Wednesday, December 19, 2012

-WENYEVITI WA VIJIJI VITANO MERU WAMFUKUZA DIWANI MERUWAMPA SIKU 14 KAMA HATAJIUZULU WAO WATAJIUZULU UCHAGUZI URUDIWE UPYA



-WENYEVITI WA VIJIJI VITANO MERU WAMFUKUZA DIWANI MERUWAMPA SIKU 14 KAMA HATAJIUZULU WAO WATAJIUZULU UCHAGUZI URUDIWE UPYA

-KISA WADAI KUWA DIWANI HUYO NI MCHOCHEZI NA ANALIPIZA KISASI KWA KUWA HAWAKUMPA KURA 2010

KATIKA hali  isiyokuwa ya kawaida Wenyeviti wa Vijiji Vitano kutoka katika kata ya Nkoaranga Wilayani Meru mkoani hapa wamemtaka diwani wa kata hiyo kujiuzulu ndani ya siku 14 na endapo kama hawatafanya hivyo basi wao watalazimika kuachia ngazi kwa kuwa wanaonewa sana na diwani huyo

Wenyeviti hao walitoa tamko hilo jana mara baada ya diwani huyo kushindwa kuwasikiliza kero zao pamoja na  za wananchi na badala yake kupewa maneno ya kashfa yakiwemo maneno ya uvaaji wa kimaskini huku pia kila siku kuna kithiri wimbi la migogoro

Wakiongea jana na “MALKIA WA MATUKIO”wilayani humo wenyeviti hao walisema kuwa wanazo sababu maalumu za kumakataa diani huyo ambaye ni Bw Goodfey Kishongo kwa kuwa yeye ndio chanzo pekee cha vurugu na Migogoro ndani ya kata  hiyo ya Nkoaranga hali ambayo imesababisha maendeleo kuwa duni sana

Wenyeviti hao ambao wanatokea katika Vijiji Vitano vya Kata hiyo ambavyo ni Njani, Nshupu,Nkoaranga,Nkoanekoli,na Sangananu walisema kuwa na endapo kama ataendelea kukaa madarakani  hata kama amepitishwa na wananchi basi baada ya siku 14 wao watajiuzulu na kupisha uchaguzi mwingine uanze upya kwani hawapati msaada wala ushirikiano wowote kutoka kwa diwani huyo na badala yake wanaambulia kasfa ya kuitwa maskini

Walisema kuwa zipo sababu maalumu ambazo zinasabababisha wao watamke hayo ingawaje wote ni chama Kimoja (CCM) kwani diwani huyo amekuwa akiwageuka mara kwa mara na hivyo kusisitiza hata migogoro ndani ya jamii huku pia akishirikiana na Vyama vya Upinzani ili waweze kutoka madarakani na kuachia wapinzani badala ya CCM

 Wakielezea kisa halisi cha kuwafanyia hivyo ilihali wao wote ni viongozi wa Serikali ya Kijiji walisema kuwa chanzo halisi diwani huyo anasema kuwa hawakumpa kura kwa mwaka 2010 za udiwani hali ambayo inafanya kila ambaye anamuhisi  hakutoa kura anamuharibia kwa wananchi tena kwa kuwagombanisha na kisha kuibua migogoro ambayo haina ukweli ndani yake .

Waliongeza kuwa mbali na kuwachukia viongozi hao wa Vijiji kama Vitano vya Kata hiyo ilihali wameshapatanishwa kama mara tatu lakini pia diwani huyo amelkuwa na tabia ya kugomea miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Kata hiyo hali ambayo  nayo inachangia sana Umaskini kwa vijiji hivyo.

Wakitaja baadhi ya Miradi ambayo diwani huyo amemwaga Sumu na kusababisha madhara makubwa kwa jamii  ni Pamoja na Mradi wa  mbuzi wa maziwa kutoka katika kijiji cha Nshupu ambao ulitolewa na TASAF ambapo mradi huo ulitekelezwa  na kikundi kimoja  lakini bado diwani huyo aliukata na hivyo kusababisha madhara makubwa  kwa wakazi wa eneo hilo.


Walisema kuwa mbali na eneo hilo la Nshupu lakini pia kwa maeneo kama vile Nkoaranga alisababisha  mwenyekiti wa Kijiji kufungiwa Nje ya Ofisi na wananchi wenye hasira kali lakini baadaye ofisi ilifunguliwa chini ya Mkurugenzi wa Halmashauri,huku kwa Kijiji cha Sangananu aliwashawishi wananchi kukata zahanati ambayo ilijengwa na wahisani,na kwa upande wa Kijiji cha Nkoanekoli napo aligomea vyanzo mbalimbali vya maji hali ambayo ilizua tafrani kubwa sana

Na katika Kijiji cha Njani napo Mgogoro mkubwa sana kwa sasa ni matumizi ya maji ya kuchimba kwa kutumia mashine ambapo kuna mvutano mkubwa sana lakini hali hiyo imesababisha baadhi ya kazi za kijamii nazo kusimama kwa kuwa hakuna umoja madhubuti.


Awali wenyeviti hao kutoka katika Vijiji vitano ambao wanatarajia kujiuzu endapo kama diwani huyo atajiuzulu ndani ya siku 14 ni pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji cha Nkoaranga bw Solomon Sarakikya,Mwenyekiti kijiji cha Njani bw Elishilia Ayo,mwenyekiti wa kijiji cha Sangananu Bw Sangito Mafie,na Mwenyekiti wa kijiji cha Nkoanekoli Bw Christopher Pallangyo

Katika hatua nyingine akiongea na “MALKIA WA MATUKIO”kwa njia ya simu diwani huyo anayetuhumiwa Bw Goodfrey Kishongo alisema kuwa yeye anachokijua ni kuwa wenyeviti hao wamejiunga na kuwa kitu kimoja kwa kuwa wote wana mapungufu tena makubwa sana hasa ya ulaji wa mali za kijiji

Bw Kishongo alisema kuwa bado haogopi kwa kauli ya wenyevit hao kwa kuwa wao si wananchi na wananchi ndio waliomchagua na kumpa kura hivyo kama wananchi watamkataa ndio ataweza kujiuzulu lakini kamwe hawezi kujiuzulu kisa wenyeviti  wa vijiji

“bado hawa wenyeviti hawajaongea jambo la msingi mimi ni ,muwazi tena ni mkweli huwa sina mambo ya kupindapinda  kamwe wajue kuwa suala la kuachia ngazi sio suala la matisho kama wanavyofikiri bali ni suala la wananchi wananchi wakisema hawananitaki hata sasa hivi naacha udiwani”alisema Bw Kishongo


Naye Mkurugenzi Mtendajiwa halmashauri hiyo Bw Trisias Kagenzi alisema kuwa bado hajapata taarifa kuhusiana na tamko hilo la wenyeviti hao lakini atahakikisha kuwa anakaa nao chini na kujua chanzo halisi

No comments:

Post a Comment