Monday, December 16, 2013

WASANII ARUSHA WAHIDIWA NEEMA


KAMPUNI ya Mkundi Production yenye makao makuu Jijini Arusha imeahidi kuibua lakini pia kuwezza kuendeleza vipaji vya  mbalimbali vya vijana ikiwa ni pamoja na kuweza kuwasaida kurekodi na kusambaza kazi zao

Aidha kwa sasa asilimia kubwa ya vijana wenye vipaji vya uimbaji wanashindwa kufikia malengo yao mbalimbali kwa kuwa hawana uwezo wa kuingia studio lakini pia kutoa na kughramikia baadhi ya gharama hali ambayo inachangia sana kupoteza vipaji vingi

Hayo yameelzezwa na mkurugenzi jmtendaji wa kampuni hiyo Carlos Mkundi mapema jana mara baada ya kuzindua Album ijulikanayo kama “NIMETOKA  MBALI”ambayo imejumuisha vijna mbalimbali wa mkoa wa Arusha

Mkundi alisema kuwa kampuni yakeimejidhatiti kuhakikisha kuwa kila msanii mwenye uwezo wa kuimba aweze kunufaika na kipaji chake na kamwe kisingizo kuwa ghrama ni chanzo kisiwepo

Aidha alidai kwa sasa wasanii wa nyimbo mbalimbali ndani ya mkoa wa Arusha wanashindwa kuimba na kutoa album zao kwa kuwa kuna changamoto lukuki sana ambazo ndizo chanzo kikubwa cha wao kushindwa kufanya vema zaidi

Wakati huo huo alisema kuwa kwa kipindi cha mwaka huu Kampuni yake tayari imeshwaweza kuwasaidia wasanii saba kuweza kurekodi album zao na hivyo mikakati zaidi bado itaendelea kuwekwa

Pia alidai kwa kila mwaka wasanii saba kutoka Jijini Arusha wataweza kurekodi kwa msaada wa kampuni hiyo lakini hata wale ambao bado hawajaweza kurekodi basi watapewa misaada mbalimbali ambayo inalenga kuinua vipaji vyao zaidi

MWISHO

No comments:

Post a Comment