sasa wameweza kuboresha ufundishaji kwa vitendo zaidi kutokana na kuwepo kwa vifaa mbalimbali tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

‘Unajua hawa wafadhili wetu wa serikali ya Poland wametusaidia sana kwani chuo hiki ni cha zamani na kilikuwa kikikabiliwa na changamoto nyingi sana  ili kuweza kutoa elimu iliyo bora hivyo kwa sasa hivi kupitia miradi hiyo imesaidia chuo chetu kuweza kuonekana cha kisasa zaidi na kuendelea kupata idadi kubwa ya wanafunzi wanaokuja chuoni hapo kila mwaka’alisema Malishi.

Alitaja changamoto kubwa ambayo inawakabili chuoni hapo na taasisi zote za eneo la LITA Tengeru  ni uhitaji mkubwa wa maji ambapo kwa makisio wanahitaji USD 110,000 ili kujenga vizima ,hivyo pendekezo hilo wamelipeleka kwa wafadhili hao wa serikali ya Poland kuona kama watawawezesha .

Naye mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Naibu Katibu mkuu wizara ya mifugo na uvuvi , Dkt Yohana Badeba alisema kuwa kuwepo kwa uhsirikiano huo mzuri katika ya serikali ya Poland na Tanzania utawezesha kwa kiasi kikubwa kuzidi kuboresha miradi mbalimbali katika chuo hicho kwani kimekuwa kikikabiliwa na changamoto nyingi sana.

Aliwashuruku wafadhili hao kwa msaada mkubwa walionyesha chuoni hapo wa kujenga miradi mbalimbali itakayowezesha chuo hicho kuweza kufikia malengo yake waliyojiwekea ,hivyo kuwasihi kuzidisha ushirikiano huo zaidi.

Alikitaka chuo hicho la mifugo LITA kutumia vifaa mbalimbali walivyokabithiwa kwa ajili ya kuboresha chuo hicho kuhakikisha wanazitumia ipasavyo na kwa manufaa ya chuo hicho kwa ujumla.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment