Thursday, November 16, 2017

WAZIRI AISHAURI SERIKALI JINSI YA KUPINGA RUSHWA KUANZIA NGAZI YA CHINI KABISA

 Na Queen Lema, Arusha

Waziri wa nchi,ofisi ya rais na utumishi George Mkuchika ameishauri wizara ya elimu kutoa elimu dhidi ya mapambano ya rushwa kwa wanafunzi kuanzia shule za msingi hadi chuo kikuu ili kuwawezesha kutambua madhara yanayotokana na rushwa.

Mkuchika aliyasema hayo  alipokuwa akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa nchi za umoja wa Afrika zinazopambana na rushwa unaoendelea jijini hapa

Alisema kuwa endapo kama elimu ya rushwa itaweza kutolewa mashuleni kuanzia ngazi za awali itawezesha kupunguza kasi ya rushwa kwa nchi husika na hivyo taifa husika kupata haki zake za msingi

Aliongeza kuwa watu wengi wanatoa rushwa kwa kushindwa kufahamu haki zao za msingi hivyo elimu hiyo ikitolewa kuqnzia ngazi za chini itapunguza vitendo vya rushwa ambavyo vimekithiri kwa baadhi ya nchi.
Alitolea mfano nchi za Norway na Sweden ambazo zimekuwa zikitoa elimu ya rushwa kuanzia ngazi za chini mpaka vyuo vikuu ambapo imesaidia kila mtu katika nchi hizo  rushwa kuwa adui wao.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Takukuru  hapa nchini Valentine Mlowola alisema kuwa kutokana na rushwa kukithiri hapa tanzania wamefanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi bilioni 14 kwa kipindi cha mwaka huu ambazo zilikuwa zikitumika kwenye rushwa.

Alidai kuwa kwa sasa rushwa imekuwa tatizo la kimataifa hivyo kupitia mkutano huo wa umoja wa nchi za afrika wataweza kupanga mikakati ya kupunguza tatizo la rushwa katika nchi hizo.

Ameongeza kuwa nchi za afrika hazitaweza kujikwamua kiuchumi bila kumaliza tatizo hilo kutokana na maliasili nyingi zinazopotea kwenye bara hili zimekuwa zikipotea kutokana na rushwa.

No comments:

Post a Comment