Monday, December 16, 2013

KIKUNDI CHA OLGILAI CHANGAMKENI YOUTH GROUP CHAFANIKIWA KUTOA MSAADA WA MADAWATI,NA VIFAA VYA SHULE YA OLGILAI


KIKUNDI CHA OLGILAI CHANGAMKENI YOUTH GROUP CHAFANIKIWA KUTOA MSAADA WA MADAWATI,NA VIFAA VYA SHULE YA OLGILAI

Na Queen Lema, Arusha


KIKUNDI cha Olgilai Changamkeni Youth Group kilichopo maeneo ya Olgilai mkoani Arusha kwa kushirikiana na wadau wengine wa elimu wameweza kutoa msaada wa madawati zaidi ya 50 pamoja na vifaa vingine kama vile meza, kabati, na viti  kwa shule ya msingi Olgilai huku lengo likiwa ni punguza changamoto za kielimu shuleni hapo

Hataivyo msaada huo ambao ulitolewa mapema jana ulienda sanjari na uzinduzi wa kikundi hicho ambacho kimelenga kutatua changamoto mbalimbali katika kijiji hicho cha Olgilai na Mkoa wa Arusha kwa ujumla.

Akiongea mara baada ya kukabidhi msaada huo kwa shule ya msingo Olgilai Mwenyekiti wa kikundi hicho Benjamini Justin alisema kuwa wameamua kuchangia zoezi zima la elimu ili kwenda sanjari na mpango wa serikali wa matokeo ya haraka(BRN)

Benjamini alidai kuwa hapo awali shule hiyo ilikuwa inakabiliwa na changamoto kubwa sana ya ukosefu wa madawati na vifaa vingine hali ambayo ilifanya wazazi wa eneo hilo ambao ni wanakikundi kuhakikisha kuwa wanatafuta mbinu ya kukabiliana na changamoto hiyo.

Alifafanua kuwa baada ya kuweka mikakati mbalimbali waliweza kuwashirikisha wadau wengine ambao nao waliweza kuungamkono na kuhakikisha kuwa wanapunguza tatizo la uhaba wa madawati kwenye shule hiyo ya Olgilai.


Wakati huo huo alidai kuwa pamoja na kuwa wameweza kufanikisha kutoa msaada huo wa madawati, meza,viti, madaftari, na kalamu lakini bado wanakabiliwa na changamoto lukuki ambazo wakati mwingine zinakwamisha jitiada zao

Alitaja changamoto hiyo kuwa ni pamoja na baadhi ya fursa za mikopo ni finyu kwa kuwa taasisi hizo hazitoi mikopo kwa vikundi jambo ambalo linakwamisha jitiada za maendeleo ya vikundi hasa vile vya mitaa.

“pamoja na kuwa leo tumeweza kutoa msaada huu kwa shule hii pamoja na kuzindua rasmi kikundi chetu bado changamoto hii tunaifikiria sana hivyo basi tunaomba taasisi za Fedha kuhakikisha kuwa zinatuangalia ili nasi tuweze kusaidia jamii kama tulivyofanya leo”aliongeza Benjamini

Wakati huo huo akiongea kwa niaba ya wanafunzi ambao ndio walengwa wa msaada huo Irene Peter alidai kuwa msaada huo wa madawati utasaidia sana kuongeza ufanisi wa elimu kwani hapo awali wanafunzi shuleni hapo walikuwa wanalazimika kuandika Miandiko mibaya kwa kuwa hawakuwa na madawati.

No comments:

Post a Comment