Monday, December 16, 2013

WANAWAKE 200,WATOTO 1000 WAFANIKIWA KUPEWA ELIMU PAMOJA NA UWEZESHWAJI KIUCHUMI KWA AJILI YA KUPAMBANA NA UMASKINI



Na Queen Lema, Arusha

ZAIDI  ya watoto elfu pamoja na wanawake mia mbili kutoka jijini
Arusha wamefanikiwa kuwezeshwa kiuchumi pamoja na kupatiwa elimu
mbalimbali ili kupunguza kasi ya ongezeko la watoto mijini lakini pia
kwenye vituo vya kulelea watoto yatima

Hataivyo watoto hao pamoja na wanawake hao wamefanikikiwa kupatiwa
elimu pamoja na uwezeshwaji hali mabyo mpaka sasa imeweza kuonesha
mafanikio ya hali ya juu sana.

Wanawake hao pamoja na watoto wamewezeshwa na Kijiji kinachotoa malezi
mbadala ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu(SoS)chini ya mradi
wa kuimarisha familia(FSP)unaotekelezwa sehemu mbalimballi nchini.

Hayo yamelezwa na Mratibu wa utetezi kutoka katika kijiji hicho cha
SOS ambaye ni John Batista wakati akiongea kwenye maazimisho ya
ukatili wa kijinsia kwa wanwake na watoto yaliyofanyiika katika eneo
la Kimnyaki Jijini Arusha mapema wiki hii

Batista alisema wanawake hao 200 pamoja na watoto elfu moja wameweza
kusaidiwa kutokan ana kampeni ambayo inaendeshwa chini ya SOS ya
kupinga nakutokomeza suala zima la unyanyasaji kwenye kwenye jamii.


Alisema kuwa kwa kuwawezesha wanawake hao pamoja na watoto kutasaidia
sana kupungua kwa umaskini kwenye jamii kwani umaskini unapokithiri
basi unachangia hata suala zima la malezi nalo kuwa duni sana.


Mbali na hayo Batista pia alitoa wito kwa jamii kuhakikisha kuwa
wanachana na ukatili dhidi ya wanawake lakini pia kwa watoto kwani
hali hiyo ndiyo chanzo cha ongezeko la watoto wa mitaani

No comments:

Post a Comment