Saturday, October 26, 2013

WAFADHILI KUTOKA UJERUMANI WATOA MSAADA WA VITABU WENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 9


MERU

WAFADHILI kutoka Ujerumani wamefanikiwa kutoa msaada wa vitabu venye thamani ya Milioni tisa kwa shule ya sekondari Leguruki iliopo Wilayani Meru mkoani Arusha kwa lengo la kuongeza ufanisi wa elimu zaidi kwenye shule hiyo.

Akiongea na wanafunzi shuleni hapo mapema jana mara baada ya kupokea msaada huo Mjumbe wa kamati ya siasa mkoa wa Arusha John Palangyo alisema kuwa msaada huo utasaidia sana shule hiyo ya sekondari ambayo pia ipo chini ya Chama cha mapinduzi.

Palangyo alisema kuwa wafadhili hao wameamua kutoa msaada huo wa vitabu venye thamani ya milioni tisa lakini ni wajibu wa wanafunzi kuhakikisha kuwa wanavisoma na kuvifanyia kazi vitabu hivyo kwani vina mitaala ya nchi ya Tanzania

Pia alsiema kuwa kama wanafaunzi wa shule ya sekondario yoyote ile hapa nchini watakuwa na tabia ya kujisomea vitabu mbalimbali basi watachangia kwa kiwango kikubwa uelewa tofauti na sasa ambapo bado wapo wanafunzi wanaosoma kwa kufundishwa na walimu pekee.

Alibainisha kuwa kuna umuhimu mkubwa sana wa walimu wenyewe kuhakikisha kuwa wanawasisitiza wanafunzi kujisomea vitabu na kuachana na tabia ya kujidanganya kuwa hata wasiposoma watakuwa na maisha mazuri tena yenye mvuto wa hali ya juu jambo ambalo nalo linachangia sana kuongeza idadi ya wanaofeli katika shule za Sekondari pamoja na Vyuo vikuu hapa nchini

“mimi napenda kuwaambia kuwa msije kuona kuwa watu wana maisha mazuri mkadhani kuwa hawakujituma kusoma vizuri shuleni ni lazima kama mnataka maisha mazuri basi mjitume kusoma kwa bidii lakini pia msikubali kujiwekea fikra ambazo zinawapotosha kwani hizo ndizo zinazochangia ninyi mje kuwa na  maisha mabaya hapo baadae”aliongeza Palangyo

Katika hatua nyingine aliwataka hata walimu kuwatengenezea wanafunzi mazingira mazuri  na kuwapa motisha wanafunzi  hasa kwenye suala zima la usomaji wa vitabu kwani kwa kufanya hivyo kutaweza kuruhusu walio wengi kupenda kujisomea vitabu.

Awali mkuu wa shule hiyo ya Leguruki Emanuel Loi alisema kuwa msaada huo wa Vitabu umekuwa na tija kubwa sana shuleni hapo kwani hapo awali shule nzima ilikuwa na vitabu 52 na sasa wameweza kufanikiwa kupata vitabu zaidi ya elfu jambo ambalo litaweza kuwanufaisha wanafunzi shuleni hapo

Alimaliiza kwa kusema kuwa hata wazazi nao wana jukumu kubwa sana la kuhakikisha shule za sekondari zinakuwa na Vitabu vya kutosha ili kuweza kuharakisha maendeleo ya elimu

No comments:

Post a Comment