Monday, December 16, 2013

WAZIRI AZITAKA NCHI ZA AFRIKA ZIUNGANE ILI KUPAMBANA NA RUSHWA


WAZIRI wa nchi ofisi ya rais anayeshughulikian utawala bora George
Mkuchika amezitaka nchi za Afrika  kujenga umoja na kupeana uzoefu
katika vita vya kupambana na rushwa huku  nchi hizo z ikitakiwa
kujenga sera za uwazi kwenye sekta nzima ya rasilimali ili waweze
kunufaika nazo ikiwa ni pamoja na kupaza sauti moja kuomba kurejeshwa
kwa fedha zilizoko nje ya bara la afrika.

Mkuchika alitoa kauli hiyo jana  alipokuwa akifunga na kusherehekea
maadhimisho ya siku ya umoja wa mataifa ya mapambano dhidi ya rushwa
yaliyofanyika jini hapa

Alisema kuwa umoja una  nguvu katika kupambana na rushwa hivyo ili
kuhakikisha kuwa swala hilo linatokomezwam nchi za afrika zinapaswa
kutekelza kwa vitendo mkataba wa umoja wa afrika dhidi ya rushwa kwa
kila nchi kujiunga moja kwa moja kwa kutoa uzoefu juu ya mapambano
dhidi ya rushwa ambayo yameonekana kurudisha nyuma maendeleo ya bara
la afrka.

Alieleza kuwa pamoja na chi za Ulaya kuwa mstari wa mbele katika
mapambano dhidi ya rushwa lakini nchi hizo zimekuwa zikikumbatia
Uhamishaji wa fedha kutoka bara la afrika na kukaa kimya
kilawanapotakiwa urejeshwaji wa fedha zilizopo kwenye mataifa hayo


Aidha alifafanua kuwa nchi 30  zimesaini mkataba wa umoja wa mataifa
wa mapambano dhidi ya rushwa kati ya nchi 44 zinazotakiwa kusain
mkataba huo hivyo kuzitaka nchi zilizobaki kujiunga na umoja huo ili
kuliletea maendeleo bara la afrika na kuwa na sauti moja ya mapambano
dhidi ya rushwa huku akizitaka nchi za bara la afrika kutambua kuwa
mapambano si ya rushwa si ya mtu moja bali ya watu wote.

Nae mkurugenzi wa takukuru nchini Drt Edward Hosea alisema kuwa bara
la afrika bado lina safari ndefu katika mapambano ya vita vya rushwa
kwani kati ya nchi za afrika 34 kati ya 44 ndizo amabzo zimesaini
mkataba wa mapambano ya rushwa huku akidai kuwa mikataba mingi
inaingia kwenye rasilimali za nchi za bara la afrka haina uwazi na
sheria zinazotumika  hazimnufaishi mwananchi wa kawaida dhidi
yamapambano ya rushwa.

Aidha aliitaka serikali kuweka sera ya uwazi kwenye mikataba ya
wawekezaji wa rasilimali ya gesi ili iweze kuwanufaisha watanzania na
sheria zitakazotungwa iwe ya uwazi na yenye faida kwa watanzania
hukuakizishawishi nchi ambazo hazijatakeleza mkataba wa umoja wa
mataifazifanye hivyo mara moja kwani bara la afrka ndilo linalohitaji
maendeleo makubwa hivyo bila kuungana hawataweza kufanikiwa.

MWISHO.

No comments:

Post a Comment