Tuesday, January 1, 2013

TEKELEZENI AHADI MLIZOZITOA WAKATI WA KUOMBA KURA-OLE NANGOLE


Na Queen Lema,Meru

TEKELEZENI AHADI MLIZOZITOA WAKATI WA KUOMBA KURA-OLE NANGOLE

MWENYEKITI wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Arusha(CCM)bw Onesmo ole Nangole amewataka Viongozi mbalimbali wa chama hasa wale ambao walitoa ahadi  kwa wananchi kwenye uombaji wa kura kuhakikisha kuwa wanatekeleza ahadi hizo kwa haraka sana kwani wale ambao hawatekelezi ahadi wanachangia sana chama hicho kuelekezewa lawama

Bw Nangole aliyasema hayo Juzi wakati akifungua Kata mpya ya Chama hicho ambayo kwa sasa inajulikana kama Kata ya Majengo iliopo Meru Mkoani Arusha.

Aidha Bw Nangole alisema kuwa tabia ya baadhi ya Viongozi ya kuwa watoa ahadi hasa nyakati za kura na kisha wakishapata kura wanasahau ahadi zao inachangia sana kuunguza Ccm kwenye jamii na kuonekana kuwa ni watoaji ahadi zisizotekelezwa.

Alisema kuwa Viongozi wote ambao walitoa ahadi mbalimbali kwa wananchi hasa katika Nyakati za Kura wanatakiwa kuhakikisha kuwa watekeleza ahadi zao na kujijengea tabia ya kuwaangalia wapiga kura wao ili kuendelea kulinda uhai wa Chama

‘msihaidi tu wakati wa kura sasa anzeni kutatua kero za wananchi pamoja na ahadi zenu kwa lkufanya hivyo mtakuwa mmetoa fursa kubwa sana kwa chama chetu lakini kama mtakuwa mnahaidi na kisha kuingia Mitini huku wananchi wakiwa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali hapo mtakuwa mmewapa Vyama vya Upinzani nafasi ya kuongea”aliongeza Bw Nangole

Mbali na hayo aliongeza kuwa Viongozi mbalimbali wa Chama hicho wanatakiwa kuangalia zaidi ilani ya chama hicho kwa kuhakikisha kuwa wanaainisha matatizo ambayo yapo kwenye jamii na kisha kuyatatua kuanzia kwenye Ngazi za Vitongoji na Vijiji.

“Suala la Maendeleo sio suala la kuanzia ngazi za juu za uongozi bali ni suala la kuanzia ngazi za chini hata ninyi viongozi wa chini mnatakiwa kuangalia Kero ambazo zinaikabili jamii na mtasaidia sana ingawaje kwa sasa wapo viongozi wa chini kabisa ambao bado nao hawajitambui katika mchakato wa kuwasaidia wananchi”aliongeza Bw Nangole

Katika hatua nyingine Katibu wa Chama hicho Wilaya ya Meru Bw Langaeli Akyoo alisema kuwa bado Wilaya hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinatakiwa zitatuliwe kwa haraka sana ingawaje umoja na ushirikiano unaitajika kwa haraka sana

Bw Akyoo alisema kuwa kama Viongozi wa Chama hicho kwa Kushirikiana na wananchi wataweza kuwa kitu kimoja basi watachangia sana Maendeleo na hata mara nyingine kutimiza ahadi mbalimbali ambazo zilihaidiwa na chama hicho lakini hazikutekelezwa.

MWISHO

No comments:

Post a Comment