Monday, December 16, 2013

UKOSEFU WA HUDUMA ZA MAJI ZA UHAKIKA CHANZO CHA NDAO NYINGI KUVUNJIKA, PIA CHANZO CHA MIMBA ZA UTOTONI





IMELEZWA kuwa ukosefu wa huduma za uhakika za maji hasa maeneo ya vijijini ni chanzo mojawapo cha ongezeko la mimba  za utotoni lakini pia uvunjikaji wa ndoa nyingi huku hali hizo zikisababisha pia ongezeko la watoto mitaani ndani ya mji wa Arusha

Pia hali hiyo ya ukosefu wa maji kwenye kaya pia inasababisha umaskini wa hali ya juu sana ingawaje Serikali kwa sasa inaweka mikakati mbalimbali ya kupambana nao.

Hayo yameelezwa na Bi Asha Shabani ambaye ni Katibu wa Mradi wa maji ujulikanao kama Mangole uliopo maeneo ya Kisongo jijini hapa,wakati akielezea mradi huo lakini pia umuhimu wa miradi ya uhakika ya maji hasa kwa maeneo ambayo yapo nje ya miji

Asha alisema kuwa ukosefu wa maji ya uhakika hasa katika maeno ambayo yapo nje kidogo ya miji ni changamoto kubwa sana kwa wanawake kwa kuwa asilimia kubwa huambulia uchovu lakini pia hata kipigo kutoka kwa wenza wao kwa kuwa hutumia muda mrefu kwa ajili ya kusaka maji

Mbali na hayo alisema kuwa ukosefu huo hauathiri pekee wanawake bali hata mabinti wadogo ambao baadhi ya vijana hutumia mwanya huo katika kuwadanganya ili waweze kuwapa maji au kuwasaidia kubeba maji kwa uraisi jambo ambalo nalo ni chanzo kikubwa cha mimba za utotoni lakini pia mdondoko wa elimu kwa watoto wa kike

Akiongelea Mradi huo wa MANGOLE ambao unawasaidia wananchi kutoka katika kata za Matevesi,Ngorobobu, na Lemguru alisema kuwa umekuwa ni faida kubwa sana kwenye jamii hiyo kwani hapo awali kulikuwa na matatizio mengi sana

Alitaja matatizo hayo ni pamoja na baadhi ya wanawake kukosa ndoa,huku wengine wakiambulia wajukuukabla ya wakati kutokana na udanganyifu ambao ulikuwa uanendelea kwa watoto wa kike na vijana pia.

“hapo awali tulikuwa tunalazimika kwenda kilomita mpaka 20 kwa siku ili kutafuta maji lakini toka mradi huu uletwe kwa hisani ya Word Vision umekuwa na faida kubwa sana na hivyo tunataka tuhakikishe kuwa hata wanawake wa maeneo mengine ndani ya mkoa wa Arusha nao wanaweza kufaidika na miradi kama hii ili waweze kuepukana na changamoto za uhaba wa maji”aliongeza Asha

Wakati huohuo Mwenyekiti wa Mradi huo ambaye ni Profesa Calvin Marealle alisema kuwa pamoja na kuwa mradi huo umekuwa ni faida kubwa sana kwa jamii lakini bado unakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile Ukosefu wa umeme wa uhakika hali ambayo wakati mwingine inasababisha baadhi ya wananchi kutoka katika vijiji hivyo vitatu kukosa maji ya uhakika

Profesa Marealle aliongeza changamoto nyingine ni pamouja na baadhi ya wananchi kuiba na kuharibu miundombinu ya maji hali ambayo ni chanzo kikubwa sana cha hasara kwenye miradi hiyo.

MWISHO

No comments:

Post a Comment