Monday, December 3, 2012

WATIENI MOYO WALE WALIOKATA TAMAA


WATIENI MOYO WALE WALIOKATA TAMAA

NA BETY ALEX,ARUSHA

MAKANISA mbalimbali hapa nchini yameshauriwa kujiwekea utaratibu wa kuhakikisha kuwa yanawatia moyo waumini wake kwa kuwakusanya sehemu moja kwani kupitia umoja huo utaweza kuwasaidia hata walio kata tamaa katika mambo mbalimbali kuweza kusonga mbele zaidi.

Akiongea na “Nyakati”mara baada ya kuwakusanya waumini wa baadhi ya  makanisa ya PEFA mjini, Mchungaji Noel Urio alisema kuwa kama makanisa hayo yataweza kufanya hivyo yatasaidia sana  kuwatia moyo

Noel alisema kuwa asilimia kubwa sana ya waumini ambao wapo makanisani sio kuwa wote wapo vizuri lakini bado kuna wengine ambao wanakabiliwa na matatizo ya hali ya juu sana lakini kama kanisa litatumia nafasi hiyo litaokoa kondoo wengi zaidi

Aliongeza kuwa waumini wanapokaa pamoja na kushiriki kwa pamoja masuala mbalimbali hata kama ni chakula cha mchana au usiku kunasababisha hata waliokata tama kuweza kuibuka tena na kufanya mabadiliko hata ya kimwili na kiroho

‘hakuna kiti kibaya sana kama mtu anapokata tama lakini faraja yake inatakiwa kupatikana makanisani na makanisani ni vema basi hata siku moja kanisa likatenga siku ya kuhakikisha kuwa wanabadilishana mawazo na kama waumini wataweza kubadilishana mawazo basi muafaka wa kukua kwa kiroho utapanda sana’aliongeza Noel

Katika hatua nyingine alisema kuwa nao waumini wanapaswa kujua na kutambua kuwa kamwe watu hawapaswi kukata tama kwani kukata tama ni dhambi kubwa sana na ukataji wa tama ndiyo nafasi shetani anayoitumia kuwarudisha watu nyuma katika msingi wa imani za leo

Alifafanua kuwa hata kama mtu akikumbwa na matatizo ya aina gani kamwe hapaswi kukata tamaa bali anapaswa kuangalia makusudi ya mungu yanavyosema na kudai na pia kabla ya kukata tamaa wanatakiwa kuangalia wachungaji wao wa makanisa ili waweze kutiwa moyo

‘Kazi kubwa sana ya kanisa ni kuwatia watu  moyo sasa unapokuja kanisa ukiwa umekata tamaa na kisha ukamlilia Mungu pamoja na kumshirikusha hata Mchungaji wako unaweza kusonga mbele zaidi kuliko kukaa kimya ,na hapo kazi ya kanisa itajulikana kwa kuwa utaweza kusimama na kutiwa Moyo hivyo utashinda tu”aliongeza Mchungaji huyo

MWISHO

No comments:

Post a Comment