Wednesday, January 30, 2013

POLISI ARUSHA WAKUSANYA BILIONI 1.2 KUTOKANA NA MAKOSA MBALIMBALI



POLISI ARUSHA WAKUSANYA BILIONI 1.2 KUTOKANA NA MAKOSA MBALIMBALI


Na Queen Lema,Arusha

Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha limefanikiwa kukusanya kiasi cha Bilioni 1.2 kwa mwaka 2012 ambapo mwaka jana jeshi hilo lilikusanya zaidi ya  Milioni  518  kutokana na makosa mbalimbali ambayo yanatozwa mara baada ya wananchi kuvunja sheria za Jeshi hilo

Akiongea na “MALKIA WA MATUKIO”jana kuhusuniana na mapato ya jeshi hilo kwa mkoa wa Arusha kamanda wa polisi mkoani hapa Liberatus Sabas alisema kuwa kuongezeka kwa fedha hizo kunatokana na jitiada mbalimbali za jeshi hilo za kupambana na uhalifu.

Sabas alisema kuwa mbali na jeshi hilo kuweza kupambana na uhalifu hivyo kukusanya kiwango kikubwa sana cha fedha  lakini hata uhalifu wenyewe, ajali za barabarani nazo zimepungua  tofauti na miaka ya nyuma kutokana na jitiada ambazo zinafanywa na Polisi

Aliongeza kuwa kwa kipindi cha mwaka 2011 matukio ya ajali za barabarani yalikuwa ni 2507 wakati mwaka 2012 matukio yatokanayo na ajali yalikuwa ni 2106 sawa na upungugu wa asilimia 16

Akiendelea kuelezea pia alisema kuwa hata  matukio ya vifo vitokanavyo na ajali navyo vimepungua kwa kiwango cha hali ya juu sana ambapo  kwa mwaka 2011 matukio yalikuwa 211 huku 2012 yalikuwa ni 175 sawa na upungufu wa asilimia 17 ambapo hali hiyo imetokana na Jitiada mbalimbali ambazo zinatokana na Jeshi hilo

Mbali na hayo pia makosa ya barabarani ambayo yamelipiwa nayo yamechangia sana kuinua pato letu la mwaka ambapo yalikuwa ni zaidi ya elfu 42 kwa mwaka 2012 tofauti na mwaka 2011 ambapo makosa hayo yalikuwa ni 1978 sawa na ongezeko la makosa ya barababarani yaliyolipiwa kwa asilimia 119


“Unaweza kuona matukio yamepungua kwa asilimia kubwa sana lakini pia hata mapato yetu nayo yameongezeka sana hivyo basi bado tunakabiliwa na changamoto ya kuhakikisha kuwa masuala ya uvunjwaji wa sheria yanakwama kabisa ndani ya mkoa wa Arusha kwani uwezekano upo na pia kama tutafanya hivyo tutaongeza mapato lakini tutaokoa maisha ya Watu wa Arusha”aliongeza Sabas

Kutokana na hali hiyo Kamanda Sabas aliwataka wananchi wa Mkoa wa Arusha kuhakikisha kuwa wanakuwa walindaji wazuri wa sheria za nchi na wala sio wavunjaji wazuri wa sheria za Nchi kwani uvunjwaji wa sheria za nchi ndio chanzo cha vifo ,Umaskini pamoja na Migogoro mikubwa sana ndani ya jamii.

MWISHO

No comments:

Post a Comment