Tuesday, January 1, 2013

TUTABORESHA HUDUMA ZA UGANI ILI KUENDELEZA KILIMO KWANZA-MKURUGENZI ARUSHA VIJIJINI


Na Queen Lema,Arusha

TUTABORESHA HUDUMA ZA UGANI ILI KUENDELEZA KILIMO KWANZA-MKURUGENZI ARUSHA VIJIJINI

HALMASHAURI ya Arusha Vijijini  imesema kuwa itaendelea kuboresha huduma za ugani ili kupitia wataalamu hao wa Ugani waweze kutatua changamoto mbalimbali ambazo bado zinaikabili sekta ya Kilimo kwanza.

Hayo yalielezwa na Mkurugenzi wa wilaya hiyo Bw khalifa Idda wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusiana na Maendeleo,mikakati na Changamoto mbalimbali ndani ya Halmashauri hiyo mapema juzi.

Bw Idda alisema kuwa Halmashauri yake imeamua kuendelea kuboresha huduma za Ugani ambapo kupitia uboreshaji huo utaweza kuruhusu mabadiliko makubwa sana kwenye sekta ya Kilimo kwa kuwa Kilimo kinachangia Pato la Halmashauri hiyo.

Alifafanua kuwa bado zipo changamoto Lukuki ambazo zinaikabili Sekta ya Kilimo lakini kama wataalamu ambao ni maafisa Ugani watakuwa na Mazingira mazuri ya kufanyia kazi basi wataweza kuruhusu mabadiliko makubwa kwani watatumia taalumu zao kwa kuwasaidia wananchi.

“tumeamua kwanza kabla ya kuimba wimbo wa kilimo kwanza,tuwaangalie hawa watendaji wakuu ambao ni maafisa ugani,ambapo tulikaa chini na kuona kuwa kama watafanikiwa kupata mahitaji ya msingi basi wataboresha ujuzi wao katika kutoa huduma za msingi kwa wakulima na wafugaji’aliongeza Bw Idda

Pia alisema kuwa,pamoja na kuendelea kuboresha mikakati mbalimbali ya kilimo kwanza ndani ya Halmashauri hiyo lakini bado Sekta ya Kilimo kwanza inakabiliwa na changamoto kubwa sana hali ambayo inafanya Halmashauri hiyo kubuni njia mbalimbali za kuokoa kilimo kwanza.

Alisema kuwa Changamoto hizo ni kama matumizi mabaya ya teknolojia duni katika shuguli za kilimo hasa jembe la mkono,kilimo kisichozingatia hifadhi ya ardhi na maji,pamoja mabadiliko ya hali ya hewa ambayo inaenda sanjari kabisa na ukame.

 Katika hatua nyingine alisema kuwa Changamoto hizo zimekuwa zikichangia mazao pamoja na mifugo kuwa hafifu sana ingawaje Halmashauri hiyo inaendelea kuweka mikakati ya kuhakikisha kuwa hali kama hiyo ya kilimo hafifu inakuwa ni historia kupitia kwa mafias Ugani.

MWISHO

No comments:

Post a Comment