Monday, January 28, 2013

ARUSHA KUZINDUA KAMPENI YA USAFI FEBRUARY MOS,ATAKAYECHAFUA MAZINGIRA KUFIKISHWA MAHAKAMANI

ARUSHA KUZINDUA KAMPENI YA USAFI FEBRUARY MOS,ATAKAYECHAFUA MAZINGIRA KUFIKISHWA MAHAKAMANI


Na Queen Lema,Arusha

Uongozi wa Jiji la Arusha kwa kushirikiana na kamati ya usafi wa Jiji linatarajia kuzindua Kampeni ya usafi wa jiji ambapo kampeni hiyo itaenda sanjari na utozwaji wa faini kwa wachafuzi wa mazingira

Akiongea na Vyombo vya habari mapema leo mwenyekiti wa kamati ya mazingira Jiji la Arusha,Adolph Ulomi alisema kuwa uzinduzi huo utafanyika FebruaryMosi na utashirikisha wananchi wote

Aidha Ulomi alisema kuwa Umoja ambao umeundwa baina ya jiji na kamati hiyo utaweza kuwasaidia kusafisha Jiji la Arusha ambapo kwa sasa kuna changamoto kubwa sana ya uchafuzi wa mazingira

Alisema kuwa kupitia Kamati hiyo ya usafi wa mazingira ambayo inaanza kampeni zake February Mosi itaweza kuhamiashisha shuguli mbalimbali za usafi sanjari na kutoa,kuratibu,vifaa mbalimbali vya usafi ambavyo  hapo awali havikuwepo

‘Tumeamua kufanya mji wa Arusha kuwa na mabadiliko ya hali ya juu sana ikiwa ni pamoja na kuhakikisha hadhi ya jiji inarudi mahala pake hivyo February Mosi tutaanza kazi rasmi ndani ya jiji na tunatarajia kampeni hizi zizinduliwe rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Arusha”alisema Ulomi

Katika hatua nyingine alisema kuwa kupitia kamati hiyo ya usafi wa Jiji la Arusha pia wataweza kusimamia sheria na kanuni  mbalimbali za usafi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa wanaovunja sheria za usafi wanafikishwa mahakamani pamoja na kutozwa faini kubwa

Aliongeza kuwa baadhi ya makosa ambayo yataweza kutiliwa mkazo mkubwa hasa ya usafi wa jiji ni pamoja na kutema mate, kukojoa ovyo ndani ya jiji,kutupa taka ovyo,pamoja na kufanya biashara ndani ya maeneo yasiyo rasmi ambapo wakosaji wote watafikishwa mahakamani.

“unaweza kuona Abiria wanatoka mikoani lakini wanapoingia ndani ya Mji wa Moshi wanaambiwa sasa unaingia Moshi hivyo wasitupe taka lakini wanapoingia katika mji wa Arusha wanaambiwa kabisa wapo huru  kuchafua hili tunataka liwe ni historia  kabisa kwani  uwezo wa kufanya jiji liwe katika hadhi yake upo kabisa”aliongeza Ulomi

Pia alibainisha kuwa Kampeni hiyo ya usafi pia itaweza kwenda sanjari na utoaji wa elimu ya mazingira ndani ya Mitaa zaidi ya 100 ambapo wananchi wataelezewa madhara ya uharibifu wa mazingira.

MWISHO

No comments:

Post a Comment