Wednesday, December 4, 2013

KANISA LATANGAZA NEEMA KWA WAHUDMU,WAHADIWA KUPEWA MASAMBA YA KILIMO KWA AJILI YA MSIMU MPYA WA KILIMO UJAO

NA BETY ALEX, ARUSHA


HUDUMA ya Maisha ya Yesu iliopo maeneo ya Kisongo jijini Arusha imesema kuwa kwa kutambua mchango wa wahudumu lakini pia wazee wa kanisa hilo wanatarajia kuwagawia mashamba ya kulima ili waweze kujiendeleza kwenye maisha yao ya kila siku na kuachana na tabia ya kuwa tegemezi

Aidha mpango huo unakuja mara baada ya kanisa hilo kuanza kutoa na kusisitiza masomo ya upendo ambayo yanalenga kumuinua zaidi Mungu kuliko mwanadamu

Akitangaza msimamo huo wa kuwasaidia wahudumu hao mchungaji kiongozi wa huduma hiyo Eliakimu molel”Channel”alisema kuwa mpango huo utasaidia sana kuongeza ufanisi wa kazi za kila siku lakini hata za kanisa

Alisema kuwa kwa kufanya hivyo wahudumu hao hasa wale ambao hawana kazi wataweza kuepukana na dhambi mbalimbali ambazo zinasababishwa na ukosefu wa kazi za kufanya

“ukiwa kama muhudumu hapa kanisani kwangu nilazima nihakikishe kuwa mnatoka siwezi kutoboa mimi mwenyewe halafu ninyi mkabaki mkiwa hamna lolote nasema nitagawa mashamba ya kulima na kila atakayweze akulima katika mashamba hayo ni lazima atoke”aliongeza Channel

Pia alisema kwa kanisa lolote lile ili liweze kusimama vema wahudumu lakini pia hatawazee wa kanisa wanapaswa kuwa makini kuanzia kiroho hadi kimwili hivyo ni wajibu wa viongozi wa makanisa kuhakikisha kuwa wanawaangalia makundi hayo

Alidai kuwa kama wakiwa dhaifu kwenye nyanja yoyote ile ni lazima kuwepo na kasoro kwenye huduma hiyo na badala yake badala ya kusonga mbele kwenye wokovu basi hata waumini watakuwa wanarudi nyuma kwenye wokovu

“wahudmu, wazee wa kansiani watu muhimu sana kwenye maendeleo ya kanisa la leo tusiwaache wakawa legelege bali tuwainue juu hata hali zao za maisha ziweze kubadilika ni faraja sana kama mhudumu wa kanisa akapanda daraja kwenye kiwango cha juu alafu pia akawa na imani basi hata mimi mchungaji nitafanya kazi yangu bila shaka ila kama akiwa legelege pepo likija linaanza nay eye kwanza”aliongeza Channel

Wakati huo huo alisema kuwa pia kanisa hilo limejiwekea hata utaratibu wa kuweza kuwasaidia wale wasiojweza kwa kuwa msaada wa vyakula ili wasiwe wakrisro wenye imani lakini pia wawe na uwezo kuamini kuwa hata kama hawana kitu bado mchungaji wao anawapenda na anaweza kufunga na kuomba juu yao ili hali za maisha ziweze kubadilika.

MWISHO

No comments:

Post a Comment