Monday, December 16, 2013

WAZEE ARUSHA WAPATIWA MSAADA


Asasi ya Informal Sector team(INSERT)imefanikiwa kutoa msaada wa Mablanketi yenye thamani ya zaidi ya milioni moja na nusu kwa Jukwaa la wazee wa mkoa wa Arusha (JUWA)huku lengo halisi likiwa ni kuhakikisha kuwa wazee wote wanaendelea kusihi maisha ya upendo na amani

Akiongea na wazee hao mara baada ya kuwapa msaada mratibu wa asasi hiyo ya INSERT,Japhet Saruni alisema kuwa msaada huo unalenga kuhakikisha kuwa afya za wazee zinaendelea kuboreka zaidi

Aidha Saruni alisema kuwa kwa sasa wazee wengi sana wamekuwa wakisahulika kwenye maslahi yao hali ambayo inachangia sana kuzorotesha hata afya zao ingawaje sera za wazee bado zipo

Alifafanua kwa kusema kuwa hali hiyo imechangia kwa kiwango kikubwa sana wazee wengi kupoteza maisha kabla ya siku zao hivyo basi ndio maana Asasi hiyo ya INSERT ikaweza kuona kuwa kuna umuhimu wa kuwasaidia wazee

Pia alisema kuwa kuna umuhimu wa jamii kuhakikisha kuwa wanatatua kero za jamii kila mara kwani kwa sasa jamii imeacha kabisa kuwasaidia wazee huku wazee nao wakikabiliwa na changamoto kubwa sana

Hataivyo alifafanua kuwa kama jamii itaweza kuwakumbuka wazee kila mara basi kasi ya ongezeko la vifo visivyo vya lazima hasa vya wazee vitaweza kupungua kwa kiwango kwani takwimu zinaonesha kuwa wazee wengi wanakufa kutokana na kuwa hawana msaada wa kuwasaidia.


Awali wazee waliopewa msaada walisema kuwa pamoja na kuwa wamepewa msaada huo bado kuna umuhimu wa sera za wazee kuweza kutekelezwa hasa kwenye sekta muhimu kwani sera hizo zipo lakini hazitekelezwi na baadhi ya watendaji tena wwa Serikali.

MWISHO

No comments:

Post a Comment