Wednesday, January 16, 2013

TANZANIA YAANZA RASMI KUTUMIA MFUMO WA KIMATAIFA NA KUACHANA NA MFUMO WA ZAMANI


TANZANIA YAANZA RASMI KUTUMIA MFUMO WA  KIMATAIFA NA KUACHANA NA MFUMO WA ZAMANI

Na Queen Lema,ARUSHA

Tanzania imeanza kutumia rasmi mfumo wa kimataifa katika masuala ya ukaguzi wa ndani ambapo mfumo huo utaweza kupunguza Viashiria mbalimbali vya ubadilifu wa fedha za umma

Hayo yamebinishwa  leo na mkaguzi mkuu wa ndani hapa Nchini Bw Mohamed Mtonga wakati akifungua mafunzo kwa wakaguzi wa ndani kutoka katika kanda ya kaskazini

Mohamed alisema kuwa mpango huo wa ukaguzi kwa mfumo wa Kimataifa umeanza kutumika rasmi hapa nchini July  Mosi ambapo utaweza kutoa na kuonesha viashiria mbalimbali ambavyo vinakwamisha shuguli za ukaguzi ndani ya Serikali kuu pamoja na  Serikali za Mitaa.

Alisema kuwa kupitia mfumo huo mpya wa kimataifa wa ukaguzi wa ndani utaweza kuboresha  na kuwafanya wakaguzi wa ndani kufanya kazi zao kwa uhuru zaidi tofauti na mfumo uliokuwa hapo awali ambao ulikua hautoi fursa kwa wakaguzi wa ndani

Alifafanua kuwa hapo awali wakaguzi wa ndani walikuwa wanashindwa kutekeleza  majukumu yao kutokana na viashiria vya vitu mbalimbali kama vile rushwa na uhusiano baina ya mkaguzi na mkaguliwa hali ambayo ilikuwa chanzo cha kukwamisha malengo mbalimbali ya ukaguzi hapa nchini ingawaje  ndani ya mfumo wa ukaguzi kimataifa suala hilo halipo kabisa.


Katika hatua nyingine alisema kuwa wakaguzi wa ndani bado wanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa bajeti hali ambayo nayo inafanya washindwe kufanya kazi na kukagua miradi kwa wakati husika

Alisema kuwa kwa sasa wakaguzi wa ndani wanashindwa kufika kwenye miradi tena  kwa wakati kutokana na uhaba wa bajeti ambazo zinatengwa na  Halmashauri huku hali hiyo pia ikichangia sana kutofikia malengo mbalimbali ya kiukaguzi ambayo  yanatakiwa kuwekwa na pia  kusaidia jamii


MWISHO

No comments:

Post a Comment