Wednesday, December 4, 2013

OFISI ZA CHADEMA ARUSHA ZACHOMWA MOTO NA WATU WASIOFAHAMIKA

Na Queen Lema, Arusha



KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida watu wasiofahamika jana(leo)wamevamia ofisi ya Chadema Kanda ya kaskazini iliopo Jijini Arusha na kisha kuanza kuwasha moto ambao ulisababisha hasara kubwa sana.

Akizungumza na “Majira”katibu wa kanda ambaye pia ni katibu wa mkoa wa Arusha Chadema, Amani golugwa alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya asubuhi katika ofisi za kanda zilizopo eneo la Ngarenaro mjini Arusha.

Golugwa alisema kuwa watu hao waliingia mara baada ya mlinzi kutoka zamu ya kulinda usiku ambapo walilazimika kuvunja kioo kikubwa na kisha kuingia ndani ili kufanya lile walilolikusudia.

Aliendelea kwa kusema kuwa baada ya kuingia ndani walipanda kwenye dari la nyumba hiyo ambapo walianza kutafuta uwiano wa chumba ambacho kinahifadhi nyaraka mbalimbali za Chama na kisha kuwasha moto

Alidai kuwa wakati wanawasha moto huo ghafla uliweza kulipuka hivyo lengo halisi halikuweza kutimia kwa haraka na badala yake walishuka na kuanza kukimbia wakati jingo letu likiwa linateketea kwa moto
Pia alisema baada ya watu hao kuona kuwa hawawezi kuchoma chumba hicho walitengeza shoti kubwa ya umeme ambayo iliweza kusababisha vyumba vya choo na bafu kuunguwa na hatimaye walishuka wakiwa wanakimbia huku moto ukiendelea kutapakaa kwenye jingo la ofisi hiyo.

“kilichofanya tuweza kusema kuwa walikuwa na lengo la kuchoma chumba hiki ambacho kinahifadhi nyaraka muhimu za chama ni baada ya kuona kuwa wameacha maeneo yote na kisha kuingia hapa na inavyoonekana lengo lao ni kupoteza ushahidi wa vitu mbalimbali ambavyo tunapambana navyo”aliongeza Golugwa

Katika hatua nyingine Golugwa alisema kuwa tukio hilo la kuchoma ofisi linaonesha kuwa wapo baadhi ya watu ambao wanatumia muda na fikra zao nyingi kuwawinda viongozi wa Chadema na kuingilia hata kwenye maisha yao ya kila siku

Aidha aliwataja watu ambao wanawindwa sana kwa ajili ya kujeruliwa ni pamoja nay eye ,mbunge wa jimbo la Arusha Mjini Goodbless Lema, pamoja na mwenyekiti wa wilaya ambaye ni Ephata Nanyaro
‘mpaka sasa tunawahisi watu watatu katika sakata hili na kwa maana hiyo tumesharipoti polisi ili waanze mara moja upelelezi wao lakini jingo letu tumeliwekea ulinzi mkubwa sana na kumbukumbu zote zipo ingawaje mpaka sasa bado hatujaweza kujua kwanza ni hasara ya shilingi ngapi tumeipata’aliongeza Golugwa

No comments:

Post a Comment